< Matendo 18 >

1 Baada ya haya, Paulo akaondoka Athene akaenda Korintho.
with/after (then *k*) this/he/she/it to separate/leave (the/this/who *k*) (Paul *K*) out from the/this/who Athens to come/go toward Corinth
2 Huko akakutana na Myahudi mmoja jina lake Akila, mwenyeji wa Ponto, ambaye alikuwa amewasili karibuni kutoka Italia pamoja na mkewe Prisila, kwa sababu Klaudio alikuwa ameamuru Wayahudi wote waondoke Rumi. Paulo akaenda kuwaona,
and to find/meet one Jew name Aquila of Pontus the/this/who family: descendant recently to come/go away from the/this/who Italy and Priscilla woman: wife it/s/he through/because of the/this/who (to direct *NK(o)*) Claudius to separate/leave all the/this/who Jew (away from *N(k)O*) the/this/who Rome to come near/agree it/s/he
3 naye kwa kuwa alikuwa mtengeneza mahema kama wao, akakaa na kufanya kazi pamoja nao.
and through/because of the/this/who of the same trade to exist to stay from/with/beside it/s/he and (to work *NK(O)*) to be for tentmaker (the/this/who skill *N(k)O*)
4 Kila Sabato Paulo alikuwa akihojiana nao katika sinagogi, akijitahidi kuwashawishi Wayahudi na Wayunani.
to dispute then in/on/among the/this/who synagogue according to all Sabbath to persuade and/both Jew and Greek, Gentile
5 Sila na Timotheo walipowasili kutoka Makedonia, walimkuta Paulo akiwa amejitolea muda wake wote katika kuhubiri, akiwashuhudia Wayahudi kwamba Yesu ndiye Kristo
as/when then to descend away from the/this/who Macedonia the/this/who and/both Silas and the/this/who Timothy to hold/oppress the/this/who (word *N(K)O*) the/this/who Paul to testify solemnly the/this/who Jew to exist the/this/who Christ Jesus
6 Wayahudi walipompinga Paulo na kukufuru, yeye aliyakungʼuta mavazi yake, akawaambia, “Damu yenu na iwe juu ya vichwa vyenu! Mimi sina hatia, nimetimiza wajibu wangu. Kuanzia sasa nitawaendea watu wa Mataifa.”
to resist then it/s/he and to blaspheme to shake out/off the/this/who clothing to say to/with it/s/he the/this/who blood you upon/to/against the/this/who head you clean I/we away from the/this/who now toward the/this/who Gentiles to travel
7 Kisha akaondoka mle kwenye sinagogi, akaenda nyumbani kwa mtu mmoja jina lake Tito Yusto, aliyekuwa mcha Mungu. Nyumba yake ilikuwa karibu na sinagogi.
and to depart from there (to enter *N(k)O*) toward home one name (Titius *N(O)*) Justus be devout the/this/who God which the/this/who home to be be next to the/this/who synagogue
8 Kiongozi wa hilo sinagogi, aliyeitwa Krispo, akamwamini Bwana, yeye pamoja na watu wote wa nyumbani mwake. Nao Wakorintho wengi waliomsikia Paulo pia wakaamini na kubatizwa.
Crispus then the/this/who synagogue leader to trust (in) the/this/who lord: God with all the/this/who house: household it/s/he and much the/this/who Corinthian to hear to trust (in) and to baptize
9 Usiku mmoja Bwana akamwambia Paulo katika maono, “Usiogope, lakini endelea kusema wala usinyamaze,
to say then the/this/who lord: God in/on/among night through/because of vision the/this/who Paul not to fear but to speak and not be quiet
10 kwa maana mimi niko pamoja nawe, wala hakuna mtu atakayeweza kukushambulia ili kukudhuru, kwa kuwa ninao watu wengi katika mji huu ambao ni watu wangu.”
because I/we to be with/after you and none to put/lay on you the/this/who to harm you because a people to be me much in/on/among the/this/who city this/he/she/it
11 Hivyo Paulo akakaa huko kwa muda wa mwaka mmoja na nusu, akiwafundisha neno la Mungu.
to seat (then *N(k)O*) year and month six to teach in/on/among it/s/he the/this/who word the/this/who God
12 Lakini wakati Galio alipokuwa msaidizi wa mwakilishi wa mtawala huko Akaya, Wayahudi waliungana kumshambulia Paulo, wakamkamata na kumpeleka mahakamani.
Gallio then proconsul to be the/this/who Achaia to attack united the/this/who Jew the/this/who Paul and to bring it/s/he upon/to/against the/this/who judgement seat
13 Wakamshtaki wakisema, “Mtu huyu anawashawishi watu wamwabudu Mungu kinyume cha sheria.”
to say that/since: that from/with/beside the/this/who law to persuade this/he/she/it the/this/who a human be devout the/this/who God
14 Paulo alipotaka kujitetea, Galio akawaambia Wayahudi, “Kama ninyi Wayahudi mlikuwa mkilalamika kuhusu makosa makubwa ya uhalifu ingekuwa haki kwangu kuwasikiliza.
to ensue then the/this/who Paul to open the/this/who mouth to say the/this/who Gallio to/with the/this/who Jew if on the other hand (therefore/then *K*) to be crime one or crime evil/bad oh! Jew according to word if (to endure *N(k)O*) you
15 Lakini kwa kuwa linahusu maneno, majina na sheria yenu, amueni ninyi wenyewe. Mimi sitakuwa mwamuzi wa mambo haya.”
if then (a question/dispute *N(K)O*) to be about word and name and law the/this/who according to you to appear it/s/he judge (for *k*) I/we this/he/she/it no to plan to exist
16 Akawafukuza kutoka mahakamani.
and to eject it/s/he away from the/this/who judgement seat
17 Ndipo wote wakamkamata Sosthene kiongozi wa sinagogi, wakampiga mbele ya mahakama, lakini Galio hakujali kitendo chao hata kidogo.
to catch then all (the/this/who Greek, Gentile *K*) Sosthenes the/this/who synagogue leader to strike before the/this/who judgement seat and none this/he/she/it the/this/who Gallio (to concern *NK(O)*)
18 Baada ya kukaa Korintho kwa muda, Paulo akaagana na wale ndugu walioamini, akasafiri kwa njia ya bahari kwenda Shamu akiwa amefuatana na Prisila na Akila. Walipofika Kenkrea, Paulo alinyoa nywele zake kwa kuwa alikuwa ameweka nadhiri.
the/this/who then Paul still to remain/persist day sufficient the/this/who brother to leave to sail out/away toward the/this/who Syria and with it/s/he Priscilla and Aquila to shear in/on/among Cenchreae the/this/who head to have/be for a vow/prayer
19 Walipofika Efeso, Paulo aliwaacha Prisila na Akila huko, lakini yeye akaingia kwenye sinagogi akawa anajadiliana na Wayahudi.
(to come to *N(K)O*) then toward Ephesus and that to leave behind there it/s/he then to enter toward the/this/who synagogue (to dispute *N(k)O*) the/this/who Jew
20 Walipomwomba akae nao kwa muda mrefu zaidi hakukubali.
to ask then it/s/he upon/to/against greater time to stay (from/with/beside it/s/he *k*) no to accept
21 Lakini alipokuwa akiondoka, akaahidi, “Nitarudi kama Mungu akipenda.” Kisha akasafiri kwa njia ya bahari kutoka Efeso.
but (to leave *N(k)O*) (and *no*) (it/s/he *k*) to say (be necessary *KO*) (me surely the/this/who festival the/this/who to come/go to do/make: do toward Jerusalem *K*) again (then *k*) to return to/with you the/this/who God to will/desire (and *k*) to lead away from the/this/who Ephesus
22 Alitia nanga Kaisaria, akaenda Yerusalemu na kulisalimu kanisa, kisha akaenda Antiokia.
and to descend toward Caesarea to ascend and to pay respects to the/this/who assembly to come/go down toward Antioch
23 Baada ya kukaa huko kwa muda, akaondoka na kwenda sehemu moja hadi nyingine huko Galatia na Frigia, akiwaimarisha wanafunzi wote.
and to do/make: spend(TIME) time one to go out to pass through in order the/this/who Galatia country and Phrygia (to strengthen *NK(o)*) all the/this/who disciple
24 Basi akaja Efeso Myahudi mmoja, jina lake Apolo, mwenyeji wa Iskanderia. Yeye alikuwa na elimu kubwa, pia alikuwa hodari katika Maandiko.
Jew then one Apollos name Alexandrian the/this/who family: descendant man learned to come to toward Ephesus able to be in/on/among the/this/who a writing
25 Alikuwa amefundishwa katika njia ya Bwana, naye alikuwa na bidii katika roho, akafundisha kwa usahihi juu ya Yesu, ingawa alijua tu ubatizo wa Yohana.
this/he/she/it to be to instruct the/this/who road the/this/who lord: God and be fervent the/this/who spirit/breath: spirit to speak and to teach exactly the/this/who about the/this/who (Jesus *N(K)O*) to know/understand alone the/this/who baptism John
26 Apolo alianza kunena kwa ujasiri mkubwa katika sinagogi. Lakini Prisila na Akila walipomsikia, walimchukua kando na kumweleza njia ya Mungu kwa ufasaha zaidi.
this/he/she/it and/both be first to preach boldly in/on/among the/this/who synagogue to hear then it/s/he Priscilla and Aquila to take it/s/he and stricter it/s/he to explain/expose the/this/who road the/this/who God
27 Naye Apolo alipotaka kwenda Akaya, ndugu wa Efeso walimtia moyo, wakawaandikia wanafunzi huko ili wamkaribishe. Alipofika huko, aliwasaidia sana wale ambao, kwa neema ya Mungu, walikuwa wameamini.
to plan then it/s/he to pass through toward the/this/who Achaia to encourage the/this/who brother to write the/this/who disciple to receive it/s/he which to come to ponder/confer much the/this/who to trust (in) through/because of the/this/who grace
28 Kwa uwezo mkubwa aliwakanusha hadharani Wayahudi waliokuwa wakipinga, akionyesha kwa njia ya Maandiko kwamba Yesu ndiye Kristo.
vehemently for the/this/who Jew to refute public to show/prove through/because of the/this/who a writing to exist the/this/who Christ Jesus

< Matendo 18 >