< Matendo 17 >
1 Wakasafiri kupitia Amfipoli na Apolonia wakafika Thesalonike, ambako kulikuwa na sinagogi la Wayahudi.
A prošedše Amfipolim a Apollonii, přišli do Tessaloniky, kdež byla škola Židovská.
2 Kama desturi yake, Paulo aliingia ndani ya sinagogi, na kwa muda wa Sabato tatu akawa anahojiana nao kutoka kwenye Maandiko,
Tedy Pavel podlé obyčeje svého všel k nim, a po tři soboty kázal jim z písem,
3 akidhihirisha wazi na kuthibitisha kwamba ilikuwa lazima Kristo ateswe na afufuke kutoka kwa wafu. Akasema, “Huyu Yesu ninayewaambia habari zake, ndiye Kristo.”
Otvíraje a předkládaje to, že měl Kristus trpěti a z mrtvých vstáti, a že ten jest Kristus Ježíš, kteréhož já zvěstuji vám.
4 Baadhi ya Wayahudi wakasadiki, wakaungana na Paulo na Sila, wakiwepo idadi kubwa ya Wayunani waliomcha Mungu na wanawake wengi mashuhuri.
I uvěřili někteří z nich, a připojili se Pavlovi a Sílovi, i Řeků nábožných veliké množství, i žen znamenitých nemalo.
5 Lakini Wayahudi ambao hawakuwa wameamini wakawa na wivu, wakawakodi watu waovu kutoka sokoni, wakakutanisha umati wa watu, wakaanzisha ghasia mjini. Wakaenda mbio nyumbani kwa Yasoni wakiwatafuta Paulo na Sila ili kuwaleta nje penye ule umati wa watu.
Ale zažženi byvše závistí Židé nepovolní, a přivzavše k sobě některé lehkomyslné a nešlechetné lidi, a shlukše se, zbouřili město, a útok učinivše na dům Jázonův, hledali jich, aby je vyvedli před lid.
6 Lakini walipowakosa wakamburuta Yasoni na ndugu wengine mbele ya maafisa wa mji, wakipiga kelele: “Watu hawa ni wale walioupindua ulimwengu wamekuja huku,
A nenalezše jich, táhli Jázona a některé bratří k starším města, křičíce: Tito, kteříž všecken svět bouří, ti sem také přišli.
7 naye Yasoni amewakaribisha nyumbani mwake. Hawa wote wanaasi amri za Kaisari wakisema yuko mfalme mwingine aitwaye Yesu.”
Kteréž přijal Jázon. A ti všickni proti ustanovení císařskému činí, pravíce býti králem jiného, totiž Ježíše.
8 Waliposikia haya, ule umati wa watu na maafisa wa mji wakaongeza ghasia.
A tak zbouřili obec i starší města, kteříž to slyšeli.
9 Nao baada ya kuchukua dhamana kwa ajili ya Yasoni na wenzake wakawaacha waende zao.
Ale přijavše dosti učinění od Jázona a jiných, propustili je.
10 Usiku ule ule, wale ndugu walioamini wakawapeleka Paulo na Sila waende zao Beroya. Walipowasili huko wakaenda kwenye sinagogi la Wayahudi.
Bratří pak hned v noci vyslali i Pavla i Sílu do Berie. Kteříž přišedše tam, vešli do školy Židovské.
11 Hawa Waberoya walikuwa waungwana zaidi kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa waliupokea ule ujumbe kwa shauku kubwa na kuyachunguza Maandiko kila siku ili kuona kama yale Paulo aliyosema yalikuwa kweli.
A ti byli udatnější nežli Tessalonitští, kteříž přijali slovo Boží se vší chtivostí, na každý den rozvažujíce písma, tak-li by ty věci byly.
12 Wayahudi wengi wakaamini pamoja na wanawake na wanaume wa Kiyunani wa tabaka la juu.
A tak mnozí z nich uvěřili, i Řecké ženy poctivé i mužů nemalo.
13 Lakini wale Wayahudi wa Thesalonike waliposikia kuwa Paulo anahubiri neno la Mungu huko Beroya, wakaenda huko ili kuwashawishi watu na kuwachochea.
A když zvěděli Židé v Tessalonice, že by i v Berii kázáno bylo slovo Boží od Pavla, přišli také tam, bouříce zástupy.
14 Mara hiyo, wale ndugu wakamsafirisha Paulo hadi pwani, lakini Sila na Timotheo wakabaki Beroya.
Ale hned bratří vyslali Pavla, aby šel jako k moři; Sílas pak a Timoteus pozůstali tu.
15 Wale waliomsindikiza Paulo wakaenda naye mpaka Athene, kisha wakarudi Beroya wakiwa na maagizo kutoka kwa Paulo kuhusu Sila na Timotheo kwamba wamfuate upesi iwezekanavyo.
Ti pak, kteříž provodili Pavla, dovedli ho až do Atén. A vzavše poručení k Sílovi a k Timoteovi, aby přišli k němu, což nejspíše mohou, šli zase.
16 Paulo alipokuwa akiwasubiri huko Athene, alisumbuka sana moyoni mwake kuona vile mji huo ulivyojaa sanamu.
A když Pavel čekal jich v Atenách, rozněcoval se v něm duch jeho, vida to město oddané býti modloslužbě.
17 Hivyo akahojiana kwenye sinagogi na Wayahudi pamoja na Wayunani waliomcha Mungu, na pia sokoni kila siku na watu aliopatana nao huko.
I rozmlouval s Židy a nábožnými v škole, ano i na rynku, po všecky dni, s těmi, kteříž se koli nahodili.
18 Kisha baadhi ya Waepikureo na Wastoiko wenye falsafa wakakutana naye. Baadhi yao wakasema, “Je, huyu mpayukaji anajaribu kusema nini?” Wengine wakasema, “Inaonekana anasema habari za miungu ya kigeni.” Walisema haya kwa sababu Paulo alikuwa anahubiri habari njema kuhusu Yesu na ufufuo wa wafu.
Tedy někteří z Epikureů a Stoických mudrců hádali se s ním. A někteří řekli: I co tento žváč chce povědíti? Jiní pak: Zdá se býti cizích bohů zvěstovatel. Nebo jim o Ježíšovi a o z mrtvých vstání vypravoval.
19 Hivyo wakamchukua na kumleta kwenye mkutano wa Areopago, walikomwambia, “Je, tunaweza kujua mafundisho haya mapya unayofundisha ni nini?
I popadše jej, vedli ho do Areopágu, řkouce: Můžeme-li věděti, jaké jest to učení nové, kteréž vypravuješ?
20 Wewe unaleta mambo mapya masikioni mwetu, hivyo tungetaka kujua maana yake ni nini.”
Nebo nové jakési věci vkládáš v uši naše, protož chceme věděti, co by to bylo.
21 (Waathene na wageni wote walioishi humo hawakutumia muda wao kufanya chochote kingine isipokuwa kueleza au kusikia mambo mapya).
(Atenští zajisté všickni, i ti, kteříž tu byli hosté, k ničemu jinému tak hotovi nebyli, než praviti neb slyšeti něco nového.)
22 Ndipo Paulo akasimama katikati ya Areopago akasema, “Enyi watu wa Athene! Ninaona kwamba katika kila jambo ninyi ni watu wa dini sana.
Tedy Pavel, stoje u prostřed Areopágu, řekl: Muži Atenští, vidím vás býti všelijak příliš nábožné lidi.
23 Kwa kuwa nilipokuwa nikitembea mjini na kuangalia kwa bidii vitu vyenu vya kuabudiwa, niliona huko madhabahu moja iliyoandikwa: Kwa Mungu Asiyejulikana. Basi sasa kile ambacho mmekuwa mkikiabudu kama kisichojulikana, ndicho ninachowahubiria.
Nebo procházeje a spatřuje náboženství vaše, nalezl jsem také oltář, na kterémž napsáno jest: Neznámému Bohu. Protož kteréhož ctíte neznajíce, tohoť já zvěstuji vám.
24 “Mungu aliyeumba dunia na vyote vilivyomo ndani yake, yeye ndiye Bwana wa mbingu na nchi, hakai katika mahekalu yaliyojengwa kwa mikono ya wanadamu.
Bůh ten, kterýž stvořil svět i všecko, což jest na něm, ten jsa Pánem nebe i země, nebydlí v chrámích rukou udělaných;
25 Wala hatumikiwi na mikono ya wanadamu kana kwamba anahitaji chochote, kwa sababu yeye mwenyewe ndiye awapaye watu wote uhai na pumzi na vitu vyote.
Aniž bývá ctěn lidskýma rukama, jako by něčeho potřeboval, poněvadž on dává všechněm život i dýchání i všecko.
26 Kutoka kwa mtu mmoja, yeye aliumba mataifa yote ya wanadamu ili waikalie dunia yote, naye akaweka nyakati za kuishi.
A učinil z jedné krve všecko lidské pokolení, aby přebývalo na tváři vší země, vyměřiv jim uložené časy a cíle přebývání jejich,
27 Mungu alifanya hivyo ili wanadamu wamtafute na huenda wakamfikia ingawa kwa kupapasapapasa ijapokuwa kwa kweli hakai mbali na kila mmoja wetu.
Aby hledali Pána, zda by snad makajíce, mohli nalezti jej, ačkoli není daleko od jednoho každého z nás.
28 ‘Kwa kuwa katika yeye tunaishi, tunatembea na kuwa na uzima wetu.’ Kama baadhi ya watunga mashairi wenu walivyosema, ‘Sisi ni watoto wake.’
Nebo jím živi jsme, a hýbeme se, i trváme, jakož i někteří z vašich poetů pověděli: Že i rodina jeho jsme.
29 “Kwa kuwa sisi ni watoto wa Mungu, haitupasi kudhani kuwa uungu ni kama sanamu ya dhahabu au ya fedha au ya jiwe, mfano uliotengenezwa kwa ubunifu na ustadi wa mwanadamu.
Rodina tedy Boží jsouce, nemámeť se domnívati, že by Bůh zlatu neb stříbru neb kamenu, řemeslem aneb důvtipem lidským vyrytému, byl podoben.
30 Zamani wakati wa ujinga, Mungu alijifanya kama haoni, lakini sasa anawaamuru watu wote kila mahali watubu.
Nebo časy této neznámosti přehlídaje Bůh, již nyní zvěstuje lidem všechněm všudy, aby pokání činili,
31 Kwa kuwa ameweka siku ambayo atauhukumu ulimwengu kwa haki akimtumia mtu aliyemchagua. Amewahakikishia watu wote mambo haya kwa kumfufua Kristo kutoka kwa wafu.”
Proto že uložil den, v kterémž souditi bude všecken svět v spravedlnosti skrze toho muže, kteréhož k tomu vystavil, slouže k víře všechněm, vzkříšením jeho z mrtvých.
32 Waliposikia habari za ufufuo wa wafu, baadhi yao wakadhihaki, lakini wengine wakasema, “Tunataka kukusikia tena ukizungumza juu ya jambo hili.”
Uslyševše pak o vzkříšení z mrtvých, někteří se posmívali, a někteří řekli: Budeme tě slyšeti o tom podruhé.
33 Kwa hiyo Paulo akaondoka katikati yao.
A tak Pavel vyšel z prostředku jejich.
34 Lakini baadhi yao wakaungana naye wakaamini. Kati yao alikuwepo Dionisio, Mwareopago na mwanamke mmoja aliyeitwa Damari na wengine wengi.
Někteří pak muži, přídržíce se ho, uvěřili, mezi kterýmiž byl i Dionyzius Areopagitský, i žena, jménem Damaris, a jiní s nimi.