< Matendo 18 >
1 Baada ya haya, Paulo akaondoka Athene akaenda Korintho.
And after (now *k*) these things having departed (*k*) (Paul *K*) from Athens he came to Corinth,
2 Huko akakutana na Myahudi mmoja jina lake Akila, mwenyeji wa Ponto, ambaye alikuwa amewasili karibuni kutoka Italia pamoja na mkewe Prisila, kwa sababu Klaudio alikuwa ameamuru Wayahudi wote waondoke Rumi. Paulo akaenda kuwaona,
And having found a certain Jew named Aquila, of Pontus a native, recently having come from Italy, and Priscilla wife of him, because of (to have commanded *NK(o)*) Claudius to depart all the Jews (out of *N(k)O*) Rome, he came to them;
3 naye kwa kuwa alikuwa mtengeneza mahema kama wao, akakaa na kufanya kazi pamoja nao.
and due to of the same trade being he was staying with them and (he was working; *NK(O)*) they were for tentmakers (by trade; *N(k)O*)
4 Kila Sabato Paulo alikuwa akihojiana nao katika sinagogi, akijitahidi kuwashawishi Wayahudi na Wayunani.
he was reasoning now in the synagogue on every Sabbath, was persuading both Jews and Greeks.
5 Sila na Timotheo walipowasili kutoka Makedonia, walimkuta Paulo akiwa amejitolea muda wake wote katika kuhubiri, akiwashuhudia Wayahudi kwamba Yesu ndiye Kristo
When now came down from Macedonia both Silas and Timothy, was occupied with the (word *N(K)O*) Paul earnestly testifying to the Jews to be the Christ Jesus.
6 Wayahudi walipompinga Paulo na kukufuru, yeye aliyakungʼuta mavazi yake, akawaambia, “Damu yenu na iwe juu ya vichwa vyenu! Mimi sina hatia, nimetimiza wajibu wangu. Kuanzia sasa nitawaendea watu wa Mataifa.”
When are opposing however they and denigrating [him], having shaken out the garments he said to them; The blood of You [be] upon the head of you, clean I myself [am]; From now on to the Gentiles I will go.
7 Kisha akaondoka mle kwenye sinagogi, akaenda nyumbani kwa mtu mmoja jina lake Tito Yusto, aliyekuwa mcha Mungu. Nyumba yake ilikuwa karibu na sinagogi.
And having departed from there (he entered *N(k)O*) to [the] house of a certain one named (Titius *N(O)*) Justus worshiping the God, of whom the house was adjoining to the synagogue.
8 Kiongozi wa hilo sinagogi, aliyeitwa Krispo, akamwamini Bwana, yeye pamoja na watu wote wa nyumbani mwake. Nao Wakorintho wengi waliomsikia Paulo pia wakaamini na kubatizwa.
Crispus now the ruler of the synagogue believed in the Lord with all the household of him, And many of the Corinthians hearing were believing and were baptized.
9 Usiku mmoja Bwana akamwambia Paulo katika maono, “Usiogope, lakini endelea kusema wala usinyamaze,
Said now the Lord in [the] night through a vision to Paul; Not do fear but do continue speaking and not may be silent,
10 kwa maana mimi niko pamoja nawe, wala hakuna mtu atakayeweza kukushambulia ili kukudhuru, kwa kuwa ninao watu wengi katika mji huu ambao ni watu wangu.”
because I myself am with you, and no [one] will lay a hand on you to harm you; because people there is to me many in city this;
11 Hivyo Paulo akakaa huko kwa muda wa mwaka mmoja na nusu, akiwafundisha neno la Mungu.
He remained (now *N(k)O*) a year and months six teaching among them the word of God.
12 Lakini wakati Galio alipokuwa msaidizi wa mwakilishi wa mtawala huko Akaya, Wayahudi waliungana kumshambulia Paulo, wakamkamata na kumpeleka mahakamani.
When Gallio however proconsul being of Achaia rose up with one accord the Jews against Paul and led him to the judgment seat,
13 Wakamshtaki wakisema, “Mtu huyu anawashawishi watu wamwabudu Mungu kinyume cha sheria.”
saying that Contrary to the law persuades this [man] men to worship God.
14 Paulo alipotaka kujitetea, Galio akawaambia Wayahudi, “Kama ninyi Wayahudi mlikuwa mkilalamika kuhusu makosa makubwa ya uhalifu ingekuwa haki kwangu kuwasikiliza.
When is being about to now Paul to open [his] mouth said Gallio to the Jews; If indeed (therefore *K*) it was unrighteousness some or crime wicked, O Jews, according to reason would (I have endured with *N(k)O*) you;
15 Lakini kwa kuwa linahusu maneno, majina na sheria yenu, amueni ninyi wenyewe. Mimi sitakuwa mwamuzi wa mambo haya.”
if however (questions *N(K)O*) it is about a word and names and law of yours, you will behold [to it] yourselves; a judge (for *k*) I myself of these things not resolve to be.
16 Akawafukuza kutoka mahakamani.
And he drove them from the judgment seat.
17 Ndipo wote wakamkamata Sosthene kiongozi wa sinagogi, wakampiga mbele ya mahakama, lakini Galio hakujali kitendo chao hata kidogo.
Having seized then all [of them] (the Greeks *K*) Sosthenes the ruler of the synagogue they were beating [him] before the judgment seat; And no [thing] about these things to Gallio (was concerning. *NK(O)*)
18 Baada ya kukaa Korintho kwa muda, Paulo akaagana na wale ndugu walioamini, akasafiri kwa njia ya bahari kwenda Shamu akiwa amefuatana na Prisila na Akila. Walipofika Kenkrea, Paulo alinyoa nywele zake kwa kuwa alikuwa ameweka nadhiri.
Now Paul more having remained days many, of the brothers having taken leave he was sailing away to Syria — and with him Priscilla and Aquila — having shaved in Cenchrea the head; he had for a vow.
19 Walipofika Efeso, Paulo aliwaacha Prisila na Akila huko, lakini yeye akaingia kwenye sinagogi akawa anajadiliana na Wayahudi.
(They came *N(K)O*) now to Ephesus; and them and them left there, He himself then having entered into the synagogue (he reasoned *N(k)O*) with the Jews.
20 Walipomwomba akae nao kwa muda mrefu zaidi hakukubali.
When are asking now they for [him] a longer time to remain (with them *k*) not he did consent;
21 Lakini alipokuwa akiondoka, akaahidi, “Nitarudi kama Mungu akipenda.” Kisha akasafiri kwa njia ya bahari kutoka Efeso.
but (having taken leave *N(k)O*) (and *no*) (to them *k*) having said (necessary *KO*) (me by all means the feast which is coming to do into Jerusalem; *K*) Again (now *k*) I will return to you God willing, (and *k*) he sailed from Ephesus.
22 Alitia nanga Kaisaria, akaenda Yerusalemu na kulisalimu kanisa, kisha akaenda Antiokia.
and having landed at Caesarea, having gone up and having greeted the church he went down to Antioch;
23 Baada ya kukaa huko kwa muda, akaondoka na kwenda sehemu moja hadi nyingine huko Galatia na Frigia, akiwaimarisha wanafunzi wote.
And having stayed time some he went forth passing through successively the Galatian region and Phrygia, (strengthening *NK(o)*) all the disciples.
24 Basi akaja Efeso Myahudi mmoja, jina lake Apolo, mwenyeji wa Iskanderia. Yeye alikuwa na elimu kubwa, pia alikuwa hodari katika Maandiko.
A Jew now certain Apollos named, of Alexandria a native, a man eloquent, came to Ephesus mighty being in the Scriptures.
25 Alikuwa amefundishwa katika njia ya Bwana, naye alikuwa na bidii katika roho, akafundisha kwa usahihi juu ya Yesu, ingawa alijua tu ubatizo wa Yohana.
He was instructed [in] the way of the Lord, And being fervent in spirit he was speaking and he was teaching earnestly the [things] concerning (Jesus *N(K)O*) knowing only the baptism of John;
26 Apolo alianza kunena kwa ujasiri mkubwa katika sinagogi. Lakini Prisila na Akila walipomsikia, walimchukua kando na kumweleza njia ya Mungu kwa ufasaha zaidi.
He then began to speak boldly in the synagogue. Having heard however him Priscilla and Aquila they took to [them] him and more accurately to him they expounded the way of God.
27 Naye Apolo alipotaka kwenda Akaya, ndugu wa Efeso walimtia moyo, wakawaandikia wanafunzi huko ili wamkaribishe. Alipofika huko, aliwasaidia sana wale ambao, kwa neema ya Mungu, walikuwa wameamini.
When is resolving then he to pass through into Achaia, having encouraged [him] the brothers wrote to the disciples to welcome him; who having arrived he helped greatly those having believed through grace;
28 Kwa uwezo mkubwa aliwakanusha hadharani Wayahudi waliokuwa wakipinga, akionyesha kwa njia ya Maandiko kwamba Yesu ndiye Kristo.
Powerfully for the Jews he was refuting publicly showing through the Scriptures to be the Christ Jesus.