< Matendo 2 >

1 Siku ya Pentekoste ilipowadia, waamini wote walikuwa mahali pamoja.
And when the days of Pentecost were completed, they were all together in the same place.
2 Ghafula sauti kama mvumo mkubwa wa upepo mkali uliotoka mbinguni ukaijaza nyumba yote walimokuwa wameketi.
And suddenly, there came a sound from heaven, like that of a wind approaching violently, and it filled the entire house where they were sitting.
3 Zikatokea ndimi kama za moto zilizogawanyika na kukaa juu ya kila mmoja wao.
And there appeared to them separate tongues, as if of fire, which settled upon each one of them.
4 Wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, wakaanza kunena kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia.
And they were all filled with the Holy Spirit. And they began to speak in various languages, just as the Holy Spirit bestowed eloquence to them.
5 Basi walikuwepo Yerusalemu Wayahudi wanaomcha Mungu kutoka kila taifa chini ya mbingu.
Now there were Jews staying in Jerusalem, pious men from every nation that is under heaven.
6 Waliposikia sauti hii, umati wa watu ulikusanyika pamoja wakistaajabu, kwa sababu kila mmoja wao aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe.
And when this sound occurred, the multitude came together and was confused in mind, because each one was listening to them speaking in his own language.
7 Wakiwa wameshangaa na kustaajabu wakauliza, “Je, hawa wote wanaozungumza si Wagalilaya?
Then all were astonished, and they wondered, saying: “Behold, are not all of these who are speaking Galileans?
8 Imekuwaje basi kila mmoja wetu anawasikia wakinena kwa lugha yake ya kuzaliwa?
And how is it that we have each heard them in our own language, into which we were born?
9 Wapathi, Wamedi, Waelami, wakazi wa Mesopotamia, Uyahudi, Kapadokia, Ponto na Asia,
Parthians and Medes and Elamites, and those who inhabit Mesopotamia, Judea and Cappadocia, Pontus and Asia,
10 Frigia, Pamfilia, Misri na pande za Libya karibu na Kirene na wageni kutoka Rumi,
Phrygia and Pamphylia, Egypt and the parts of Libya which are around Cyrene, and new arrivals of the Romans,
11 Wayahudi na waongofu, Wakrete na Waarabu, sote tunawasikia watu hawa wakisema mambo makuu ya ajabu ya Mungu katika lugha zetu wenyewe.”
likewise Jews and new converts, Cretans and Arabs: we have heard them speaking in our own languages the mighty deeds of God.”
12 Wakiwa wameshangaa na kufadhaika wakaulizana, “Ni nini maana ya mambo haya?”
And they were all astonished, and they wondered, saying to one another: “But what does this mean?”
13 Lakini wengine wakawadhihaki wakasema, “Hawa wamelewa divai!”
But others mockingly said, “These men are full of new wine.”
14 Ndipo Petro akasimama pamoja na wale mitume kumi na mmoja, akainua sauti yake na kuhutubia ule umati wa watu, akasema: “Wayahudi wenzangu na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, jueni jambo hili mkanisikilize.
But Peter, standing up with the eleven, lifted up his voice, and he spoke to them: “Men of Judea, and all those who are staying in Jerusalem, let this be known to you, and incline your ears to my words.
15 Hakika watu hawa hawakulewa kama mnavyodhania, kwa kuwa sasa ni saa tatu asubuhi!
For these men are not inebriated, as you suppose, for it is the third hour of the day.
16 La, hili ni jambo lililotabiriwa na nabii Yoeli, akisema:
But this is what was spoken of by the prophet Joel:
17 “‘Katika siku za mwisho, asema Mungu, nitamimina Roho wangu juu ya wote wenye mwili. Wana wenu na binti zenu watatabiri, vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.
‘And this shall be: in the last days, says the Lord, I will pour out, from my Spirit, upon all flesh. And your sons and your daughters shall prophesy. And your youths shall see visions, and your elders shall dream dreams.
18 Hata juu ya watumishi wangu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile nitamimina Roho wangu, nao watatabiri.
And certainly, upon my men and women servants in those days, I will pour out from my Spirit, and they shall prophesy.
19 Nami nitaonyesha maajabu juu mbinguni, na ishara chini duniani: damu, moto, na mawimbi ya moshi.
And I will bestow wonders in heaven above, and signs on earth below: blood and fire and the vapor of smoke.
20 Jua litakuwa giza na mwezi utakuwa mwekundu kama damu, kabla ya kuja siku ile kuu ya Bwana iliyo tukufu.
The sun shall be turned into darkness and the moon into blood, before the great and manifest day of the Lord arrives.
21 Na kila mtu atakayeliitia jina la Bwana, ataokolewa.’
And this shall be: whoever shall invoke the name of the Lord will be saved.’
22 “Enyi Waisraeli, sikilizeni maneno haya nisemayo: Yesu wa Nazareti alikuwa mtu aliyethibitishwa kwenu na Mungu kwa miujiza, maajabu na ishara, ambayo Mungu alitenda miongoni mwenu kupitia kwake, kama ninyi wenyewe mjuavyo.
Men of Israel, hear these words: Jesus the Nazarene is a man confirmed by God among you through the miracles and wonders and signs that God accomplished through him in your midst, just as you also know.
23 Huyu mtu akiisha kutolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa kwa kujua kwake Mungu tangu zamani, ninyi, kwa mikono ya watu wabaya, mlimuua kwa kumgongomea msalabani.
This man, under the definitive plan and foreknowledge of God, was delivered by the hands of the unjust, afflicted, and put to death.
24 Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu akamwondolea uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana yeye kushikiliwa na nguvu za mauti.
And he whom God has raised up has broken the sorrows of Hell, for certainly it was impossible for him to be held by it. (questioned)
25 Kwa maana Daudi asema kumhusu yeye: “‘Nalimwona Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.
For David said about him: ‘I foresaw the Lord always in my sight, for he is at my right hand, so that I may not be moved.
26 Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika kwa tumaini.
Because of this, my heart has rejoiced, and my tongue has exulted. Moreover, my flesh shall also rest in hope.
27 Kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Aliye Mtakatifu wako kuona uharibifu. (Hadēs g86)
For you will not abandon my soul to Hell, nor will you allow your Holy One to see corruption. (Hadēs g86)
28 Umenionyesha njia za uzima, utanijaza na furaha mbele zako.’
You have made known to me the ways of life. You will completely fill me with happiness by your presence.’
29 “Ndugu zangu Waisraeli, nataka niwaambie kwa uhakika kwamba baba yetu Daudi alikufa na kuzikwa, nalo kaburi lake lipo hapa mpaka leo.
Noble brothers, permit me to speak freely to you about the Patriarch David: for he passed away and was buried, and his sepulcher is with us, even to this very day.
30 Lakini alikuwa nabii na alijua ya kuwa Mungu alikuwa amemwahidi kwa kiapo kwamba angemweka mmoja wa wazao wake penye kiti chake cha enzi.
Therefore, he was a prophet, for he knew that God had sworn an oath to him about the fruit of his loins, about the One who would sit upon his throne.
31 Daudi, akiona mambo yaliyoko mbele, akanena juu ya kufufuka kwa Kristo, kwamba hakuachwa kaburini, wala mwili wake haukuona uharibifu. (Hadēs g86)
Foreseeing this, he was speaking about the Resurrection of the Christ. For he was neither left behind in Hell, nor did his flesh see corruption. (Hadēs g86)
32 Mungu alimfufua huyu Yesu na sisi sote ni mashahidi wa jambo hilo.
This Jesus, God raised up again, and of this we are all witnesses.
33 Basi ikiwa yeye ametukuzwa kwa mkono wa kuume wa Mungu, amepokea kutoka kwa Baba ahadi ya Roho Mtakatifu, naye amemimina kile mnachoona sasa na kusikia.
Therefore, being exalted to the right hand of God, and having received from the Father the Promise of the Holy Spirit, he poured this out, just as you now see and hear.
34 Kwa kuwa Daudi hakupaa kwenda mbinguni, lakini anasema, “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume,
For David did not ascend into heaven. But he himself said: ‘The Lord said to my Lord: Sit at my right hand,
35 hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
until I make your enemies your footstool.’
36 “Kwa hiyo Israeli wote na wajue jambo hili kwa uhakika kwamba: Mungu amemfanya huyu Yesu, ambaye ninyi mlimsulubisha, kuwa Bwana na Kristo.”
Therefore, may the entire house of Israel know most certainly that God has made this same Jesus, whom you crucified, both Lord and Christ.”
37 Watu waliposikia maneno haya yakawachoma mioyo yao, wakawauliza Petro na wale mitume wengine, “Ndugu zetu tufanye nini?”
Now when they had heard these things, they were contrite in heart, and they said to Peter and to the other Apostles: “What should we do, noble brothers?”
38 Petro akawajibu, “Tubuni, mkabatizwe kila mmoja wenu kwa jina la Yesu Kristo, ili mpate kusamehewa dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
Yet truly, Peter said to them: “Do penance; and be baptized, each one of you, in the name of Jesus Christ, for the remission of your sins. And you shall receive the gift of the Holy Spirit.
39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu na watoto wenu, na kwa wote walio mbali, na kila mtu ambaye Bwana Mungu wetu atamwita amjie.”
For the Promise is for you and for your sons, and for all who are far away: for whomever the Lord our God will have called.”
40 Petro akawaonya kwa maneno mengine mengi na kuwasihi akisema, “Jiepusheni na kizazi hiki kilichopotoka.”
And then, with very many other words, he testified and he exhorted them, saying, “Save yourselves from this depraved generation.”
41 Wale wote waliopokea ujumbe wa Petro kwa furaha wakabatizwa na siku ile waliongezeka watu wapatao 3,000.
Therefore, those who accepted his discourse were baptized. And about three thousand souls were added on that day.
42 Nao wakawa wanadumu katika mafundisho ya mitume, katika ushirika, katika kumega mkate na katika kusali.
Now they were persevering in the doctrine of the Apostles, and in the communion of the breaking of the bread, and in the prayers.
43 Kila mtu akaingiwa na hofu ya Mungu, nayo miujiza mingi na ishara zikafanywa na mitume.
And fear developed in every soul. Also, many miracles and signs were accomplished by the Apostles in Jerusalem. And there was a great awe in everyone.
44 Walioamini wote walikuwa mahali pamoja, nao walikuwa na kila kitu shirika.
And then all who believed were together, and they held all things in common.
45 Waliuza mali zao na vitu walivyokuwa navyo, kila mtu akagawiwa kadiri ya mahitaji yake.
They were selling their possessions and belongings, and dividing them to all, just as any of them had need.
46 Siku zote kwa moyo mmoja walikutana ndani ya ukumbi wa Hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, wakila chakula chao kwa furaha na moyo mweupe,
Also, they continued, daily, to be of one accord in the temple and to break bread among the houses; and they took their meals with exultation and simplicity of heart,
47 wakimsifu Mungu na kuwapendeza watu wote. Kila siku Bwana akaliongeza kanisa wale waliokuwa wakiokolewa.
praising God greatly, and holding favor with all the people. And every day, the Lord increased those who were being saved among them.

< Matendo 2 >