< Matendo 24 >
1 Baada ya siku tano, kuhani mkuu Anania akashuka akiwa amefuatana na baadhi ya wazee pamoja na mwanasheria mmoja aitwaye Tertulo, nao wakaleta mashtaka yao dhidi ya Paulo mbele ya mtawala.
Po pěti pak dnech sstoupil nejvyšší kněz Ananiáš s staršími a s nějakým Tertullem řečníkem. Kteříž postavili se před vládařem proti Pavlovi.
2 Paulo alipoitwa aingie ndani, Tertulo akaanza kutoa mashtaka akisema, “Mtukufu Feliksi, kwa muda mrefu tumefurahia amani na matengenezo mengi mazuri yamefanywa kwa ajili ya watu hawa kwa sababu ya upeo wako wa kuona mambo ya mbele.
A když povolán byl, počal žalovati Tertullus, řka:
3 Wakati wote na kila mahali, kwa namna yoyote, mtukufu sana Feliksi, tumeyapokea mambo haya yote kwa shukrani nyingi.
Kterak mnohý pokoj způsoben jest nám skrze tebe, a mnohé věci v tomto národu výborně se dějí skrze tvou opatrnost, to my i všelijak i všudy se vším děkováním vyznáváme, výborný Felix.
4 Lakini nisije nikakuchosha zaidi, ningekuomba kwa hisani yako utusikilize kwa kifupi.
Ale abych tě déle nezaměstknával, prosím, vyslyšiž nás maličko podlé obyčeje přívětivosti své.
5 “Tumemwona mtu huyu kuwa ni msumbufu, anayechochea ghasia miongoni mwa Wayahudi duniani pote. Yeye ndiye kiongozi wa dhehebu la Wanazarayo,
Nalezli jsme zajisté muže tohoto nešlechetného, a vzbuzujícího různice mezi všemi Židy po všem světě, a vůdci té sekty Nazaretské.
6 na hata amejaribu kulinajisi Hekalu, hivyo tukamkamata; [tukataka kumhukumu kufuatana na sheria zetu.
Kterýž také i o to se pokoušel, aby chrámu poškvrnil; a kteréhož javše, vedlé zákona svého chtěli jsme souditi.
7 Lakini jemadari Lisia alitujia na nguvu nyingi, akamwondoa mikononi mwetu,
Ale přišed hejtman Lyziáš s mocí velikou, vzal ho z rukou našich,
8 akiwaamuru washtaki wake waje mbele yako: ili] kwa kumchunguza wewe mwenyewe unaweza kujua kutoka kwake mambo yote tunayomshtaki kwayo.”
Rozkázav, aby žalobníci jeho šli k tobě. Od něhož ty sám budeš moci, vyptaje se, zvěděti o tom o všem, z čeho my jej viníme.
9 Pia wale Wayahudi wakaunga mkono wakithibitisha kuwa mashtaka yote haya ni kweli.
A k tomu se přimluvili i Židé, pravíce, že to tak jest.
10 Mtawala Feliksi alipompungia Paulo mkono ili ajitetee, yeye akajibu, “Najua kwamba wewe umekuwa hakimu katika taifa hili kwa miaka mingi, hivyo natoa utetezi wangu kwa furaha.
Tedy Pavel odpověděl, když mu návěští dal vládař, aby mluvil: Od mnohých let věda tebe býti soudcím národu tomuto představeným, s lepší myslí k tomu, což se mne dotýče, odpovídati budu,
11 Unaweza kuhakikisha kwa urahisi kuwa hazijapita zaidi ya siku kumi na mbili tangu nilipopanda kwenda Yerusalemu kuabudu.
Poněvadž ty můžeš to věděti, že není tomu dní více než dvanácte, jakž jsem přišel do Jeruzaléma, abych se modlil.
12 Hawa wanaonishtaki hawakunikuta nikibishana na mtu yeyote Hekaluni au kuchochea umati wa watu katika sinagogi au mahali pengine popote mjini.
A aniž mne nalezli v chrámě s někým se hádajícího, aneb činícího roty v zástupu, ani v školách, ani v městě,
13 Wala hawawezi kabisa kukuthibitishia mashtaka haya wanayonishtaki kwayo.
Aniž toho prokázati mohou, což na mne nyní žalují.
14 Lakini, ninakubali kwamba mimi namwabudu Mungu wa baba zetu, mfuasi wa Njia, ile ambayo wao wanaiita dhehebu. Ninaamini kila kitu kinachokubaliana na Sheria na kile kilichoandikwa katika Manabii,
Ale totoť před tebou vyznávám, že podlé té cesty, kterouž nazývají kacířstvím, tak sloužím Bohu otců, věře všemu, cožkoli psáno jest v zákoně a v prorocích,
15 nami ninalo tumaini kwa Mungu, ambalo hata wao wenyewe wanalikubali kwamba kutakuwa na ufufuo wa wafu, kwa wenye haki na wasio na haki.
Maje naději v Bohu, že bude, jehož i oni čekají, vzkříšení z mrtvých, i spravedlivých i nespravedlivých.
16 Kwa hiyo ninajitahidi siku zote kuwa na dhamiri safi mbele za Mungu na mbele za wanadamu.
Sám pak o to pracuji, abych měl svědomí bez úrazu před Bohem i před lidmi vždycky.
17 “Basi, baada ya kutokuwepo kwa miaka mingi nilikuja Yerusalemu ili kuwaletea watu wangu msaada kwa ajili ya maskini na kutoa dhabihu.
Po mnohých pak letech přišel jsem, almužny nesa národu svému a oběti.
18 Nilikuwa nimeshatakaswa kwa taratibu za kiibada waliponikuta Hekaluni nikifanya mambo haya. Hapakuwa na umati wa watu, pamoja nami wala aliyehusika kwenye fujo yoyote.
Při čemž mne nalezli v chrámě očištěného, ne s zástupem, ani s bouřkou, někteří Židé z Azie,
19 Lakini kulikuwa na baadhi ya Wayahudi kutoka Asia, ambao wangelazimika wawepo hapa mbele yako ili watoe mashtaka kama wanalo jambo lolote dhidi yangu.
Kteříž by měli tuto také před tebou státi a žalovati, měli-li by co proti mně.
20 Au, watu hawa walioko hapa waseme ni uhalifu gani walioniona nao waliponisimamisha mbele ya baraza,
Aneb nechať tito sami povědí, nalezli-li na mně jakou nepravost, když jsem stál v radě.
21 isipokuwa ni kuhusu jambo hili moja nililopiga kelele mbele yao kwamba, ‘Mimi nashtakiwa mbele yenu leo kwa sababu ya ufufuo wa wafu.’”
Leč to jedno promluvení, že jsem zavolal, stoje mezi nimi: Pro vzkříšení z mrtvých já k soudu potažen jsem dnes od vás.
22 Basi Feliksi ambaye alikuwa anafahamu vizuri habari za Njia ile, akaahirisha shauri lile kwa maelezo yake akisema, “Wakati jemadari Lisia atakapoteremka huku, nitaamua shauri lako.”
A vyslyšav to Felix, odložil jim, řka: Až bych o té cestě něco místnějšího vyzvěděl, když hejtman Lyziáš sem přijede, posoudím té pře vaší.
23 Ndipo akaamuru kiongozi wa askari amweke chini ya ulinzi lakini ampe uhuru na kuwaruhusu rafiki zake wamhudumie.
I poručil setníkovi, aby Pavla ostříhal, a polehčil mu, a nebránil žádnému z přátel jeho posluhovati jemu aneb navštěvovati ho.
24 Baada ya siku kadhaa, Feliksi alikuja pamoja na Drusila mkewe, ambaye alikuwa Myahudi. Alituma aitiwe Paulo, naye akamsikiliza alipokuwa akinena juu ya imani katika Kristo Yesu.
Po několika pak dnech přišed Felix s Druzillou, manželkou svou, kteráž byla Židovka, zavolal Pavla, a slyšel od něho o víře v Krista.
25 Naye Paulo alipokuwa akinena juu ya haki, kuwa na kiasi na juu ya hukumu ijayo, Feliksi aliingiwa na hofu na kusema, “Hiyo yatosha sasa! Waweza kuondoka. Nitakapokuwa na wasaa nitakuita.”
A když on vypravoval o spravedlnosti a o zdrželivosti a o budoucím soudu, ulekl se Felix, a odpověděl: Nyní odejdi, a v čas příhodný povolám tě.
26 Wakati huo Feliksi alitazamia kwamba Paulo angempa rushwa. Hivyo akawa anamwita mara kwa mara na kuzungumza naye.
Přitom pak nadál se, že jemu Pavel dá peníze, aby jej propustil, pročež i tím častěji, povolávaje ho, mluvíval s ním.
27 Baada ya miaka miwili kupita, Porkio Festo akaingia kwenye utawala mahali pa Feliksi, lakini kwa kuwa Feliksi alitaka kuwapendeza Wayahudi, akamwacha Paulo gerezani.
Po dvou pak letech měl po sobě náměstka Felix Porcia Festa, a chtěje se zalíbiti Židům Felix, nechal Pavla v vězení.