< Matendo 26 >

1 Ndipo Agripa akamwambia Paulo, “Unayo ruhusa kujitetea.” Hivyo Paulo akawaashiria kwa mkono wake, akaanza kujitetea, akasema:
And Agrippa seide to Poul, It is suffrid to thee, to speke for thi silf. Thanne Poul helde forth the hoond, and bigan to yelde resoun.
2 “Mfalme Agripa, najiona kuwa na heri kusimama mbele yako leo ninapojitetea kuhusu mashtaka yote ya Wayahudi,
Of alle thingis, in whiche Y am accusid of the Jewis, thou king Agrippa, Y gesse me blessid at thee, whanne Y schal defende me this dai;
3 hasa kwa sababu unajua vyema desturi zote za Kiyahudi na ya kuwa wewe unajua kwa undani mila na masuala ya mabishano. Kwa hiyo, nakusihi unisikilize kwa uvumilivu.
moost for thou knowist alle thingis that ben among Jewis, customes and questiouns. For which thing, Y biseche, here me pacientli.
4 “Wayahudi wote wanajua jinsi nilivyoishi tangu nilipokuwa mtoto, kuanzia mwanzo wa maisha yangu katika nchi yangu na pia huko Yerusalemu.
For alle Jewis that bifor knewen me fro the bigynnyng, knewen my lijf fro yongthe; that fro the bigynnyng was in my folc in Jerusalem,
5 Wao wamefahamu kwa muda mrefu na wanaweza kushuhudia kama wakipenda, ya kwamba kutokana na misimamo mikali sana ya dhehebu letu kwenye dini yetu, niliishi nikiwa Farisayo.
if thei wolen bere witnessing, that bi the moost certeyn sect of oure religioun, Y lyuede a Farisee.
6 Nami sasa ni kwa sababu ya tumaini langu katika kile ambacho Mungu aliwaahidi baba zetu, ninashtakiwa leo.
And now for the hope of repromyssioun, that is maad to oure fadris of God, Y stonde suget in dom;
7 Hii ndiyo ahadi ambayo makabila yetu kumi na mawili yanatarajia kuiona ikitimizwa wanapomtumikia Mungu kwa bidii usiku na mchana. Ee mfalme, ninashtakiwa na Wayahudi kwa ajili ya tumaini hili.
in which hope oure twelue lynagis seruynge niyt and dai hopen to come; of which hope, sir king, Y am accusid of the Jewis.
8 Kwa nini yeyote miongoni mwenu afikiri kwamba ni jambo lisilosadikika Mungu kufufua wafu?
What vnbileueful thing is demed at you, if God reisith deed men?
9 “Mimi pia nilikuwa nimeshawishika kwamba imenipasa kufanya yote yale yaliyowezekana kupinga Jina la Yesu wa Nazareti.
And sotheli Y gesside, that Y ouyte do many contrarie thingis ayens the name of Jhesu Nazarene.
10 Nami hayo ndiyo niliyoyafanya huko Yerusalemu. Kwa mamlaka ya viongozi wa makuhani, niliwatia wengi wa watakatifu gerezani na walipokuwa wakiuawa, nilipiga kura yangu kuunga mkono.
Which thing also Y dide in Jerusalem, and Y encloside manye of the seyntis in prisoun, whanne Y hadde take powere of the princis of preestis. And whanne thei weren slayn, Y brouyte the sentence.
11 Mara nyingi nilikwenda kutoka sinagogi moja hadi ingine nikiamuru waadhibiwe, nami nilijaribu kuwalazimisha wakufuru. Katika shauku yangu dhidi yao, hata nilikwenda miji ya kigeni ili kuwatesa.
And bi alle synagogis ofte Y punyschide hem, and constreynede to blasfeme; and more Y wex wood ayens hem, and pursuede in to alien citees.
12 “Siku moja nilipokuwa katika mojawapo ya safari hizi nikiwa ninakwenda Dameski, nilikuwa na mamlaka na agizo kutoka kwa kiongozi wa makuhani.
In whiche, the while Y wente to Damask, with power and suffring of princis of preestis,
13 Ilikuwa yapata adhuhuri, ee mfalme, nilipokuwa njiani, niliona nuru kutoka mbinguni kali kuliko jua, ikingʼaa kunizunguka pande zote mimi na wale niliokuwa pamoja nao.
at myddai, in the weie Y say, sir king, that fro heuene liyt schynede aboute me, passing the schynyng of the sunne, and aboute hem that weren togidir with me.
14 Wote tulipokuwa tumeanguka chini, nikasikia sauti ikisema nami kwa lugha ya Kiebrania, ‘Sauli, Sauli, mbona unanitesa? Ni vigumu kwako kuupiga teke mchokoo.’
And whanne we alle hadden falle doun in to the erthe, Y herde a vois seiynge to me in Ebrew tunge, Saul, Saul, what pursuest thou me? it is hard to thee, to kicke ayens the pricke.
15 “Nikauliza, ‘Ni nani wewe, Bwana?’ “Naye Bwana akajibu, ‘Ni Mimi Yesu unayemtesa.
And Y seide, Who art thou, Lord? And the Lord seide, Y am Jhesus, whom thou pursuest.
16 Sasa inuka usimame kwa miguu yako. Nimekutokea ili nikuteue uwe mtumishi na shahidi wa mambo ambayo umeyaona, na yale nitakayokuonyesha.
But rise vp, and stoond on thi feet. For whi to this thing Y apperide to thee, that Y ordeyne thee mynystre and witnesse of tho thingis that thou hast seyn, and of tho in whiche Y schal schewe to thee.
17 Nitakuokoa kutoka kwa watu wako na watu wa Mataifa ambao ninakutuma kwao,
And Y schal delyuere thee fro puplis and folkis, to whiche now Y sende thee,
18 uyafumbue macho yao ili wageuke kutoka gizani waingie nuruni, na kutoka kwenye nguvu za Shetani wamgeukie Mungu, ili wapate msamaha wa dhambi na sehemu miongoni mwa wale waliotakaswa kwa kuniamini mimi.’
to opene the iyen of hem, that thei ben conuertid fro derknesse to liyt, and fro power of Sathnas to God, that thei take remyssioun of synnes, and part among seyntis, bi feith that is in me.
19 “Hivyo basi, Mfalme Agripa, sikuacha kuyatii yale maono yaliyotoka mbinguni,
Wherfor, sir kyng Agrippa, Y was not vnbileueful to the heuenli visioun;
20 bali niliyatangaza kwanza kwa wale wa Dameski, kisha Yerusalemu na katika vijiji vyote vya Uyahudi na pia kwa watu wa Mataifa, kwamba inawapasa kutubu na kumgeukia Mungu na kuthibitisha toba yao kwa matendo yao.
but Y tolde to hem that been at Damask first, and at Jerusalem, and bi al the cuntre of Judee, and to hethene men, that thei schulden do penaunce, and be conuertid to God, and do worthi werkis of penaunce.
21 Ni kwa sababu hii Wayahudi walinikamata nilipokuwa Hekaluni, wakataka kuniua.
For this cause Jewis token me, whanne Y was in the temple, to sle me.
22 Hadi leo nimepata msaada kutoka kwa Mungu, na hivyo nasimama hapa nikishuhudia kwa wakubwa na wadogo. Sisemi chochote zaidi ya yale ambayo manabii na Mose walisema yatatukia:
But Y was holpun bi the helpe of God in to this dai, and stonde, witnessinge to lesse and to more. And Y seye no thing ellis than whiche thingis the prophetis and Moises spaken that schulen come,
23 kwamba Kristo atateswa, na kwamba yeye atakuwa wa kwanza kufufuka kutoka kwa wafu, na atatangaza nuru kwa watu wake na kwa watu wa Mataifa.”
if Crist is to suffre, if he is the firste of the ayenrising of deed men, that schal schewe liyt to the puple and to hethene men.
24 Paulo alipokuwa akifanya utetezi huu, Festo akasema kwa sauti kubwa, “Paulo, wewe umerukwa na akili! Kusoma kwingi kunakufanya uwe kichaa!”
Whanne he spak these thingis, and yeldide resoun, Festus seide with greet vois, Poul, thou maddist; many lettris turnen thee to woodnesse.
25 Lakini Paulo akajibu, “Mimi sijarukwa na akili, mtukufu sana Festo, bali nanena kweli nikiwa na akili zangu timamu.
And Poul seide, Y madde not, thou beste Festus, but Y speke out the wordis of treuthe and of sobernesse.
26 Naam, Mfalme anajua kuhusu mambo haya yote, nami nasema naye kwa uhuru. Kwa sababu nina hakika kwamba hakuna hata mojawapo ya mambo haya asilolijua, kwa kuwa hayakufanyika mafichoni.
For also the king, to whom Y speke stidfastli, woot of these thingis; for Y deme, that no thing of these is hid fro hym; for nether in a cornere was ouyt of these thingis don.
27 Mfalme Agripa, je, unaamini manabii? Najua kuwa unaamini.”
Bileuest thou, king Agrippa, `to prophetis? Y woot that thou bileuest.
28 Agripa akamwambia Paulo, “Je, unanishawishi kwa haraka namna hii niwe Mkristo?”
And Agrippa seide to Poul, In litil thing thou counseilist me to be maad a cristen man.
29 Paulo akasema, “Ikiwa ni kwa haraka au la, namwomba Mungu, si wewe peke yako bali pia wale wote wanaonisikiliza leo, wawe kama mimi nilivyo, kasoro minyororo hii.”
And Poul seide, Y desire anentis God, bothe in litil and in greet, not oneli thee, but alle these that heren to dai, to be maad sich as Y am, outakun these boondis.
30 Baada ya kusema hayo, mfalme akainuka pamoja na mtawala na Bernike na wale waliokuwa wameketi pamoja nao.
And the kyng roos vp, and the president, and Beronyce, and thei that saten niy to hem.
31 Walipokuwa wakiondoka, wakaambiana, “Mtu huyu hafanyi jambo lolote linalostahili kufa au kufungwa.”
And whanne thei wenten awei, thei spaken togider, and seiden, That this man hath not don ony thing worthi deth, nether boondis.
32 Agripa akamwambia Festo, “Mtu huyu angeachwa huru kama hangekuwa amekata rufaa kwa Kaisari.”
And Agrippa seide to Festus, This man miyt be delyuerid, if he hadde not appelid to the emperour.

< Matendo 26 >