< Matendo 2 >

1 Siku ya Pentekoste ilipowadia, waamini wote walikuwa mahali pamoja.
五旬节那天,使徒们聚集在一起。
2 Ghafula sauti kama mvumo mkubwa wa upepo mkali uliotoka mbinguni ukaijaza nyumba yote walimokuwa wameketi.
忽然天上发出响动,仿佛强风填满了他们所在的整个房屋。
3 Zikatokea ndimi kama za moto zilizogawanyika na kukaa juu ya kila mmoja wao.
他们又看到看似舌头一般的火焰,落在每个人的身上。
4 Wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, wakaanza kunena kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia.
圣灵充满每个人的身体,他们开始通晓不同国家的语言,这也是圣灵赋予他们的能力。
5 Basi walikuwepo Yerusalemu Wayahudi wanaomcha Mungu kutoka kila taifa chini ya mbingu.
当时,耶路撒冷住着很多来自不同国家的虔诚犹太人。
6 Waliposikia sauti hii, umati wa watu ulikusanyika pamoja wakistaajabu, kwa sababu kila mmoja wao aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe.
听到响动,众人便聚了过来。听见使徒能够讲述他们各自的母语,他们倍感困惑。
7 Wakiwa wameshangaa na kustaajabu wakauliza, “Je, hawa wote wanaozungumza si Wagalilaya?
他们万分惊讶地说:“看这些说话的人,他们都是加利利人,是不是?
8 Imekuwaje basi kila mmoja wetu anawasikia wakinena kwa lugha yake ya kuzaliwa?
但我们怎么听见他们在讲我们的母语呢?
9 Wapathi, Wamedi, Waelami, wakazi wa Mesopotamia, Uyahudi, Kapadokia, Ponto na Asia,
我们来自帕提亚、玛代人、以拦、美索不达米亚、犹太、加帕多家、本都、亚西亚、
10 Frigia, Pamfilia, Misri na pande za Libya karibu na Kirene na wageni kutoka Rumi,
弗吕家、旁非利亚、埃及以及靠近古利奈的利比亚的各地,还有来自罗马的犹太人和归信犹太教之人,
11 Wayahudi na waongofu, Wakrete na Waarabu, sote tunawasikia watu hawa wakisema mambo makuu ya ajabu ya Mungu katika lugha zetu wenyewe.”
以及克里特人和阿拉伯之人——但现在,我们听到他们用我们本地的语言,讲述上帝的伟大事迹。”
12 Wakiwa wameshangaa na kufadhaika wakaulizana, “Ni nini maana ya mambo haya?”
众人感到惊讶困扰,彼此询问:“这意味着什么?”
13 Lakini wengine wakawadhihaki wakasema, “Hawa wamelewa divai!”
但也有人讥嘲笑道:“他们就是酒喝太多,醉了。”
14 Ndipo Petro akasimama pamoja na wale mitume kumi na mmoja, akainua sauti yake na kuhutubia ule umati wa watu, akasema: “Wayahudi wenzangu na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, jueni jambo hili mkanisikilize.
彼得和另外 11 名使徒站起来,他高声对众人说:“犹太人和所有住在耶路撒冷的朋友啊,仔细听好了,我要向你们解释这一切。
15 Hakika watu hawa hawakulewa kama mnavyodhania, kwa kuwa sasa ni saa tatu asubuhi!
这些人并非如你们所想喝醉了,现在只是上午九点钟而已。
16 La, hili ni jambo lililotabiriwa na nabii Yoeli, akisema:
所发生的一切正如约珥先知所言:
17 “‘Katika siku za mwisho, asema Mungu, nitamimina Roho wangu juu ya wote wenye mwili. Wana wenu na binti zenu watatabiri, vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.
上帝说:‘在末日到来的日子,我要将我的圣灵施与所有人,你们的儿女将会说出预言,你们的青年人将看到异象,你们的老年人将会梦到梦境。
18 Hata juu ya watumishi wangu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile nitamimina Roho wangu, nao watatabiri.
我将把我的圣灵施于我的仆人,无论男女,他们都将说出预言。
19 Nami nitaonyesha maajabu juu mbinguni, na ishara chini duniani: damu, moto, na mawimbi ya moshi.
我要在天堂和大地向你们显化神迹,有血、有火、有旋转的烟雾!
20 Jua litakuwa giza na mwezi utakuwa mwekundu kama damu, kabla ya kuja siku ile kuu ya Bwana iliyo tukufu.
在主的伟大荣耀之日降临之前,太阳将变得黑暗,月亮将变为血红。
21 Na kila mtu atakayeliitia jina la Bwana, ataokolewa.’
但只要呼唤主的名字,必会得救。’
22 “Enyi Waisraeli, sikilizeni maneno haya nisemayo: Yesu wa Nazareti alikuwa mtu aliyethibitishwa kwenu na Mungu kwa miujiza, maajabu na ishara, ambayo Mungu alitenda miongoni mwenu kupitia kwake, kama ninyi wenyewe mjuavyo.
以色列人,听好了:正如你们所知,上帝通过拿撒勒人耶稣在你们之中显化惊人的奇迹和神迹,证明他就是上帝所确定之人。
23 Huyu mtu akiisha kutolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa kwa kujua kwake Mungu tangu zamani, ninyi, kwa mikono ya watu wabaya, mlimuua kwa kumgongomea msalabani.
上帝早已预知将会发生什么,他按照自己的计划,决定将耶稣交给你们。但你们却借由恶人之手,把他钉上了十字架。
24 Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu akamwondolea uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana yeye kushikiliwa na nguvu za mauti.
但上帝让他起死回生,无需遭受死亡的痛苦,因为死亡没有困住他的力量。
25 Kwa maana Daudi asema kumhusu yeye: “‘Nalimwona Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.
大卫这样说耶稣:‘我总是会看见主在我面前。因为他就在我身边,我必不会动摇。
26 Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika kwa tumaini.
所以我才会如此快乐,所以我的言语中充满喜悦,所以我的身体充满希望。
27 Kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Aliye Mtakatifu wako kuona uharibifu. (Hadēs g86)
因你不会弃我于坟墓,也不会让圣者腐朽。 (Hadēs g86)
28 Umenionyesha njia za uzima, utanijaza na furaha mbele zako.’
你向我指引了生命之路,让我因你在身旁而充满欢喜。’
29 “Ndugu zangu Waisraeli, nataka niwaambie kwa uhakika kwamba baba yetu Daudi alikufa na kuzikwa, nalo kaburi lake lipo hapa mpaka leo.
兄弟姐妹们,让我坦白地告诉你们,我们的祖先大卫已经死去并被埋葬,至今他的坟墓仍在人间。
30 Lakini alikuwa nabii na alijua ya kuwa Mungu alikuwa amemwahidi kwa kiapo kwamba angemweka mmoja wa wazao wake penye kiti chake cha enzi.
但他是先知,知晓上帝向他做出的誓言,要从他的后裔中选择一人接替他的王位。
31 Daudi, akiona mambo yaliyoko mbele, akanena juu ya kufufuka kwa Kristo, kwamba hakuachwa kaburini, wala mwili wake haukuona uharibifu. (Hadēs g86)
大卫已看见了即将发生的事,曾这样讲述基督的复活:‘基督不会被弃于坟墓,他的肉身也不腐朽。’ (Hadēs g86)
32 Mungu alimfufua huyu Yesu na sisi sote ni mashahidi wa jambo hilo.
上帝让这位耶稣复活,我们都是这件事的见证人。
33 Basi ikiwa yeye ametukuzwa kwa mkono wa kuume wa Mungu, amepokea kutoka kwa Baba ahadi ya Roho Mtakatifu, naye amemimina kile mnachoona sasa na kusikia.
现在他已被高举到上帝的右边,获得天父承诺给予他的圣灵,在被施与圣灵后,你们所见所闻就会倾吐而出。
34 Kwa kuwa Daudi hakupaa kwenda mbinguni, lakini anasema, “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume,
大卫并没有升入天堂,但他却说:‘主对我主说:坐在我右边,
35 hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
让我把你的仇敌成为你的脚凳。’
36 “Kwa hiyo Israeli wote na wajue jambo hili kwa uhakika kwamba: Mungu amemfanya huyu Yesu, ambaye ninyi mlimsulubisha, kuwa Bwana na Kristo.”
现在要让以色列所有人都确信:被你们钉上十字架上的这位耶稣,上帝已经让他成为主和基督!”
37 Watu waliposikia maneno haya yakawachoma mioyo yao, wakawauliza Petro na wale mitume wengine, “Ndugu zetu tufanye nini?”
众人听到这一切,心中倍感痛苦。他们询问彼得和其他使徒说:“兄弟们,我们应该怎么办?”
38 Petro akawajibu, “Tubuni, mkabatizwe kila mmoja wenu kwa jina la Yesu Kristo, ili mpate kusamehewa dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
彼得说:“悔改!所有人都要以耶稣基督之名受洗,以便你们的罪获得救赎,这样就能获得圣灵馈赠。
39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu na watoto wenu, na kwa wote walio mbali, na kila mtu ambaye Bwana Mungu wetu atamwita amjie.”
这承诺给予你们、你们的儿女、以及所有远方之人,我们主上帝召来的所有人。”
40 Petro akawaonya kwa maneno mengine mengi na kuwasihi akisema, “Jiepusheni na kizazi hiki kilichopotoka.”
彼得继续讲述,给出更多证明。他警告众人,说:“从这个扭曲的世界拯救自己吧!”
41 Wale wote waliopokea ujumbe wa Petro kwa furaha wakabatizwa na siku ile waliongezeka watu wapatao 3,000.
那些接受他这番话的人都受了洗,这一天内的门徒数量就增加了约三千人。
42 Nao wakawa wanadumu katika mafundisho ya mitume, katika ushirika, katika kumega mkate na katika kusali.
他们立下承诺要遵守门徒的教诲,对其他信徒也立下承诺,共同“分享饼”和共同祈祷。
43 Kila mtu akaingiwa na hofu ya Mungu, nayo miujiza mingi na ishara zikafanywa na mitume.
众人敬畏地看到使徒们做出的奇迹和神迹。
44 Walioamini wote walikuwa mahali pamoja, nao walikuwa na kila kitu shirika.
所有信徒都聚在一起,分享自己的所有。
45 Waliuza mali zao na vitu walivyokuwa navyo, kila mtu akagawiwa kadiri ya mahitaji yake.
他们变卖房屋和财物,按照个人所需分享变卖所得。
46 Siku zote kwa moyo mmoja walikutana ndani ya ukumbi wa Hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, wakila chakula chao kwa furaha na moyo mweupe,
他们日夜持续地在圣殿中聚会,在家中共同进餐,以谦卑幸福的心情享用食物。他们赞美上帝,所有人都赞赏他们。
47 wakimsifu Mungu na kuwapendeza watu wote. Kila siku Bwana akaliongeza kanisa wale waliokuwa wakiokolewa.
他们的数量不断增加,因为主将所拯救之人带到这里。

< Matendo 2 >