< Matendo 17 >

1 Wakasafiri kupitia Amfipoli na Apolonia wakafika Thesalonike, ambako kulikuwa na sinagogi la Wayahudi.
And, travelling through Amphipolis and Apollonia, they came to Thessalonica, where was a synagogue of the Jews;
2 Kama desturi yake, Paulo aliingia ndani ya sinagogi, na kwa muda wa Sabato tatu akawa anahojiana nao kutoka kwenye Maandiko,
and, according to Paul’s custom, he went in unto them, and, for three sabbaths, reasoned with them from the Scriptures, —
3 akidhihirisha wazi na kuthibitisha kwamba ilikuwa lazima Kristo ateswe na afufuke kutoka kwa wafu. Akasema, “Huyu Yesu ninayewaambia habari zake, ndiye Kristo.”
opening up, and setting forth, that it was needful for, the Christ, to suffer, and to arise from among the dead; and [saying], This, is the Christ, —Jesus, whom, I, am declaring unto you.
4 Baadhi ya Wayahudi wakasadiki, wakaungana na Paulo na Sila, wakiwepo idadi kubwa ya Wayunani waliomcha Mungu na wanawake wengi mashuhuri.
And, some from among them, were persuaded, and cast in their lot with Paul and Silas; also, of the devout Greeks, a great throng, and, of the chief women, not a few.
5 Lakini Wayahudi ambao hawakuwa wameamini wakawa na wivu, wakawakodi watu waovu kutoka sokoni, wakakutanisha umati wa watu, wakaanzisha ghasia mjini. Wakaenda mbio nyumbani kwa Yasoni wakiwatafuta Paulo na Sila ili kuwaleta nje penye ule umati wa watu.
But the Jews, being, jealous, and taking unto themselves certain wicked men, of the rabble, and making a riot, were setting the city in an uproar; and, besieging the house of Jason, were seeking to lead them forth unto the populace, —
6 Lakini walipowakosa wakamburuta Yasoni na ndugu wengine mbele ya maafisa wa mji, wakipiga kelele: “Watu hawa ni wale walioupindua ulimwengu wamekuja huku,
and, not finding them, they began dragging Jason and certain brethren unto the city-rulers, shouting—They who have thrown the inhabited earth into confusion, the same, hither also, are come, —
7 naye Yasoni amewakaribisha nyumbani mwake. Hawa wote wanaasi amri za Kaisari wakisema yuko mfalme mwingine aitwaye Yesu.”
unto whom Jason hath given welcome; and, these all, contrary to the decrees of Caesar, are acting, —saying that there is another king, Jesus.
8 Waliposikia haya, ule umati wa watu na maafisa wa mji wakaongeza ghasia.
And they troubled the multitude and the city-rulers, when they heard these things;
9 Nao baada ya kuchukua dhamana kwa ajili ya Yasoni na wenzake wakawaacha waende zao.
and, taking security from Jason and the rest, they let them go.
10 Usiku ule ule, wale ndugu walioamini wakawapeleka Paulo na Sila waende zao Beroya. Walipowasili huko wakaenda kwenye sinagogi la Wayahudi.
But, the brethren, straightway, during the night, sent away both Paul and Silas unto Beroea, who, indeed, arriving, unto the synagogue of the Jews, went off;
11 Hawa Waberoya walikuwa waungwana zaidi kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa waliupokea ule ujumbe kwa shauku kubwa na kuyachunguza Maandiko kila siku ili kuona kama yale Paulo aliyosema yalikuwa kweli.
and, these, were more noble than those in Thessalonica, in that they welcomed the word with all readiness of mind, daily, searching the Scriptures, —whether these things could be so.
12 Wayahudi wengi wakaamini pamoja na wanawake na wanaume wa Kiyunani wa tabaka la juu.
Many, therefore, from among them, believed, and, of the Grecian women of the higher class, and of men, not a few.
13 Lakini wale Wayahudi wa Thesalonike waliposikia kuwa Paulo anahubiri neno la Mungu huko Beroya, wakaenda huko ili kuwashawishi watu na kuwachochea.
But, when the Jews from Thessalonica came to know that, in Beroea also, had the word of God been declared by Paul, they came thither also, stirring up and troubling the multitudes.
14 Mara hiyo, wale ndugu wakamsafirisha Paulo hadi pwani, lakini Sila na Timotheo wakabaki Beroya.
Howbeit, then, immediately, the brethren sent away, Paul, to be journeying as far as unto the sea; and both Silas and Timothy stayed behind, there.
15 Wale waliomsindikiza Paulo wakaenda naye mpaka Athene, kisha wakarudi Beroya wakiwa na maagizo kutoka kwa Paulo kuhusu Sila na Timotheo kwamba wamfuate upesi iwezekanavyo.
But, they who were conducting Paul, brought him as far as Athens, and, receiving a commandment unto Silas and Timothy, that with, all possible speed, they would come unto him, they departed.
16 Paulo alipokuwa akiwasubiri huko Athene, alisumbuka sana moyoni mwake kuona vile mji huo ulivyojaa sanamu.
But, while, in Athens, Paul was expecting them, his spirit within him was being urged on, seeing how the city was given to idols.
17 Hivyo akahojiana kwenye sinagogi na Wayahudi pamoja na Wayunani waliomcha Mungu, na pia sokoni kila siku na watu aliopatana nao huko.
So then, he began reasoning in the synagogue with the Jews, and with them who worshipped; and, in the market-place, every day, with them who happened to be at hand.
18 Kisha baadhi ya Waepikureo na Wastoiko wenye falsafa wakakutana naye. Baadhi yao wakasema, “Je, huyu mpayukaji anajaribu kusema nini?” Wengine wakasema, “Inaonekana anasema habari za miungu ya kigeni.” Walisema haya kwa sababu Paulo alikuwa anahubiri habari njema kuhusu Yesu na ufufuo wa wafu.
But, certain both of the Epicurean and of the Stoic philosophers, were encountering him; and some were saying—What might this picker-up-of-scraps wish to be saying? And, others—Of foreign demons, he seemeth to be a declarer: because, of Jesus and the Resurrection, he was announcing the joyful tidings.
19 Hivyo wakamchukua na kumleta kwenye mkutano wa Areopago, walikomwambia, “Je, tunaweza kujua mafundisho haya mapya unayofundisha ni nini?
And so, laying hold of him, they brought him up, to the Hill of Mars, saying—Can we get to know what this new teaching is, which, by thee, is being spoken.
20 Wewe unaleta mambo mapya masikioni mwetu, hivyo tungetaka kujua maana yake ni nini.”
For, certain foreign things, art thou bringing into our hearing: We are minded to get to know, therefore, what these things please to be!
21 (Waathene na wageni wote walioishi humo hawakutumia muda wao kufanya chochote kingine isipokuwa kueleza au kusikia mambo mapya).
Now, all Athenians and the sojourning foreigners, unto nothing else, were devoting their leisure, than to be telling or hearing, something newer.
22 Ndipo Paulo akasimama katikati ya Areopago akasema, “Enyi watu wa Athene! Ninaona kwamba katika kila jambo ninyi ni watu wa dini sana.
And Paul taking his stand in the midst of the Hill of Mars, said—Ye men of Athens! In every way, how unusually reverent of the demons ye are, I perceive.
23 Kwa kuwa nilipokuwa nikitembea mjini na kuangalia kwa bidii vitu vyenu vya kuabudiwa, niliona huko madhabahu moja iliyoandikwa: Kwa Mungu Asiyejulikana. Basi sasa kile ambacho mmekuwa mkikiabudu kama kisichojulikana, ndicho ninachowahubiria.
For, passing through, and carefully observing your objects of devotion, I found an altar also, in which was inscribed—Unto an Unknown God. What, therefore, not knowing, ye reverence, the same, do, I, declare unto you.
24 “Mungu aliyeumba dunia na vyote vilivyomo ndani yake, yeye ndiye Bwana wa mbingu na nchi, hakai katika mahekalu yaliyojengwa kwa mikono ya wanadamu.
The God that made the world and all things that are therein, the same, being, Lord, of heaven and earth, not in hand-made shrines, doth dwell,
25 Wala hatumikiwi na mikono ya wanadamu kana kwamba anahitaji chochote, kwa sababu yeye mwenyewe ndiye awapaye watu wote uhai na pumzi na vitu vyote.
nor, by human hands, is waited upon, as though in want of anything, himself, giving unto all life and breath and all things;
26 Kutoka kwa mtu mmoja, yeye aliumba mataifa yote ya wanadamu ili waikalie dunia yote, naye akaweka nyakati za kuishi.
he made also, of one, every nation of men to dwell upon all the face of the earth, —marking out fitting opportunities, and the bounds of their dwelling place,
27 Mungu alifanya hivyo ili wanadamu wamtafute na huenda wakamfikia ingawa kwa kupapasapapasa ijapokuwa kwa kweli hakai mbali na kila mmoja wetu.
that they might be seeking God—if, after all, indeed, they might feel after him and find him, —although, in truth, he is already not far from any one of us.
28 ‘Kwa kuwa katika yeye tunaishi, tunatembea na kuwa na uzima wetu.’ Kama baadhi ya watunga mashairi wenu walivyosema, ‘Sisi ni watoto wake.’
For, in him, we live and move and are: as, even some of your own poets, have said—For, his offspring also, we are.
29 “Kwa kuwa sisi ni watoto wa Mungu, haitupasi kudhani kuwa uungu ni kama sanamu ya dhahabu au ya fedha au ya jiwe, mfano uliotengenezwa kwa ubunifu na ustadi wa mwanadamu.
Being, then, offspring, of God, we ought not to be supposing that, unto gold or silver or stone, graven by art and device of man, the Divine, is like.
30 Zamani wakati wa ujinga, Mungu alijifanya kama haoni, lakini sasa anawaamuru watu wote kila mahali watubu.
The times of ignorance, therefore, overlooking, God, as things now are, is charging all men everywhere to repent,
31 Kwa kuwa ameweka siku ambayo atauhukumu ulimwengu kwa haki akimtumia mtu aliyemchagua. Amewahakikishia watu wote mambo haya kwa kumfufua Kristo kutoka kwa wafu.”
inasmuch as he hath appointed a day, in which he is about to be judging the habitable earth in righteousness, by a man whom he hath pointed out, —offering faith unto all, by raising him from among the dead?
32 Waliposikia habari za ufufuo wa wafu, baadhi yao wakadhihaki, lakini wengine wakasema, “Tunataka kukusikia tena ukizungumza juu ya jambo hili.”
Now, when they heard of raising the dead, some, indeed, began to mock, while, others, said—We will hear thee, concerning this, even again.
33 Kwa hiyo Paulo akaondoka katikati yao.
Thus, Paul, came forth out of their midst.
34 Lakini baadhi yao wakaungana naye wakaamini. Kati yao alikuwepo Dionisio, Mwareopago na mwanamke mmoja aliyeitwa Damari na wengine wengi.
But, certain persons, joining themselves unto him, believed; among whom were even Dionysius the Mars-hill judge, and a woman by name Damaris, and others with them.

< Matendo 17 >