< Matendo 21 >

1 Tulipokwisha kujitenga nao, tukaanza safari kwa njia ya bahari moja kwa moja mpaka Kosi. Siku ya pili yake tukafika Rodo na kutoka huko tukaenda Patara.
When at least we had torn ourselves away, and had set sail, we ran a straight course to Cos, and next day to Rhodes, and from there to Patara.
2 Hapo tukapata meli iliyokuwa inavuka kwenda Foinike tukapanda tukasafiri nayo.
And when we had found a ship bound for Phoenicia, we went aboard and set sail.
3 Tulipokiona kisiwa cha Kipro, tukakizunguka tukakiacha upande wetu wa kushoto, tukasafiri mpaka Shamu, tukatia nanga katika bandari ya Tiro ambapo meli yetu ilikuwa ipakue shehena yake.
After sighting Cyprus and leaving it on the left hand, we sailed for Syria, and put in at Tyre; for there the ship was to unload her cargo.
4 Baada ya kuwatafuta wanafunzi wa huko, tukakaa nao kwa siku saba. Wale wanafunzi wakiongozwa na Roho wakamwambia Paulo asiende Yerusalemu.
We looked up the local disciples and remained there seven days; and these disciples kept telling Paul, through the Spirit, that he should not set foot in Jerusalem.
5 Lakini muda wetu ulipokwisha, tukaondoka tukaendelea na safari yetu. Wale wanafunzi pamoja na wake zao na watoto wakatusindikiza hadi nje ya mji. Wote tukapiga magoti pale pwani tukaomba.
When, however, our time was up, we left and started on our journey; and all of them, with wives and children, were escorting us on our way until we were out of the city; then, kneeling down on the beach, we prayed,
6 Baada ya kuagana, tukapanda melini, nao wakarudi majumbani mwao.
and said good-bye, and went on board the ship, while they returned home again.
7 Tukaendelea na safari yetu toka Tiro tukafika Tolemai, tukawasalimu ndugu wa huko, tukakaa nao kwa siku moja.
And when we had finished the voyage from Tyre, we reached Ptolemais, and greeted the brothers and stayed with them one day.
8 Siku iliyofuata tukaondoka, tukafika Kaisaria. Huko tukaenda nyumbani kwa mwinjilisti mmoja jina lake Filipo, aliyekuwa mmoja wa wale Saba, tukakaa kwake.
On the morrow we started for Caesarea, where we went into the house of Philip, the evangelist, who was one of the seven, and stayed with him.
9 Filipo alikuwa na binti wanne mabikira waliokuwa wanatoa unabii.
Now Philip had four unmarried daughters who prophesied,
10 Baada ya kukaa kwa siku kadhaa, akateremka nabii mmoja kutoka Uyahudi jina lake Agabo.
and while we remained there many days, a prophet named Agabus came down from Judea.
11 Alipotufikia akachukua mshipi wa Paulo akajifunga, akautumia kufunga mikono na miguu yake mwenyewe akasema, “Roho Mtakatifu anasema: ‘Hivi ndivyo Wayahudi wa Yerusalemu watakavyomfunga mwenye mshipi huu na kumkabidhi kwa watu wa Mataifa.’”
He came to us, and taking Paul’s girdle, he bound his own feet and hands, saying, "Thus says the Holy Spirit, ‘so will the Jews at Jerusalem bind the owner of this girdle, and deliver him into the hands of the Gentiles.’"
12 Tuliposikia maneno haya sisi na ndugu wengine tukamsihi Paulo asiende Yerusalemu.
As soon as we heard these words, both we and those who were standing near entreated Paul not to go up to Jerusalem.
13 Lakini Paulo akajibu, “Kwa nini mnalia na kunivunja moyo? Mimi niko tayari si kufungwa tu, bali hata kufa huko Yerusalemu kwa ajili ya jina la Bwana Yesu.”
"What do you mean by thus breaking my heart with your grief?" answered Paul. "For I am ready not to be bound only, but also to die at Jerusalem, for the name of the Lord Jesus."
14 Alipokuwa hashawishiki, tukaacha kumsihi, tukasema, “Mapenzi ya Bwana na yatendeke.”
And when he would not be persuaded, we ceased, saying, "The will of the Lord be done."
15 Baada ya haya, tukajiandaa, tukaondoka kwenda Yerusalemu.
A few days after this we took up our luggage and went up to Jerusalem.
16 Baadhi ya wanafunzi kutoka Kaisaria wakafuatana nasi na kutupeleka nyumbani kwa Mnasoni, ambaye tungekaa kwake. Yeye alikuwa mtu wa Kipro, mmoja wa wanafunzi wa zamani.
And some of the disciples from Caesarea accompanied us. They led us to the house of Mnason, a Cypriote, a disciple of long standing, with whom we were to lodge.
17 Tulipofika Yerusalemu ndugu wakatukaribisha kwa furaha.
At length we reached Jerusalem, and the brothers there received us gladly.
18 Kesho yake Paulo pamoja na wengine wetu tulikwenda kumwona Yakobo, na wazee wote walikuwepo.
On the following day we went with Paul to call on James, and all the elders were present.
19 Baada ya kuwasalimu, Paulo akatoa taarifa kamili ya mambo yote ambayo Mungu alikuwa amefanya miongoni mwa watu wa Mataifa kupitia huduma yake.
After saluting them Paul rehearsed, one by one, the things that God had done among the Gentiles by his ministry.
20 Baada ya kusikia mambo haya wakamwadhimisha Mungu. Ndipo wakamwambia Paulo, “Ndugu, unaona kulivyo na maelfu ya Wayahudi walioamini, nao wote wana juhudi kwa ajili ya sheria.
And they, when they heard it, glorified God, and said to him. "You see, brother, how many thousands there are among the Jews, of those who have believed, and they are all zealous for the Law.
21 Lakini wameambiwa habari zako kwamba unafundisha Wayahudi wote waishio miongoni mwa watu wa Mataifa kumkataa Mose, na kwamba unawaambia wasiwatahiri watoto wao wala kufuata desturi zetu.
"Now what they have been told about you, again and again, is that you teach all the Jews who are among the Gentiles, to forsake Moses, and not to circumcise their children, nor to follow the old customs.
22 Sasa tufanyeje? Bila shaka watasikia kwamba umekuja Yerusalemu.
"What then ought to be done? They will certainly hear that you are come.
23 Kwa hiyo fanya lile tunalokuambia. Tunao watu wanne hapa ambao wameweka nadhiri.
"So do this that we tell you.
24 Jiunge na watu hawa, mfanye utaratibu wa ibada ya kujitakasa pamoja nao, na ulipe gharama ili wanyoe nywele zao. Kwa njia hii kila mtu atafahamu ya kuwa mambo waliyosikia si ya kweli na kwamba wewe unaishika sheria.
"We have four men here under a vow; associate yourself with them, purify yourself with them, and pay their expenses so that they may have their heads shaved; then every one will know that there is no truth in the rumors that they have heard about you; but that you yourself walk orderly obeying the law.
25 Lakini kuhusu wale watu wa Mataifa walioamini, tumewaandikia uamuzi wetu: kwamba wajitenge na vyakula vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, au kula nyama ya mnyama aliyenyongwa, na wajiepushe na uasherati.”
"As for the Gentile believers, we wrote giving judgment that they should abstain from anything sacrificed to an idol, from blood, from what is strangled, and from fornication."
26 Ndipo kesho yake Paulo akawachukua wale watu na akajitakasa pamoja nao. Akaingia ndani ya hekalu ili atoe taarifa ya tarehe ambayo siku zao za utakaso zingemalizika na sadaka ingetolewa kwa ajili ya kila mmoja wao.
Then Paul took the men, and after purifying himself with them next day, went into the temple to declare the fulfilment of the days of purification, until the offering was offered for every one of them.
27 Zile siku saba zilipokaribia kumalizika, baadhi ya Wayahudi kutoka sehemu za Asia waliokuwa wamemwona Paulo ndani ya Hekalu, wakachochea umati wote wa watu, nao wakamkamata.
But when the seven days were almost over, the Asiatic Jews caught sight of him in the temple, and began to stir up all the crowd, and laid hands on him, shouting.
28 Wakapiga kelele wakisema, “Waisraeli wenzetu, tusaidieni! Huyu ndiye yule mtu anayefundisha kila mtu na kila mahali, kinyume na watu wetu, sheria zetu na hata Hekalu hili. Zaidi ya hayo amewaleta Wayunani ndani ya Hekalu na kupanajisi mahali hapa patakatifu.”
"Men of Israel, help! This is the man who goes everywhere preaching to everybody against the people, and the Law, and this place. And he has actually brought Gentiles even into the temple, and has desecrated the holy place."
29 (Walikuwa wamemwona Trofimo, mwenyeji wa Efeso, akiwa mjini pamoja na Paulo wakadhani kuwa Paulo alikuwa amemwingiza Hekaluni.)
(For they had formerly seen Trophimus, the Ephesian, with him in the city, and supposed that Paul had brought him into the temple.)
30 Mji wote ukataharuki, watu wakaja wakikimbia kutoka pande zote wakamkamata Paulo, wakamburuta kutoka Hekaluni. Milango ya Hekalu ikafungwa.
The whole city was thrown into uproar. The mob surged together, seized Paul, and began to drag him outside the temple. Whereupon the doors were at once shut.
31 Walipokuwa wakitaka kumuua, habari zikamfikia jemadari wa jeshi la askari wa Kirumi kwamba mji wa Yerusalemu wote ulikuwa katika machafuko.
While they were attempting to kill him, news came to the tribune commander of the garrison that all Jerusalem was in an uproar.
32 Mara yule jemadari akachukua maafisa wengine wa jeshi pamoja na askari wakakimbilia kwenye ile ghasia, wale watu waliokuwa wakifanya ghasia walipomwona yule jemadari na askari wakija, wakaacha kumpiga Paulo.
At once he took soldiers and centurions, and rushed down upon them. When they saw the tribune and the troops, they left off beating Paul.
33 Yule jemadari akaja, akamkamata Paulo akaamuru afungwe kwa minyororo miwili. Akauliza yeye ni nani, na alikuwa amefanya nini.
Then the tribune came up and seized him, and ordered that he be bound with two chains. "Who is he?" he began asking, "and what has he done?"
34 Baadhi ya watu katika ule umati wakapiga kelele, hawa wakisema hili na wengine lile. Yule jemadari alipoona kuwa hawezi kupata hakika ya habari kwa sababu ya zile kelele, akaamuru Paulo apelekwe katika ngome ya jeshi.
Some among the crowd kept shouting one thing, some another; and when the tribune could not learn the facts because of the uproar, he ordered Paul into the barracks.
35 Paulo alipofika penye ngazi, ilibidi askari wambebe juu juu kwa sababu fujo za ule umati wa watu zilikuwa kubwa.
When was going up the steps, he had to be carried by the soldiers, because of the violence of the mob,
36 Umati wa watu ulikuwa ukifuata ukiendelea kupiga kelele ukisema, “Mwondoe huyu!”
for the whole mass of the people were following him, shouting, "Away with him!"
37 Mara tu Paulo alipokaribia kuingizwa kwenye ngome ya jeshi, akamwambia yule jemadari, “Je, naweza kukuambia jambo moja?” Yule jemadari akamjibu, “Je, unajua Kiyunani?
Just as he was about to be taken into the barracks, Paul said to the tribune, "May I speak to you?"
38 Je, wewe si yule Mmisri ambaye siku hizi za karibuni alianzisha uasi akaongoza kundi la magaidi 4,000 wenye silaha jangwani?”
"Do you know Greek?" said the tribune; "Are you not, then, the Egyptian who in days gone by stirred up to sedition, and let into the wilderness the four thousand cutthroats?"
39 Paulo akajibu, “Mimi ni Myahudi, mzaliwa wa Tarso, huko Kilikia, raiya wa mji maarufu. Tafadhali niruhusu nizungumze na hawa watu.”
"I am a Jew," answered Paul, "a native of Tarsus in Cilicia, a citizen of no mean city. And I pray you, give me permission to speak to the people."
40 Akiisha kupata ruhusa ya yule jemadari, Paulo akasimama penye ngazi akawapungia watu mkono ili wanyamaze. Wote waliponyamaza kimya, Paulo akazungumza nao kwa lugha ya Kiebrania, akasema:
So when he had given leave, Paul stood on the stairs, beckoning with his hands to the people. There came a great hush, and he spoke to them as follows, in Hebrew.

< Matendo 21 >