< Matendo 18 >
1 Baada ya haya, Paulo akaondoka Athene akaenda Korintho.
After these things, Paul departed from Athens, and came to Corinth;
2 Huko akakutana na Myahudi mmoja jina lake Akila, mwenyeji wa Ponto, ambaye alikuwa amewasili karibuni kutoka Italia pamoja na mkewe Prisila, kwa sababu Klaudio alikuwa ameamuru Wayahudi wote waondoke Rumi. Paulo akaenda kuwaona,
And found a certain Jew named Aquila, born in Pontus, lately come from Italy, with his wife Priscilla (because that Claudius had commanded all Jews to depart from Rome) and [he] came to them.
3 naye kwa kuwa alikuwa mtengeneza mahema kama wao, akakaa na kufanya kazi pamoja nao.
And because he was of the same occupation, he abode with them, and wrought (for by their occupation they were tent-makers)
4 Kila Sabato Paulo alikuwa akihojiana nao katika sinagogi, akijitahidi kuwashawishi Wayahudi na Wayunani.
And he reasoned in the synagogue every sabbath, and persuaded the Jews and the Greeks.
5 Sila na Timotheo walipowasili kutoka Makedonia, walimkuta Paulo akiwa amejitolea muda wake wote katika kuhubiri, akiwashuhudia Wayahudi kwamba Yesu ndiye Kristo
And when Silas and Timothy had come from Macedonia, Paul was pressed in spirit, and testified to the Jews, [that] Jesus [was] Christ.
6 Wayahudi walipompinga Paulo na kukufuru, yeye aliyakungʼuta mavazi yake, akawaambia, “Damu yenu na iwe juu ya vichwa vyenu! Mimi sina hatia, nimetimiza wajibu wangu. Kuanzia sasa nitawaendea watu wa Mataifa.”
And when they opposed themselves, and blasphemed, he shook [his] raiment, and said to them, Your blood [be] upon your own heads: I [am] clean: from henceforth I will go to the Gentiles.
7 Kisha akaondoka mle kwenye sinagogi, akaenda nyumbani kwa mtu mmoja jina lake Tito Yusto, aliyekuwa mcha Mungu. Nyumba yake ilikuwa karibu na sinagogi.
And he departed thence, and entered into the house of a certain man named Justus, [one] that worshiped God, whose house joined close to the synagogue.
8 Kiongozi wa hilo sinagogi, aliyeitwa Krispo, akamwamini Bwana, yeye pamoja na watu wote wa nyumbani mwake. Nao Wakorintho wengi waliomsikia Paulo pia wakaamini na kubatizwa.
And Crispus the chief ruler of the synagogue believed on the Lord with all his house: and many of the Corinthians hearing, believed, and were baptized.
9 Usiku mmoja Bwana akamwambia Paulo katika maono, “Usiogope, lakini endelea kusema wala usinyamaze,
Then the Lord spoke to Paul in the night by a vision, Be not afraid, but speak, and hold not thy peace:
10 kwa maana mimi niko pamoja nawe, wala hakuna mtu atakayeweza kukushambulia ili kukudhuru, kwa kuwa ninao watu wengi katika mji huu ambao ni watu wangu.”
For I am with thee, and no man shall lay hands on thee, to hurt thee: for I have many people in this city.
11 Hivyo Paulo akakaa huko kwa muda wa mwaka mmoja na nusu, akiwafundisha neno la Mungu.
And he continued [there] a year and six months, teaching the word of God among them.
12 Lakini wakati Galio alipokuwa msaidizi wa mwakilishi wa mtawala huko Akaya, Wayahudi waliungana kumshambulia Paulo, wakamkamata na kumpeleka mahakamani.
And when Gallio was the deputy of Achaia, the Jews made insurrection with one accord against Paul, and brought him to the judgment-seat,
13 Wakamshtaki wakisema, “Mtu huyu anawashawishi watu wamwabudu Mungu kinyume cha sheria.”
Saying, This [man] persuadeth men to worship God contrary to the law.
14 Paulo alipotaka kujitetea, Galio akawaambia Wayahudi, “Kama ninyi Wayahudi mlikuwa mkilalamika kuhusu makosa makubwa ya uhalifu ingekuwa haki kwangu kuwasikiliza.
And when Paul was now about to open [his] mouth, Gallio said to the Jews, If it were a matter of wrong, or hainous crime, O [ye] Jews, reason would that I should bear with you:
15 Lakini kwa kuwa linahusu maneno, majina na sheria yenu, amueni ninyi wenyewe. Mimi sitakuwa mwamuzi wa mambo haya.”
But if it is a question of words and names, and [of] your law, look ye [to it]: for I will be no judge of such [matters].
16 Akawafukuza kutoka mahakamani.
And he drove them from the judgment-seat.
17 Ndipo wote wakamkamata Sosthene kiongozi wa sinagogi, wakampiga mbele ya mahakama, lakini Galio hakujali kitendo chao hata kidogo.
Then all the Greeks took Sosthenes, the chief ruler of the synagogue, and beat [him] before the judgment-seat. And Gallio cared for none of those things.
18 Baada ya kukaa Korintho kwa muda, Paulo akaagana na wale ndugu walioamini, akasafiri kwa njia ya bahari kwenda Shamu akiwa amefuatana na Prisila na Akila. Walipofika Kenkrea, Paulo alinyoa nywele zake kwa kuwa alikuwa ameweka nadhiri.
And Paul [after this] tarried [there] yet a good while, and took his leave of the brethren, and sailed thence into Syria, and with him Priscilla and Aquila; having shorn [his] head in Cenchrea: for he had a vow.
19 Walipofika Efeso, Paulo aliwaacha Prisila na Akila huko, lakini yeye akaingia kwenye sinagogi akawa anajadiliana na Wayahudi.
And he came to Ephesus, and left them there: but he himself entered into the synagogue, and reasoned with the Jews.
20 Walipomwomba akae nao kwa muda mrefu zaidi hakukubali.
When they desired [him] to tarry longer time with them, he consented not:
21 Lakini alipokuwa akiondoka, akaahidi, “Nitarudi kama Mungu akipenda.” Kisha akasafiri kwa njia ya bahari kutoka Efeso.
But bade them farewell, saying, I must by all means keep this feast that cometh in Jerusalem: but I will return to you, if God will. And he sailed from Ephesus.
22 Alitia nanga Kaisaria, akaenda Yerusalemu na kulisalimu kanisa, kisha akaenda Antiokia.
And when he had landed at Cesarea, and gone up and saluted the church, he went down to Antioch.
23 Baada ya kukaa huko kwa muda, akaondoka na kwenda sehemu moja hadi nyingine huko Galatia na Frigia, akiwaimarisha wanafunzi wote.
And after he had spent some time [there], he departed and went over [all] the country of Galatia and Phrygia in order, strengthening all the disciples.
24 Basi akaja Efeso Myahudi mmoja, jina lake Apolo, mwenyeji wa Iskanderia. Yeye alikuwa na elimu kubwa, pia alikuwa hodari katika Maandiko.
And a certain Jew named Apollos, born at Alexandria, an eloquent man, [and] mighty in the scriptures, came to Ephesus.
25 Alikuwa amefundishwa katika njia ya Bwana, naye alikuwa na bidii katika roho, akafundisha kwa usahihi juu ya Yesu, ingawa alijua tu ubatizo wa Yohana.
This man was instructed in the way of the Lord: and being fervent in the spirit, he spoke and taught diligently the things of the Lord, knowing only the baptism of John.
26 Apolo alianza kunena kwa ujasiri mkubwa katika sinagogi. Lakini Prisila na Akila walipomsikia, walimchukua kando na kumweleza njia ya Mungu kwa ufasaha zaidi.
And he began to speak boldly in the synagogue: Whom, when Aquila and Priscilla had heard, they took him to [them], and expounded to him the way of God more perfectly.
27 Naye Apolo alipotaka kwenda Akaya, ndugu wa Efeso walimtia moyo, wakawaandikia wanafunzi huko ili wamkaribishe. Alipofika huko, aliwasaidia sana wale ambao, kwa neema ya Mungu, walikuwa wameamini.
And when he was disposed to pass into Achaia, the brethren wrote, exhorting the disciples to receive him: who, when he had come, helped them much who had believed through grace.
28 Kwa uwezo mkubwa aliwakanusha hadharani Wayahudi waliokuwa wakipinga, akionyesha kwa njia ya Maandiko kwamba Yesu ndiye Kristo.
For he mightily convinced the Jews, [and that] publicly, showing by the scriptures, that Jesus was Christ.