< Matendo 19 >

1 Apolo alipokuwa huko Korintho, Paulo alisafiri sehemu za bara, akafika Efeso. Huko akawakuta wanafunzi kadhaa,
Now it came to pass, that while Apollos was at Corinth, Paul, having passed through the upper parts, came to Ephesus: and finding there some disciples,
2 akawauliza, “Je, mlipokea Roho Mtakatifu mlipoamini?” Wakajibu, “Hapana, hata hatukusikia kuwa kuna Roho Mtakatifu.”
he said to them, Have you, on your believing, received the Holy Spirit? And they replied to him, No; we have not so much as heard whether the Holy Spirit is received.
3 Ndipo Paulo akawauliza, “Je, mlibatizwa kwa ubatizo gani?” Wakajibu, “Kwa ubatizo wa Yohana.”
And he said to them, Into what, then, were you immersed? And they said, Into John's immersion.
4 Paulo akasema, “Ubatizo wa Yohana ulikuwa wa toba, aliwaambia watu wamwamini yeye atakayekuja baada yake, yaani, Yesu.”
And Paul said, John, indeed, administered the immersion of reformation, telling the people that they should believe in Him that was to come after him: that is, in Jesus.
5 Waliposikia haya, wakabatizwa katika jina la Bwana Yesu.
And hearing this, they were immersed into the name of the Lord Jesus.
6 Paulo alipoweka mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu akawashukia, nao wakanena kwa lugha mpya na kutabiri.
And Paul, laying his hands, on them, the Holy Spirit came upon them; and they spoke with tongues, and prophesied.
7 Walikuwa kama wanaume kumi na wawili.
And they were, in all, about twelve men.
8 Paulo akaingia katika sinagogi na kunena humo kwa ujasiri kwa muda wa miezi mitatu, akijadiliana na watu na kuwashawishi katika mambo ya Ufalme wa Mungu.
And he went into the synagogue, and discoursed with boldness, disputing for the space of three months, and evincing the things which related to the kingdom of God.
9 Lakini baadhi yao walikaidi. Walikataa kuamini, na wakakashifu ujumbe wake mbele ya umati wa watu. Basi Paulo aliachana nao. Akawachukua wanafunzi naye, akahojiana nao kila siku katika darasa la Tirano.
But as some were hardened, and would not believe, speaking reproachfully of this way before the multitude, he departed from them, and separated the disciples, disputing daily in the school of one Tyrannus.
10 Jambo hili likaendelea kwa muda wa miaka miwili, kiasi kwamba Wayahudi na Wayunani wote walioishi huko Asia wakawa wamesikia neno la Bwana.
And this was done for the space of two years, so that all the inhabitants of Asia, both Jews and Greeks, heard the word of the Lord.
11 Mungu akafanya miujiza mingi isiyo ya kawaida kwa mkono wa Paulo,
And God wrought extraordinary miracles by the hands of Paul:
12 hivi kwamba leso au vitambaa vilivyokuwa vimegusa mwili wa Paulo viliwekwa juu ya wagonjwa, nao wakapona magonjwa yao, na pepo wachafu wakawatoka.
so that handkerchiefs, or aprons, were carried from his body to those who were sick, and the diseases removed from them, and the evil spirits came out.
13 Basi baadhi ya Wayahudi wenye kutangatanga huku na huko wakitoa pepo wachafu wakajaribu kutumia jina la Bwana Yesu wale wenye pepo wakisema, “Kwa jina la Yesu, yule anayehubiriwa na Paulo, nakuamuru utoke.”
And some of the strolling Jews, who were exorcists, undertook to name the name of the Lord Jesus, over those who had evil spirits, saying, We adjure you by Jesus, whom Paul preaches.
14 Wana saba wa Skewa, Myahudi aliyekuwa kiongozi wa makuhani, walikuwa wanafanya hivyo.
And there were seven sons of one Sceva, a Jewish chief priest, who did this.
15 Lakini pepo mchafu akawajibu, “Yesu namjua na Paulo pia namjua, lakini ninyi ni nani?”
But the evil spirit answering, said, Jesus I know, and Paul I know; but who are you?
16 Kisha yule mtu aliyekuwa na pepo mchafu akawarukia, akawashambulia vikali, akawashinda nguvu wote, wakatoka ndani ya ile nyumba wakikimbia wakiwa uchi na wenye majeraha.
And the man in whom the evil spirit was, sprung upon them, and getting master of them prevailed against them, so that they fled out of the house, naked and wounded.
17 Habari hii ikajulikana kwa Wayahudi wote na Wayunani waliokaa Efeso, hofu ikawajaa wote, nalo jina la Bwana Yesu likaheshimiwa sana.
And this was known to all the Jews, and Greeks also dwelling at Ephesus; and fear fell upon them all, and the name of the Lord Jesus was magnified.
18 Wengi wa wale waliokuwa wameamini wakati huu wakaja na kutubu waziwazi kuhusu matendo yao maovu.
And many of them, who believed, came and confessed, and made a declaration of their deeds.
19 Idadi kubwa ya wale waliofanya mambo ya uganga wakaleta vitabu vyao na kuviteketeza kwa moto hadharani. Walipofanya hesabu ya thamani ya vitabu vilivyoteketezwa ilikuwa drakma 50,000 za fedha.
And a considerable number of those who had curious arts, bringing their books together, burnt them before all: and they computed the value of them, and found it fifty thousand pieces of silver:
20 Hivyo neno la Bwana likaenea sana na kuwa na nguvu.
so powerfully did the word of the Lord grow, and prevail.
21 Baada ya mambo haya kutukia, Paulo akakusudia rohoni kwenda Yerusalemu kupitia Makedonia na Akaya. Akasema, “Baada ya kufika huko, yanipasa pia kwenda Rumi.”
Now when these things were fulfilled, Paul proposed in spirit, that, passing through Macedonia and Achaia, he would go to Jerusalem, saying, After I have been there, it is necessary for me also to see Rome.
22 Hivyo akatuma wasaidizi wake wawili, Timotheo na Erasto, waende Makedonia, wakati yeye mwenyewe alibaki kwa muda kidogo huko Asia.
And sending two of those that ministered to him, Timothy and Erastus, into Macedonia, he himself staid some time in Asia.
23 Wakati huo huo pakatokea dhiki kubwa kwa sababu ya Njia ile ya Bwana.
And there happened, about that time, no small tumult concerning that way.
24 Mtu mmoja jina lake Demetrio mfua fedha aliyekuwa akitengeneza vinyago vya fedha vya Artemi na kuwapatia mafundi wake biashara kubwa,
For a man whose name was Demetrius, a silversmith, by making silver shrines of Diana, procured no small gain to the artificers:
25 aliwaita pamoja watu wengine waliofanya kazi ya ufundi kama yake na kusema, “Enyi watu, mnajua ya kuwa utajiri wetu unatokana na biashara hii!
whom he gathered together, with the workmen employed about the business, and said, Men, you know that our maintenance arises from this manufacture;
26 Pia ninyi mmeona na kusikia jinsi ambavyo si huku Efeso peke yake lakini ni karibu Asia yote, huyu Paulo amewashawishi na kuvuta idadi kubwa ya watu kwa kusema kuwa miungu iliyotengenezwa na watu si miungu.
and you see and hear that this Paul has persuaded great numbers of people, not only of Ephesus, but almost of all Asia, and has turned them aside, saying that they are not deities which are made with hands;
27 Kwa hiyo kuna hatari si kwa kazi yetu kudharauliwa tu, bali pia hata hekalu la mungu mke Artemi, aliye mkuu, anayeabudiwa Asia yote na ulimwengu wote, litakuwa limepokonywa fahari yake ya kiungu.”
so that there is danger, not only that this occupation of ours should be depreciated, but also that the people of the great goddess Diana should be despised, and her grandeur destroyed; whom all Asia and the world worship.
28 Waliposikia maneno haya, wakaghadhibika, wakaanza kupiga kelele, “Artemi wa Waefeso ni mkuu!”
And hearing this, they were filled with rage; and cried out, saying, Great is Diana of the Ephesians!
29 Mara mji wote ukajaa ghasia. Wakawakamata Gayo na Aristarko, watu wa Makedonia waliokuwa wakisafiri pamoja na Paulo, na watu wakakimbilia katika ukumbi wa michezo kama mtu mmoja.
And the whole city was filled with confusion; and they rushed with one accord into the theater, dragging thither Gaius and Aristarchus, Macedonians, Paul's fellow-travelers.
30 Paulo akataka kuingia katikati ya umati huo, lakini wanafunzi hawakumruhusu.
And when Paul would have gone in to the people, the disciples would not permit him.
31 Hata baadhi ya viongozi wa sehemu ile, waliokuwa rafiki zake Paulo, wakatuma watu wakitamani asiingie katika ule ukumbi.
And some, too, the principal officers of Asia, as they had a friendship for him, sent to him, and desired that he would not venture himself into the theater.
32 Ule umati ulikuwa na taharuki. Wengine walikuwa wakipiga kelele, hawa wakisema hili na wengine lile. Idadi kubwa ya watu hawakujua hata ni kwa nini walikuwa wamekusanyika huko.
Some, therefore, were crying one thing, and some another; for the congregation was confused, and the greater part did not know for what they were come together.
33 Wayahudi wakamsukumia Aleksanda mbele na baadhi ya watu kwenye ule umati wakampa maelekezo. Akawaashiria kwa mkono ili watulie aweze kujitetea mbele ya watu.
And they thrust forth forward Alexander, from amongst the multitude, the Jews urging him on. And Alexander, beckoning with his hand, would have made a defense to the people.
34 Lakini walipotambua kwamba alikuwa Myahudi, wote wakapiga kelele kwa sauti moja kwa karibu muda wa saa mbili, wakisema, “Artemi wa Efeso ni mkuu!”
But when they knew that he was a Jew, one voice arose from them all, crying out, for about the space of two hours, Great is Diana of the Ephesians!
35 Baadaye karani wa mji akaunyamazisha ule umati wa watu na kusema, “Enyi watu wa Efeso, je, ulimwengu wote haujui ya kuwa mji wa Efeso ndio unaotunza hekalu la Artemi aliye mkuu na ile sanamu yake iliyoanguka kutoka mbinguni?
But the chancellor, having pacified the people, said Ephesians, what man is there that does not know that the city of the Ephesians is devoted to the great Diana, and to the image that fell down from Jupiter.
36 Kwa hiyo, kwa kuwa mambo haya hayakanushiki, inawapasa mnyamaze na wala msifanye lolote kwa haraka.
Since, then, these things are incontestable, it is necessary for you to be quiet, and to do nothing in a precipitate manner;
37 Kwa kuwa mmewaleta hawa watu hapa, ingawa hawajaiba hekaluni wala kumkufuru huyu mungu wetu wa kike.
for you have brought these men, who are neither robbers of temples, nor blasphemers of your goddess.
38 Basi, ikiwa Demetrio na mafundi wenzake wana jambo zito dhidi ya mtu yeyote, mahakama ziko wazi na wasaidizi wa mwakilishi wa mtawala. Wanaweza kufungua mashtaka.
If, therefore, Demetrius, and the artificers that are with him, have a charge against any one, courts are held; and there are the proconsuls; let them implead together.
39 Lakini kama kuna jambo jingine lolote zaidi mnalotaka kulileta, itabidi lisuluhishwe katika kusanyiko halali.
But if you are inquiring anything concerning other matters, it shall be determined in a legal congregation.
40 Kama ilivyo sasa, tuko hatarini kushtakiwa kwa kufanya ghasia kwa sababu ya tukio la leo. Kwa kuwa hakuna sababu tutakayoweza kutoa kuhalalisha msukosuko huu.”
And, indeed, we are in danger of being called in question for the insurrection which has happened this day, as there is no cause by which we can account for this concourse.
41 Baada ya kusema haya akavunja mkutano.
And when he had said these things, he dismissed the congregation.

< Matendo 19 >