< Matendo 16 >

1 Paulo akafika Derbe na kisha Listra, ambako kulikuwa na mwanafunzi mmoja jina lake Timotheo, ambaye mama yake alikuwa Myahudi aliyeamini, lakini baba yake alikuwa Myunani.
He also came to Derbe and to Lystra. At Lystra he found a disciple, Timothy by name--the son of a Christian Jewess, though he had a Greek father.
2 Alikuwa amesifiwa sana na wale ndugu waliokuwa wameamini huko Listra na Ikonio
Timothy was well spoken of by the brethren at Lystra and Iconium,
3 Paulo alitaka Timotheo afuatane naye, hivyo akamchukua na kumtahiri kwa sababu ya Wayahudi waliokuwa wanaishi eneo lile kwa maana wote walimjua baba yake ni Myunani.
and Paul desiring that he should accompany him on his journey, took him and circumcised him on account of the Jews in those parts, for they all knew that his father was a Greek.
4 Walipokuwa wakienda mji kwa mji, wakawa wanawapa maamuzi yaliyotolewa na mitume na wazee huko Yerusalemu ili wayafuate.
As they journeyed on from town to town, they handed to the brethren for their observance the decisions which had been arrived at by the Apostles and Elders in Jerusalem.
5 Hivyo makanisa yakawa imara katika imani na kuongezeka kiidadi kila siku.
So the Churches went on gaining a stronger faith and growing in numbers from day to day.
6 Paulo pamoja na wenzake wakasafiri sehemu za Frigia na Galatia, kwa kuwa Roho Mtakatifu hakuwaruhusu kulihubiri neno huko Asia.
Then Paul and his companions passed through Phrygia and Galatia, having been forbidden by the Holy Spirit to proclaim the Message in the province of Asia.
7 Walipofika mpaka wa Misia, wakajaribu kuingia Bithinia lakini Roho wa Yesu hakuwaruhusu.
When they reached the frontier of Mysia, they were about to enter Bithynia, but the Spirit of Jesus would not permit this.
8 Kwa hiyo wakapita Misia, wakafika Troa.
So, passing along Mysia, they came to Troas.
9 Wakati wa usiku Paulo akaona maono, mtu wa Makedonia amesimama akimsihi, “Vuka uje huku Makedonia utusaidie.”
Here, one night, Paul saw a vision. There was a Macedonian who was standing, entreating him and saying, "Come over into Macedonia and help us."
10 Baada ya Paulo kuona maono haya, tulijiandaa kwa haraka kuondoka kwenda Makedonia tukiwa tumesadiki kuwa Mungu alikuwa ametuita kuhubiri habari njema huko.
So when he had seen the vision, we immediately looked out for an opportunity of passing on into Macedonia, confidently inferring that God had called us to proclaim the Good News to the people there.
11 Tukasafiri kwa njia ya bahari kutoka Troa na kwenda moja kwa moja hadi Samothrake, kesho yake tukafika Neapoli.
Accordingly we put out to sea from Troas, and ran a straight course to Samothrace. The next day we came to Neapolis,
12 Kutoka huko tukasafiri hadi Filipi, mji mkuu wa jimbo hilo la Makedonia, uliokuwa koloni ya Warumi. Nasi tukakaa huko siku kadhaa.
and thence to Philippi, which is a city in Macedonia, the first in its district, a Roman colony. And there we stayed some little time.
13 Siku ya Sabato tukaenda nje ya lango la mji kando ya mto, mahali ambapo tulitarajia tungepata mahali pa kufanyia maombi. Tukaketi, tukaanza kuongea na baadhi ya wanawake waliokuwa wamekusanyika huko.
On the Sabbath we went beyond the city gate to the riverside, where we had reason to believe that there was a place for prayer; and sitting down we talked with the women who had come together.
14 Mmoja wa wale wanawake waliotusikiliza aliitwa Lidia, mfanyabiashara wa nguo za zambarau, mwenyeji wa mji wa Thiatira, aliyekuwa mcha Mungu. Bwana akaufungua moyo wake akaupokea ujumbe wa Paulo.
Among our hearers was one named Lydia, a dealer in purple goods. She belonged to the city of Thyateira, and was a worshipper of the true God. The Lord opened her heart, so that she gave attention to what Paul was saying.
15 Basi alipokwisha kubatizwa yeye na watu wa nyumba yake, alitukaribisha nyumbani kwake akisema, “Kama mmeona kweli mimi nimemwamini Bwana, karibuni mkae nyumbani mwangu.” Naye akatushawishi.
When she and her household had been baptized, she urged us, saying, "If in your judgement I am a believer in the Lord, come and stay at my house." And she made us go there.
16 Siku moja, tulipokuwa tukienda mahali pa kusali, tulikutana na mtumwa mmoja wa kike ambaye alikuwa na pepo wa uaguzi. Naye alikuwa amewapa mabwana zake mapato makubwa ya fedha kwa ubashiri.
One day, as we were on our way to the place of prayer, a slave girl met us who claimed to be inspired and was accustomed to bring her owners large profits by telling fortunes.
17 Huyu msichana alikuwa akimfuata Paulo na sisi akipiga kelele, “Watu hawa ni watumishi wa Mungu Aliye Juu Sana, wao wanawatangazieni njia ya wokovu.”
She kept following close behind Paul and the rest of us, crying aloud, "These men are the bondservants of the Most High God, and are proclaiming to you the way of salvation."
18 Akaendelea kufanya hivi kwa siku nyingi, lakini Paulo akiwa ameudhika sana, akageuka na kumwambia yule pepo mchafu, “Ninakuamuru katika jina la Yesu Kristo, umtoke!” Yule pepo mchafu akamtoka saa ile ile.
This she persisted in for a considerable time, until Paul, wearied out, turned round and said to the spirit, "I command you in the name of Jesus Christ to come out of her." And it came out immediately.
19 Basi mabwana wa yule mtumwa wa kike walipoona kuwa tumaini lao la kuendelea kujipatia fedha limetoweka, wakawakamata Paulo na Sila wakawaburuta mpaka sokoni mbele ya viongozi wa mji.
But when her owners saw that their hopes of gain were gone, they seized Paul and Silas and dragged them off to the magistrates in the public square.
20 Baada ya kuwafikisha mbele ya mahakimu wakawashtaki wakisema, “Hawa watu wanaleta ghasia katika mji wetu, nao ni Wayahudi.
Then they brought them before the praetors. "These men," they said, "are creating a great disturbance in our city.
21 Wanafundisha desturi ambazo sisi raiya wa Kirumi hatuwezi kuzikubali au kuzitimiza.”
They are Jews, and are teaching customs which we, as Romans, are not permitted to adopt or practise."
22 Umati wa watu waliokuwepo wakajiunga katika kuwashambulia Paulo na Sila na wale mahakimu wakaamuru wavuliwe nguo zao na wachapwe viboko.
The crowd, too, joined in the outcry against them, till at length the praetors ordered them to be stripped and beaten with rods;
23 Baada ya kuwachapa sana, wakawatupa gerezani na kumwagiza mkuu wa gereza awalinde kikamilifu.
and, after severely flogging them, they threw them into jail and bade the jailer keep them safely.
24 Kufuata maelekezo haya, yule mkuu wa gereza akawaweka katika chumba cha ndani sana mle gerezani, na akawafunga miguu yao kwa minyororo.
He, having received an order like that, lodged them in the inner prison, and secured their feet in the stocks.
25 Ilipokaribia usiku wa manane, Paulo na Sila walikuwa wakiomba na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, nao wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza.
About midnight Paul and Silas were praying and singing hymns to God, and the prisoners were listening to them,
26 Ghafula pakatokea tetemeko kubwa la ardhi, hata msingi wa gereza ukatikisika. Mara milango ya gereza ikafunguka na ile minyororo iliyowafunga kila mmoja ikafunguka.
when suddenly there was such a violent shock of earthquake that the prison shook to its foundations. Instantly the doors all flew open, and the chains fell off from every prisoner.
27 Yule mkuu wa gereza alipoamka na kuona milango ya gereza iko wazi, akachomoa upanga wake akataka kujiua, akidhani ya kuwa wafungwa wote wametoroka.
Starting up from sleep and seeing the doors of the jail wide open, the jailer drew his sword and was on the point of killing himself, supposing that the prisoners had escaped.
28 Lakini Paulo akapiga kelele kwa sauti kubwa, akasema, “Usijidhuru kwa maana sisi sote tuko hapa!”
But Paul shouted loudly to him, saying, "Do yourself no injury: we are all here.
29 Yule askari wa gereza akaagiza taa ziletwe, akaingia ndani ya kile chumba cha gereza, akapiga magoti akitetemeka mbele ya Paulo na Sila.
Then, calling for lights, he sprang in and fell trembling at the feet of Paul and Silas;
30 Kisha akawaleta nje akisema, “Bwana zangu, nifanye nini nipate kuokoka?”
and, bringing them out of the prison, he exclaimed, "O sirs, what must I do to be saved?"
31 Wakamjibu, “Mwamini Bwana Yesu Kristo, nawe utaokoka, pamoja na watu wa nyumbani mwako.”
"Believe on the Lord Jesus," they replied, "and both you and your household will be saved."
32 Wakamwambia neno la Bwana yeye pamoja na wote waliokuwako nyumbani mwake.
And they told the Lord's Message to him as well as to all who were in his house.
33 Wakati ule ule, yule mkuu wa gereza akawachukua, akawaosha majeraha yao, kisha akabatizwa yeye pamoja na wote waliokuwa nyumbani mwake bila kuchelewa.
Then he took them, even at that time of night, washed their wounds, and he and all his household were immediately baptized;
34 Akawapandisha nyumbani mwake akawaandalia chakula, yeye pamoja na nyumba yake yote wakafurahi sana kwa kuwa sasa walikuwa wamemwamini Mungu.
and bringing the Apostles up into his house, he spread a meal for them, and was filled with gladness, with his whole household, his faith resting on God.
35 Kulipopambazuka wale mahakimu wakawatuma maafisa wao kwa mkuu wa gereza wakiwa na agizo linalosema, “Wafungue wale watu, waache waende zao.”
In the morning the praetors sent their lictors with the order, "Release those men."
36 Mkuu wa gereza akamwambia Paulo “Mahakimu wameagiza niwaache huru, kwa hiyo tokeni na mwende zenu kwa amani.”
So the jailer brought Paul word, saying, "The praetors have sent orders for you to be released. Now therefore you can go, and proceed on your way in peace."
37 Lakini Paulo akawaambia wale maafisa, “Wametupiga hadharani bila kutufanyia mashtaka na kutuhoji, nao wakatutupa gerezani, hata ingawa sisi ni raiya wa Rumi. Nao sasa wanataka kututoa gerezani kwa siri? Hapana! Wao na waje wenyewe watutoe humu gerezani.”
But Paul said to them, "After cruelly beating us in public, without trial, Roman citizens though we are, they have thrown us into prison, and are they now going to send us away privately? No, indeed! Let them come in person and fetch us out."
38 Wale maafisa wakarudi na kuwaambia wale mahakimu maneno haya, wakaogopa sana walipofahamu kuwa Paulo na Sila ni raiya wa Rumi.
This answer the lictors took back to the praetors, who were alarmed when they were told that Paul and Silas were Roman citizens.
39 Kwa hiyo wakaja wakawaomba msamaha, wakawatoa gerezani, wakawaomba waondoke katika ule mji.
Accordingly they came and apologized to them; and, bringing them out, asked them to leave the city.
40 Baada ya Paulo na Sila kutoka gerezani walikwenda nyumbani kwa Lidia, ambapo walikutana na wale ndugu walioamini, wakawatia moyo, ndipo wakaondoka.
Then Paul and Silas, having come out of the prison, went to Lydia's house; and, after seeing the brethren and encouraging them, they left Philippi.

< Matendo 16 >