< Matendo 26 >
1 Ndipo Agripa akamwambia Paulo, “Unayo ruhusa kujitetea.” Hivyo Paulo akawaashiria kwa mkono wake, akaanza kujitetea, akasema:
Linu Agiripa chawamba kwa Paulusi, “Uwola kuli wambilila.” Lyahanu Paulusi cha wotolola iyanza lyakwe nikuli sileleza.
2 “Mfalme Agripa, najiona kuwa na heri kusimama mbele yako leo ninapojitetea kuhusu mashtaka yote ya Wayahudi,
“Nilizuwa kuti nilukuluhite Mulena Agiripa, kutenda indava yangu havusu vwako sunu hewulu lyazintu zonse zivava nihambilizi ma Juda;
3 hasa kwa sababu unajua vyema desturi zote za Kiyahudi na ya kuwa wewe unajua kwa undani mila na masuala ya mabishano. Kwa hiyo, nakusihi unisikilize kwa uvumilivu.
sihulu, kakuli wichaziva wechizo cha ma Juda ni mpuzo. Linu ni kumbila kuti unizuwe chentokomelo.
4 “Wayahudi wote wanajua jinsi nilivyoishi tangu nilipokuwa mtoto, kuanzia mwanzo wa maisha yangu katika nchi yangu na pia huko Yerusalemu.
Cheniti, ma Juda vonse vezi muniva halili kuzwa kuvuhwile vwangu mwi nkanda yangu ni mwa Jerusalema.
5 Wao wamefahamu kwa muda mrefu na wanaweza kushuhudia kama wakipenda, ya kwamba kutokana na misimamo mikali sana ya dhehebu letu kwenye dini yetu, niliishi nikiwa Farisayo.
Vavanizi kuzwa kuma tangilo vawola kuzumina kuti nivahali neli ni mu Falisi, yavali wachiyemba ahulu cha chilumeli chetu.
6 Nami sasa ni kwa sababu ya tumaini langu katika kile ambacho Mungu aliwaahidi baba zetu, ninashtakiwa leo.
Lyahanu nizimana hanu kuti ni atulwe kakuli ni lolete che nsepiso yaba tendi Ireeza ku veshetu.
7 Hii ndiyo ahadi ambayo makabila yetu kumi na mawili yanatarajia kuiona ikitimizwa wanapomtumikia Mungu kwa bidii usiku na mchana. Ee mfalme, ninashtakiwa na Wayahudi kwa ajili ya tumaini hili.
Cheyi insepiso masika etu ekumi ni tobele vava lisepise kutambula niva kwatilile kulumbeka Ireeza masiku ni musihali. Nji cheyi insepo, Simwine mukando Agiripa, Juda chingi ivanihambiliza.
8 Kwa nini yeyote miongoni mwenu afikiri kwamba ni jambo lisilosadikika Mungu kufufua wafu?
Chinzi zumwi kwenu hazeza kuti kulotu kuti Ireeza uvusa vafu.
9 “Mimi pia nilikuwa nimeshawishika kwamba imenipasa kufanya yote yale yaliyowezekana kupinga Jina la Yesu wa Nazareti.
Ka imwi inako nivazezi kuti niswanela kutenda zintu zingi zilwisanisa izina lya Jesu wa Nazareta.
10 Nami hayo ndiyo niliyoyafanya huko Yerusalemu. Kwa mamlaka ya viongozi wa makuhani, niliwatia wengi wa watakatifu gerezani na walipokuwa wakiuawa, nilipiga kura yangu kuunga mkono.
Niva tendi izi mwa Jerusalema. Niva sumini valumeli vangi mwi ntolongo cha maata aniva wani ku mupurisita mukulwana, have haiwa, nivali kuvika inketisa zangu h havo.
11 Mara nyingi nilikwenda kutoka sinagogi moja hadi ingine nikiamuru waadhibiwe, nami nilijaribu kuwalazimisha wakufuru. Katika shauku yangu dhidi yao, hata nilikwenda miji ya kigeni ili kuwatesa.
Niva kuvaha inkoto mwi nako zingi mu ma Sinagoge ni kulika kuva hambiliza kuti vanyanse. Nivava vengeli ahulu nikuva nyandisa nanga mu muleneñi muvasazwi.
12 “Siku moja nilipokuwa katika mojawapo ya safari hizi nikiwa ninakwenda Dameski, nilikuwa na mamlaka na agizo kutoka kwa kiongozi wa makuhani.
Anivali kupanga ichi, nivayendi kwa Damaseka ni maata ni ntaelo zizwa kumu purisita mukulwana;
13 Ilikuwa yapata adhuhuri, ee mfalme, nilipokuwa njiani, niliona nuru kutoka mbinguni kali kuliko jua, ikingʼaa kunizunguka pande zote mimi na wale niliokuwa pamoja nao.
linu mwi nzila, musihali, Simwine mukulwana, nivavoni iseli livakuzwa mwiwulu liva kuvenya kuhita izuva imi livatondezi kwetu niva kwame vani va kuyenda navo.
14 Wote tulipokuwa tumeanguka chini, nikasikia sauti ikisema nami kwa lugha ya Kiebrania, ‘Sauli, Sauli, mbona unanitesa? Ni vigumu kwako kuupiga teke mchokoo.’
Twense hatuwila hansi, niva zuwi inzwi liwamba kwangu mumushovo we chi Heveru, 'Saule, Saule, chinzi honi nyandisa? Ku kukutu kwako ku raha muso.
15 “Nikauliza, ‘Ni nani wewe, Bwana?’ “Naye Bwana akajibu, ‘Ni Mimi Yesu unayemtesa.
China wamba kuti njewe ni, Simwine? Simwine chetava, njeme Jesu yo nyandisa.
16 Sasa inuka usimame kwa miguu yako. Nimekutokea ili nikuteue uwe mtumishi na shahidi wa mambo ambayo umeyaona, na yale nitakayokuonyesha.
Linu vuke uzimane cha matende ako; nji cheli ivaka haniva voneki kwako, kuketa iwe kuva umuhikana ni mpaki kuamana ni zintu ziwizi zangu hanu nizintu zete ni kutondeze chitwe kalakala;
17 Nitakuokoa kutoka kwa watu wako na watu wa Mataifa ambao ninakutuma kwao,
imi kani kulamulele kuvantu ni ku machava kuni kutuma,
18 uyafumbue macho yao ili wageuke kutoka gizani waingie nuruni, na kutoka kwenye nguvu za Shetani wamgeukie Mungu, ili wapate msamaha wa dhambi na sehemu miongoni mwa wale waliotakaswa kwa kuniamini mimi.’
kwiyalula menso avo kuazwisa mwififi ni kuatwala mwi seli ni ku ziho za Satani kwa Ireeza, njikuti vatambule kwa Ireeza maiswalelo ezivi zavo nikuyola zete nivahe ni kuli kauhanya kwangu che ntumelo ina kwangu.
19 “Hivyo basi, Mfalme Agripa, sikuacha kuyatii yale maono yaliyotoka mbinguni,
Chikwina vulyo, Simwine mukando Agiripa, kena navikila kwimbali chivono chewulu;
20 bali niliyatangaza kwanza kwa wale wa Dameski, kisha Yerusalemu na katika vijiji vyote vya Uyahudi na pia kwa watu wa Mataifa, kwamba inawapasa kutubu na kumgeukia Mungu na kuthibitisha toba yao kwa matendo yao.
kono kwavo vena mwa damaseka che ntanzi, navana vena kwa Jereusalema, ni nkanda yonse ya Judea, ni kumachava, niva kutazi kuti vavakile zivi zavo vavole kwa Ireeza, kuvonisa mitendo ivonisa kuvaka kwavo.
21 Ni kwa sababu hii Wayahudi walinikamata nilipokuwa Hekaluni, wakataka kuniua.
Cheli ivaka ma Juda vava nisumini niku lika kuni haya.
22 Hadi leo nimepata msaada kutoka kwa Mungu, na hivyo nasimama hapa nikishuhudia kwa wakubwa na wadogo. Sisemi chochote zaidi ya yale ambayo manabii na Mose walisema yatatukia:
Ireeza avanitusi kusika hanu, cwale niziima nikuha vupaki kuvantu feela niku va tompeha nizimwi zihita zivawambwa kuma porofita ni Mushe kuti muzipangahale;
23 kwamba Kristo atateswa, na kwamba yeye atakuwa wa kwanza kufufuka kutoka kwa wafu, na atatangaza nuru kwa watu wake na kwa watu wa Mataifa.”
kuti keresite uswanela kunyanda, ni kuta kuti mwave we ntanzi kukuvuka kuvafu niku zimana kupaka iseli kuma Juda ni machava.
24 Paulo alipokuwa akifanya utetezi huu, Festo akasema kwa sauti kubwa, “Paulo, wewe umerukwa na akili! Kusoma kwingi kunakufanya uwe kichaa!”
Paulusi hamana kuli lamulela, fesitusi chawamba chenzwi li katukite, “Paulusi, uvurumuka; intuto yako inkando iku vulumuna.”
25 Lakini Paulo akajibu, “Mimi sijarukwa na akili, mtukufu sana Festo, bali nanena kweli nikiwa na akili zangu timamu.
Kono Paulusi chati, kani vurumuki, hande ahulu Fesitusi; kono cho vundume niwamba manzwi ovusakusima ninisa nywine.
26 Naam, Mfalme anajua kuhusu mambo haya yote, nami nasema naye kwa uhuru. Kwa sababu nina hakika kwamba hakuna hata mojawapo ya mambo haya asilolijua, kwa kuwa hayakufanyika mafichoni.
Kakuli Simwine mukando wizi izi zintu; njikuti, niwamba kwali nini lukuluhite, kakuli ni susuweze kuti kakwina zi patitwe kwali; mukuti izi kena ziva pangilwa kuliungwiile.
27 Mfalme Agripa, je, unaamini manabii? Najua kuwa unaamini.”
Uzumina kuvaporofita, Mulena Agiripa? Nizi kuti uzumina.”
28 Agripa akamwambia Paulo, “Je, unanishawishi kwa haraka namna hii niwe Mkristo?”
Agiripa chawamba kwa Paulusi, “Mu nako infuhi moni susuweze nive ni mulumeli?”
29 Paulo akasema, “Ikiwa ni kwa haraka au la, namwomba Mungu, si wewe peke yako bali pia wale wote wanaonisikiliza leo, wawe kama mimi nilivyo, kasoro minyororo hii.”
Paulusi chati, “Ni lapela kwa Ireeza, kuti kapa munfuhi kapa inde inako, insiñi iwe wenke, kono nivonse vanizuwa sunu, muvave uvu njeme, kono nikusena anu mahaka entorongo.”
30 Baada ya kusema hayo, mfalme akainuka pamoja na mtawala na Bernike na wale waliokuwa wameketi pamoja nao.
Linu Mulena chazima mwiwulu, ni muyendisi, ni Bernise naye, ni vonse vavekele naavo;
31 Walipokuwa wakiondoka, wakaambiana, “Mtu huyu hafanyi jambo lolote linalostahili kufa au kufungwa.”
lyahanu hava siya uwo muyaho, vavawambi hamwina nikuti, “Uzu mukwame kakwina zavapangi ziswanela lufu ni ku suminwa.”
32 Agripa akamwambia Festo, “Mtu huyu angeachwa huru kama hangekuwa amekata rufaa kwa Kaisari.”
Agiripa cha wambila Fesitusi, “Uzu mukwame ava kuwola kulukululwa kambe kena ava likumbili kwa Sizare.”