< Matendo 16 >
1 Paulo akafika Derbe na kisha Listra, ambako kulikuwa na mwanafunzi mmoja jina lake Timotheo, ambaye mama yake alikuwa Myahudi aliyeamini, lakini baba yake alikuwa Myunani.
Il arriva à Derbe et à Lystre. Et voici, il y avait là un disciple nommé Timothée, fils d'une Juive croyante, mais dont le père était Grec.
2 Alikuwa amesifiwa sana na wale ndugu waliokuwa wameamini huko Listra na Ikonio
Les frères qui étaient à Lystre et à Iconium rendaient sur lui un bon témoignage.
3 Paulo alitaka Timotheo afuatane naye, hivyo akamchukua na kumtahiri kwa sababu ya Wayahudi waliokuwa wanaishi eneo lile kwa maana wote walimjua baba yake ni Myunani.
Paul voulut l'emmener avec lui, et il le prit et le circoncit, à cause des Juifs qui étaient dans ces contrées; car tous savaient que son père était grec.
4 Walipokuwa wakienda mji kwa mji, wakawa wanawapa maamuzi yaliyotolewa na mitume na wazee huko Yerusalemu ili wayafuate.
Pendant qu'ils traversaient les villes, ils leur remettaient les décrets à observer, qui avaient été ordonnés par les apôtres et les anciens qui étaient à Jérusalem.
5 Hivyo makanisa yakawa imara katika imani na kuongezeka kiidadi kila siku.
Les assemblées étaient ainsi fortifiées dans la foi, et leur nombre augmentait chaque jour.
6 Paulo pamoja na wenzake wakasafiri sehemu za Frigia na Galatia, kwa kuwa Roho Mtakatifu hakuwaruhusu kulihubiri neno huko Asia.
Lorsqu'ils eurent traversé la région de la Phrygie et de la Galatie, l'Esprit Saint leur interdit d'annoncer la parole en Asie.
7 Walipofika mpaka wa Misia, wakajaribu kuingia Bithinia lakini Roho wa Yesu hakuwaruhusu.
Arrivés en face de la Mysie, ils essayèrent d'aller en Bithynie, mais l'Esprit ne le leur permit pas.
8 Kwa hiyo wakapita Misia, wakafika Troa.
Passant par Mysia, ils descendirent à Troas.
9 Wakati wa usiku Paulo akaona maono, mtu wa Makedonia amesimama akimsihi, “Vuka uje huku Makedonia utusaidie.”
Une vision apparut à Paul pendant la nuit. Il y avait là un homme de Macédoine, qui le suppliait et lui disait: « Passe en Macédoine et aide-nous. »
10 Baada ya Paulo kuona maono haya, tulijiandaa kwa haraka kuondoka kwenda Makedonia tukiwa tumesadiki kuwa Mungu alikuwa ametuita kuhubiri habari njema huko.
Après avoir eu cette vision, nous cherchâmes aussitôt à nous rendre en Macédoine, concluant que le Seigneur nous avait appelés à leur annoncer la Bonne Nouvelle.
11 Tukasafiri kwa njia ya bahari kutoka Troa na kwenda moja kwa moja hadi Samothrake, kesho yake tukafika Neapoli.
Partant donc de Troas, nous fîmes route directe vers Samothrace, puis le lendemain vers Néapolis,
12 Kutoka huko tukasafiri hadi Filipi, mji mkuu wa jimbo hilo la Makedonia, uliokuwa koloni ya Warumi. Nasi tukakaa huko siku kadhaa.
et de là vers Philippes, ville de Macédoine, la plus importante du district, colonie romaine. Nous séjournâmes quelques jours dans cette ville.
13 Siku ya Sabato tukaenda nje ya lango la mji kando ya mto, mahali ambapo tulitarajia tungepata mahali pa kufanyia maombi. Tukaketi, tukaanza kuongea na baadhi ya wanawake waliokuwa wamekusanyika huko.
Le jour du sabbat, nous nous rendîmes hors de la ville, au bord d'un fleuve, où nous pensions qu'il y avait un lieu de prière, et nous nous assîmes pour parler aux femmes qui s'étaient rassemblées.
14 Mmoja wa wale wanawake waliotusikiliza aliitwa Lidia, mfanyabiashara wa nguo za zambarau, mwenyeji wa mji wa Thiatira, aliyekuwa mcha Mungu. Bwana akaufungua moyo wake akaupokea ujumbe wa Paulo.
Une femme nommée Lydie, vendeuse de pourpre, de la ville de Thyatire, qui adorait Dieu, nous écouta. Le Seigneur lui ouvrit le cœur pour qu'elle écoute ce que disait Paul.
15 Basi alipokwisha kubatizwa yeye na watu wa nyumba yake, alitukaribisha nyumbani kwake akisema, “Kama mmeona kweli mimi nimemwamini Bwana, karibuni mkae nyumbani mwangu.” Naye akatushawishi.
Lorsqu'elle fut baptisée avec sa famille, elle nous supplia en disant: « Si vous m'avez jugée fidèle au Seigneur, venez dans ma maison et restez-y. » Elle nous a donc persuadés.
16 Siku moja, tulipokuwa tukienda mahali pa kusali, tulikutana na mtumwa mmoja wa kike ambaye alikuwa na pepo wa uaguzi. Naye alikuwa amewapa mabwana zake mapato makubwa ya fedha kwa ubashiri.
Comme nous allions prier, nous rencontrâmes une jeune fille douée d'un esprit de divination, qui rapportait beaucoup à ses maîtres en leur disant la bonne aventure.
17 Huyu msichana alikuwa akimfuata Paulo na sisi akipiga kelele, “Watu hawa ni watumishi wa Mungu Aliye Juu Sana, wao wanawatangazieni njia ya wokovu.”
Suivant Paul et nous, elle s'écriait: « Ces hommes sont des serviteurs du Dieu Très-Haut, qui nous annoncent un chemin de salut! »
18 Akaendelea kufanya hivi kwa siku nyingi, lakini Paulo akiwa ameudhika sana, akageuka na kumwambia yule pepo mchafu, “Ninakuamuru katika jina la Yesu Kristo, umtoke!” Yule pepo mchafu akamtoka saa ile ile.
Elle a agi ainsi pendant plusieurs jours. Mais Paul, très irrité, se retourne et dit à l'esprit: « Je t'ordonne, au nom de Jésus-Christ, de sortir d'elle. » Il sortit à l'heure même.
19 Basi mabwana wa yule mtumwa wa kike walipoona kuwa tumaini lao la kuendelea kujipatia fedha limetoweka, wakawakamata Paulo na Sila wakawaburuta mpaka sokoni mbele ya viongozi wa mji.
Mais, voyant que l'espoir de gain avait disparu, ses maîtres se saisirent de Paul et de Silas et les traînèrent sur la place publique devant les magistrats.
20 Baada ya kuwafikisha mbele ya mahakimu wakawashtaki wakisema, “Hawa watu wanaleta ghasia katika mji wetu, nao ni Wayahudi.
Les ayant amenés devant les magistrats, ceux-ci dirent: « Ces hommes, qui sont Juifs, agitent notre ville
21 Wanafundisha desturi ambazo sisi raiya wa Kirumi hatuwezi kuzikubali au kuzitimiza.”
et préconisent des coutumes qu'il ne nous est pas permis d'accepter ni d'observer, étant Romains. »
22 Umati wa watu waliokuwepo wakajiunga katika kuwashambulia Paulo na Sila na wale mahakimu wakaamuru wavuliwe nguo zao na wachapwe viboko.
La foule se souleva contre eux et les magistrats leur arrachèrent leurs vêtements, puis ils ordonnèrent qu'on les batte avec des verges.
23 Baada ya kuwachapa sana, wakawatupa gerezani na kumwagiza mkuu wa gereza awalinde kikamilifu.
Après leur avoir fait subir de nombreux coups de verges, ils les jetèrent en prison, en chargeant le geôlier de les garder en sécurité.
24 Kufuata maelekezo haya, yule mkuu wa gereza akawaweka katika chumba cha ndani sana mle gerezani, na akawafunga miguu yao kwa minyororo.
Ayant reçu cet ordre, il les jeta dans la prison intérieure et leur fixa les pieds dans les ceps.
25 Ilipokaribia usiku wa manane, Paulo na Sila walikuwa wakiomba na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, nao wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza.
Vers minuit, Paul et Silas priaient et chantaient des cantiques à Dieu, et les prisonniers les écoutaient.
26 Ghafula pakatokea tetemeko kubwa la ardhi, hata msingi wa gereza ukatikisika. Mara milango ya gereza ikafunguka na ile minyororo iliyowafunga kila mmoja ikafunguka.
Tout à coup, il se fit un grand tremblement de terre, en sorte que les fondements de la prison furent ébranlés; à l'instant même, toutes les portes s'ouvrirent, et les liens de chacun furent rompus.
27 Yule mkuu wa gereza alipoamka na kuona milango ya gereza iko wazi, akachomoa upanga wake akataka kujiua, akidhani ya kuwa wafungwa wote wametoroka.
Le geôlier, réveillé par le sommeil et voyant les portes de la prison ouvertes, tira son épée et allait se tuer, pensant que les prisonniers s'étaient échappés.
28 Lakini Paulo akapiga kelele kwa sauti kubwa, akasema, “Usijidhuru kwa maana sisi sote tuko hapa!”
Mais Paul cria d'une voix forte: « Ne te fais pas de mal, car nous sommes tous ici. »
29 Yule askari wa gereza akaagiza taa ziletwe, akaingia ndani ya kile chumba cha gereza, akapiga magoti akitetemeka mbele ya Paulo na Sila.
Il demanda des lumières, entra, se jeta en tremblant devant Paul et Silas,
30 Kisha akawaleta nje akisema, “Bwana zangu, nifanye nini nipate kuokoka?”
les fit sortir, et dit: « Messieurs, que dois-je faire pour être sauvé? »
31 Wakamjibu, “Mwamini Bwana Yesu Kristo, nawe utaokoka, pamoja na watu wa nyumbani mwako.”
Ils dirent: « Crois au Seigneur Jésus-Christ, et tu seras sauvé, toi et ta famille. »
32 Wakamwambia neno la Bwana yeye pamoja na wote waliokuwako nyumbani mwake.
Ils lui annoncèrent la parole du Seigneur, ainsi qu'à tous ceux qui étaient dans sa maison.
33 Wakati ule ule, yule mkuu wa gereza akawachukua, akawaosha majeraha yao, kisha akabatizwa yeye pamoja na wote waliokuwa nyumbani mwake bila kuchelewa.
Il les prit à l'heure même de la nuit, lava leurs plaies, et fut aussitôt baptisé, lui et toute sa famille.
34 Akawapandisha nyumbani mwake akawaandalia chakula, yeye pamoja na nyumba yake yote wakafurahi sana kwa kuwa sasa walikuwa wamemwamini Mungu.
Il les fit monter dans sa maison, leur servit à manger, et se réjouit beaucoup avec toute sa famille, parce qu'ils avaient cru en Dieu.
35 Kulipopambazuka wale mahakimu wakawatuma maafisa wao kwa mkuu wa gereza wakiwa na agizo linalosema, “Wafungue wale watu, waache waende zao.”
Mais quand le jour fut venu, les magistrats envoyèrent les sergents dire: « Laissez partir ces hommes. »
36 Mkuu wa gereza akamwambia Paulo “Mahakimu wameagiza niwaache huru, kwa hiyo tokeni na mwende zenu kwa amani.”
Le geôlier rapporta ces paroles à Paul, en disant: « Les magistrats ont envoyé te relâcher; sors donc et va en paix. »
37 Lakini Paulo akawaambia wale maafisa, “Wametupiga hadharani bila kutufanyia mashtaka na kutuhoji, nao wakatutupa gerezani, hata ingawa sisi ni raiya wa Rumi. Nao sasa wanataka kututoa gerezani kwa siri? Hapana! Wao na waje wenyewe watutoe humu gerezani.”
Mais Paul leur dit: « Ils nous ont battus publiquement sans jugement, des Romains, et ils nous ont jetés en prison! Vont-ils maintenant nous libérer secrètement? Non, très certainement, mais qu'ils viennent eux-mêmes et nous fassent sortir! ».
38 Wale maafisa wakarudi na kuwaambia wale mahakimu maneno haya, wakaogopa sana walipofahamu kuwa Paulo na Sila ni raiya wa Rumi.
Les sergents rapportèrent ces paroles aux magistrats, qui furent effrayés d'apprendre que c'étaient des Romains,
39 Kwa hiyo wakaja wakawaomba msamaha, wakawatoa gerezani, wakawaomba waondoke katika ule mji.
et ils vinrent les supplier. Lorsqu'ils les eurent fait sortir, ils les prièrent de quitter la ville.
40 Baada ya Paulo na Sila kutoka gerezani walikwenda nyumbani kwa Lidia, ambapo walikutana na wale ndugu walioamini, wakawatia moyo, ndipo wakaondoka.
Ils sortirent de la prison et entrèrent dans la maison de Lydie. Après avoir vu les frères, ils les encouragèrent, puis ils partirent.