< Matendo 2 >
1 Siku ya Pentekoste ilipowadia, waamini wote walikuwa mahali pamoja.
And when the day of Pentecost was now accomplishing, they were all together in one place.
2 Ghafula sauti kama mvumo mkubwa wa upepo mkali uliotoka mbinguni ukaijaza nyumba yote walimokuwa wameketi.
And there came suddenly a sound out of heaven as of a violent impetuous blowing, and filled all the house where they were sitting.
3 Zikatokea ndimi kama za moto zilizogawanyika na kukaa juu ya kila mmoja wao.
And there appeared to them parted tongues, as of fire, and it sat upon each one of them.
4 Wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, wakaanza kunena kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia.
And they were all filled with [the] Holy Spirit, and began to speak with other tongues as the Spirit gave to them to speak forth.
5 Basi walikuwepo Yerusalemu Wayahudi wanaomcha Mungu kutoka kila taifa chini ya mbingu.
Now there were dwelling at Jerusalem Jews, pious men, from every nation of those under heaven.
6 Waliposikia sauti hii, umati wa watu ulikusanyika pamoja wakistaajabu, kwa sababu kila mmoja wao aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe.
But the rumour of this having spread, the multitude came together and were confounded, because each one heard them speaking in his own dialect.
7 Wakiwa wameshangaa na kustaajabu wakauliza, “Je, hawa wote wanaozungumza si Wagalilaya?
And all were amazed and wondered, saying, Behold, are not all these who are speaking Galilaeans?
8 Imekuwaje basi kila mmoja wetu anawasikia wakinena kwa lugha yake ya kuzaliwa?
and how do we hear [them] each in our own dialect in which we have been born,
9 Wapathi, Wamedi, Waelami, wakazi wa Mesopotamia, Uyahudi, Kapadokia, Ponto na Asia,
Parthians, and Medes, and Elamites, and those who inhabit Mesopotamia, and Judaea, and Cappadocia, Pontus and Asia,
10 Frigia, Pamfilia, Misri na pande za Libya karibu na Kirene na wageni kutoka Rumi,
both Phrygia and Pamphylia, Egypt, and the parts of Libya which adjoin Cyrene, and the Romans sojourning [here], both Jews and proselytes,
11 Wayahudi na waongofu, Wakrete na Waarabu, sote tunawasikia watu hawa wakisema mambo makuu ya ajabu ya Mungu katika lugha zetu wenyewe.”
Cretans and Arabians, we hear them speaking in our own tongues the great things of God?
12 Wakiwa wameshangaa na kufadhaika wakaulizana, “Ni nini maana ya mambo haya?”
And they were all amazed and in perplexity, saying one to another, What would this mean?
13 Lakini wengine wakawadhihaki wakasema, “Hawa wamelewa divai!”
But others mocking said, They are full of new wine.
14 Ndipo Petro akasimama pamoja na wale mitume kumi na mmoja, akainua sauti yake na kuhutubia ule umati wa watu, akasema: “Wayahudi wenzangu na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, jueni jambo hili mkanisikilize.
But Peter, standing up with the eleven, lifted up his voice and spoke forth to them, Men of Judaea, and all ye inhabitants of Jerusalem, let this be known to you, and give heed to my words:
15 Hakika watu hawa hawakulewa kama mnavyodhania, kwa kuwa sasa ni saa tatu asubuhi!
for these are not full of wine, as ye suppose, for it is the third hour of the day;
16 La, hili ni jambo lililotabiriwa na nabii Yoeli, akisema:
but this is that which was spoken through the prophet Joel,
17 “‘Katika siku za mwisho, asema Mungu, nitamimina Roho wangu juu ya wote wenye mwili. Wana wenu na binti zenu watatabiri, vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.
And it shall be in the last days, saith God, [that] I will pour out of my Spirit upon all flesh; and your sons and your daughters shall prophesy, and your young men shall see visions, and your elders shall dream with dreams;
18 Hata juu ya watumishi wangu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile nitamimina Roho wangu, nao watatabiri.
yea, even upon my bondmen and upon my bondwomen in those days will I pour out of my Spirit, and they shall prophesy.
19 Nami nitaonyesha maajabu juu mbinguni, na ishara chini duniani: damu, moto, na mawimbi ya moshi.
And I will give wonders in the heaven above and signs on the earth below, blood, and fire, and vapour of smoke:
20 Jua litakuwa giza na mwezi utakuwa mwekundu kama damu, kabla ya kuja siku ile kuu ya Bwana iliyo tukufu.
the sun shall be changed to darkness and the moon to blood, before the great and gloriously appearing day of [the] Lord come.
21 Na kila mtu atakayeliitia jina la Bwana, ataokolewa.’
And it shall be that whosoever shall call upon the name of [the] Lord shall be saved.
22 “Enyi Waisraeli, sikilizeni maneno haya nisemayo: Yesu wa Nazareti alikuwa mtu aliyethibitishwa kwenu na Mungu kwa miujiza, maajabu na ishara, ambayo Mungu alitenda miongoni mwenu kupitia kwake, kama ninyi wenyewe mjuavyo.
Men of Israel, hear these words: Jesus the Nazaraean, a man borne witness to by God to you by works of power and wonders and signs, which God wrought by him in your midst, as yourselves know
23 Huyu mtu akiisha kutolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa kwa kujua kwake Mungu tangu zamani, ninyi, kwa mikono ya watu wabaya, mlimuua kwa kumgongomea msalabani.
— him, given up by the determinate counsel and foreknowledge of God, ye, by [the] hand of lawless [men], have crucified and slain.
24 Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu akamwondolea uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana yeye kushikiliwa na nguvu za mauti.
Whom God has raised up, having loosed the pains of death, inasmuch as it was not possible that he should be held by its power;
25 Kwa maana Daudi asema kumhusu yeye: “‘Nalimwona Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.
for David says as to him, I foresaw the Lord continually before me, because he is at my right hand that I may not be moved.
26 Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika kwa tumaini.
Therefore has my heart rejoiced and my tongue exulted; yea more, my flesh also shall dwell in hope,
27 Kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Aliye Mtakatifu wako kuona uharibifu. (Hadēs )
for thou wilt not leave my soul in hades, nor wilt thou give thy gracious one to see corruption. (Hadēs )
28 Umenionyesha njia za uzima, utanijaza na furaha mbele zako.’
Thou hast made known to me [the] paths of life, thou wilt fill me with joy with thy countenance.
29 “Ndugu zangu Waisraeli, nataka niwaambie kwa uhakika kwamba baba yetu Daudi alikufa na kuzikwa, nalo kaburi lake lipo hapa mpaka leo.
Brethren, let it be allowed to speak with freedom to you concerning the patriarch David, that he has both died and been buried, and his monument is amongst us unto this day.
30 Lakini alikuwa nabii na alijua ya kuwa Mungu alikuwa amemwahidi kwa kiapo kwamba angemweka mmoja wa wazao wake penye kiti chake cha enzi.
Being therefore a prophet, and knowing that God had sworn to him with an oath, of the fruit of his loins to set upon his throne;
31 Daudi, akiona mambo yaliyoko mbele, akanena juu ya kufufuka kwa Kristo, kwamba hakuachwa kaburini, wala mwili wake haukuona uharibifu. (Hadēs )
he, seeing [it] before, spoke concerning the resurrection of the Christ, that neither has he been left in hades nor his flesh seen corruption. (Hadēs )
32 Mungu alimfufua huyu Yesu na sisi sote ni mashahidi wa jambo hilo.
This Jesus has God raised up, whereof all we are witnesses.
33 Basi ikiwa yeye ametukuzwa kwa mkono wa kuume wa Mungu, amepokea kutoka kwa Baba ahadi ya Roho Mtakatifu, naye amemimina kile mnachoona sasa na kusikia.
Having therefore been exalted by the right hand of God, and having received of the Father the promise of the Holy Spirit, he has poured out this which ye behold and hear.
34 Kwa kuwa Daudi hakupaa kwenda mbinguni, lakini anasema, “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume,
For David has not ascended into the heavens, but he says himself, The Lord said unto my Lord, Sit at my right hand
35 hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
until I have put thine enemies [to be] the footstool of thy feet.
36 “Kwa hiyo Israeli wote na wajue jambo hili kwa uhakika kwamba: Mungu amemfanya huyu Yesu, ambaye ninyi mlimsulubisha, kuwa Bwana na Kristo.”
Let the whole house of Israel therefore know assuredly that God has made him, this Jesus whom ye have crucified, both Lord and Christ.
37 Watu waliposikia maneno haya yakawachoma mioyo yao, wakawauliza Petro na wale mitume wengine, “Ndugu zetu tufanye nini?”
And having heard [it] they were pricked in heart, and said to Peter and the other apostles, What shall we do, brethren?
38 Petro akawajibu, “Tubuni, mkabatizwe kila mmoja wenu kwa jina la Yesu Kristo, ili mpate kusamehewa dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
And Peter said to them, Repent, and be baptised, each one of you, in the name of Jesus Christ, for remission of sins, and ye will receive the gift of the Holy Spirit.
39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu na watoto wenu, na kwa wote walio mbali, na kila mtu ambaye Bwana Mungu wetu atamwita amjie.”
For to you is the promise and to your children, and to all who [are] afar off, as many as [the] Lord our God may call.
40 Petro akawaonya kwa maneno mengine mengi na kuwasihi akisema, “Jiepusheni na kizazi hiki kilichopotoka.”
And with many other words he testified and exhorted them, saying, Be saved from this perverse generation.
41 Wale wote waliopokea ujumbe wa Petro kwa furaha wakabatizwa na siku ile waliongezeka watu wapatao 3,000.
Those then who had accepted his word were baptised; and there were added in that day about three thousand souls.
42 Nao wakawa wanadumu katika mafundisho ya mitume, katika ushirika, katika kumega mkate na katika kusali.
And they persevered in the teaching and fellowship of the apostles, in breaking of bread and prayers.
43 Kila mtu akaingiwa na hofu ya Mungu, nayo miujiza mingi na ishara zikafanywa na mitume.
And fear was upon every soul, and many wonders and signs took place through the apostles' means.
44 Walioamini wote walikuwa mahali pamoja, nao walikuwa na kila kitu shirika.
And all that believed were together, and had all things common,
45 Waliuza mali zao na vitu walivyokuwa navyo, kila mtu akagawiwa kadiri ya mahitaji yake.
and sold their possessions and substance, and distributed them to all, according as any one might have need.
46 Siku zote kwa moyo mmoja walikutana ndani ya ukumbi wa Hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, wakila chakula chao kwa furaha na moyo mweupe,
And every day, being constantly in the temple with one accord, and breaking bread in [the] house, they received their food with gladness and simplicity of heart,
47 wakimsifu Mungu na kuwapendeza watu wote. Kila siku Bwana akaliongeza kanisa wale waliokuwa wakiokolewa.
praising God, and having favour with all the people; and the Lord added [to the assembly] daily those that were to be saved.