< Matendo 16 >
1 Paulo akafika Derbe na kisha Listra, ambako kulikuwa na mwanafunzi mmoja jina lake Timotheo, ambaye mama yake alikuwa Myahudi aliyeamini, lakini baba yake alikuwa Myunani.
Přišel pak do Derben a do Lystry, aj, učedlník jeden tu byl, jménem Timoteus, syn nějaké ženy Židovky věřící, ale otce měl Řeka.
2 Alikuwa amesifiwa sana na wale ndugu waliokuwa wameamini huko Listra na Ikonio
Tomu svědectví vydávali bratří ti, kteříž byli v Lystře a v Ikonii.
3 Paulo alitaka Timotheo afuatane naye, hivyo akamchukua na kumtahiri kwa sababu ya Wayahudi waliokuwa wanaishi eneo lile kwa maana wote walimjua baba yake ni Myunani.
Toho sobě oblíbil Pavel, aby s ním šel. I pojav ho, obřezal jej, pro Židy, kteříž byli v těch místech; nebo věděli všickni, že otec jeho byl Řek.
4 Walipokuwa wakienda mji kwa mji, wakawa wanawapa maamuzi yaliyotolewa na mitume na wazee huko Yerusalemu ili wayafuate.
A když chodili po městech, vydávali jim k ostříhání ustanovení zřízená od apoštolů a od starších, kteříž byli v Jeruzalémě.
5 Hivyo makanisa yakawa imara katika imani na kuongezeka kiidadi kila siku.
A tak církve utvrzovaly se u víře, a rozmáhaly se v počtu na každý den.
6 Paulo pamoja na wenzake wakasafiri sehemu za Frigia na Galatia, kwa kuwa Roho Mtakatifu hakuwaruhusu kulihubiri neno huko Asia.
A prošedše Frygii i Galatskou krajinu, když jim zabráněno od Ducha svatého, aby nemluvili slova v Azii,
7 Walipofika mpaka wa Misia, wakajaribu kuingia Bithinia lakini Roho wa Yesu hakuwaruhusu.
Přišedše do Myzie, pokoušeli se jíti do Bitynie. Ale nedal jim Duch.
8 Kwa hiyo wakapita Misia, wakafika Troa.
Tedy pominuvše Myzii, šli do Troady.
9 Wakati wa usiku Paulo akaona maono, mtu wa Makedonia amesimama akimsihi, “Vuka uje huku Makedonia utusaidie.”
I ukázalo se Pavlovi v noci vidění. Muž nějaký Macedonský stál, prose ho a řka: Přijda do Macedonie, pomoz nám.
10 Baada ya Paulo kuona maono haya, tulijiandaa kwa haraka kuondoka kwenda Makedonia tukiwa tumesadiki kuwa Mungu alikuwa ametuita kuhubiri habari njema huko.
A jakž to vidění viděl, i hned jsme usilovali o to, abychom šli do Macedonie, tím ujištěni jsouce, že nás povolal Pán, abychom jim kázali evangelium.
11 Tukasafiri kwa njia ya bahari kutoka Troa na kwenda moja kwa moja hadi Samothrake, kesho yake tukafika Neapoli.
Protož pustivše se od Troady, přímým během připlavili jsme se do Samotracie, a nazejtří do Neapolis,
12 Kutoka huko tukasafiri hadi Filipi, mji mkuu wa jimbo hilo la Makedonia, uliokuwa koloni ya Warumi. Nasi tukakaa huko siku kadhaa.
A odtud do Filippis, kteréž jest první město krajiny Macedonské, obyvateli cizími osazené. I zůstali jsme v tom městě za několik dní.
13 Siku ya Sabato tukaenda nje ya lango la mji kando ya mto, mahali ambapo tulitarajia tungepata mahali pa kufanyia maombi. Tukaketi, tukaanza kuongea na baadhi ya wanawake waliokuwa wamekusanyika huko.
V den pak sobotní vyšli jsme ven za město k řece, kdež býval obyčej modliti se. A usadivše se, mluvili jsme ženám, kteréž se tu byly sešly.
14 Mmoja wa wale wanawake waliotusikiliza aliitwa Lidia, mfanyabiashara wa nguo za zambarau, mwenyeji wa mji wa Thiatira, aliyekuwa mcha Mungu. Bwana akaufungua moyo wake akaupokea ujumbe wa Paulo.
Jedna pak žena, jménem Lydia, kteráž šarlaty prodávala v městě Tyatirských, bohabojící, poslouchala. Jejíž srdce otevřel Pán, aby to pilně rozsuzovala, co se od Pavla pravilo.
15 Basi alipokwisha kubatizwa yeye na watu wa nyumba yake, alitukaribisha nyumbani kwake akisema, “Kama mmeona kweli mimi nimemwamini Bwana, karibuni mkae nyumbani mwangu.” Naye akatushawishi.
A když pokřtěna byla i dům její, prosila, řkuci: Poněvadž jste mne soudili věrnou Pánu býti, vejdouce, v domě mém pobuďte. I přinutila nás.
16 Siku moja, tulipokuwa tukienda mahali pa kusali, tulikutana na mtumwa mmoja wa kike ambaye alikuwa na pepo wa uaguzi. Naye alikuwa amewapa mabwana zake mapato makubwa ya fedha kwa ubashiri.
I stalo se, když jsme šli k modlitbě, že děvečka nějaká, mající ducha věštího, potkala se s námi, kteráž veliký užitek přinášela pánům svým budoucích věcí předpovídáním.
17 Huyu msichana alikuwa akimfuata Paulo na sisi akipiga kelele, “Watu hawa ni watumishi wa Mungu Aliye Juu Sana, wao wanawatangazieni njia ya wokovu.”
Ta šedši za Pavlem a za námi, volala, řkuci: Tito lidé jsou služebníci Boha nejvyššího, kteříž zvěstují nám cestu spasení.
18 Akaendelea kufanya hivi kwa siku nyingi, lakini Paulo akiwa ameudhika sana, akageuka na kumwambia yule pepo mchafu, “Ninakuamuru katika jina la Yesu Kristo, umtoke!” Yule pepo mchafu akamtoka saa ile ile.
A to činívala za mnoho dní. Pavel pak těžce to nesa, a obrátiv se, řekl duchu tomu: Přikazuji tobě ve jménu Ježíše Krista, abys vyšel z ní. I vyšel hned té chvíle.
19 Basi mabwana wa yule mtumwa wa kike walipoona kuwa tumaini lao la kuendelea kujipatia fedha limetoweka, wakawakamata Paulo na Sila wakawaburuta mpaka sokoni mbele ya viongozi wa mji.
A viděvše páni její, že odešla naděje zisku jejich, chytivše Pavla a Sílu, vedli je na rynk před úřad.
20 Baada ya kuwafikisha mbele ya mahakimu wakawashtaki wakisema, “Hawa watu wanaleta ghasia katika mji wetu, nao ni Wayahudi.
A postavivše je před úředníky, řekli: Tito lidé bouří město naše, jsouce Židé,
21 Wanafundisha desturi ambazo sisi raiya wa Kirumi hatuwezi kuzikubali au kuzitimiza.”
A zvěstují obyčeje, kterýchž nám nesluší přijíti ani zachovávati, poněvadž jsme Římané.
22 Umati wa watu waliokuwepo wakajiunga katika kuwashambulia Paulo na Sila na wale mahakimu wakaamuru wavuliwe nguo zao na wachapwe viboko.
I povstala obec proti nim. A úředníci, roztrhše sukně jejich, kázali je metlami mrskati.
23 Baada ya kuwachapa sana, wakawatupa gerezani na kumwagiza mkuu wa gereza awalinde kikamilifu.
A množství ran jim davše, vsadili do žaláře, přikázavše strážnému žaláře, aby jich pilně ostříhal.
24 Kufuata maelekezo haya, yule mkuu wa gereza akawaweka katika chumba cha ndani sana mle gerezani, na akawafunga miguu yao kwa minyororo.
Tedy on takové maje přikázaní, vsadil je do nejhlubšího žaláře, a nohy jejich sevřel kladou.
25 Ilipokaribia usiku wa manane, Paulo na Sila walikuwa wakiomba na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, nao wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza.
O půlnoci pak Pavel a Sílas modléce se, zpívali písničky o Bohu, tak že je slyšeli vězňové.
26 Ghafula pakatokea tetemeko kubwa la ardhi, hata msingi wa gereza ukatikisika. Mara milango ya gereza ikafunguka na ile minyororo iliyowafunga kila mmoja ikafunguka.
A v tom pojednou země třesení stalo se veliké, až se pohnuli gruntové žaláře, a hned se všecky dvéře otevřely, a všech okovové spadli.
27 Yule mkuu wa gereza alipoamka na kuona milango ya gereza iko wazi, akachomoa upanga wake akataka kujiua, akidhani ya kuwa wafungwa wote wametoroka.
A procítiv strážný žaláře, a viděv dvéře žaláře otevřené, vytrhl meč, aby se zabil, domnívaje se, že vězňové utekli.
28 Lakini Paulo akapiga kelele kwa sauti kubwa, akasema, “Usijidhuru kwa maana sisi sote tuko hapa!”
I zkřikl Pavel hlasem velikým, řka: Nečiň sobě nic zlého, však jsme teď všickni.
29 Yule askari wa gereza akaagiza taa ziletwe, akaingia ndani ya kile chumba cha gereza, akapiga magoti akitetemeka mbele ya Paulo na Sila.
A požádav světla, vběhl k nim, a třesa se, padl u Pavla a Síly.
30 Kisha akawaleta nje akisema, “Bwana zangu, nifanye nini nipate kuokoka?”
I vyved je ven, řekl: Páni, co já mám činiti, abych spasen byl?
31 Wakamjibu, “Mwamini Bwana Yesu Kristo, nawe utaokoka, pamoja na watu wa nyumbani mwako.”
A oni řekli: Věř v Pána Ježíše Krista, a budeš spasen ty i dům tvůj.
32 Wakamwambia neno la Bwana yeye pamoja na wote waliokuwako nyumbani mwake.
I mluvili jemu slovo Páně, i všechněm, kteříž byli v domě jeho.
33 Wakati ule ule, yule mkuu wa gereza akawachukua, akawaosha majeraha yao, kisha akabatizwa yeye pamoja na wote waliokuwa nyumbani mwake bila kuchelewa.
A pojav je v tu hodinu v noci, umyl jim rány. I pokřtěn jest hned on i všickni domácí jeho.
34 Akawapandisha nyumbani mwake akawaandalia chakula, yeye pamoja na nyumba yake yote wakafurahi sana kwa kuwa sasa walikuwa wamemwamini Mungu.
A když je uvedl do domu svého, připravil stůl, a veselil se, že se vším domem svým uvěřil Bohu.
35 Kulipopambazuka wale mahakimu wakawatuma maafisa wao kwa mkuu wa gereza wakiwa na agizo linalosema, “Wafungue wale watu, waache waende zao.”
A když bylo ve dne, poslali úředníci služebníky, řkouce: Vypusť ty lidi.
36 Mkuu wa gereza akamwambia Paulo “Mahakimu wameagiza niwaache huru, kwa hiyo tokeni na mwende zenu kwa amani.”
I oznámil strážný žaláře slova ta Pavlovi: Že poslali úředníci, abyste byli propuštěni. Protož nyní vyjdouce, jdětež v pokoji.
37 Lakini Paulo akawaambia wale maafisa, “Wametupiga hadharani bila kutufanyia mashtaka na kutuhoji, nao wakatutupa gerezani, hata ingawa sisi ni raiya wa Rumi. Nao sasa wanataka kututoa gerezani kwa siri? Hapana! Wao na waje wenyewe watutoe humu gerezani.”
Ale Pavel řekl jim: Zmrskavše nás zjevně a bez vyslyšení, lidi Římany, vsázeli do žaláře, a nyní nás chtějí tajně vyhnati? Nikoli, ale nechať sami přijdou, a vyvedou nás.
38 Wale maafisa wakarudi na kuwaambia wale mahakimu maneno haya, wakaogopa sana walipofahamu kuwa Paulo na Sila ni raiya wa Rumi.
Tedy pověděli úředníkům služebníci slova ta. I báli se, uslyšavše, že by Římané byli.
39 Kwa hiyo wakaja wakawaomba msamaha, wakawatoa gerezani, wakawaomba waondoke katika ule mji.
A přišedše, prosili jich; a vyvedše je, žádali jich, aby šli z města.
40 Baada ya Paulo na Sila kutoka gerezani walikwenda nyumbani kwa Lidia, ambapo walikutana na wale ndugu walioamini, wakawatia moyo, ndipo wakaondoka.
I vyšedše z žaláře, vešli k Lydii, a uzřevše bratří, potěšili jich, a odešli.