< Matendo 27 >
1 Ilipoamuliwa kwamba tungesafiri kwa njia ya bahari kwenda Italia, Paulo na wafungwa wengine wakakabidhiwa kwa kiongozi mmoja wa askari aliyeitwa Juliasi, aliyekuwa wa Kikosi cha Walinzi wa Kaisari.
Men da det var besluttet, at vi skulde afsejle til Italien, overgave de baade Paulus og nogle andre Fanger til en Høvedsmand ved Navn Julius af den kejserlige Afdeling.
2 Tulipanda meli iliyotoka Adramitio, iliyokuwa inakaribia kusafiri kwenda kwenye bandari zilizopo pwani ya Asia, tukaanza safari yetu tukiwa pamoja na Aristarko, Mmakedonia kutoka Thesalonike.
Vi gik da om Bord paa et adramyttisk Skib, som skulde gaa til Stederne langs med Asiens Kyster, og vi sejlede af Sted; og Aristarkus, en Makedonier fra Thessalonika, var med os.
3 Kesho yake tukatia nanga Sidoni, naye Juliasi akamfanyia wema Paulo, akamruhusu aende kwa rafiki zake ili wamtimizie mahitaji yake.
Og den næste Dag anløb vi Sidon. Og Julius, som behandlede Paulus venligt, tilstedte ham at gaa hen til sine Venner og nyde Pleje.
4 Kutoka huko tukaingia baharini tena na tukapita upande wa chini wa kisiwa cha Kipro kwa sababu upepo ulikuwa wa mbisho.
Og vi fore bort derfra og sejlede ind under Kypern, fordi Vinden var imod.
5 Baada ya sisi kuvuka bahari iliyoko upande wa Kilikia na Pamfilia, tukafika Mira huko Likia.
Og vi sejlede igennem Farvandet ved Kilikien og Pamfylien og kom til Myra i Lykien.
6 Huko yule kiongozi wa askari akapata meli ya Iskanderia ikielekea Italia, akatupandisha humo.
Og der fandt Høvedsmanden et aleksandrinsk Skib, som sejlede til Italien, og bragte os over i det.
7 Tukasafiri polepole kwa siku nyingi na kwa shida, hatimaye tukafika karibu na Nido. Kwa kuwa upepo wa mbisho ulituzuia tusiweze kushika mwelekeo tuliokusudia, tukapita chini ya Krete mkabala na Salmone.
Men da Sejladsen i mange Dage gik langsomt, og vi med Nød og næppe naaede henimod Knidus (thi Vinden føjede os ikke), holdt vi ned under Kreta ved Salmone.
8 Tukaambaa na pwani kwa shida, tukafika sehemu iitwayo Bandari Nzuri, karibu na mji wa Lasea.
Med Nød og næppe sejlede vi der forbi og kom til et Sted, som kaldes „Gode Havne”, nær ved Byen Lasæa.
9 Muda mwingi ulikuwa umepotea na kusafiri baharini kulikuwa hatari kwa sababu wakati huu ulikuwa baada ya siku za kufunga. Hivyo Paulo akawaonya akasema,
Men da en rum Tid var forløben, og Sejladsen allerede var farlig, saasom endog Fasten allerede var forbi, formanede Paulus dem og sagde:
10 “Mabwana, naona kuwa hii safari ni yenye maafa na ya kuleta hasara kubwa kwa meli na shehena, pia kwa maisha yetu.”
„I Mænd! jeg ser, at Sejladsen vil medføre Ulykke og megen Skade, ikke alene paa Ladning og Skib, men ogsaa paa vort Liv.”
11 Lakini badala ya yule kiongozi wa askari kusikiliza yale Paulo aliyosema, akafuata zaidi ushauri wa nahodha na mwenye meli.
Men Høvedsmanden stolede mere paa Styrmanden og Skipperen end paa det, som Paulus sagde.
12 Kwa kuwa ile bandari ilikuwa haifai kukaa wakati wa majira ya baridi, wengi wakashauri kwamba tuendelee na safari wakitarajia kufika Foinike na kukaa huko kwa majira ya baridi. Hii ilikuwa bandari iliyoko katika kisiwa cha Krete ikikabili upande wa kusini-magharibi na kaskazini-magharibi.
Og da Havnen ikke egnede sig til Vinterleje, besluttede de fleste, at man skulde sejle derfra, om man muligt kunde naa hen og overvintre i Føniks, en Havn paa Kreta, som vender imod Sydvest og Nordvest.
13 Upepo mtulivu ulipoanza kuvuma toka kusini, wakadhani kuwa wangeweza kufikia lengo lao, hivyo wakangʼoa nanga na kusafiri wakipita kandokando ya pwani ya kisiwa cha Krete.
Da der nu blæste en Søndenvind op, mente de at have naaet deres Hensigt, lettede Anker og sejlede langs med og nærmere ind under Kreta.
14 Lakini baada ya muda mfupi ikavuma tufani kubwa iitwayo “Eurakilo” toka kisiwa cha Krete.
Men ikke længe derefter for der en heftig Storm ned over den, den saakaldte „Eurakvilo”.
15 Meli ikapigwa na dhoruba na haikuweza kushindana na ule upepo, tukarudishwa baharini upepo ulikokuwa unaelekea.
Og da Skibet reves med og ikke kunde holde op imod Vinden, opgave vi det og lode os drive.
16 Hatimaye tukisafiri kupita chini ya kisiwa kidogo kiitwacho Kauda, ambapo kwa kuwa tulikuwa tumekingiwa upepo na hicho kisiwa, tuliweza kwa shida kuifunga mashua ya kuokolea watu.
Men da vi løb ind under en lille Ø, som kaldes Klavde, formaaede vi med Nød og næppe at bjærge Baaden.
17 Watu walipokwisha kuivuta mashua hiyo na kuiingiza katika meli, waliifunga kwa kamba chini ya meli yenyewe ili kuzishikanisha pamoja. Wakiogopa kupelekwa kwenye mchanga karibu na pwani ya Sirti, wakashusha matanga wakaiacha meli isukumwe na huo upepo.
Men efter at have trukket den op, anvendte de Nødmidler og omsurrede Skibet; og da de frygtede for, at de skulde blive kastede ned i Syrten, firede de Sejlene ned og lode sig saaledes drive.
18 Tulikuwa tunapigwa na dhoruba kwa nguvu, kiasi kwamba kesho yake walianza kutupa shehena toka melini.
Og da vi maatte kæmpe haardt med Stormen, begyndte de næste Dag at kaste over Bord.
19 Siku ya tatu, wakatupa vyombo vya meli baharini kwa mikono yao wenyewe.
Og paa den tredje Dag udkastede de med egne Hænder Skibets Redskaber.
20 Kulipokuwa hakuna kuonekana kwa jua wala nyota kwa siku nyingi, nayo dhoruba ikiwa inaendelea kuwa kali, hatimaye tulikata kabisa tamaa ya kuokoka.
Men da hverken Sol eller Stjerner lode sig se i flere Dage, og vi havde et Uvejr over os, som ikke var ringe, blev fra nu af alt Haab om Redning os betaget.
21 Baada ya watu kukaa siku nyingi bila kula chakula, Paulo akasimama katikati yao akasema, “Enyi watu, iliwapasa kunisikiliza na kuacha kusafiri baharini kutoka Krete, ndipo ninyi mngekuwa mmejinusuru na uharibifu huu na hasara hii.
Og da man længe ikke havde taget Føde til sig, saa stod Paulus frem midt iblandt dem og sagde: „I Mænd! man burde have adlydt mig og ikke være sejlet bort fra Kreta og have sparet os denne Ulykke og Skade.
22 Sasa ninawasihi sana, jipeni moyo mkuu kwa kuwa hakuna hata mmoja wenu atakayepoteza maisha yake, ila meli itaangamia.
Og nu formaner jeg eder til at være ved godt Mod; thi ingen Sjæl af eder skal forgaa, men alene Skibet.
23 Jana usiku, malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake na ambaye ninamwabudu alisimama karibu nami,
Thi i denne Nat stod der en Engel hos mig fra den Gud, hvem jeg tilhører, hvem jeg ogsaa tjener, og sagde:
24 naye akasema, ‘Paulo usiogope, kwa kuwa ni lazima usimame mbele ya Kaisari, naye Mungu amekupa kwa neema uhai wa wote wanaosafiri pamoja nawe.
„Frygt ikke, Paulus! du skal blive stillet for Kejseren; og se, Gud har skænket dig alle dem, som sejle med dig.”
25 Hivyo jipeni moyo, enyi watu, kwa kuwa ninamwamini Mungu kwamba yatakuwa kama vile alivyoniambia.’
Derfor, I Mænd! værer ved godt Mod; thi jeg har den Tillid til Gud, at det skal ske saaledes, som der er blevet talt til mig.
26 Lakini hata hivyo meli yetu itakwama kwenye kisiwa fulani.”
Men vi maa strande paa en Ø.”
27 Usiku wa kumi na nne ulipofika, tulikuwa bado tunasukumwa na upepo katika Bahari ya Adria. Ilipokuwa yapata usiku wa manane, mabaharia wakahisi kwamba walikuwa wanakaribia nchi kavu.
Men da den fjortende Nat kom, og vi dreve i det adriatiske Hav, kom det Skibsfolkene for ved Midnatstid, at der var Land i Nærheden.
28 Kwa hiyo wakapima kina cha maji na kukuta kilikuwa pima ishirini, baada ya kuendelea mbele kidogo wakapima tena wakapata kina cha pima kumi na tano.
Og da de loddede, fik de tyve Favne, og da de lidt længere fremme atter loddede, fik de femten Favne.
29 Wakiogopa kwamba meli yetu ingegonga kwenye miamba, wakashusha nanga nne za nyuma ya meli, wakawa wanaomba kupambazuke.
Og da de frygtede, at vi skulde støde paa Skær, kastede de fire Ankere ud fra Bagstavnen og bade til, at det maatte blive Dag.
30 Katika jaribio la kutoroka kutoka kwenye meli, mabaharia wakashusha mashua ya kuokolea watu baharini, wakijifanya kwamba wanakwenda kushusha nanga za omo.
Men da Skibsfolkene gjorde Forsøg paa at flygte fra Skibet og firede Baaden ned i Søen under Paaskud af, at de vilde lægge Ankere ud fra Forstavnen,
31 Ndipo Paulo akamwambia yule jemadari na askari, “Hawa watu wasipobaki katika meli, hamtaweza kuokoka.”
da sagde Paulus til Høvedsmanden og til Stridsmændene: „Dersom disse ikke blive i Skibet, kunne I ikke reddes.”
32 Hivyo basi wale askari wakakata kamba zilizoshikilia ile mashua ya kuokolea watu kwenye meli, wakaiacha ianguke humo baharini.
Da kappede Stridsmændene Baadens Tove og lode den falde ned.
33 Kabla ya mapambazuko, Paulo akawasihi watu wote wale chakula akisema, “Leo ni siku ya kumi na nne mmekuwa katika wasiwasi mkiwa mmefunga na bila kula chochote.
Men indtil det vilde dages, formanede Paulus alle til at tage Næring til sig og sagde: „Det er i Dag den fjortende Dag, I have ventet og tilbragt uden at spise og intet taget til eder.
34 Kwa hiyo nawasihi mle chakula, kwa maana itawasaidia ili mweze kuishi. Kwa kuwa hakuna hata mmoja wenu atakayepoteza unywele hata mmoja kutoka kichwani mwake.”
Derfor formaner jeg eder til at tage Næring til eder, thi dette hører med til eders Redning; ikke et Haar paa Hovedet skal gaa tabt for nogen af eder.”
35 Baada ya kusema maneno haya, Paulo akachukua mkate, akamshukuru Mungu mbele yao wote, akaumega akaanza kula.
Men da han havde sagt dette, tog han Brød og takkede Gud for alles Øjne og brød det og begyndte at spise.
36 Ndipo wote wakatiwa moyo, wakaanza kula chakula.
Da bleve de alle frimodige og toge ogsaa Næring til sig.
37 Ndani ya meli tulikuwa jumla ya watu 276.
Men vi vare i Skibet i alt to Hundrede og seks og halvfjerdsindstyve Sjæle.
38 Baada ya watu wote kula chakula cha kutosha, wakapunguza uzito wa meli kwa kutupa ngano baharini.
Og da de vare blevne mættede med Føde, lettede de Skibet ved at kaste Levnedsmidlerne i Søen.
39 Kulipopambazuka, mabaharia hawakuitambua ile nchi, lakini waliona ghuba yenye ufuko wa mchanga, ambako waliamua kuipweleza meli kama ingewezekana.
Men da det blev Dag, kendte de ikke Landet; men de bemærkede en Vig med en Forstrand, som de besluttede, om muligt, at sætte Skibet ind paa.
40 Kwa hiyo wakatupa nanga zote na kuziacha baharini, na wakati huo huo wakalegeza kamba zilizokuwa zikishikilia usukani wa meli. Kisha wakatweka tanga la mbele lishike upepo na kuisukuma meli kuelekea pwani.
Og de kappede Ankrene, som de lode blive i Søen, og løste tillige Rortovene, og idet de satte Raasejlet til for Vinden, holdt de ind paa Strandbredden.
41 Lakini wakafika mahali ambapo bahari mbili zinakutana, wakaipweleza meli ufuoni, omo ikakwama sana, ikawa haiwezi kuondolewa, lakini sehemu ya shetri ikavunjika vipande vipande kwa kule kupiga kwa mawimbi yenye nguvu.
Men de stødte paa en Grund med dybt Vand paa begge Sider, og der satte de Skibet, og Forstavnen borede sig fast og stod urokkelig, men Bagstavnen sloges sønder af Bølgernes Magt.
42 Wale askari wakapanga kuwaua wale wafungwa ili kuzuia hata mmoja wao asiogelee na kutoroka.
Det var nu Stridsmændenes Raad, at man skulde ihjelslaa Fangerne, for at ingen skulde svømme bort og undkomme.
43 Lakini yule jemadari alitaka kuokoa maisha ya Paulo, basi akawazuia askari wasitekeleze mpango wao. Akaamuru wale wanaoweza kuogelea wajitupe baharini kwanza, waogelee mpaka nchi kavu.
Men Høvedsmanden, som vilde frelse Paulus, forhindrede dem i dette Forehavende og bød, at de, som kunde svømme, skulde først kaste sig ud og slippe i Land,
44 Waliosalia wangefika nchi kavu kwa kutumia mbao au vipande vya meli iliyovunjika, hivyo ikatimia kwamba wote wakaokoka na kufika nchi kavu salama.
og de andre bjærge sig, nogle paa Brædder, andre paa Stykker af Skibet. Og saaledes skete det, at alle bleve reddede i Land.