< Matendo 15 >

1 Baadhi ya watu wakashuka Antiokia kutoka Uyahudi, nao wakawa wanawafundisha wandugu: “Msipotahiriwa kufuatana na desturi aliyofundisha Mose, hamwezi kuokoka.”
A niektórzy przybysze z Judei nauczali braci: Jeśli nie zostaniecie obrzezani według zwyczaju Mojżesza, nie możecie być zbawieni.
2 Baada ya Paulo na Barnaba kutokubaliana nao kukawa na mabishano makali, Paulo na Barnaba na baadhi ya wengine miongoni mwao wakachaguliwa kwenda Yerusalemu ili kujadiliana jambo hili na mitume na wazee.
Kiedy doszło do niemałych sporów i zatargów między nimi a Pawłem i Barnabą, postanowili, że Paweł i Barnaba oraz jeszcze kilku z nich pójdą w sprawie tego sporu do apostołów i starszych do Jerozolimy.
3 Hivyo wakasafirishwa na kanisa, wakiwa njiani wakapitia nchi ya Foinike na Samaria, wakawaeleza jinsi watu wa Mataifa walivyookoka. Habari hizi zikaleta furaha kubwa kwa ndugu wote.
Wyprawieni przez kościół, szli przez Fenicję i Samarię, opowiadając o nawróceniu pogan, czym sprawili wielką radość wszystkim braciom.
4 Walipofika Yerusalemu, walipokelewa na kanisa na mitume pamoja na wazee, ndipo Paulo na Barnaba wakawaarifu kila kitu Mungu alichokuwa amefanya kupitia kwao.
A gdy przybyli do Jerozolimy, zostali przyjęci przez kościół, apostołów i starszych. I opowiedzieli o wszystkim, czego Bóg przez nich dokonał.
5 Ndipo baadhi ya walioamini wa madhehebu ya Mafarisayo wakasimama na kusema, “Hao watu wa Mataifa lazima watahiriwe na waagizwe kutii sheria ya Mose.”
Lecz niektórzy ze stronnictwa faryzeuszy, którzy uwierzyli, powstali i powiedzieli: Trzeba ich obrzezać i nakazać, żeby zachowywali Prawo Mojżesza.
6 Mitume na wazee wakakutana pamoja ili kufikiri jambo hili.
Apostołowie i starsi zebrali się więc, aby rozstrzygnąć tę sprawę.
7 Baada ya majadiliano mengi, Petro akasimama na kusema, “Ndugu zangu, mnajua kwamba siku za kwanza Mungu alinichagua ili kwa midomo yangu watu wa Mataifa wapate kusikia ujumbe wa Injili na kuamini.
A gdy był wielki spór [o to], Piotr powstał i powiedział do nich: Mężowie bracia, wiecie, że Bóg już dawno wybrał [mnie] spośród was, aby z moich ust poganie usłyszeli słowa ewangelii i uwierzyli.
8 Mungu, yeye ajuaye mioyo, alionyesha kwamba anawakubali kwa kuwapa Roho Mtakatifu kama vile alivyotupa sisi.
A Bóg, który zna serca, wydał im świadectwo, dając im Ducha Świętego, tak samo jak nam.
9 Mungu hakutofautisha kati yetu na wao, bali alitakasa mioyo yao kwa imani.
I nie uczynił [żadnej] różnicy między nami a nimi, oczyszczając przez wiarę ich serca.
10 Sasa basi, mbona mnataka kumjaribu Mungu kwa kuweka kongwa shingoni mwa wanafunzi ambalo baba zetu wala sisi hatukuweza kulibeba?
Dlaczego więc teraz wystawiacie Boga na próbę, wkładając na kark uczniów jarzmo, którego ani nasi ojcowie, ani my nie mogliśmy udźwignąć?
11 Lakini sisi tunaamini ya kuwa tunaokolewa kwa neema ya Bwana Yesu Kristo, kama wao wanavyookolewa.”
Lecz wierzymy, że przez łaskę Pana Jezusa Chrystusa będziemy zbawieni, tak samo i oni.
12 Kusanyiko lote likakaa kimya, wakawasikiliza Paulo na Barnaba wakieleza jinsi Mungu alivyowatumia kutenda ishara na maajabu kwa watu wa Mataifa.
I całe zgromadzenie umilkło, a [potem] słuchali Barnaby i Pawła, którzy opowiadali, jak wielkie znaki i cuda Bóg uczynił przez nich wśród pogan.
13 Walipomaliza kunena, Yakobo akasema, “Ndugu zangu, nisikilizeni.
A gdy i oni umilkli, odezwał się Jakub: Mężowie bracia, posłuchajcie mnie.
14 Simoni amekwisha kutueleza jinsi Mungu, kwa mara ya kwanza alivyoonyesha kuhusika kwa kujichagulia watu kutoka watu wa Mataifa kwa ajili ya Jina lake.
Szymon powiedział, jak najpierw Bóg wejrzał na pogan, aby [z nich] wybrać lud dla swego imienia.
15 Maneno ya manabii yanakubaliana na jambo hili, kama ilivyoandikwa:
A z tym się zgadzają słowa proroków, jak jest napisane:
16 “‘Baada ya mambo haya nitarudi, nami nitajenga upya nyumba ya Daudi iliyoanguka. Nitajenga tena magofu yake na kuisimamisha,
Potem powrócę i odbuduję upadły przybytek Dawida; odbuduję jego ruiny i wzniosę go;
17 ili wanadamu wengine wote wapate kumtafuta Bwana, hata wale watu wa Mataifa wote ambao wanaitwa kwa Jina langu, asema Bwana, afanyaye mambo haya’
Aby ludzie, którzy pozostali, szukali Pana, i wszystkie narody, nad którymi wzywane jest moje imię – mówi Pan, który to wszystko sprawia.
18 ambayo yamejulikana tangu zamani. (aiōn g165)
Znane są Bogu od wieków wszystkie jego sprawy. (aiōn g165)
19 “Kwa hivyo uamuzi wangu ni kwamba, tusiwataabishe watu wa Mataifa wanaomgeukia Mungu.
Dlatego uważam, że nie należy czynić trudności tym spośród pogan, którzy się nawracają do Boga;
20 Badala yake, tuwaandikie kwamba wajiepushe na vyakula vilivyonajisiwa kwa kutolewa sanamu, wajiepushe na uasherati, au kula mnyama aliyenyongwa, na damu.
Ale napisać im, aby wstrzymywali się od splugawienia bożków, od nierządu, od tego, co uduszone, i od krwi.
21 Kwa maana katika kila mji kwa vizazi vilivyopita, Mose amekuwa na wale wanaotangaza sheria yake kwa kuwa imekuwa ikisomwa kwa sauti kubwa katika masinagogi kila Sabato.”
Mojżesz bowiem od dawien dawna ma w każdym mieście takich, którzy go głoszą, gdyż w synagogach co szabat czytają go.
22 Mitume na wazee pamoja na kanisa lote, wakaamua kuwachagua baadhi ya watu wao na kuwatuma Antiokia pamoja na Paulo na Barnaba. Wakamchagua Yuda aitwaye Barsaba pamoja na Sila, watu wawili waliokuwa viongozi miongoni mwa ndugu.
Wtedy apostołowie i starsi wraz z całym kościołem uznali za słuszne posłać do Antiochii z Pawłem i Barnabą wybranych spośród siebie ludzi: Judę, zwanego Barsabą, i Sylasa, przodujących wśród braci.
23 Wakatumwa na barua ifuatayo: Sisi mitume na wazee, ndugu zenu, Kwa ndugu Mataifa mlioamini mlioko Antiokia, Shamu na Kilikia: Salamu.
Posłali przez nich [takie pismo]: Apostołowie, starsi i bracia przesyłają pozdrowienia braciom pochodzącym z pogan, którzy są w Antiochii, Syrii i Cylicji.
24 Tumesikia kwamba kuna baadhi ya watu waliokuja huko kutoka kwetu bila ruhusa yetu na kuwasumbua, wakiyataabisha mawazo yenu.
Ponieważ słyszeliśmy, że pewni ludzie wyszli od nas i zaniepokoili was słowami, i wzburzyli wasze dusze, mówiąc, że musicie zostać obrzezani i zachowywać prawo, czego im nie przykazaliśmy;
25 Hivyo tumekubaliana wote kuwachagua baadhi ya watu na kuwatuma kwenu pamoja na wapendwa wetu Barnaba na Paulo,
Zgromadzeni jednomyślnie, postanowiliśmy posłać do was wybranych ludzi wraz z naszymi umiłowanymi Barnabą i Pawłem;
26 watu ambao wamehatarisha maisha yao kwa ajili ya jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
Ludźmi, którzy poświęcili swe życie dla imienia naszego Pana Jezusa Chrystusa.
27 Kwa hiyo tunawatuma Yuda na Sila, kuthibitisha kwa maneno ya mdomo mambo haya tunayowaandikia.
Dlatego posłaliśmy Judę i Sylasa, którzy powtórzą wam ustnie to samo.
28 Kwa maana imempendeza Roho Mtakatifu na sisi tusiwatwike mzigo wowote mkubwa zaidi ya mambo haya yafuatayo ambayo ni ya lazima:
Uznał bowiem Duch Święty za słuszne, i my też, nie nakładać na was żadnego ciężaru oprócz tego, co konieczne.
29 Kwamba mjiepushe na vyakula vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, au kula nyama ya mnyama aliyenyongwa, na mjiepushe na uasherati. Mkiyaepuka mambo haya, mtakuwa mmefanya vyema. Kwaherini.
Wstrzymujcie się od [ofiar] składanych bożkom, od krwi, od tego, co uduszone, i od nierządu. Dobrze uczynicie, jeśli będziecie się tego wystrzegać. Bywajcie zdrowi.
30 Hivyo wakaagwa, wakashuka kwenda Antiokia. Baada ya kulikusanya kanisa pamoja, wakawapa ile barua.
Tak więc oni, będąc odprawieni, przybyli do Antiochii, zwołali zgromadzenie i oddali list.
31 Nao hao watu wakiisha kuisoma, wakafurahishwa sana kwa ujumbe wake wa kutia moyo.
Gdy [go] przeczytali, uradowali się z tego pocieszania.
32 Yuda na Sila, ambao wenyewe walikuwa manabii, wakanena maneno mengi ya kuwatia moyo na kuwajenga katika imani wale ndugu walioamini.
A Juda i Sylas, którzy również byli prorokami, w licznych mowach zachęcali i umacniali braci.
33 Baada ya kukaa huko Antiokia kwa muda, wakaagwa kwa amani na wale ndugu ili waende kwa wale waliowatuma. [
A gdy przebywali [tam] jakiś czas, zostali odprawieni z [życzeniem] pokoju od braci do apostołów.
34 Lakini Sila bado akaendelea kukaa huko.]
Lecz upodobało się Sylasowi tam pozostać.
35 Lakini Paulo na Barnaba walibaki Antiokia ambako wao pamoja na wengine wengi walifundisha na kuhubiri neno la Bwana.
Również Paweł i Barnaba przebywali w Antiochii, nauczając i głosząc z wieloma innymi słowo Pana.
36 Baada ya muda, Paulo akamwambia Barnaba, “Turudi tukawatembelee ndugu katika miji yote tuliyohubiri neno la Bwana tuone jinsi wanavyoendelea.”
Po kilku dniach Paweł powiedział do Barnaby: Wróćmy i odwiedźmy naszych braci we wszystkich miastach, w których głosiliśmy słowo Pańskie, [aby zobaczyć], jak się mają.
37 Barnaba alitaka wamchukue Yohana aitwaye Marko waende naye.
Barnaba chciał również wziąć ze sobą Jana, zwanego Markiem.
38 Lakini Paulo aliona si vyema kwa sababu aliwahi kuwaacha walipokuwa huko Pamfilia, hakutaka kuendelea kufanya kazi naye.
Ale Paweł nie chciał zabrać ze sobą tego, który odszedł od nich w Pamfilii i nie uczestniczył z nimi w tej pracy.
39 Pakatokea ubishi mkali kati ya Paulo na Barnaba kuhusu jambo hili, hivyo wakagawanyika. Barnaba akamchukua Yohana Marko wakasafiri baharini kwenda Kipro.
I doszło [między nimi] do ostrej kłótni, tak że się rozdzielili: Barnaba wziął ze sobą Marka i popłynął na Cypr;
40 Lakini Paulo akamchagua Sila na akaondoka baada ya ndugu kuwatakia neema ya Bwana.
Paweł zaś wybrał sobie Sylasa i wyruszył, polecony przez braci łasce Boga.
41 Akapitia Shamu na Kilikia, akiimarisha makanisa ya huko.
I przechodził Syrię i Cylicję, umacniając kościoły.

< Matendo 15 >