< Matendo 17 >
1 Wakasafiri kupitia Amfipoli na Apolonia wakafika Thesalonike, ambako kulikuwa na sinagogi la Wayahudi.
Torej ko sta šla skozi Amfípolo in Apolonijo sta prišla do Tesaloníke, kjer je bila judovska sinagoga.
2 Kama desturi yake, Paulo aliingia ndani ya sinagogi, na kwa muda wa Sabato tatu akawa anahojiana nao kutoka kwenye Maandiko,
In kakor je bila njegova navada, je Pavel vstopil k njim in tri šabatne dneve z njimi razpravljal iz pisem,
3 akidhihirisha wazi na kuthibitisha kwamba ilikuwa lazima Kristo ateswe na afufuke kutoka kwa wafu. Akasema, “Huyu Yesu ninayewaambia habari zake, ndiye Kristo.”
razkrival in trdil, da je Kristus brezpogojno moral trpeti in ponovno vstati od mrtvih in da je ta Jezus, ki vam ga oznanjam, Kristus.
4 Baadhi ya Wayahudi wakasadiki, wakaungana na Paulo na Sila, wakiwepo idadi kubwa ya Wayunani waliomcha Mungu na wanawake wengi mashuhuri.
In nekateri izmed njih so verovali in se družili s Pavlom in Silom, in velika množica izmed predanih Grkov ter ne malo izmed vodilnih žensk.
5 Lakini Wayahudi ambao hawakuwa wameamini wakawa na wivu, wakawakodi watu waovu kutoka sokoni, wakakutanisha umati wa watu, wakaanzisha ghasia mjini. Wakaenda mbio nyumbani kwa Yasoni wakiwatafuta Paulo na Sila ili kuwaleta nje penye ule umati wa watu.
Toda Judje, ki niso verovali, so prevzeti z zavistjo, vzeli k sebi neke ničvredne pajdaše iz prostaške sorte in zbrali skupino in po vsem mestu zanetili vstajo ter napadli Jazonovo hišo in si prizadevali, da ju privedejo k ljudstvu [dežele].
6 Lakini walipowakosa wakamburuta Yasoni na ndugu wengine mbele ya maafisa wa mji, wakipiga kelele: “Watu hawa ni wale walioupindua ulimwengu wamekuja huku,
Ko pa ju niso našli, so Jazona in neke brate odvlekli k vladarjem mesta ter kričali: »Tile, ki so obrnili svet na glavo, so prišli tudi sèm,
7 naye Yasoni amewakaribisha nyumbani mwake. Hawa wote wanaasi amri za Kaisari wakisema yuko mfalme mwingine aitwaye Yesu.”
ki jih je sprejel Jazon, in vsi ti delajo nasprotno cesarjevim odlokom, rekoč, da obstaja drug kralj, nek Jezus.«
8 Waliposikia haya, ule umati wa watu na maafisa wa mji wakaongeza ghasia.
In vznemirili so množico in mestne vladarje, ko so slišali te stvari.
9 Nao baada ya kuchukua dhamana kwa ajili ya Yasoni na wenzake wakawaacha waende zao.
In ko so od Jazona in od drugih prejeli varščino, so jih izpustili.
10 Usiku ule ule, wale ndugu walioamini wakawapeleka Paulo na Sila waende zao Beroya. Walipowasili huko wakaenda kwenye sinagogi la Wayahudi.
In bratje so Pavla ter Sila takoj ponoči odposlali v Berójo. Ko sta prispela tja, sta odšla v judovsko sinagogo.
11 Hawa Waberoya walikuwa waungwana zaidi kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa waliupokea ule ujumbe kwa shauku kubwa na kuyachunguza Maandiko kila siku ili kuona kama yale Paulo aliyosema yalikuwa kweli.
Ti so bili plemenitejši, kakor tisti v Tesaloníki, ker so z vso prisebnostjo sprejeli besedo in dnevno preiskovali pisma, če so bile te stvari take.
12 Wayahudi wengi wakaamini pamoja na wanawake na wanaume wa Kiyunani wa tabaka la juu.
Zato so mnogi izmed njih verovali, tudi častitljive ženske, ki so bile Grkinje in izmed mož ne malo.
13 Lakini wale Wayahudi wa Thesalonike waliposikia kuwa Paulo anahubiri neno la Mungu huko Beroya, wakaenda huko ili kuwashawishi watu na kuwachochea.
Toda ko so Judje iz Tesaloníke spoznali, da je Pavel Božjo besedo oznanjal v Beróji, so prišli tudi tja in razvneli množico.
14 Mara hiyo, wale ndugu wakamsafirisha Paulo hadi pwani, lakini Sila na Timotheo wakabaki Beroya.
In potem so bratje Pavla takoj odposlali, da gre, kot bi bilo k morju, toda Sila in Timótej sta še vedno ostala tam.
15 Wale waliomsindikiza Paulo wakaenda naye mpaka Athene, kisha wakarudi Beroya wakiwa na maagizo kutoka kwa Paulo kuhusu Sila na Timotheo kwamba wamfuate upesi iwezekanavyo.
In ti, ki so spremljali Pavla, so ga privedli v Atene in ko so prejeli zapoved za Sila in Timóteja, naj z vso naglico prideta k njemu, so odšli.
16 Paulo alipokuwa akiwasubiri huko Athene, alisumbuka sana moyoni mwake kuona vile mji huo ulivyojaa sanamu.
Torej medtem ko je Pavel v Atenah čakal nanju, je bil njegov duh v njem razvnet, ko je videl mesto v celoti predano malikovanju.
17 Hivyo akahojiana kwenye sinagogi na Wayahudi pamoja na Wayunani waliomcha Mungu, na pia sokoni kila siku na watu aliopatana nao huko.
Zato se je v sinagogi prerekal z Judi in s predanimi osebami in vsakodnevno na trgu s temi, ki so se srečevali z njim.
18 Kisha baadhi ya Waepikureo na Wastoiko wenye falsafa wakakutana naye. Baadhi yao wakasema, “Je, huyu mpayukaji anajaribu kusema nini?” Wengine wakasema, “Inaonekana anasema habari za miungu ya kigeni.” Walisema haya kwa sababu Paulo alikuwa anahubiri habari njema kuhusu Yesu na ufufuo wa wafu.
Potem so mu ugovarjali neki filozofi izmed epikurejcev in izmed stoikov. In nekateri so rekli: »Kaj hoče povedati ta blebetavec?« Drugi nekako: »Zdi se, da je oznanjevalec tujih bogov, « ker jim je oznanjal Jezusa in vstajenje.
19 Hivyo wakamchukua na kumleta kwenye mkutano wa Areopago, walikomwambia, “Je, tunaweza kujua mafundisho haya mapya unayofundisha ni nini?
In prijeli so ga ter ga privedli na Areopag, rekoč: »Ali lahko izvemo, kakšen je ta novi nauk, o katerem govoriš?«
20 Wewe unaleta mambo mapya masikioni mwetu, hivyo tungetaka kujua maana yake ni nini.”
Kajti v naša ušesa prinašaš nekatere čudne besede. Hočemo torej izvedeti, kaj te stvari pomenijo.
21 (Waathene na wageni wote walioishi humo hawakutumia muda wao kufanya chochote kingine isipokuwa kueleza au kusikia mambo mapya).
(Kajti vsi Atenci in tujci, ki so bili tam, svojega časa niso porabljali za nič drugega, razen da so ali govorili ali poslušali kako novo stvar.)
22 Ndipo Paulo akasimama katikati ya Areopago akasema, “Enyi watu wa Athene! Ninaona kwamba katika kila jambo ninyi ni watu wa dini sana.
Tedaj je Pavel na sredi Marsovega hriba vstal in rekel: » Vi atenski možje, zaznavam, da ste v vseh stvareh preveč vraževerni.
23 Kwa kuwa nilipokuwa nikitembea mjini na kuangalia kwa bidii vitu vyenu vya kuabudiwa, niliona huko madhabahu moja iliyoandikwa: Kwa Mungu Asiyejulikana. Basi sasa kile ambacho mmekuwa mkikiabudu kama kisichojulikana, ndicho ninachowahubiria.
Kajti ko sem šel mimo in gledal vaše predmete čaščenja, sem našel oltar s tem napisom: NEPOZNANEMU BOGU. Katerega torej vi nevedno obožujete, tega vam jaz razglašam.
24 “Mungu aliyeumba dunia na vyote vilivyomo ndani yake, yeye ndiye Bwana wa mbingu na nchi, hakai katika mahekalu yaliyojengwa kwa mikono ya wanadamu.
Bog, ki je naredil svet in vse stvari na njem, glede na to, da je on Gospodar neba in zemlje, ne prebiva v templjih, narejenimi z rokami,
25 Wala hatumikiwi na mikono ya wanadamu kana kwamba anahitaji chochote, kwa sababu yeye mwenyewe ndiye awapaye watu wote uhai na pumzi na vitu vyote.
tudi ni oboževan s človeškimi rokami, kakor da karkoli potrebuje, glede na to, da vsem daje življenje in dihanje in vse stvari
26 Kutoka kwa mtu mmoja, yeye aliumba mataifa yote ya wanadamu ili waikalie dunia yote, naye akaweka nyakati za kuishi.
in je iz ene krvi naredil vse narode ljudi, da prebivajo na vsem obličju zemlje in je vnaprej določil določene čase in meje njihovega prebivanja,
27 Mungu alifanya hivyo ili wanadamu wamtafute na huenda wakamfikia ingawa kwa kupapasapapasa ijapokuwa kwa kweli hakai mbali na kila mmoja wetu.
da bi iskali Gospoda, če bi ga morda dotipali in ga našli, čeprav ni daleč od vsakega izmed nas.
28 ‘Kwa kuwa katika yeye tunaishi, tunatembea na kuwa na uzima wetu.’ Kama baadhi ya watunga mashairi wenu walivyosema, ‘Sisi ni watoto wake.’
Kajti v njem živimo in se gibljemo in obstajamo, kakor so rekli celó nekateri izmed vaših lastnih pesnikov: ›Kajti tudi mi smo njegovo potomstvo.‹
29 “Kwa kuwa sisi ni watoto wa Mungu, haitupasi kudhani kuwa uungu ni kama sanamu ya dhahabu au ya fedha au ya jiwe, mfano uliotengenezwa kwa ubunifu na ustadi wa mwanadamu.
Kot smo torej zagotovo potomstvo Boga, ne bi smeli misliti, da je Božanstvo podobno zlatu ali srebru ali kamnu, vrezanemu od umetnika in [s] človeško pripravo.
30 Zamani wakati wa ujinga, Mungu alijifanya kama haoni, lakini sasa anawaamuru watu wote kila mahali watubu.
In nad časi te nevednosti je Bog zamižal, toda sedaj povsod vsem ljudem zapoveduje, da se pokesajo,
31 Kwa kuwa ameweka siku ambayo atauhukumu ulimwengu kwa haki akimtumia mtu aliyemchagua. Amewahakikishia watu wote mambo haya kwa kumfufua Kristo kutoka kwa wafu.”
kajti določil je dan, na katerega bo sodil svet v pravičnosti, po tem možu, ki ga je določil. O tem je dal zagotovilo vsem ljudem, ker ga je obudil od mrtvih.«
32 Waliposikia habari za ufufuo wa wafu, baadhi yao wakadhihaki, lakini wengine wakasema, “Tunataka kukusikia tena ukizungumza juu ya jambo hili.”
Ko pa so slišali o vstajenju mrtvih, so se nekateri posmehovali, drugi pa so rekli: »Oh tej zadevi te bomo ponovno poslušali.«
33 Kwa hiyo Paulo akaondoka katikati yao.
Tako je Pavel odšel izmed njih.
34 Lakini baadhi yao wakaungana naye wakaamini. Kati yao alikuwepo Dionisio, Mwareopago na mwanamke mmoja aliyeitwa Damari na wengine wengi.
Vendar so se mu določeni možje trdno pridružili in verovali, med katerimi je bil Dionizij Areopagít in ženska, po imenu Dámaris in drugi z njima.