< Matendo 22 >
1 “Ndugu zangu na baba zangu, sikilizeni utetezi wangu.”
« Mes frères et mes pères, écoutez ce que j’ai maintenant à vous dire pour ma défense. » —
2 Waliposikia akisema kwa lugha ya Kiebrania, wakanyamaza kimya kabisa. Ndipo Paulo akasema,
Dès qu’ils entendirent qu’il leur parlait en langue hébraïque, ils firent encore plus de silence.
3 “Mimi ni Myahudi, niliyezaliwa Tarso huko Kilikia, lakini nimelelewa katika mji huu. Miguuni mwa Gamalieli, nilifundishwa kikamilifu katika sheria ya baba zetu, na nikawa mwenye juhudi kwa ajili ya Mungu kama kila mmoja wenu alivyo leo.
Et Paul dit: « Je suis Juif, né à Tarse en Cilicie; mais j’ai été élevé dans cette ville et instruit aux pieds de Gamaliel dans la connaissance exacte de la Loi de nos pères, étant plein de zèle pour Dieu, comme vous l’êtes tous aujourd’hui.
4 Niliwatesa watu wa Njia hii hadi kufa, nikiwakamata waume kwa wake na kuwatupa gerezani,
C’est moi qui ai persécuté cette secte jusqu’à la mort, chargeant de chaînes et jetant en prison hommes et femmes:
5 kama kuhani mkuu na baraza zima la wazee wanavyoweza kushuhudia kunihusu. Hata nilipokea barua kutoka kwao kwenda kwa ndugu wale wa Dameski, nami nikaenda huko ili kuwaleta watu hawa Yerusalemu kama wafungwa ili waadhibiwe.
le grand-prêtre et tous les Anciens m’en sont témoins. Ayant même reçu d’eux des lettres pour les frères, je partis pour Damas afin d’amener enchaînés à Jérusalem ceux qui se trouvaient là, et de les faire punir.
6 “Nilipokuwa njiani kuelekea Dameski, yapata saa sita mchana, ghafula nuru kubwa kutoka mbinguni ikanimulika kotekote.
Mais comme j’étais en chemin, et déjà près de Damas, tout à coup, vers midi, une vive lumière venant du ciel resplendit autour de moi.
7 Nikaanguka chini, nikasikia sauti ikiniambia, ‘Sauli, Sauli! Mbona unanitesa?’
Je tombai par terre, et j’entendis une voix qui me disait: Saul, Saul, pourquoi me persécutes-tu?
8 “Nikajibu, ‘Wewe ni nani Bwana?’ “Naye akaniambia, ‘Mimi ni Yesu wa Nazareti unayemtesa.’
Je répondis: Qui êtes-vous, Seigneur? Et il me dit: Je suis Jésus de Nazareth, que tu persécutes.
9 Basi wale watu waliokuwa pamoja nami waliiona ile nuru, lakini hawakuisikia sauti ya yule aliyekuwa akisema nami.
Ceux qui étaient avec moi virent bien la lumière, mais ils n’entendirent pas la voix de celui qui me parlait.
10 “Nikauliza, ‘Nifanye nini Bwana?’ “Naye Bwana akaniambia, ‘Inuka uingie Dameski, huko utaambiwa yote yakupasayo kufanya.’
Alors je dis: Que dois-je faire, Seigneur? Et le Seigneur me répondit: Lève-toi, va à Damas, et là on te dira tout ce que tu dois faire.
11 Kwa kuwa nilikuwa siwezi kuona kwa ajili ya mngʼao wa ile nuru, wenzangu wakanishika mkono wakaniongoza kuingia Dameski.
Et comme par suite de l’éclat de cette lumière je ne voyais plus, ceux qui étaient avec moi me prirent par la main, et j’arrivai à Damas.
12 “Mtu mmoja mcha Mungu, jina lake Anania, alikuja kuniona. Alizishika sana sheria zetu, na aliheshimiwa sana na Wayahudi waliokuwa wakiishi huko Dameski.
Or un homme pieux selon la Loi, nommé Ananie, et de qui tous les Juifs de la ville rendaient un bon témoignage,
13 Akasimama karibu nami, akasema, ‘Ndugu Sauli, pata kuona tena!’ Saa ile ile nikapata kuona tena, nami nikaweza kumwona.
vint me voir, et s’étant approché de moi, me dit: Saul, mon frère, recouvre la vue. Et au même instant je le vis.
14 “Akasema, ‘Mungu wa baba zetu amekuchagua wewe ili ujue mapenzi yake, umwone yeye Aliye Mwenye Haki na upate kusikia maneno kutoka kinywani mwake.
Il dit alors: Le Dieu de nos pères t’a prédestiné à connaître sa volonté, à voir le Juste et entendre les paroles de sa bouche.
15 Kwa kuwa utakuwa shahidi wake kwa watu kuhusu kile ulichokiona na kukisikia.
Car tu lui serviras de témoin, devant tous les hommes, des choses que tu as vues et entendues.
16 Sasa basi, mbona unakawia? Inuka, ukabatizwe na dhambi zako zikasafishwe, ukiliita Jina lake.’
Et maintenant que tardes-tu? Lève-toi, reçois le baptême et purifie-toi de tes péchés, en invoquant son nom. —
17 “Baada ya kurudi Yerusalemu, nilipokuwa ninaomba Hekaluni, nilipitiwa na usingizi wa ghafula
De retour à Jérusalem, comme je priais dans le temple, il m’arriva d’être ravi en esprit,
18 nikamwona Bwana akiniambia, ‘Harakisha utoke Yerusalemu upesi, maana hawataukubali ushuhuda wako kunihusu mimi.’
et je vis le Seigneur qui me disait: Hâte-toi et sors au plus tôt de Jérusalem, parce qu’on n’y recevra pas le témoignage que tu rendras de moi. —
19 “Nami nikasema, ‘Bwana, wao wenyewe wanajua jinsi nilivyokwenda kwenye kila sinagogi ili kuwatupa gerezani na kuwapiga wale waliokuamini.
Seigneur, répondis-je, ils savent eux-mêmes que je faisais mettre en prison et battre de verges dans les synagogues ceux qui croyaient en vous,
20 Wakati damu ya shahidi wako Stefano ilipomwagwa, mimi mwenyewe nilikuwa nimesimama kando, nikikubaliana na kitendo hicho na kutunza mavazi ya wale waliomuua.’
et lorsqu’on répandit le sang d’Étienne, votre témoin, j’étais moi-même présent, joignant mon approbation à celle des autres et gardant les vêtements de ceux qui le lapidaient.
21 “Ndipo Bwana akaniambia, ‘Nenda, kwa maana nitakutuma mbali, kwa watu wa Mataifa.’”
Alors il me dit: Va, c’est aux nations lointaines que je veux t’envoyer. »
22 Ule umati wa watu wakamsikiliza Paulo mpaka aliposema neno hilo, ndipo wakapaza sauti zao na kupiga kelele wakisema, “Mwondoeni duniani, hafai kuishi!”
Les Juifs l’avaient écouté jusqu’à ces mots; ils élevèrent alors la voix, en disant: « Ote de la terre un pareil homme; il n’est pas digne de vivre. »
23 Walipokuwa wakipiga kelele na kutoa mavazi yao huku wakirusha mavumbi juu hewani,
Et comme ils poussaient de grands cris, jetant leurs manteaux et lançant de la poussière en l’air,
24 yule jemadari akaamuru Paulo aingizwe kwenye ngome. Akaelekeza kwamba achapwe viboko na aulizwe ili kujua kwa nini watu walikuwa wanampigia kelele namna hiyo.
le tribun ordonna de faire entrer Paul dans la forteresse et de lui donner la question par le fouet, afin de savoir pour quel motif ils criaient ainsi contre lui.
25 Lakini walipokwisha kumfunga kwa kamba za ngozi ili wamchape viboko, Paulo akamwambia kiongozi wa askari aliyekuwa amesimama pale karibu naye, “Je, ni halali kwenu kwa mujibu wa sheria kumchapa mtu ambaye ni raiya wa Rumi hata kabla hajapatikana na hatia?”
Déjà les soldats l’avaient lié avec les courroies, lorsque Paul dit au centurion qui était là: « Vous est-il permis de flageller un citoyen romain, qui n’est pas même condamné? »
26 Yule kiongozi aliposikia maneno haya, alimwendea yule jemadari na kumwambia, “Unataka kufanya nini? Kwa maana huyu mtu ni raiya wa Rumi.”
À ces mots, le centurion alla trouver le tribun pour l’avertir, et lui dit: « Que vas-tu faire? Cet homme est citoyen romain. »
27 Yule jemadari akaja akamuuliza Paulo, “Niambie, wewe ni raiya wa Rumi?” Paulo akajibu, “Naam, hakika ndiyo.”
Le tribun vint et dit à Paul: « Dis-moi, es-tu citoyen romain? » « Oui, » répondit-il;
28 Ndipo yule jemadari akasema, “Mimi ilinigharimu kiasi kikubwa cha fedha kupata uraia wangu.” Paulo akasema “Lakini mimi ni raiya wa Rumi kwa kuzaliwa.”
et le tribun repris: « Moi, j’ai acheté bien cher ce droit de cité. » — « Et moi, dit Paul, je l’ai par ma naissance. »
29 Mara wale waliokuwa wanataka kumhoji wakajiondoa haraka, naye yule jemadari akaingiwa na hofu alipotambua ya kuwa amemfunga Paulo, ambaye ni raia wa Rumi, kwa minyororo.
Aussitôt ceux qui se disposaient à lui donner la question se retirèrent; et le tribun aussi eut peur, quand il sut que Paul était citoyen romain et qu’il l’avait fait lier.
30 Kesho yake, kwa kuwa yule jemadari alitaka kujua hakika kwa nini Paulo alikuwa anashutumiwa na Wayahudi, alimfungua, na akawaagiza viongozi wa makuhani na baraza lote likutane. Kisha akamleta Paulo, akamsimamisha mbele yao.
Le lendemain, voulant savoir exactement de quoi les Juifs l’accusaient, il lui fit ôter ses liens, et donna l’ordre aux princes des prêtres et à tout le Sanhédrin de se réunir; puis, ayant fait descendre Paul, il le plaça au milieu d’eux.