< Matendo 19 >

1 Apolo alipokuwa huko Korintho, Paulo alisafiri sehemu za bara, akafika Efeso. Huko akawakuta wanafunzi kadhaa,
Zgodí se pa, ko je bil Apolo v Korintu, da Pavel, prehodivši gorenje strani, pride v Efez; in ko je našel nekaj učencev,
2 akawauliza, “Je, mlipokea Roho Mtakatifu mlipoamini?” Wakajibu, “Hapana, hata hatukusikia kuwa kuna Roho Mtakatifu.”
Reče jim: Ali ste prejeli Duha svetega, ko ste postali verni? Oni mu pa rekó: Saj še slišali nismo, da je sveti Duh.
3 Ndipo Paulo akawauliza, “Je, mlibatizwa kwa ubatizo gani?” Wakajibu, “Kwa ubatizo wa Yohana.”
In reče jim: Na kaj torej ste se krstili? Oni pa rekó: Na krst Janezov.
4 Paulo akasema, “Ubatizo wa Yohana ulikuwa wa toba, aliwaambia watu wamwamini yeye atakayekuja baada yake, yaani, Yesu.”
Pavel pa reče: Janez je krstil s krstom spokore, govoreč ljudstvu, da naj verujejo v tega, kteri bo za njim prišel, to je v Kristusa Jezusa.
5 Waliposikia haya, wakabatizwa katika jina la Bwana Yesu.
Ko so pa to slišali, krstili so se v ime Gospoda Jezusa.
6 Paulo alipoweka mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu akawashukia, nao wakanena kwa lugha mpya na kutabiri.
In ko je položil Pavel roke na-nje, prišel je sveti Duh na-nje, in govorili so jezike in prerokovali.
7 Walikuwa kama wanaume kumi na wawili.
Bilo je pa vseh móž kakih dvanajst.
8 Paulo akaingia katika sinagogi na kunena humo kwa ujasiri kwa muda wa miezi mitatu, akijadiliana na watu na kuwashawishi katika mambo ya Ufalme wa Mungu.
In ko je prišel v shajališče, govoril je srčno, tri mesece prepirajoč se in učeč o kraljestvu Božjem.
9 Lakini baadhi yao walikaidi. Walikataa kuamini, na wakakashifu ujumbe wake mbele ya umati wa watu. Basi Paulo aliachana nao. Akawachukua wanafunzi naye, akahojiana nao kila siku katika darasa la Tirano.
Ko so bili pa nekteri otrpneli in niso hoteli pokorni biti, hudo govoreč o potu Gospodovem pred množico, odstopil je od njih, in odločil je učence, in učil je vsak dan v šoli nekega Tirana.
10 Jambo hili likaendelea kwa muda wa miaka miwili, kiasi kwamba Wayahudi na Wayunani wote walioishi huko Asia wakawa wamesikia neno la Bwana.
In to se je godilo dve leti, tako, da so vsi, kteri so prebivali v Aziji, slišali besedo Gospoda Jezusa, Judje in Grki.
11 Mungu akafanya miujiza mingi isiyo ya kawaida kwa mkono wa Paulo,
In čudeže ne majhne je delal Bog po rokah Pavlovih;
12 hivi kwamba leso au vitambaa vilivyokuwa vimegusa mwili wa Paulo viliwekwa juu ya wagonjwa, nao wakapona magonjwa yao, na pepo wachafu wakawatoka.
Tako, da so na bolnike pokladali potne prte od života njegovega in opasnike, in puščale so jih bolezni, in duhovi hudobni so izhajali iž njih.
13 Basi baadhi ya Wayahudi wenye kutangatanga huku na huko wakitoa pepo wachafu wakajaribu kutumia jina la Bwana Yesu wale wenye pepo wakisema, “Kwa jina la Yesu, yule anayehubiriwa na Paulo, nakuamuru utoke.”
In izkušali so nekteri izmed Judov, kteri so okrog hodili in hudiče rotili, klicati na tiste, kteri so imeli duhove hudobne, ime Gospoda Jezusa, govoreč: Zaklinjamo vas pri Jezusu, kterega Pavel oznanjuje.
14 Wana saba wa Skewa, Myahudi aliyekuwa kiongozi wa makuhani, walikuwa wanafanya hivyo.
Bilo je pa nekih sedem sinov Skeve Juda, vélikega duhovna, kteri so to delali.
15 Lakini pepo mchafu akawajibu, “Yesu namjua na Paulo pia namjua, lakini ninyi ni nani?”
Odgovarjajoč pa duh hudobni, reče: Jezusa poznam, in Pavla vém; vi pa, kdo ste?
16 Kisha yule mtu aliyekuwa na pepo mchafu akawarukia, akawashambulia vikali, akawashinda nguvu wote, wakatoka ndani ya ile nyumba wakikimbia wakiwa uchi na wenye majeraha.
In skočivši človek, v kterem je bil duh hudobni, na-nje, premagal jih je, in zdelal jih je tako, da so nagi in ranjeni ubežali iz tiste hiše.
17 Habari hii ikajulikana kwa Wayahudi wote na Wayunani waliokaa Efeso, hofu ikawajaa wote, nalo jina la Bwana Yesu likaheshimiwa sana.
To je pa prišlo na znanje vsem Judom in Grkom, kteri so prebivali v Efezu; in obšel jih je strah vse, in poveličevalo se je ime Gospoda Jezusa.
18 Wengi wa wale waliokuwa wameamini wakati huu wakaja na kutubu waziwazi kuhusu matendo yao maovu.
In mnogo teh, kteri so verovali, dohajalo je in izpovedovali so se, in razodevali so dela svoja.
19 Idadi kubwa ya wale waliofanya mambo ya uganga wakaleta vitabu vyao na kuviteketeza kwa moto hadharani. Walipofanya hesabu ya thamani ya vitabu vilivyoteketezwa ilikuwa drakma 50,000 za fedha.
A mnogi tistih, kteri so uganjali vraže, znesli so bukve, in sežgali so jih pred vsemi; in ko so preudarili njih ceno, našli so, da so veljale petdeset tisoči srebrnikov.
20 Hivyo neno la Bwana likaenea sana na kuwa na nguvu.
Tako krepko je beseda Božja rastla in utrjevala se.
21 Baada ya mambo haya kutukia, Paulo akakusudia rohoni kwenda Yerusalemu kupitia Makedonia na Akaya. Akasema, “Baada ya kufika huko, yanipasa pia kwenda Rumi.”
A ko se je to dopolnilo, nameni Pavel v duhu, da prehodivši Macedonijo in Ahajo, pojde v Jeruzalem, in reče: Po tem, ko bom tam, moram tudi Rim videti.
22 Hivyo akatuma wasaidizi wake wawili, Timotheo na Erasto, waende Makedonia, wakati yeye mwenyewe alibaki kwa muda kidogo huko Asia.
In poslal je v Macedonijo dva od tistih, kteri so mu služili, Timoteja in Erasta; a sam je ostal nekaj časa v Aziji.
23 Wakati huo huo pakatokea dhiki kubwa kwa sababu ya Njia ile ya Bwana.
Vstal je pa v ta čas ne majhen hrup za voljo pota Gospodovega.
24 Mtu mmoja jina lake Demetrio mfua fedha aliyekuwa akitengeneza vinyago vya fedha vya Artemi na kuwapatia mafundi wake biashara kubwa,
Neki Demetrij namreč po imenu, srebrar, ki je delal Dijani srebrne cerkvice, dajal je umetnikom ne malo dela;
25 aliwaita pamoja watu wengine waliofanya kazi ya ufundi kama yake na kusema, “Enyi watu, mnajua ya kuwa utajiri wetu unatokana na biashara hii!
In sklicavši te, in druge takošne delalce, reče: Možjé! véste, da imamo od tega dela zaslužek svoj;
26 Pia ninyi mmeona na kusikia jinsi ambavyo si huku Efeso peke yake lakini ni karibu Asia yote, huyu Paulo amewashawishi na kuvuta idadi kubwa ya watu kwa kusema kuwa miungu iliyotengenezwa na watu si miungu.
In vidite in slišite, da ne samo v Efezu, nego skoro po vsej Aziji je ta Pavel veliko ljudstva pregovoril in odvrnil, govoreč, da bogovi, kteri so z rokami narejeni, niso bogovi.
27 Kwa hiyo kuna hatari si kwa kazi yetu kudharauliwa tu, bali pia hata hekalu la mungu mke Artemi, aliye mkuu, anayeabudiwa Asia yote na ulimwengu wote, litakuwa limepokonywa fahari yake ya kiungu.”
Ni pa samo to v nevarnosti, da bo delo naše na nič prišlo, nego tudi vélike boginje Dijane tempelj se bo za nič štel, in poginilo bo veličastvo te, ktero vsa Azija in ves svet častí.
28 Waliposikia maneno haya, wakaghadhibika, wakaanza kupiga kelele, “Artemi wa Waefeso ni mkuu!”
Ko so pa to slišali, napolnijo se jeze, in kričali so, govoreč: Velika je Dijana Efežanov!
29 Mara mji wote ukajaa ghasia. Wakawakamata Gayo na Aristarko, watu wa Makedonia waliokuwa wakisafiri pamoja na Paulo, na watu wakakimbilia katika ukumbi wa michezo kama mtu mmoja.
In napolni se vse mesto zmešnjave; in zaženó se enodušno na gledališče, in zgrabijo Gaja in Aristarha, Macedonca tovariša Pavlova.
30 Paulo akataka kuingia katikati ya umati huo, lakini wanafunzi hawakumruhusu.
Ko je pa Pavel hotel vniti med ljudstvo, niso mu pustili.
31 Hata baadhi ya viongozi wa sehemu ile, waliokuwa rafiki zake Paulo, wakatuma watu wakitamani asiingie katika ule ukumbi.
Pa tudi nekteri od Azijskih poglavarjev, kteri so mu bili prijatelji, poslali so k njemu, in prosili so ga, naj se ne podá v gledališče.
32 Ule umati ulikuwa na taharuki. Wengine walikuwa wakipiga kelele, hawa wakisema hili na wengine lile. Idadi kubwa ya watu hawakujua hata ni kwa nini walikuwa wamekusanyika huko.
Vpili so pa eni to, drugi drugo; kajti bil je zbor poln zmešnjave, in največ jih je bilo med njimi, kteri niso vedeli, po kaj so se sešli.
33 Wayahudi wakamsukumia Aleksanda mbele na baadhi ya watu kwenye ule umati wakampa maelekezo. Akawaashiria kwa mkono ili watulie aweze kujitetea mbele ya watu.
A nekteri izmed ljudstva so izvlekli Aleksandra, ko so ga Judje naprej tiščali; Aleksander pa zamahme z rokó, da naj umolknejo, in hotel je ljudstvu odgovoriti.
34 Lakini walipotambua kwamba alikuwa Myahudi, wote wakapiga kelele kwa sauti moja kwa karibu muda wa saa mbili, wakisema, “Artemi wa Efeso ni mkuu!”
Ko so pa spoznali, da je Jud, vzdignejo vsi en glas, in vpili so kaki dve uri: Velika je Dijana Efežanov!
35 Baadaye karani wa mji akaunyamazisha ule umati wa watu na kusema, “Enyi watu wa Efeso, je, ulimwengu wote haujui ya kuwa mji wa Efeso ndio unaotunza hekalu la Artemi aliye mkuu na ile sanamu yake iliyoanguka kutoka mbinguni?
Pisar pa, ko je ljudstvo upokojil, reče: Možjé Efežani! kdo pa je človek, kteri ne vé, da mesto Efežanov častí véliko boginjo Dijano in od Jupiterja padlo podobo?
36 Kwa hiyo, kwa kuwa mambo haya hayakanushiki, inawapasa mnyamaze na wala msifanye lolote kwa haraka.
Ker se torej to ne more tajiti, treba je, da se umirite, in ne delate nič naglo.
37 Kwa kuwa mmewaleta hawa watu hapa, ingawa hawajaiba hekaluni wala kumkufuru huyu mungu wetu wa kike.
Kajti pripeljali ste te ljudí, kteri niso ne tempeljna oropali, ne boginje vaše preklinjali.
38 Basi, ikiwa Demetrio na mafundi wenzake wana jambo zito dhidi ya mtu yeyote, mahakama ziko wazi na wasaidizi wa mwakilishi wa mtawala. Wanaweza kufungua mashtaka.
Če imajo pa Demetrij in umetniki, kteri so ž njim, tožbo zoper koga, sodnije so, in namestniki so; naj tožijo eden drugega.
39 Lakini kama kuna jambo jingine lolote zaidi mnalotaka kulileta, itabidi lisuluhishwe katika kusanyiko halali.
Če pa kaj drugega iščete, obravnalo se bo v postavnem zboru.
40 Kama ilivyo sasa, tuko hatarini kushtakiwa kwa kufanya ghasia kwa sababu ya tukio la leo. Kwa kuwa hakuna sababu tutakayoweza kutoa kuhalalisha msukosuko huu.”
Kajti v nevarnosti smo, da bomo zatoženi za voljo današnjega punta, ko nimamo nobenega vzroka, s kterim bi mogli odgovor dati za ta hrup.
41 Baada ya kusema haya akavunja mkutano.
In rekši to, razpustil je zbor.

< Matendo 19 >