< Matendo 28 >

1 Baada ya kufika nchi kavu salama, ndipo tukafahamu kwamba jina la kile kisiwa ni Malta.
Following the rescue, they learned that the island was called Malta.
2 Wenyeji wa kile kisiwa wakatufanyia ukarimu usio wa kawaida. Waliwasha moto na kutukaribisha sisi sote kwa sababu mvua ilikuwa inanyesha na kulikuwa na baridi.
Now the natives showed us unusual kindness, in that they kindled a fire and welcomed us all, because it had begun to rain and was cold.
3 Paulo alikuwa amekusanya mzigo wa kuni na alipokuwa anaweka kwenye moto kwa ajili ya joto, nyoka mwenye sumu akatoka humo na kujisokotea mkononi mwake.
But when Paul had gathered a bundle of sticks and placed them on the fire, because of the heat a viper came out and fastened itself on his hand.
4 Wale wenyeji wa kile kisiwa walipomwona yule nyoka akiningʼinia mkononi mwa Paulo, wakaambiana, “Huyu mtu lazima awe ni muuaji, ingawa ameokoka kutoka baharini, haki haijamwacha aishi.”
So when the natives saw the beast hanging from his hand, they started saying to each other, “This man must be a murderer, whom Justice has not allowed to live, even though rescued from the sea.”
5 Lakini Paulo akamkungʼutia yule nyoka ndani ya moto wala yeye hakupata madhara yoyote.
But he just shook the beast off into the fire and suffered no harm.
6 Watu walikuwa wanangoja avimbe au aanguke ghafula na kufa. Lakini baada ya kungoja kwa muda mrefu na kuona kwamba hakuna chochote kisicho cha kawaida kilichomtokea, wakabadili mawazo yao na kuanza kusema kwamba yeye ni mungu.
Well they were expecting him to swell up, or suddenly fall down dead; but after waiting for quite a while and seeing nothing unusual happening to him, they changed their mind and started saying he was a god.
7 Basi karibu na sehemu ile, palikuwa na shamba kubwa la mtu mmoja kiongozi wa kile kisiwa, aliyeitwa Publio. Alitupokea na akatuhudumia kwa ukarimu mkubwa kwa muda wa siku tatu.
Now in that region there were properties belonging to the chief man of the island, named Publius, who welcomed us and in a friendly manner took care of us for three days.
8 Baba yake Publio alikuwa mgonjwa kitandani, akiwa anaumwa homa na kuhara damu. Paulo akaingia ndani ili kumwona na baada ya maombi, akaweka mikono juu yake na kumponya.
Well it happened that the father of Publius was sick in bed with fever and dysentery; Paul went in to him, prayed, and laying his hands on him, healed him.
9 Jambo hili lilipotukia, watu wote wa kisiwa kile waliokuwa wagonjwa wakaja, nao wakaponywa.
So, when this had happened, the rest of those on the island who had diseases started coming and being healed;
10 Wakatupa heshima nyingi, nasi tulipokuwa tayari kusafiri kwa njia ya bahari, wakapakia melini vitu vyote tulivyokuwa tunavihitaji.
who also honored us in many ways, and when we put to sea they provided the necessary things.
11 Miezi mitatu baadaye tukaanza safari kwa meli iliyokuwa imetia nanga kwenye kisiwa hicho kwa ajili ya majira ya baridi. Hii ilikuwa meli ya Iskanderia yenye alama ya miungu pacha waitwao Kasta na Poluksi.
Now after three months we put to sea in an Alexandrian ship that had wintered in the island, whose figurehead was ‘the Twin Brothers’.
12 Kituo chetu cha kwanza kilikuwa Sirakusa na tukakaa huko siku tatu.
We put in at Syracuse and stayed there three days;
13 Kisha tukangʼoa nanga, tukafika Regio. Siku iliyofuata, upepo mkali wa kusi ukavuma, na siku ya pili yake tukafika Puteoli.
from there we tacked back and forth and arrived at Rhegium. After one day a south wind sprang up, and on the second day we came to Puteoli,
14 Huko tukawakuta ndugu, nasi tukakaribishwa tukae nao kwa siku saba. Hivyo tukaendelea na safari mpaka Rumi.
where we found brothers who urged us to stay there seven days—that was how we went toward Rome.
15 Ndugu wa huko Rumi waliposikia habari zetu, walikuja mpaka Soko la Apio na mahali paitwapo Mikahawa Mitatu kutulaki. Paulo alipowaona, alimshukuru Mungu akatiwa moyo.
And the brothers there, when they heard about our circumstances, came out to meet us as far as Appii Forum and Three Inns. When Paul saw them he thanked God and took courage.
16 Tulipofika Rumi, Paulo aliruhusiwa kuishi peke yake akiwa na askari wa kumlinda.
Now when we entered Rome, the centurion delivered the prisoners to the commander; but Paul was allowed to live by himself, with the soldier who guarded him.
17 Siku tatu baadaye Paulo akawaita pamoja viongozi wa Kiyahudi. Walipokwisha kukusanyika akawaambia, “Ndugu zangu, ingawa sikufanya jambo lolote dhidi ya watu wetu au dhidi ya desturi za baba zetu, lakini nilikamatwa huko Yerusalemu nikakabidhiwa kwa Warumi.
It happened that after three days Paul called together the leaders of the Jews; and when they had assembled he said to them: “Men, brothers, though I had done nothing against ‘the people’ or the ancestral customs, still I was delivered as a prisoner from Jerusalem into the hands of the Romans,
18 Wao walipokwisha kunihoji, wakataka kuniachia huru kwa sababu hawakuona kosa lolote nililolifanya linalostahili adhabu ya kifo.
who, when they had examined me, were intending to release me, because I was not guilty of any crime deserving death.
19 Lakini Wayahudi walipopinga uamuzi huo, nililazimika kukata rufaa kwa Kaisari, ingawa sikuwa na lalamiko lolote juu ya taifa langu.
But when the Jews spoke against it, I was compelled to appeal to Caesar; not that I had anything about which to accuse my nation.
20 Basi hii ndiyo sababu nimewatumania, ili niseme nanyi. Kwa kuwa ni kwa ajili ya tumaini la Israeli nimefungwa kwa minyororo.”
For this reason therefore I asked to see you and speak with you; it is because of the hope of Israel that I am bound with this chain.”
21 Wakamjibu, “Hatujapokea barua zozote kutoka Uyahudi zinazokuhusu, wala hapana ndugu yeyote aliyekuja hapa ambaye ametoa taarifa au kuzungumza jambo lolote baya juu yako.
So they said to him: “We have neither received letters from Judea concerning you, nor have any of the brothers who came reported or spoken any evil about you.
22 Lakini tungependa kusikia kutoka kwako unalofikiri kwa sababu tunajua kwamba kila mahali watu wanazungumza mabaya kuhusu jamii hii.”
But we desire to hear from you what you think; because as for this sect, we know that it is spoken against everywhere.”
23 Baada ya kupanga siku ya kuonana naye, watu wengi wakaja kuanzia asubuhi hadi jioni akawaeleza na kutangaza kuhusu Ufalme wa Mungu akijaribu kuwahadithia juu ya Yesu kutoka Sheria ya Mose na kutoka Manabii.
So arranging a day with him, even more people came to him at his lodging, to whom he kept expounding from morning until evening: solemnly testifying about the Kingdom of God and trying to convince them concerning Jesus, from both the Law of Moses and the Prophets.
24 Baadhi wakasadiki yale aliyosema, lakini wengine hawakuamini.
Well some were persuaded by what had been said, and some kept refusing to believe.
25 Hivyo hawakukubaliana, nao walipokuwa wanaondoka, Paulo akatoa kauli moja zaidi: “Roho Mtakatifu alinena kweli na baba zenu aliposema mambo yale yaliyomhusu Bwana Yesu kwa kinywa cha nabii Isaya kwamba:
So being in disagreement among themselves they started to leave, after Paul had said this one word: “The Holy Spirit spoke correctly to our fathers through Isaiah the prophet,
26 “‘Nenda kwa watu hawa na useme, “Hakika mtasikiliza lakini hamtaelewa; na pia mtatazama, lakini hamtaona.”
saying: ‘Go to this people and say, “You will keep on hearing, but never understand; you will keep on seeing, but never perceive”;
27 Kwa kuwa mioyo ya watu hawa imekuwa migumu; hawasikii kwa masikio yao, na wamefumba macho yao. Wasije wakaona kwa macho yao, na wakasikiliza kwa masikio yao, wakaelewa kwa mioyo yao, na kugeuka nami nikawaponya.’
because the heart of this people has become sluggish, and their ears are hard of hearing, and their eyes they have closed; in order that they not see with their eyes, nor hear with their ears, nor understand with their heart, nor turn back, so I could heal them.’
28 “Basi na ijulikane kwenu kwamba, huu wokovu wa Mungu umepelekwa kwa watu wa Mataifa, nao watasikiliza.” [
Therefore let it be known to you that the salvation of God has been sent to the Gentiles; they will listen!”
29 Naye akiisha kusema maneno haya, Wayahudi wakaondoka wakiwa na hoja nyingi miongoni mwao.]
And when he had said these things the Jews went their way, having a great dispute among themselves.
30 Kwa miaka miwili mizima Paulo alikaa huko kwa nyumba aliyokuwa amepanga. Akawakaribisha wote waliokwenda kumwona.
Paul stayed two whole years in his own rented house, and received all who came to see him,
31 Akahubiri Ufalme wa Mungu na kufundisha mambo yale yaliyomhusu Bwana Yesu Kristo, kwa ujasiri wote na bila kizuizi chochote.
proclaiming the Kingdom of God and teaching the things concerning the Lord Jesus Christ, with all boldness, without hindrance.

< Matendo 28 >