< Matendo 19 >

1 Apolo alipokuwa huko Korintho, Paulo alisafiri sehemu za bara, akafika Efeso. Huko akawakuta wanafunzi kadhaa,
亚波罗在哥林多期间,保罗从内陆抵达以弗所,在那里找到了若干信徒。
2 akawauliza, “Je, mlipokea Roho Mtakatifu mlipoamini?” Wakajibu, “Hapana, hata hatukusikia kuwa kuna Roho Mtakatifu.”
他问他们说:“当你们信了上帝的时候,是否领取了圣灵?”他们说:“没有,我们甚至都没听说过圣灵这件事情。”
3 Ndipo Paulo akawauliza, “Je, mlibatizwa kwa ubatizo gani?” Wakajibu, “Kwa ubatizo wa Yohana.”
保罗问:“那么你们接受的是何种施洗?” 他们说:“是约翰的施洗。”
4 Paulo akasema, “Ubatizo wa Yohana ulikuwa wa toba, aliwaambia watu wamwamini yeye atakayekuja baada yake, yaani, Yesu.”
保罗说:“约翰提供的是悔改施洗,他告诉众人应该相信在他之后到来的那个人,也就是他们应该相信耶稣。”
5 Waliposikia haya, wakabatizwa katika jina la Bwana Yesu.
众人听罢,便以主耶稣之名进行受洗。
6 Paulo alipoweka mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu akawashukia, nao wakanena kwa lugha mpya na kutabiri.
保罗为他们按手,圣灵就便降临在他们身上,他们开始用不同的语言说话,还可以进行预言。
7 Walikuwa kama wanaume kumi na wawili.
这些人总计大约十二人。
8 Paulo akaingia katika sinagogi na kunena humo kwa ujasiri kwa muda wa miezi mitatu, akijadiliana na watu na kuwashawishi katika mambo ya Ufalme wa Mungu.
在三个月的时间内,保罗一直都在会堂里向那里的人大胆宣讲,与他们进行讨论,努力说服他们相信上帝之国。
9 Lakini baadhi yao walikaidi. Walikataa kuamini, na wakakashifu ujumbe wake mbele ya umati wa watu. Basi Paulo aliachana nao. Akawachukua wanafunzi naye, akahojiana nao kila siku katika darasa la Tirano.
但有些人始终顽固不化,拒绝接受他的宣讲,还在众人面前毁谤道。所以保罗放弃了他们,离开了会堂,将信徒们也一并带走。之后,他每天都在推喇奴讲堂与大家进行讨论。
10 Jambo hili likaendelea kwa muda wa miaka miwili, kiasi kwamba Wayahudi na Wayunani wote walioishi huko Asia wakawa wamesikia neno la Bwana.
就这样过了两年,所有亚西亚省的居民,无论犹太人或希腊人,都听到了主的道。
11 Mungu akafanya miujiza mingi isiyo ya kawaida kwa mkono wa Paulo,
上帝通过保罗显化很多不同寻常的神迹。
12 hivi kwamba leso au vitambaa vilivyokuwa vimegusa mwili wa Paulo viliwekwa juu ya wagonjwa, nao wakapona magonjwa yao, na pepo wachafu wakawatoka.
甚至有人会拿走保罗曾经触碰的手帕或围巾,去医治病患和赶走邪灵。
13 Basi baadhi ya Wayahudi wenye kutangatanga huku na huko wakitoa pepo wachafu wakajaribu kutumia jina la Bwana Yesu wale wenye pepo wakisema, “Kwa jina la Yesu, yule anayehubiriwa na Paulo, nakuamuru utoke.”
几个犹太人打着耶稣的名号四处驱鬼,向身上附着之人说:“我以保罗所言耶稣之名,命令你们出来。”
14 Wana saba wa Skewa, Myahudi aliyekuwa kiongozi wa makuhani, walikuwa wanafanya hivyo.
一位名叫士基瓦的犹太人司长,他的七个儿子都在做这件事,一个是犹太人,一个是大祭司。
15 Lakini pepo mchafu akawajibu, “Yesu namjua na Paulo pia namjua, lakini ninyi ni nani?”
但有一天当他们驱魔时,邪灵却回答到:“我认识耶稣,也认识保罗,但你们是谁?”
16 Kisha yule mtu aliyekuwa na pepo mchafu akawarukia, akawashambulia vikali, akawashinda nguvu wote, wakatoka ndani ya ile nyumba wakikimbia wakiwa uchi na wenye majeraha.
邪灵附体那人扑到他们身上将其制服,一番痛殴后,他们赤裸着身体从那房子逃了出来,满身是伤。
17 Habari hii ikajulikana kwa Wayahudi wote na Wayunani waliokaa Efeso, hofu ikawajaa wote, nalo jina la Bwana Yesu likaheshimiwa sana.
所有住在以弗所的犹太人和希腊人都知道此事,纷纷表示敬畏,主耶稣之名获得了广泛尊重。
18 Wengi wa wale waliokuwa wameamini wakati huu wakaja na kutubu waziwazi kuhusu matendo yao maovu.
也有许多信主之人前来忏悔他们的罪,公开坦诚他们曾经做过的恶行。
19 Idadi kubwa ya wale waliofanya mambo ya uganga wakaleta vitabu vyao na kuviteketeza kwa moto hadharani. Walipofanya hesabu ya thamani ya vitabu vilivyoteketezwa ilikuwa drakma 50,000 za fedha.
其中有许多曾经施行巫术之人,把他们关于巫术的书堆在一起当众烧掉。他们估算了一下书价,总计五万银币。
20 Hivyo neno la Bwana likaenea sana na kuwa na nguvu.
通过这种方式,主的道日益强大,广为传播。
21 Baada ya mambo haya kutukia, Paulo akakusudia rohoni kwenda Yerusalemu kupitia Makedonia na Akaya. Akasema, “Baada ya kufika huko, yanipasa pia kwenda Rumi.”
在这之后,保罗决定穿过马其顿和亚该亚去往耶路撒冷。他说:“我到了那边以后,必须去罗马看看。”
22 Hivyo akatuma wasaidizi wake wawili, Timotheo na Erasto, waende Makedonia, wakati yeye mwenyewe alibaki kwa muda kidogo huko Asia.
他派了两名帮手提摩太和以拉都两人去马其顿,自己则暂时留在亚西亚省。
23 Wakati huo huo pakatokea dhiki kubwa kwa sababu ya Njia ile ya Bwana.
就在这期间,发生了很多关于道的骚乱,
24 Mtu mmoja jina lake Demetrio mfua fedha aliyekuwa akitengeneza vinyago vya fedha vya Artemi na kuwapatia mafundi wake biashara kubwa,
有一位名叫低米丢的银匠,以制造亚底米女神的小银龛为生,这门手艺给他这样的工匠带来了不少生意。
25 aliwaita pamoja watu wengine waliofanya kazi ya ufundi kama yake na kusema, “Enyi watu, mnajua ya kuwa utajiri wetu unatokana na biashara hii!
他把同行和相似行业的工人们聚起来,说:“工友们,你们知道,我们就是靠这门生意赚钱。
26 Pia ninyi mmeona na kusikia jinsi ambavyo si huku Efeso peke yake lakini ni karibu Asia yote, huyu Paulo amewashawishi na kuvuta idadi kubwa ya watu kwa kusema kuwa miungu iliyotengenezwa na watu si miungu.
毫无疑问,通过你们看见和听见的事情,你们也应该意识到这个叫保罗的人,不仅在以弗所、还几乎在整个亚西亚游说和误导众人,说人类所制造的都不是上帝的创造。
27 Kwa hiyo kuna hatari si kwa kazi yetu kudharauliwa tu, bali pia hata hekalu la mungu mke Artemi, aliye mkuu, anayeabudiwa Asia yote na ulimwengu wote, litakuwa limepokonywa fahari yake ya kiungu.”
这不仅导致我们这一行可能会受人鄙视,就连伟大女神亚底米的庙也会遭人摒弃,亚西亚和普天下所敬拜的女神将失去其威严。”
28 Waliposikia maneno haya, wakaghadhibika, wakaanza kupiga kelele, “Artemi wa Waefeso ni mkuu!”
这话掀起了众人的怒火,他们高喊到:“以弗所人的亚底米,伟大的神!”
29 Mara mji wote ukajaa ghasia. Wakawakamata Gayo na Aristarko, watu wa Makedonia waliokuwa wakisafiri pamoja na Paulo, na watu wakakimbilia katika ukumbi wa michezo kama mtu mmoja.
全城陷入大骚动,他们捉住了与保罗同行的马其顿人该犹和亚里达古,一起冲进了剧场。
30 Paulo akataka kuingia katikati ya umati huo, lakini wanafunzi hawakumruhusu.
保罗想去直面暴徒,但其他信徒不让他这么做。
31 Hata baadhi ya viongozi wa sehemu ile, waliokuwa rafiki zake Paulo, wakatuma watu wakitamani asiingie katika ule ukumbi.
保罗有几名省长官的朋友,也捎来口信,叮嘱他不要去剧场那里。
32 Ule umati ulikuwa na taharuki. Wengine walikuwa wakipiga kelele, hawa wakisema hili na wengine lile. Idadi kubwa ya watu hawakujua hata ni kwa nini walikuwa wamekusanyika huko.
但暴徒们并不知道聚集的原因,如一群无头苍蝇一般,口中胡乱喊叫着。
33 Wayahudi wakamsukumia Aleksanda mbele na baadhi ya watu kwenye ule umati wakampa maelekezo. Akawaashiria kwa mkono ili watulie aweze kujitetea mbele ya watu.
人群中的犹太人把亚历山大推到前面,他做了个让大家安静的手势,想要解释给众人听。
34 Lakini walipotambua kwamba alikuwa Myahudi, wote wakapiga kelele kwa sauti moja kwa karibu muda wa saa mbili, wakisema, “Artemi wa Efeso ni mkuu!”
众人认出他是犹太人,便异口同声高喊:“以弗所人的亚底米,伟大的神!”足足喊了两个小时。
35 Baadaye karani wa mji akaunyamazisha ule umati wa watu na kusema, “Enyi watu wa Efeso, je, ulimwengu wote haujui ya kuwa mji wa Efeso ndio unaotunza hekalu la Artemi aliye mkuu na ile sanamu yake iliyoanguka kutoka mbinguni?
后来书记官设法安抚了民众。他说:“以弗所人呐!你们的城是看守伟大亚底米的神庙,也看守来自天堂的神像。这一点谁不知道呢?
36 Kwa hiyo, kwa kuwa mambo haya hayakanushiki, inawapasa mnyamaze na wala msifanye lolote kwa haraka.
这些都是不可辩驳的事实,你们应当保持平静,不可冲动行事。
37 Kwa kuwa mmewaleta hawa watu hapa, ingawa hawajaiba hekaluni wala kumkufuru huyu mungu wetu wa kike.
你们抓到这里的两个人,既没有打劫庙宇,也没有亵渎我们的女神。
38 Basi, ikiwa Demetrio na mafundi wenzake wana jambo zito dhidi ya mtu yeyote, mahakama ziko wazi na wasaidizi wa mwakilishi wa mtawala. Wanaweza kufungua mashtaka.
如果低米丢和其他工匠想要控告谁,完全可以去找总督或提交法庭,可以在那里提交诉状。
39 Lakini kama kuna jambo jingine lolote zaidi mnalotaka kulileta, itabidi lisuluhishwe katika kusanyiko halali.
如果还有其他问题,就应该进行合法的集会予以解决。
40 Kama ilivyo sasa, tuko hatarini kushtakiwa kwa kufanya ghasia kwa sababu ya tukio la leo. Kwa kuwa hakuna sababu tutakayoweza kutoa kuhalalisha msukosuko huu.”
今天的骚乱毫无来由,我们实在无法评判,事实上,我们甚至可能需要为这件事情负责。”
41 Baada ya kusema haya akavunja mkutano.
说罢这番话,他就让暴徒们散去了。

< Matendo 19 >