< Matendo 3 >

1 Siku moja Petro na Yohana walikuwa wanapanda kwenda Hekaluni kusali yapata saa tisa alasiri.
ܘܗܘܐ ܕܟܕ ܤܠܩܝܢ ܫܡܥܘܢ ܟܐܦܐ ܘܝܘܚܢܢ ܐܟܚܕܐ ܠܗܝܟܠܐ ܒܥܕܢܐ ܕܨܠܘܬܐ ܕܬܫܥ ܫܥܝܢ
2 Basi palikuwa na mtu mmoja aliyekuwa kiwete tangu kuzaliwa. Alichukuliwa na kuwekwa kwenye lango la Hekalu liitwalo Zuri, kila siku ili aombe msaada kwa watu wanaoingia Hekaluni.
ܘܗܐ ܓܒܪܐ ܚܕ ܚܓܝܪܐ ܕܡܢ ܟܪܤ ܐܡܗ ܫܩܝܠܝܢ ܗܘܘ ܐܢܫܐ ܐܝܠܝܢ ܕܡܥܕܝܢ ܗܘܘ ܡܝܬܝܢ ܘܤܝܡܝܢ ܠܗ ܒܬܪܥܐ ܕܗܝܟܠܐ ܕܡܬܩܪܐ ܫܦܝܪܐ ܕܢܗܘܐ ܫܐܠ ܙܕܩܬܐ ܡܢ ܗܢܘܢ ܕܥܐܠܝܢ ܠܗܝܟܠܐ
3 Huyu mtu alipowaona Petro na Yohana wakikaribia kuingia Hekaluni, akawaomba wampe sadaka.
ܗܢܐ ܟܕ ܚܙܐ ܠܫܡܥܘܢ ܘܠܝܘܚܢܢ ܕܥܐܠܝܢ ܠܗܝܟܠܐ ܒܥܐ ܗܘܐ ܡܢܗܘܢ ܕܢܬܠܘܢ ܠܗ ܙܕܩܬܐ
4 Wakamkazia macho, kisha Petro akamwambia, “Tutazame sisi.”
ܘܚܪܘ ܒܗ ܫܡܥܘܢ ܘܝܘܚܢܢ ܘܐܡܪܘ ܠܗ ܚܘܪ ܒܢ
5 Hivyo yule mtu akawatazama, akitazamia kupata kitu kutoka kwao.
ܗܘ ܕܝܢ ܚܪ ܒܗܘܢ ܟܕ ܤܒܪ ܗܘܐ ܠܡܤܒ ܡܢܗܘܢ ܡܕܡ
6 Ndipo Petro akamwambia, “Sina fedha wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, tembea!”
ܐܡܪ ܠܗ ܫܡܥܘܢ ܕܗܒܐ ܘܤܐܡܐ ܠܝܬ ܠܝ ܐܠܐ ܡܕܡ ܕܐܝܬ ܠܝ ܝܗܒ ܐܢܐ ܠܟ ܒܫܡܗ ܕܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܢܨܪܝܐ ܩܘܡ ܗܠܟ
7 Petro akamshika yule mtu kwa mkono wa kuume akamwinua, mara nyayo zake na vifundo vya miguu yake vikapata nguvu.
ܘܐܚܕܗ ܒܐܝܕܗ ܕܝܡܝܢܐ ܘܐܩܝܡܗ ܘܒܗ ܒܫܥܬܐ ܫܪ ܪܓܠܘܗܝ ܘܥܩܒܘܗܝ
8 Akaruka juu na kusimama, akaanza kutembea. Kisha akaingia Hekaluni pamoja na Petro na Yohana, huku akitembea na kurukaruka na kumsifu Mungu.
ܘܫܘܪ ܩܡ ܘܗܠܟ ܘܥܠ ܥܡܗܘܢ ܠܗܝܟܠܐ ܟܕ ܡܗܠܟ ܘܡܫܘܪ ܘܡܫܒܚ ܠܐܠܗܐ
9 Watu wote walipomwona akitembea na kumsifu Mungu,
ܘܚܙܐܘܗܝ ܟܠܗ ܥܡܐ ܟܕ ܡܗܠܟ ܘܡܫܒܚ ܠܐܠܗܐ
10 wakamtambua kuwa ni yule mtu aliyekuwa akiketi nje ya Hekalu penye lango liitwalo Zuri akiomba msaada, nao wakajawa na mshangao, wakastaajabu juu ya yale yaliyomtukia.
ܘܐܫܬܘܕܥܘ ܕܗܘܝܘ ܗܘ ܚܕܘܪܐ ܕܝܬܒ ܗܘܐ ܟܠܝܘܡ ܘܫܐܠ ܙܕܩܬܐ ܥܠ ܬܪܥܐ ܕܡܬܩܪܐ ܫܦܝܪܐ ܘܐܬܡܠܝܘ ܬܡܗܐ ܘܕܘܡܪܐ ܥܠ ܡܕܡ ܕܗܘܐ
11 Aliyeponywa alipokuwa akiambatana na Petro na Yohana, watu wote walishangaa mno, wakaja wakiwakimbilia pale ukumbi wa Solomoni.
ܘܟܕ ܐܚܝܕ ܗܘܐ ܠܫܡܥܘܢ ܘܠܝܘܚܢܢ ܪܗܛ ܟܠܗ ܥܡܐ ܟܕ ܬܗܝܪ ܠܘܬܗܘܢ ܠܐܤܛܘܐ ܕܡܬܩܪܐ ܕܫܠܝܡܘܢ
12 Petro alipoona watu wamekusanyika akawaambia, “Enyi Waisraeli, kwa nini mnastaajabu kuhusu jambo hili? Mbona mnatukazia macho kwa mshangao kana kwamba ni kwa uwezo wetu au utakatifu wetu tumemfanya mtu huyu kutembea?
ܘܟܕ ܚܙܐ ܫܡܥܘܢ ܥܢܐ ܘܐܡܪ ܠܗܘܢ ܓܒܪܐ ܒܢܝ ܐܝܤܪܝܠ ܡܢܐ ܡܬܕܡܪܝܢ ܐܢܬܘܢ ܒܗܢܐ ܐܘ ܒܢ ܡܢܐ ܚܝܪܝܢ ܐܢܬܘܢ ܐܝܟ ܗܘ ܕܒܚܝܠܐ ܕܝܠܢ ܐܘ ܒܫܘܠܛܢܢ ܥܒܕܢ ܗܕܐ ܕܢܗܠܟ ܗܢܐ
13 Mungu wa Abrahamu na Isaki na Yakobo, Mungu wa baba zetu amemtukuza Mwanawe Yesu, ambaye ninyi mlimtoa ahukumiwe kifo na mkamkana mbele ya Pilato, ingawa yeye alikuwa ameamua kumwachia aende zake.
ܐܠܗܗ ܗܘ ܕܐܒܪܗܡ ܘܕܐܝܤܚܩ ܘܕܝܥܩܘܒ ܐܠܗܐ ܕܐܒܗܬܢ ܫܒܚ ܠܒܪܗ ܝܫܘܥ ܗܘ ܕܐܢܬܘܢ ܐܫܠܡܬܘܢ ܘܟܦܪܬܘܢ ܒܗ ܩܕܡ ܐܦܘܗܝ ܕܦܝܠܛܘܤ ܟܕ ܗܘ ܙܕܩ ܗܘܐ ܕܢܫܪܝܘܗܝ
14 Ninyi mlimkataa huyo Mtakatifu na Mwenye Haki mkaomba mpewe yule muuaji.
ܐܢܬܘܢ ܕܝܢ ܒܩܕܝܫܐ ܘܙܕܝܩܐ ܟܦܪܬܘܢ ܘܫܐܠܬܘܢ ܠܟܘܢ ܠܓܒܪܐ ܩܛܘܠܐ ܕܢܬܝܗܒ ܠܟܘܢ
15 Hivyo mkamuua aliye chanzo cha uzima, lakini Mungu akamfufua kutoka kwa wafu. Sisi tu mashahidi wa mambo haya.
ܘܠܗܘ ܪܫܐ ܕܚܝܐ ܩܛܠܬܘܢ ܕܠܗ ܐܩܝܡ ܐܠܗܐ ܡܢ ܒܝܬ ܡܝܬܐ ܘܚܢܢ ܟܠܢ ܤܗܕܘܗܝ
16 Kwa imani katika jina la Yesu, huyu mtu mnayemwona na kumfahamu ametiwa nguvu. Ni kwa jina la Yesu na imani itokayo kwake ambayo imemponya kabisa huyu mtu, kama ninyi wote mnavyoona.
ܘܒܗܝܡܢܘܬܐ ܕܫܡܗ ܠܗܢܐ ܕܚܙܝܢ ܐܢܬܘܢ ܘܝܕܥܝܢ ܐܢܬܘܢ ܗܘ ܐܫܪ ܘܐܤܝ ܘܗܝܡܢܘܬܐ ܕܒܗ ܝܗܒܬ ܠܗ ܗܕܐ ܚܠܝܡܘܬܐ ܩܕܡ ܟܠܟܘܢ
17 “Sasa ndugu zangu, najua ya kuwa ninyi mlitenda bila kujua, kama walivyofanya viongozi wenu.
ܒܪܡ ܗܫܐ ܐܚܝ ܝܕܥ ܐܢܐ ܕܒܛܘܥܝܝ ܥܒܕܬܘܢ ܗܕܐ ܐܝܟ ܕܥܒܕܘ ܪܫܝܟܘܢ
18 Lakini kwa njia hii Mungu alitimiza kile ambacho alikuwa ametabiri kwa vinywa vya manabii wake wote, kwamba Kristo atateswa.
ܘܐܠܗܐ ܐܝܟ ܡܕܡ ܕܩܕܡ ܐܟܪܙ ܒܦܘܡ ܟܠܗܘܢ ܢܒܝܐ ܕܢܚܫ ܡܫܝܚܗ ܡܠܝ ܗܟܢܐ
19 Tubuni basi mkamgeukie Mungu, dhambi zenu zifutwe, ili zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwepo kwake Bwana,
ܬܘܒܘ ܗܟܝܠ ܘܐܬܦܢܘ ܐܝܟܢܐ ܕܢܬܥܛܘܢ ܚܛܗܝܟܘܢ ܘܢܐܬܘܢ ܠܟܘܢ ܙܒܢܐ ܕܢܝܚܬܐ ܡܢ ܩܕܡ ܦܪܨܘܦܗ ܕܡܪܝܐ
20 naye apate kumtuma Kristo, ambaye ameteuliwa kwa ajili yenu, yaani Yesu.
ܘܢܫܕܪ ܠܟܘܢ ܠܐܝܢܐ ܕܡܛܝܒ ܗܘܐ ܠܟܘܢ ܠܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ
21 Ilimpasa mbingu zimpokee mpaka wakati wa kufanywa upya kila kitu, kama Mungu alivyoahidi zamani kupitia kwa vinywa vya manabii wake watakatifu. (aiōn g165)
ܕܠܗ ܘܠܐ ܠܫܡܝܐ ܕܢܩܒܠܘܢ ܥܕܡܐ ܠܡܘܠܝܐ ܕܙܒܢܐ ܕܟܠܗܝܢ ܐܝܠܝܢ ܕܡܠܠ ܐܠܗܐ ܒܦܘܡܐ ܕܢܒܝܘܗܝ ܩܕܝܫܐ ܕܡܢ ܥܠܡ (aiōn g165)
22 Kwa maana Mose alisema, ‘Bwana Mungu wenu atawainulia nabii kama mimi kutoka miongoni mwa ndugu zenu. Itawapasa kumtii huyo kwa kila jambo atakalowaambia.
ܡܘܫܐ ܓܝܪ ܐܡܪ ܕܢܒܝܐ ܢܩܝܡ ܠܟܘܢ ܡܪܝܐ ܡܢ ܐܚܝܟܘܢ ܐܟܘܬܝ ܠܗ ܫܡܥܘ ܒܟܠ ܡܐ ܕܢܡܠܠ ܥܡܟܘܢ
23 Mtu yeyote ambaye hatamsikiliza huyo nabii, atatupiliwa mbali kabisa na watu wake.’
ܘܬܗܘܐ ܟܠ ܢܦܫܐ ܐܝܕܐ ܕܠܐ ܬܫܡܥ ܠܢܒܝܐ ܗܘ ܬܐܒܕ ܢܦܫܐ ܗܝ ܡܢ ܥܡܗ
24 “Naam, manabii wote tangu Samweli na waliokuja baada yake, wote walitabiri kuhusu siku hizi.
ܘܢܒܝܐ ܟܠܗܘܢ ܡܢ ܫܡܘܐܝܠ ܘܐܝܠܝܢ ܕܡܢ ܒܬܪܗ ܗܘܘ ܡܠܠܘ ܘܐܟܪܙܘ ܥܠ ܝܘܡܬܐ ܗܢܘܢ
25 Ninyi ndio wana wa manabii na wa Agano ambalo Mungu alifanya na baba zenu, akimwambia Abrahamu, ‘Kupitia kwa uzao wako, watu wote wa ulimwengu watabarikiwa.’
ܐܢܬܘܢ ܐܢܘܢ ܒܢܝܗܘܢ ܕܢܒܝܐ ܘܕܕܝܬܩܐ ܐܝܕܐ ܕܤܡ ܐܠܗܐ ܠܐܒܗܬܢ ܟܕ ܐܡܪ ܠܐܒܪܗܡ ܕܒܙܪܥܟ ܢܬܒܪܟܢ ܟܠܗܝܢ ܫܪܒܬܐ ܕܐܪܥܐ
26 Mungu alipomfufua Yesu Mwanawe, alimtuma kwenu kwanza, ili awabariki kwa kumgeuza kila mmoja wenu kutoka njia yake mbaya.”
ܠܟܘܢ ܡܢ ܩܕܝܡ ܐܩܝܡ ܘܫܕܪ ܐܠܗܐ ܠܒܪܗ ܟܕ ܡܒܪܟ ܠܟܘܢ ܐܢ ܬܬܦܢܘܢ ܘܬܬܘܒܘܢ ܡܢ ܒܝܫܬܟܘܢ

< Matendo 3 >