< Matendo 20 >

1 Baada ya zile ghasia kumalizika, Paulo aliwaita wanafunzi pamoja akawatia moyo, akawaaga, akaanza safari kwenda Makedonia.
And after the tumult had stilled, Paulos called the disciples and consoled them and kissed them, and going forth went unto Makedunia.
2 Alipita katika sehemu zile, akinena na watu maneno mengi ya kuwatia moyo. Ndipo hatimaye akawasili Uyunani,
And when he had itinerated those regions, and had consoled them with many words, he came into the country of Hales,
3 ambako alikaa kwa muda wa miezi mitatu. Alipokuwa anakaribia kuanza safari kwa njia ya bahari kwenda Shamu, kwa sababu Wayahudi walikuwa wamefanya shauri baya dhidi yake, aliamua kurudi kupitia njia ya Makedonia.
and was there three months. But the Jihudoyee wrought treachery against him, when he was about to go into Syria, and had thought to return into Makedunia.
4 Paulo alikuwa amefuatana na Sopatro mwana wa Piro, Mberoya, Aristarko na Sekundo kutoka Thesalonike na Gayo, mtu wa Derbe, Timotheo pamoja na Tikiko na Trofimo kutoka sehemu ya Asia.
And (there) went forth with him into Asia Supatros who was from Berula, the city; and Aristarkos and Sakundos, who (were) from Thessalonika; and Gaios, who was from Derbe the city; and Timotheos, who was from Lystra; and from Asia, Tukikos and Trophimos.
5 Hawa watu walitutangulia wakaenda kutungojea Troa.
These went before us, and waited for us in Troas.
6 Lakini sisi tukasafiri kwa njia ya bahari kwa siku tano kutoka Filipi baada ya siku za Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, nasi tukaungana na wengine huko Troa, ambako tulikaa kwa siku saba.
But we went forth from Philipos, a city of the Makedunoyee, after the days of the Phatiree, and voyaged by sea and came to Troas in five days, and there were we seven days.
7 Siku ya kwanza ya juma tulikutana pamoja kwa ajili ya kumega mkate. Paulo akaongea na watu, naye kwa kuwa alikuwa amekusudia kuondoka kesho yake, aliendelea kuongea mpaka usiku wa manane.
AND on the first day in the week, when we were assembled to break the eucharist, Paulos discoursed with them, because the day following he was to depart; and he prolonged his discourse until the dividing of the night.
8 Kwenye chumba cha ghorofani walimokuwa wamekutania kulikuwa na taa nyingi.
And there were many lamps of fire in the high-room where we were assembled.
9 Kijana mmoja jina lake Eutiko, alikuwa amekaa dirishani, wakati Paulo alipokuwa akihubiri kwa muda mrefu, alipatwa na usingizi mzito, akaanguka kutoka ghorofa ya tatu, wakamwinua akiwa amekufa.
And a certain youth whose name was Eutikos sat in a window and heard. And he had sunk into a heavy sleep while Paulos prolonged his discourse, and in his sleep he fell from the third floor, and was taken up as dead.
10 Paulo akashuka chini, akajitupa juu yake na kumkumbatia, akasema, “Msishtuke, uzima wake bado umo ndani yake.”
And Paulos descended, and fell upon him and embraced him, and said, Be not agitated, for his life is in him.
11 Kisha Paulo akapanda tena ghorofani, akamega mkate na kula. Baada ya kuongea mpaka mapambazuko, akaondoka.
When he had gone up, he broke bread and tasted, speaking with them until the morning arose; and then went he forth to proceed by land.
12 Watu wakamrudisha yule kijana nyumbani akiwa hai nao wakafarijika sana.
And they brought the young man alive, and rejoiced over him greatly.
13 Tukatangulia melini tukasafiri mpaka Aso ambako tungempakia Paulo. Alikuwa amepanga hivyo kwa maana alitaka kufika kwa miguu.
But we went down to the ship, and voyaged to the port of Thesos, because there we were to receive Paulos, for thus he had instructed us, while he himself would proceed by land.
14 Alipotukuta huko Aso, tulimpakia melini, tukasafiri wote mpaka Mitilene.
But when we had received him from Thesos, we took him up into the ship and came to Mitylene.
15 Kutoka huko tuliendelea kwa njia ya bahari, na kesho yake tukafika mahali panapokabili Kio. Siku iliyofuata tukavuka kwenda Samo, na kesho yake tukawasili Mileto.
And from thence the day after we voyaged over against Kios the island, and again the day after we came to Samos; and we tarried at Trogalium, and the day after we came to Militos:
16 Paulo alikuwa ameamua tusipitie Efeso ili asitumie muda mwingi huko sehemu za Asia, kwa sababu alikuwa anatamani kama ikiwezekana kufika Yerusalemu kabla ya siku ya Pentekoste.
for Paulos had decided with himself to pass by Ephesos, that he might not be hindered there, because he hastened, that, if it were possible, on the day of the Pentecost in Urishlem he might work.
17 Paulo akiwa Mileto, alituma mjumbe kwenda Efeso kuwaita wazee wa kanisa waje wakutane naye.
AND from Militos he sent to bring the presbyters of the church of Ephesos;
18 Walipofika akawaambia, “Ninyi wenyewe mnajua jinsi nilivyoishi katikati yenu muda wote tangu siku ya kwanza nilipokanyaga hapa Asia.
and when they came to him, he said to them: You know, that from the first day that I entered Asia, how I was with you all time,
19 Nilimtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote na kwa machozi nikivumilia taabu na mapingamizi yaliyonipata kutokana na hila za Wayahudi.
serving Aloha in much lowliness and with tears, and in those temptations which passed upon me through the devices of the Jihudoyee.
20 Mnajua kwamba sikusita kuhubiri jambo lolote ambalo lingekuwa la kuwafaa ninyi, lakini nilifundisha hadharani na nyumba kwa nyumba.
Neither neglected I any thing that was profitable for your souls, that I might preach to you and teach in public places and in houses,
21 Nimewashuhudia Wayahudi na Wayunani kwamba inawapasa kumgeukia Mungu kwa kutubu dhambi na kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo.
while I testified to Jihudoyee and to Aramoyee concerning repentance that is toward Aloha, and faith which is in our Lord Jeshu Meshiha.
22 “Nami sasa nimesukumwa na Roho, ninakwenda Yerusalemu wala sijui ni nini kitakachonipata huko.
And now I, bound in the Spirit, go to Urishlem; not knowing what I shall know in her.
23 Ila ninachojua tu ni kwamba Roho Mtakatifu amenionya kuwa vifungo na mateso vinaningoja.
Nevertheless, the Spirit of Holiness in every city testifieth to me and saith, that bonds and afflictions are for me.
24 Lakini siyahesabu maisha yangu kuwa ya thamani kwangu, kama kuyamaliza mashindano na kukamilisha ile kazi Bwana Yesu aliyonipa, yaani, kazi ya kuishuhudia Injili ya neema ya Mungu.
But by me my life is reckoned nothing, so that I may accomplish my course, and the ministry I have received from our Lord Jeshu, to bear witness concerning the gospel of the grace of Aloha.
25 “Nami sasa najua ya kuwa hakuna hata mmoja miongoni mwenu ambaye nimemhubiria Ufalme wa Mungu katika kwenda kwangu huku na huko, atakayeniona uso tena.
And now, I know that again my face you will not see, you, all, among whom I have gone about, preaching to you the kingdom of Aloha.
26 Kwa hiyo nawatangazia leo, sina hatia ya damu ya mtu awaye yote.
I testify to you this very day, that I am pure from the blood of you all.
27 Kwa kuwa sikusita kuwatangazia mapenzi yote ya Mungu.
For I have not shunned to make known to you all the will of Aloha.
28 Jilindeni nafsi zenu na mlilinde lile kundi lote ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi wake. Lichungeni kanisa lake Mungu alilolinunua kwa damu yake mwenyewe.
Take heed therefore to yourselves, and to the whole flock over which the Spirit of Holiness hath constituted you the bishops; to pasture the church of the Meshiha which he hath purchased with his blood.
29 Najua kwamba baada yangu kuondoka, mbwa mwitu wakali watakuja katikati yenu ambao hawatalihurumia kundi.
For I know that after I shall have gone, there will enter with you furious wolves which will not spare the flock.
30 Hata kutoka miongoni mwenu watainuka watu na kuupotosha ukweli ili wawavute wanafunzi wawafuate.
And also from you, of yourselves, will men arise speaking perverse things to turn away disciples to go after them.
31 Hivyo jilindeni! Kumbukeni kwamba kwa miaka mitatu sikuacha kamwe kuwaonya kila mmoja kwa machozi usiku na mchana.
On account of this be watchful, and remember, that for three years I ceased not by night and by day with tears to instruct every one of you.
32 “Sasa nawakabidhi kwa Mungu na kwa neno la neema yake, linaloweza kuwajenga na kuwapa ninyi urithi miongoni mwa wote ambao wametakaswa.
And now I commend you to Aloha, and to the word of his grace, who is able to build you up, and to give you an inheritance with all the saints.
33 Sikutamani fedha wala dhahabu wala vazi la mtu yeyote.
Silver, or gold, or raiment have I not coveted;
34 Ninyi wenyewe mnajua kwamba mikono yangu hii imetumika kwa mahitaji yangu na ya wale waliokuwa pamoja nami.
and you know to the necessity of myself, and of those who are with me, these hands have ministered.
35 Katika kila jambo nimewaonyesha kwamba kwa njia hii ya kufanya kazi kwa bidii imetupasa kuwasaidia wadhaifu, mkikumbuka maneno ya Bwana Yesu mwenyewe jinsi alivyosema, ‘Ni heri kutoa kuliko kupokea.’”
And I have shown you every thing, (that) so it behoveth to labour, and to be careful of those who are infirm, and to remember the word of our Lord Jeshu, that he said, He is blessed who giveth, more than he who receiveth.
36 Paulo alipomaliza kusema haya akapiga magoti pamoja nao wote akaomba.
And when these he had said, he kneeled on his knees and prayed, and all the men with him.
37 Wote wakalia, wakamkumbatia Paulo na kumbusu,
And there was a great weeping with all of them, and they embraced him and kissed him;
38 Kilichowahuzunisha zaidi ni kwa sababu ya yale maneno aliyosema kwamba kamwe hawatauona uso wake tena. Wakaenda naye mpaka kwenye meli.
but most agonized (were they) by that word which he had spoken, that again they were not to see his face. And they accompanied him to the ship.

< Matendo 20 >