< Matendo 28 >

1 Baada ya kufika nchi kavu salama, ndipo tukafahamu kwamba jina la kile kisiwa ni Malta.
And when they were come safe, then they knewe that the Yle was called Melita.
2 Wenyeji wa kile kisiwa wakatufanyia ukarimu usio wa kawaida. Waliwasha moto na kutukaribisha sisi sote kwa sababu mvua ilikuwa inanyesha na kulikuwa na baridi.
And the Barbarians shewed vs no litle kindnesse: for they kindled a fire, and receiued vs euery one, because of the present showre, and because of the colde.
3 Paulo alikuwa amekusanya mzigo wa kuni na alipokuwa anaweka kwenye moto kwa ajili ya joto, nyoka mwenye sumu akatoka humo na kujisokotea mkononi mwake.
And when Paul had gathered a nomber of stickes, and laid them on the fire, there came a viper out of the heate, and leapt on his hand.
4 Wale wenyeji wa kile kisiwa walipomwona yule nyoka akiningʼinia mkononi mwa Paulo, wakaambiana, “Huyu mtu lazima awe ni muuaji, ingawa ameokoka kutoka baharini, haki haijamwacha aishi.”
Nowe when ye Barbarians saw the worme hang on his hand, they said among themselues, This man surely is a murtherer, whom, though he hath escaped the sea, yet Vengeance hath not suffered to liue.
5 Lakini Paulo akamkungʼutia yule nyoka ndani ya moto wala yeye hakupata madhara yoyote.
But he shooke off the worme into the fire, and felt no harme.
6 Watu walikuwa wanangoja avimbe au aanguke ghafula na kufa. Lakini baada ya kungoja kwa muda mrefu na kuona kwamba hakuna chochote kisicho cha kawaida kilichomtokea, wakabadili mawazo yao na kuanza kusema kwamba yeye ni mungu.
Howbeit they wayted whe he should haue swolne, or fallen downe dead suddenly: but after they had looked a great while, and sawe no inconuenience come to him, they changed their mindes, and said, That he was a God.
7 Basi karibu na sehemu ile, palikuwa na shamba kubwa la mtu mmoja kiongozi wa kile kisiwa, aliyeitwa Publio. Alitupokea na akatuhudumia kwa ukarimu mkubwa kwa muda wa siku tatu.
In the same quarters, the chiefe man of the Yle (whose name was Publius) had possessions: the same receiued vs, and lodged vs three dayes courteously.
8 Baba yake Publio alikuwa mgonjwa kitandani, akiwa anaumwa homa na kuhara damu. Paulo akaingia ndani ili kumwona na baada ya maombi, akaweka mikono juu yake na kumponya.
And so it was, that the father of Publius lay sicke of the feauer, and of a bloodie flixe: to whom Paul entred in, and when he prayed, he laide his hands on him, and healed him.
9 Jambo hili lilipotukia, watu wote wa kisiwa kile waliokuwa wagonjwa wakaja, nao wakaponywa.
When this then was done, other also in the Yle, which had diseases, came to him, and were healed,
10 Wakatupa heshima nyingi, nasi tulipokuwa tayari kusafiri kwa njia ya bahari, wakapakia melini vitu vyote tulivyokuwa tunavihitaji.
Which also did vs great honour: and when we departed, they laded vs with things necessarie.
11 Miezi mitatu baadaye tukaanza safari kwa meli iliyokuwa imetia nanga kwenye kisiwa hicho kwa ajili ya majira ya baridi. Hii ilikuwa meli ya Iskanderia yenye alama ya miungu pacha waitwao Kasta na Poluksi.
Nowe after three moneths we departed in a shippe of Alexandria, which had wintred in the Yle, whose badge was Castor and Pollux.
12 Kituo chetu cha kwanza kilikuwa Sirakusa na tukakaa huko siku tatu.
And when we arriued at Syracuse, we taried there three dayes.
13 Kisha tukangʼoa nanga, tukafika Regio. Siku iliyofuata, upepo mkali wa kusi ukavuma, na siku ya pili yake tukafika Puteoli.
And from thence we set a compasse, and came to Rhegium: and after one day, the South wind blewe, and we came the seconde day to Putioli:
14 Huko tukawakuta ndugu, nasi tukakaribishwa tukae nao kwa siku saba. Hivyo tukaendelea na safari mpaka Rumi.
Where we found brethren, and were desired to tary with them seuen dayes, and so we went toward Rome.
15 Ndugu wa huko Rumi waliposikia habari zetu, walikuja mpaka Soko la Apio na mahali paitwapo Mikahawa Mitatu kutulaki. Paulo alipowaona, alimshukuru Mungu akatiwa moyo.
And from thence, when the brethren heard of vs, they came to meete vs at the Market of Appius, and at the Three tauernes, whom when Paul sawe, he thanked God, and waxed bolde.
16 Tulipofika Rumi, Paulo aliruhusiwa kuishi peke yake akiwa na askari wa kumlinda.
So when we came to Rome, the Centurion deliuered the prisoners to the generall Captaine: but Paul was suffered to dwell by him selfe with a souldier that kept him.
17 Siku tatu baadaye Paulo akawaita pamoja viongozi wa Kiyahudi. Walipokwisha kukusanyika akawaambia, “Ndugu zangu, ingawa sikufanya jambo lolote dhidi ya watu wetu au dhidi ya desturi za baba zetu, lakini nilikamatwa huko Yerusalemu nikakabidhiwa kwa Warumi.
And the third day after, Paul called the chiefe of the Iewes together: and when they were come, he said vnto them, Men and brethren, though I haue committed nothing against the people, or Lawes of the fathers, yet was I deliuered prisoner from Hierusalem into the handes of the Romanes.
18 Wao walipokwisha kunihoji, wakataka kuniachia huru kwa sababu hawakuona kosa lolote nililolifanya linalostahili adhabu ya kifo.
Who when they had examined me, would haue let me goe, because there was no cause of death in me.
19 Lakini Wayahudi walipopinga uamuzi huo, nililazimika kukata rufaa kwa Kaisari, ingawa sikuwa na lalamiko lolote juu ya taifa langu.
But when the Iewes spake contrary, I was constrained to appeale vnto Cesar, not because I had ought to accuse my nation of.
20 Basi hii ndiyo sababu nimewatumania, ili niseme nanyi. Kwa kuwa ni kwa ajili ya tumaini la Israeli nimefungwa kwa minyororo.”
For this cause therefore haue I called for you, to see you, and to speake with you: for that hope of Israels sake, I am bound with this chaine.
21 Wakamjibu, “Hatujapokea barua zozote kutoka Uyahudi zinazokuhusu, wala hapana ndugu yeyote aliyekuja hapa ambaye ametoa taarifa au kuzungumza jambo lolote baya juu yako.
Then they saide vnto him, We neither receiued letters out of Iudea concerning thee, neither came any of the brethren that shewed or spake any euill of thee.
22 Lakini tungependa kusikia kutoka kwako unalofikiri kwa sababu tunajua kwamba kila mahali watu wanazungumza mabaya kuhusu jamii hii.”
But we will heare of thee what thou thinkest: for as concerning this sect, we knowe that euery where it is spoken against.
23 Baada ya kupanga siku ya kuonana naye, watu wengi wakaja kuanzia asubuhi hadi jioni akawaeleza na kutangaza kuhusu Ufalme wa Mungu akijaribu kuwahadithia juu ya Yesu kutoka Sheria ya Mose na kutoka Manabii.
And when they had appointed him a day, there came many vnto him into his lodging, to whom he expounded testifying the kingdome of God, and persuading them those things that concerne Iesus, both out of the Lawe of Moses, and out of the Prophets, from morning to night.
24 Baadhi wakasadiki yale aliyosema, lakini wengine hawakuamini.
And some were persuaded with ye things which were spoken, and some beleeued not.
25 Hivyo hawakukubaliana, nao walipokuwa wanaondoka, Paulo akatoa kauli moja zaidi: “Roho Mtakatifu alinena kweli na baba zenu aliposema mambo yale yaliyomhusu Bwana Yesu kwa kinywa cha nabii Isaya kwamba:
Therefore when they agreed not among themselues, they departed, after that Paul had spoken one word, to wit, Well spake the holy Ghost by Esaias the Prophet vnto our fathers,
26 “‘Nenda kwa watu hawa na useme, “Hakika mtasikiliza lakini hamtaelewa; na pia mtatazama, lakini hamtaona.”
Saying, Goe vnto this people, and say, By hearing ye shall heare, and shall not vnderstand, and seeing ye shall see, and not perceiue.
27 Kwa kuwa mioyo ya watu hawa imekuwa migumu; hawasikii kwa masikio yao, na wamefumba macho yao. Wasije wakaona kwa macho yao, na wakasikiliza kwa masikio yao, wakaelewa kwa mioyo yao, na kugeuka nami nikawaponya.’
For the heart of this people is waxed fatte, and their eares are dull of hearing, and with their eyes haue they winked, least they shoulde see with their eyes, and heare with their eares, and vnderstand with their heartes, and should returne that I might heale them.
28 “Basi na ijulikane kwenu kwamba, huu wokovu wa Mungu umepelekwa kwa watu wa Mataifa, nao watasikiliza.” [
Be it knowen therefore vnto you, that this saluation of God is sent to the Gentiles, and they shall heare it.
29 Naye akiisha kusema maneno haya, Wayahudi wakaondoka wakiwa na hoja nyingi miongoni mwao.]
And when he had saide these things, the Iewes departed, and had great reasoning among themselues.
30 Kwa miaka miwili mizima Paulo alikaa huko kwa nyumba aliyokuwa amepanga. Akawakaribisha wote waliokwenda kumwona.
And Paul remained two yeeres full in an house hired for himselfe, and receiued all that came in vnto him,
31 Akahubiri Ufalme wa Mungu na kufundisha mambo yale yaliyomhusu Bwana Yesu Kristo, kwa ujasiri wote na bila kizuizi chochote.
Preaching the kingdome of God, and teaching those things which concerne the Lord Iesus Christ, with all boldnesse of speache, without let.

< Matendo 28 >