< Matendo 16 >
1 Paulo akafika Derbe na kisha Listra, ambako kulikuwa na mwanafunzi mmoja jina lake Timotheo, ambaye mama yake alikuwa Myahudi aliyeamini, lakini baba yake alikuwa Myunani.
Przybył do Derbe i Listry. A oto był tam pewien uczeń imieniem Tymoteusz, syn pewnej Żydówki, która uwierzyła, ojca natomiast Greka.
2 Alikuwa amesifiwa sana na wale ndugu waliokuwa wameamini huko Listra na Ikonio
Bracia z Listry i Ikonium dawali o nim [dobre] świadectwo.
3 Paulo alitaka Timotheo afuatane naye, hivyo akamchukua na kumtahiri kwa sababu ya Wayahudi waliokuwa wanaishi eneo lile kwa maana wote walimjua baba yake ni Myunani.
Paweł chciał go zabrać ze sobą, więc obrzezał go ze względu na Żydów, którzy mieszkali w tamtych stronach. Wszyscy bowiem wiedzieli, że jego ojciec był Grekiem.
4 Walipokuwa wakienda mji kwa mji, wakawa wanawapa maamuzi yaliyotolewa na mitume na wazee huko Yerusalemu ili wayafuate.
A gdy chodzili po miastach, przekazywali im nakazy ustanowione przez apostołów i starszych w Jerozolimie, których mieli przestrzegać.
5 Hivyo makanisa yakawa imara katika imani na kuongezeka kiidadi kila siku.
I tak kościoły utwierdzały się w wierze i każdego dnia wzrastały liczebnie.
6 Paulo pamoja na wenzake wakasafiri sehemu za Frigia na Galatia, kwa kuwa Roho Mtakatifu hakuwaruhusu kulihubiri neno huko Asia.
Gdy przeszli Frygię i krainę galacką, Duch Święty zabronił im głosić słowo [Boże] w Azji.
7 Walipofika mpaka wa Misia, wakajaribu kuingia Bithinia lakini Roho wa Yesu hakuwaruhusu.
Gdy przybyli do Myzji, próbowali pójść do Bitynii, ale im Duch nie pozwolił.
8 Kwa hiyo wakapita Misia, wakafika Troa.
Przeszli więc Myzję i zeszli do Troady.
9 Wakati wa usiku Paulo akaona maono, mtu wa Makedonia amesimama akimsihi, “Vuka uje huku Makedonia utusaidie.”
I w nocy Paweł miał widzenie: jakiś Macedończyk stał i prosił go: Przepraw się do Macedonii i pomóż nam!
10 Baada ya Paulo kuona maono haya, tulijiandaa kwa haraka kuondoka kwenda Makedonia tukiwa tumesadiki kuwa Mungu alikuwa ametuita kuhubiri habari njema huko.
Zaraz po tym widzeniu staraliśmy się wyruszyć do Macedonii, będąc tego pewni, że Pan nas powołał, abyśmy im głosili ewangelię.
11 Tukasafiri kwa njia ya bahari kutoka Troa na kwenda moja kwa moja hadi Samothrake, kesho yake tukafika Neapoli.
Odpłynąwszy więc z Troady, zdążaliśmy wprost do Samotraki, a nazajutrz do Neapolu;
12 Kutoka huko tukasafiri hadi Filipi, mji mkuu wa jimbo hilo la Makedonia, uliokuwa koloni ya Warumi. Nasi tukakaa huko siku kadhaa.
Stamtąd zaś do Filippi, [rzymskiej] kolonii i głównego miasta tej części Macedonii, i zostaliśmy w tym mieście przez kilka dni.
13 Siku ya Sabato tukaenda nje ya lango la mji kando ya mto, mahali ambapo tulitarajia tungepata mahali pa kufanyia maombi. Tukaketi, tukaanza kuongea na baadhi ya wanawake waliokuwa wamekusanyika huko.
A w dzień szabatu wyszliśmy za miasto nad rzekę, gdzie zwykle odbywały się modlitwy. Usiedliśmy i rozmawialiśmy z kobietami, które się [tam] zeszły.
14 Mmoja wa wale wanawake waliotusikiliza aliitwa Lidia, mfanyabiashara wa nguo za zambarau, mwenyeji wa mji wa Thiatira, aliyekuwa mcha Mungu. Bwana akaufungua moyo wake akaupokea ujumbe wa Paulo.
Przysłuchiwała się [temu] też pewna bogobojna kobieta, imieniem Lidia, z miasta Tiatyry, sprzedająca purpurę, której to serce otworzył Pan, aby uważnie słuchała tego, co mówił Paweł.
15 Basi alipokwisha kubatizwa yeye na watu wa nyumba yake, alitukaribisha nyumbani kwake akisema, “Kama mmeona kweli mimi nimemwamini Bwana, karibuni mkae nyumbani mwangu.” Naye akatushawishi.
A gdy została ochrzczona razem ze swoim domem, poprosiła: Jeśli uznaliście mnie za wierną Panu, wejdźcie do mojego domu i zamieszkajcie w nim. I wymogła to na nas.
16 Siku moja, tulipokuwa tukienda mahali pa kusali, tulikutana na mtumwa mmoja wa kike ambaye alikuwa na pepo wa uaguzi. Naye alikuwa amewapa mabwana zake mapato makubwa ya fedha kwa ubashiri.
I stało się, gdy szliśmy na modlitwę, że zabiegła nam [drogę] pewna dziewczyna, która miała ducha wieszczego i swoimi wróżbami przynosiła wielki dochód swoim panom.
17 Huyu msichana alikuwa akimfuata Paulo na sisi akipiga kelele, “Watu hawa ni watumishi wa Mungu Aliye Juu Sana, wao wanawatangazieni njia ya wokovu.”
A chodząc za Pawłem i za nami, wołała: Ci ludzie są sługami Boga Najwyższego i zwiastują nam drogę zbawienia.
18 Akaendelea kufanya hivi kwa siku nyingi, lakini Paulo akiwa ameudhika sana, akageuka na kumwambia yule pepo mchafu, “Ninakuamuru katika jina la Yesu Kristo, umtoke!” Yule pepo mchafu akamtoka saa ile ile.
A robiła to przez wiele dni. Lecz Paweł, bolejąc nad tym, odwrócił się i powiedział do ducha: Rozkazuję ci w imię Jezusa Chrystusa, abyś z niej wyszedł. I w tej chwili wyszedł.
19 Basi mabwana wa yule mtumwa wa kike walipoona kuwa tumaini lao la kuendelea kujipatia fedha limetoweka, wakawakamata Paulo na Sila wakawaburuta mpaka sokoni mbele ya viongozi wa mji.
Gdy jej panowie zobaczyli, że przepadła nadzieja ich zysku, schwytali Pawła i Sylasa, zawlekli ich na rynek przed władzę;
20 Baada ya kuwafikisha mbele ya mahakimu wakawashtaki wakisema, “Hawa watu wanaleta ghasia katika mji wetu, nao ni Wayahudi.
Stawili ich przed pretorami i powiedzieli: Ci ludzie, którzy są Żydami, sieją zamęt w naszym mieście.
21 Wanafundisha desturi ambazo sisi raiya wa Kirumi hatuwezi kuzikubali au kuzitimiza.”
I głoszą zwyczaje, których nam, jako Rzymianom, nie wolno przyjmować ani zachowywać.
22 Umati wa watu waliokuwepo wakajiunga katika kuwashambulia Paulo na Sila na wale mahakimu wakaamuru wavuliwe nguo zao na wachapwe viboko.
I wystąpił tłum przeciwko nim, a pretorzy zdarli z nich szaty i kazali wychłostać [ich] rózgami.
23 Baada ya kuwachapa sana, wakawatupa gerezani na kumwagiza mkuu wa gereza awalinde kikamilifu.
Po wymierzeniu wielu razów wtrącili [ich] do więzienia, przykazując strażnikowi, żeby ich dobrze pilnował.
24 Kufuata maelekezo haya, yule mkuu wa gereza akawaweka katika chumba cha ndani sana mle gerezani, na akawafunga miguu yao kwa minyororo.
Otrzymawszy taki rozkaz, wtrącił ich do wewnętrznego lochu, a ich nogi zakuł w dyby.
25 Ilipokaribia usiku wa manane, Paulo na Sila walikuwa wakiomba na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, nao wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza.
O północy Paweł i Sylas modlili się i śpiewem chwalili Boga, a więźniowie słyszeli ich.
26 Ghafula pakatokea tetemeko kubwa la ardhi, hata msingi wa gereza ukatikisika. Mara milango ya gereza ikafunguka na ile minyororo iliyowafunga kila mmoja ikafunguka.
Nagle powstało silne trzęsienie [ziemi], tak że zachwiały się fundamenty więzienia. I natychmiast otworzyły się wszystkie drzwi i wszystkim rozwiązały się więzy.
27 Yule mkuu wa gereza alipoamka na kuona milango ya gereza iko wazi, akachomoa upanga wake akataka kujiua, akidhani ya kuwa wafungwa wote wametoroka.
A gdy strażnik więzienia obudził się i zobaczył otwarte drzwi więzienia, dobył miecz i chciał się zabić, sądząc, że więźniowie pouciekali.
28 Lakini Paulo akapiga kelele kwa sauti kubwa, akasema, “Usijidhuru kwa maana sisi sote tuko hapa!”
Lecz Paweł zawołał donośnym głosem: Nie rób sobie nic złego, bo jesteśmy tu wszyscy.
29 Yule askari wa gereza akaagiza taa ziletwe, akaingia ndani ya kile chumba cha gereza, akapiga magoti akitetemeka mbele ya Paulo na Sila.
Wtedy zażądał światła i wskoczył do środka, a drżąc, padł [do nóg] Pawła i Sylasa.
30 Kisha akawaleta nje akisema, “Bwana zangu, nifanye nini nipate kuokoka?”
A wyprowadziwszy ich z więzienia, powiedział: Panowie, co mam czynić, abym był zbawiony?
31 Wakamjibu, “Mwamini Bwana Yesu Kristo, nawe utaokoka, pamoja na watu wa nyumbani mwako.”
A oni odpowiedzieli: Uwierz w Pana Jezusa Chrystusa, a będziesz zbawiony, ty i twój dom.
32 Wakamwambia neno la Bwana yeye pamoja na wote waliokuwako nyumbani mwake.
I głosili słowo Pańskie jemu i wszystkim jego domownikom.
33 Wakati ule ule, yule mkuu wa gereza akawachukua, akawaosha majeraha yao, kisha akabatizwa yeye pamoja na wote waliokuwa nyumbani mwake bila kuchelewa.
Tej samej godziny w nocy wziął [ich ze sobą], obmył ich rany i natychmiast się ochrzcił, on i wszyscy jego [domownicy].
34 Akawapandisha nyumbani mwake akawaandalia chakula, yeye pamoja na nyumba yake yote wakafurahi sana kwa kuwa sasa walikuwa wamemwamini Mungu.
Wprowadził ich do swego domu, zastawił [przed nimi] stół i weselił się, uwierzywszy Bogu z całym swoim domem.
35 Kulipopambazuka wale mahakimu wakawatuma maafisa wao kwa mkuu wa gereza wakiwa na agizo linalosema, “Wafungue wale watu, waache waende zao.”
Kiedy nastał dzień, pretorzy posłali służbę miejską ze słowami: Zwolnij tych ludzi.
36 Mkuu wa gereza akamwambia Paulo “Mahakimu wameagiza niwaache huru, kwa hiyo tokeni na mwende zenu kwa amani.”
I strażnik więzienia oznajmił Pawłowi: Pretorzy przysłali [polecenie], żeby was wypuścić. Teraz więc wyjdźcie i idźcie w pokoju.
37 Lakini Paulo akawaambia wale maafisa, “Wametupiga hadharani bila kutufanyia mashtaka na kutuhoji, nao wakatutupa gerezani, hata ingawa sisi ni raiya wa Rumi. Nao sasa wanataka kututoa gerezani kwa siri? Hapana! Wao na waje wenyewe watutoe humu gerezani.”
Lecz Paweł powiedział do nich: Publicznie, bez sądu biczowali i wtrącili do więzienia nas, obywateli rzymskich, a teraz potajemnie nas wyrzucają? Nic z tego! Niech sami przyjdą i wyprowadzą nas.
38 Wale maafisa wakarudi na kuwaambia wale mahakimu maneno haya, wakaogopa sana walipofahamu kuwa Paulo na Sila ni raiya wa Rumi.
Słudzy miejscy przekazali te słowa pretorom. A gdy [tamci] usłyszeli, że są Rzymianami, przestraszyli się.
39 Kwa hiyo wakaja wakawaomba msamaha, wakawatoa gerezani, wakawaomba waondoke katika ule mji.
Przyszli, przeprosili ich i wyprowadziwszy, prosili, aby opuścili miasto.
40 Baada ya Paulo na Sila kutoka gerezani walikwenda nyumbani kwa Lidia, ambapo walikutana na wale ndugu walioamini, wakawatia moyo, ndipo wakaondoka.
Kiedy wyszli z więzienia, wstąpili do [domu] Lidii, a gdy zobaczyli się z braćmi, pocieszyli ich i odeszli.