< Matendo 21 >
1 Tulipokwisha kujitenga nao, tukaanza safari kwa njia ya bahari moja kwa moja mpaka Kosi. Siku ya pili yake tukafika Rodo na kutoka huko tukaenda Patara.
Amimi am kami ngtai käna, mlawng am cit u lü Kotah kami pha lawki. Acunüng, angawi üng Rodih pha u lü, acun üngka naw cit u lü, Patarah kami phaki.
2 Hapo tukapata meli iliyokuwa inavuka kwenda Foinike tukapanda tukasafiri nayo.
Phonisia cit khaia mlawng mat hmu u ngüse, acun ngcum u lü kami citki.
3 Tulipokiona kisiwa cha Kipro, tukakizunguka tukakiacha upande wetu wa kushoto, tukasafiri mpaka Shamu, tukatia nanga katika bandari ya Tiro ambapo meli yetu ilikuwa ipakue shehena yake.
Kuparuh hmunaka cit u lü, cumlama cit u lü Siria kami phaki. Acunüng Turah tui pei kami phaki. Acua mlawng üngka phüihe jah lawh vaia kyase.
4 Baada ya kuwatafuta wanafunzi wa huko, tukakaa nao kwa siku saba. Wale wanafunzi wakiongozwa na Roho wakamwambia Paulo asiende Yerusalemu.
Acunüng, jumeikie jah hmu u lü, acua mhnüp khyüh kami veki; acunüng, anini naw Pawluh cun Ngmüimkhya am mtheh u lü, Jerusalema käh a ceh vaia ami mtheh.
5 Lakini muda wetu ulipokwisha, tukaondoka tukaendelea na safari yetu. Wale wanafunzi pamoja na wake zao na watoto wakatusindikiza hadi nje ya mji. Wote tukapiga magoti pale pwani tukaomba.
Acunsepi, acuna mhnüp päih law se, jah tak hüt lü kami kdungki u lü, cit u ngü se, ami van naw, ami khyucae mah maha mlüh khaw kpung üngkhyüh tui pei cäpa am jah tha law; acua mkhuk msüm u lü kami ktaiyüki.
6 Baada ya kuagana, tukapanda melini, nao wakarudi majumbani mwao.
“Mya lü bä” ti u lü mat jah mat mtheh lü mlawng üng kami ngcum üng amimi cun ami ima nghlat bekie.
7 Tukaendelea na safari yetu toka Tiro tukafika Tolemai, tukawasalimu ndugu wa huko, tukakaa nao kwa siku moja.
Acunüng, Turah üngka naw mlawng am kami ceh law päng üng, Potalemaia kami phaki, acua jumeikie jah hnukset u lü, ami veia mhnüp mät kami veki.
8 Siku iliyofuata tukaondoka, tukafika Kaisaria. Huko tukaenda nyumbani kwa mwinjilisti mmoja jina lake Filipo, aliyekuwa mmoja wa wale Saba, tukakaa kwake.
A ngawi be tü üng, Ketarih kami phaki; acua thangkdaw sangki Philipa ima kami lutki, ani cun Jerusalema jah kpüi khaia xü, khyühe üngka mata kyase a veia kami veki.
9 Filipo alikuwa na binti wanne mabikira waliokuwa wanatoa unabii.
Ani cun nghnumica phyü jah ca naki. Amimi naw Pamhnama ngthu sang hükie.
10 Baada ya kukaa kwa siku kadhaa, akateremka nabii mmoja kutoka Uyahudi jina lake Agabo.
Acua mhnüp khawvei kami vekie, acuna üng Judah hnea ka Akabas ngming naki sahma mat lawki.
11 Alipotufikia akachukua mshipi wa Paulo akajifunga, akautumia kufunga mikono na miguu yake mwenyewe akasema, “Roho Mtakatifu anasema: ‘Hivi ndivyo Wayahudi wa Yerusalemu watakavyomfunga mwenye mshipi huu na kumkabidhi kwa watu wa Mataifa.’”
Kami veia law lü, Pawluha ksawmyüi lo lü amäta kut khawe jah khit lü, “Jerusalema Judahe naw hikba hina ksawmyüi ka naki khit u lü, khyangmjükceea kut üng ap khaie, Ngmüimkhya Ngcim naw a pyen ni” a ti.
12 Tuliposikia maneno haya sisi na ndugu wengine tukamsihi Paulo asiende Yerusalemu.
Acuna ngthu kami ngjak ja, Pawluh cun Jerusalema käh cit khaia keimi jah akcee naw kami nghuinak.
13 Lakini Paulo akajibu, “Kwa nini mnalia na kunivunja moyo? Mimi niko tayari si kufungwa tu, bali hata kufa huko Yerusalemu kwa ajili ya jina la Bwana Yesu.”
Pawluh naw, “I vai kyap u lü, ka mlung nami na puksetsaki ni? Bawipa Jesuha ngminga phäha ta Jerusalema ami na khih däka am kya lü thih vaia pi ka lingki ni” a ti.
14 Alipokuwa hashawishiki, tukaacha kumsihi, tukasema, “Mapenzi ya Bwana na yatendeke.”
Mtheh lü am ng’yah se, “Bawipa hlüeia kya kawm” kami ti.
15 Baada ya haya, tukajiandaa, tukaondoka kwenda Yerusalemu.
Acua kcün kami sumei käna kami phüie jah pitpyang u lü, Jerusalema kami citki.
16 Baadhi ya wanafunzi kutoka Kaisaria wakafuatana nasi na kutupeleka nyumbani kwa Mnasoni, ambaye tungekaa kwake. Yeye alikuwa mtu wa Kipro, mmoja wa wanafunzi wa zamani.
Ketariha üngka axüisawe avang kami hlawnga law hngakie naw, Manatung ngming naki jumei kcük üngka, Kuparuha ka mat, kami cehnaka ami ngkhahpüi hnga.
17 Tulipofika Yerusalemu ndugu wakatukaribisha kwa furaha.
Jerusalem mlüh kami pha üng jumeikie naw hlimtui khaia ami ja na khinnak.
18 Kesho yake Paulo pamoja na wengine wetu tulikwenda kumwona Yakobo, na wazee wote walikuwepo.
A ngawi üng, Pawluh naw Jakuka ima jah cehpüi se, acua sangcim ngvaie veki.
19 Baada ya kuwasalimu, Paulo akatoa taarifa kamili ya mambo yote ambayo Mungu alikuwa amefanya miongoni mwa watu wa Mataifa kupitia huduma yake.
Pawluh naw amimi jah hnukset law päng lü, a khüibinak summangei lü Pamhnam naw khyangmjükceea veia bi a bisak naküt avan a jah mtheh.
20 Baada ya kusikia mambo haya wakamwadhimisha Mungu. Ndipo wakamwambia Paulo, “Ndugu, unaona kulivyo na maelfu ya Wayahudi walioamini, nao wote wana juhudi kwa ajili ya sheria.
Amimi naw acuna ngthu ami ngjak üng Pamhnam mhlünmtai u lü, Pawluha veia, “Pawluh aw, Judah khyange thawng khawhah jumei lawki ja ami van naw Thum pi kthanakie;
21 Lakini wameambiwa habari zako kwamba unafundisha Wayahudi wote waishio miongoni mwa watu wa Mataifa kumkataa Mose, na kwamba unawaambia wasiwatahiri watoto wao wala kufuata desturi zetu.
acunsepi, khyangmjükceea veia vekiea Judahea veia, ami cae ami vun käh ami jah mawih vai ja Mosia Thum ami hawih vaia na ja mtheiki tia pyenkie.
22 Sasa tufanyeje? Bila shaka watasikia kwamba umekuja Yerusalemu.
Ihawkba kya hlüki ni? Na pha law pi ngjakie ni.
23 Kwa hiyo fanya lile tunalokuambia. Tunao watu wanne hapa ambao wameweka nadhiri.
Acunakyase, na veia kami pawh vai cun hin ni. Khyütam taeiki khyang kphyü kami vekie.
24 Jiunge na watu hawa, mfanye utaratibu wa ibada ya kujitakasa pamoja nao, na ulipe gharama ili wanyoe nywele zao. Kwa njia hii kila mtu atafahamu ya kuwa mambo waliyosikia si ya kweli na kwamba wewe unaishika sheria.
Acune jah ngkhahpüi lü, ngcimcaihnak pawia va ngpüi hnga lü, lu kteinaka phu jah pet pe kaw pi. Acunüng, khyange naw, ami ngjak am kcangki tia, namät kung naw Mosi thum na läki tia ksing khaie.
25 Lakini kuhusu wale watu wa Mataifa walioamini, tumewaandikia uamuzi wetu: kwamba wajitenge na vyakula vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, au kula nyama ya mnyama aliyenyongwa, na wajiepushe na uasherati.”
Khyangmjükce jumeikie am, juktuh üng peta eiawk, khisa thi, khisa ami kbüh ja hüipawmnake üng ami ngcimcaih vaia kyaki tia, ca kami yuk päng ni” ami ti.
26 Ndipo kesho yake Paulo akawachukua wale watu na akajitakasa pamoja nao. Akaingia ndani ya hekalu ili atoe taarifa ya tarehe ambayo siku zao za utakaso zingemalizika na sadaka ingetolewa kwa ajili ya kila mmoja wao.
Acuna ngawi üng Pawluh naw, acuna kpamie jah ngkhahpüiki naw, ami veia ngcimcaih hnga lü, Templea k'uma lutki naw, ami ngkhäa phäha petnak akce pawh lü ngcimcaihnaka mhnüpa kümnak vaia mhnüp cun ivei hjo khai ti cun a jah mtheh.
27 Zile siku saba zilipokaribia kumalizika, baadhi ya Wayahudi kutoka sehemu za Asia waliokuwa wamemwona Paulo ndani ya Hekalu, wakachochea umati wote wa watu, nao wakamkamata.
Mhnüp khyüh a küm law hlü üng, Asah üngka Judahe naw Pawluh templea k'uma hmu u lü, khyange naküt jah ksükie naw ami man.
28 Wakapiga kelele wakisema, “Waisraeli wenzetu, tusaidieni! Huyu ndiye yule mtu anayefundisha kila mtu na kila mahali, kinyume na watu wetu, sheria zetu na hata Hekalu hili. Zaidi ya hayo amewaleta Wayunani ndani ya Hekalu na kupanajisi mahali hapa patakatifu.”
Ngpyang u lü, “Isarel khyange aw, jah kpüi law ua, hin naw khaw naküt üng khyang naküta veia, Judah khyangea thume, hina Temple jah kse na ve; acun däk am ni, templea k'uma pi Krik khyange jah luhpüi lü, hina Temple ngcimcaiki pi mtüihkhehsaki ni” ami ti. (
29 (Walikuwa wamemwona Trofimo, mwenyeji wa Efeso, akiwa mjini pamoja na Paulo wakadhani kuwa Paulo alikuwa amemwingiza Hekaluni.)
Am acun ham üng Epheta ka Throphimah naki Pawluh naw mlüh k'uma a ceh hü püi hmu u se, templea k'uma cehpüikia pi ami ngaih.)
30 Mji wote ukataharuki, watu wakaja wakikimbia kutoka pande zote wakamkamata Paulo, wakamburuta kutoka Hekaluni. Milango ya Hekalu ikafungwa.
Mlüh üngka ami van üng ngthang hü lü, ngbäm lawki he naw, Pawluh man u lü, temple kpunga kaih lawki he naw, asäng üng ksawhe ami jah khaih law.
31 Walipokuwa wakitaka kumuua, habari zikamfikia jemadari wa jeshi la askari wa Kirumi kwamba mji wa Yerusalemu wote ulikuwa katika machafuko.
Pawluh hnim vaia ami bü ja, Jerusalema khyange naküt aktäa suksak lawki he tia ngthu cun Romah yekap ngvai säiha veia phaki.
32 Mara yule jemadari akachukua maafisa wengine wa jeshi pamoja na askari wakakimbilia kwenye ile ghasia, wale watu waliokuwa wakifanya ghasia walipomwona yule jemadari na askari wakija, wakaacha kumpiga Paulo.
Acunüng, ani naw yekape ja yekap ngvaie jah cehpüi lü, ami veia dawng ktäi se; yekap ngvai säih ja yekape jah hmu u lü, Pawluh ami kpai cun ami hjaüh.
33 Yule jemadari akaja, akamkamata Paulo akaamuru afungwe kwa minyororo miwili. Akauliza yeye ni nani, na alikuwa amefanya nini.
Yekap ngvai säih naw Pawluh law sih lü, manki naw, mthiyüi nghngih am jah khisak lü, ua kyaki, i pawh khawiki tia a kthäh.
34 Baadhi ya watu katika ule umati wakapiga kelele, hawa wakisema hili na wengine lile. Yule jemadari alipoona kuwa hawezi kupata hakika ya habari kwa sababu ya zile kelele, akaamuru Paulo apelekwe katika ngome ya jeshi.
Khyange akce pyen u lü ngpyang u se, i ami pyen am ksing thei lü, Pawluh cun yekapea venaka ami cehpüi.
35 Paulo alipofika penye ngazi, ilibidi askari wambebe juu juu kwa sababu fujo za ule umati wa watu zilikuwa kubwa.
Acunüng, khyange naw aktäa kutban na hlü u se thukcakia ceh u lü, yekape naw kawt u lü Pawluh cun ami cehpüi.
36 Umati wa watu ulikuwa ukifuata ukiendelea kupiga kelele ukisema, “Mwondoe huyu!”
Khyang naküt naw, “hnim ua” tia Pawluha hnua ngpyangkie.
37 Mara tu Paulo alipokaribia kuingizwa kwenye ngome ya jeshi, akamwambia yule jemadari, “Je, naweza kukuambia jambo moja?” Yule jemadari akamjibu, “Je, unajua Kiyunani?
Pawluh naw yekapea venaka ami luh law hlüpüi üng yekap ngvai säiha veia, “Na veia ngthu pyen lü ng’yah khai aw?” a ti. Acunüng, ani naw, “Krik ngthu pyen theiki aw? ti lü akthäh.
38 Je, wewe si yule Mmisri ambaye siku hizi za karibuni alianzisha uasi akaongoza kundi la magaidi 4,000 wenye silaha jangwani?”
Nang ajana, yea ngthawn lü, khyang thawng kphyü ye vaia kpyawnga ja dawngpüikia Egypt khyanga am na kyaki aw?” a ti.
39 Paulo akajibu, “Mimi ni Myahudi, mzaliwa wa Tarso, huko Kilikia, raiya wa mji maarufu. Tafadhali niruhusu nizungumze na hawa watu.”
Pawluh naw, “Kei cun Kilikih hne, Tasuh mlüha ngtüikia Judah khyanga ka kyaki, ka venaka mlüh pi sawxata am kya, mlüh ktung ni, na bä ni hina khyangea veia ngthu na pyensaka” a ti.
40 Akiisha kupata ruhusa ya yule jemadari, Paulo akasimama penye ngazi akawapungia watu mkono ili wanyamaze. Wote waliponyamaza kimya, Paulo akazungumza nao kwa lugha ya Kiebrania, akasema:
Acunüng, yekap ngvai säih naw täng se, Pawluh naw khyak üng ngdüi lü, khyangea ngdümnak vaia a kut kha lü ami ngdüm law ja, Hebru ngthu am: