< Matendo 15 >
1 Baadhi ya watu wakashuka Antiokia kutoka Uyahudi, nao wakawa wanawafundisha wandugu: “Msipotahiriwa kufuatana na desturi aliyofundisha Mose, hamwezi kuokoka.”
In the meantime, some, who came down from Judea, taught the brethren, Except you be circumcised, according to the manner of Moses, you can not be saved.
2 Baada ya Paulo na Barnaba kutokubaliana nao kukawa na mabishano makali, Paulo na Barnaba na baadhi ya wengine miongoni mwao wakachaguliwa kwenda Yerusalemu ili kujadiliana jambo hili na mitume na wazee.
There being, therefore, a contention, and no small debate with them, on the part of Paul and Barnabas; they resolved that Paul and Barnabas, and some others of their number, should go up to the Apostles and elders at Jerusalem, about this question.
3 Hivyo wakasafirishwa na kanisa, wakiwa njiani wakapitia nchi ya Foinike na Samaria, wakawaeleza jinsi watu wa Mataifa walivyookoka. Habari hizi zikaleta furaha kubwa kwa ndugu wote.
They, therefore, being brought forward on their journey, by the congregation, went through Phenicia and Samaria, relating the conversion of the Gentiles; and they occasioned great joy to all the brethren.
4 Walipofika Yerusalemu, walipokelewa na kanisa na mitume pamoja na wazee, ndipo Paulo na Barnaba wakawaarifu kila kitu Mungu alichokuwa amefanya kupitia kwao.
And being arrived at Jerusalem, they were received by the congregation, and by the Apostles and elders: and they related what things God had done with them.
5 Ndipo baadhi ya walioamini wa madhehebu ya Mafarisayo wakasimama na kusema, “Hao watu wa Mataifa lazima watahiriwe na waagizwe kutii sheria ya Mose.”
But some of the sect of the Pharisees that believed, rose up and said, that it was necessary to circumcise them, and to charge them to keep the law of Moses.
6 Mitume na wazee wakakutana pamoja ili kufikiri jambo hili.
And the Apostles and elders were gathered together to consult upon this affair.
7 Baada ya majadiliano mengi, Petro akasimama na kusema, “Ndugu zangu, mnajua kwamba siku za kwanza Mungu alinichagua ili kwa midomo yangu watu wa Mataifa wapate kusikia ujumbe wa Injili na kuamini.
And after much debate, Peter rose up and said to them, Brethren, you know that, some considerable time since, God among us, chose, that the Gentiles, by my mouth, should hear the word of the gospel, and believe.
8 Mungu, yeye ajuaye mioyo, alionyesha kwamba anawakubali kwa kuwapa Roho Mtakatifu kama vile alivyotupa sisi.
And God, who knows the heart, bore witness to them, giving them the Holy Spirit, even as he did to us:
9 Mungu hakutofautisha kati yetu na wao, bali alitakasa mioyo yao kwa imani.
and made no distinction between us and them, having purified their hearts by faith.
10 Sasa basi, mbona mnataka kumjaribu Mungu kwa kuweka kongwa shingoni mwa wanafunzi ambalo baba zetu wala sisi hatukuweza kulibeba?
Now, therefore, why do you tempt God by imposing on the neck of the disciples a yoke which neither our fathers nor we have been able to bear?
11 Lakini sisi tunaamini ya kuwa tunaokolewa kwa neema ya Bwana Yesu Kristo, kama wao wanavyookolewa.”
But we believe that we are saved by the grace of the Lord Jesus, in the same manner as they.
12 Kusanyiko lote likakaa kimya, wakawasikiliza Paulo na Barnaba wakieleza jinsi Mungu alivyowatumia kutenda ishara na maajabu kwa watu wa Mataifa.
And the whole multitude kept silence, and attended to Barnabas and Paul; relating what signs and wonders God had done among the heathen, by them.
13 Walipomaliza kunena, Yakobo akasema, “Ndugu zangu, nisikilizeni.
Then after they had done speaking, James answered, saying, Brethren, hearken to me.
14 Simoni amekwisha kutueleza jinsi Mungu, kwa mara ya kwanza alivyoonyesha kuhusika kwa kujichagulia watu kutoka watu wa Mataifa kwa ajili ya Jina lake.
Simeon has been relating how God first looked down on the Gentiles, to take from among them a people for his name.
15 Maneno ya manabii yanakubaliana na jambo hili, kama ilivyoandikwa:
And the words of the prophets harmonize with this; as it is written,
16 “‘Baada ya mambo haya nitarudi, nami nitajenga upya nyumba ya Daudi iliyoanguka. Nitajenga tena magofu yake na kuisimamisha,
"After this, I will return, and will rebuild the tabernacle of David, which is fallen down; yes, I will rebuild its ruins, and set it upright again:
17 ili wanadamu wengine wote wapate kumtafuta Bwana, hata wale watu wa Mataifa wote ambao wanaitwa kwa Jina langu, asema Bwana, afanyaye mambo haya’
that the remainder of men may seek the Lord, even all the heathen upon whom my name is called,
18 ambayo yamejulikana tangu zamani. (aiōn )
says the Lord," who does all these things, known to him from the beginning. (aiōn )
19 “Kwa hivyo uamuzi wangu ni kwamba, tusiwataabishe watu wa Mataifa wanaomgeukia Mungu.
Wherefore, my judgment is not to disquiet those who, from among the Gentiles, are converted to God;
20 Badala yake, tuwaandikie kwamba wajiepushe na vyakula vilivyonajisiwa kwa kutolewa sanamu, wajiepushe na uasherati, au kula mnyama aliyenyongwa, na damu.
but to write to them, that they abstain from the pollutions of idols, and from fornication, and from that which is strangled, and from blood.
21 Kwa maana katika kila mji kwa vizazi vilivyopita, Mose amekuwa na wale wanaotangaza sheria yake kwa kuwa imekuwa ikisomwa kwa sauti kubwa katika masinagogi kila Sabato.”
For Moses has, from ancient generations, those who preach him, in every city, being read in the synagogues every Sabbath day.
22 Mitume na wazee pamoja na kanisa lote, wakaamua kuwachagua baadhi ya watu wao na kuwatuma Antiokia pamoja na Paulo na Barnaba. Wakamchagua Yuda aitwaye Barsaba pamoja na Sila, watu wawili waliokuwa viongozi miongoni mwa ndugu.
Then it seemed good to the Apostles and elders, and all the congregation, to send to Antioch, with Paul and Barnabas, chosen men from among themselves, namely, Judas, surnamed Barsabas, and Silas, men of principal account among the brethren;
23 Wakatumwa na barua ifuatayo: Sisi mitume na wazee, ndugu zenu, Kwa ndugu Mataifa mlioamini mlioko Antiokia, Shamu na Kilikia: Salamu.
writing by their hands these things: The Apostles, and elders, and brethren, to the brethren from among the Gentiles in Antioch, and Syria, and Cilicia, greeting:
24 Tumesikia kwamba kuna baadhi ya watu waliokuja huko kutoka kwetu bila ruhusa yetu na kuwasumbua, wakiyataabisha mawazo yenu.
Forasmuch as we have been informed that, some going out from among us, to whom we gave no commission, have troubled you with discourses, unsettling your minds, saying, that you must be circumcised, and keep the law:
25 Hivyo tumekubaliana wote kuwachagua baadhi ya watu na kuwatuma kwenu pamoja na wapendwa wetu Barnaba na Paulo,
we, being unanimously assembled, have thought proper to send you chosen men, with out beloved Barnabas and Paul;
26 watu ambao wamehatarisha maisha yao kwa ajili ya jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
men that have exposed their lives for the name of our Lord Jesus Christ.
27 Kwa hiyo tunawatuma Yuda na Sila, kuthibitisha kwa maneno ya mdomo mambo haya tunayowaandikia.
We have, therefore, sent Judas and Silas, who will also tell you by word of mouth, the same things.
28 Kwa maana imempendeza Roho Mtakatifu na sisi tusiwatwike mzigo wowote mkubwa zaidi ya mambo haya yafuatayo ambayo ni ya lazima:
For it has seemed good to the Holy Spirit, and to us, to impose no further burden upon you besides these necessary things;
29 Kwamba mjiepushe na vyakula vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, au kula nyama ya mnyama aliyenyongwa, na mjiepushe na uasherati. Mkiyaepuka mambo haya, mtakuwa mmefanya vyema. Kwaherini.
that you abstain from things offered to idols, and from blood, and from anything strangled, and from fornication: from which you will do well to keep yourselves. Farewell.
30 Hivyo wakaagwa, wakashuka kwenda Antiokia. Baada ya kulikusanya kanisa pamoja, wakawapa ile barua.
They, therefore, being dismissed, came to Antioch; and assembling the multitude, delivered the epistle.
31 Nao hao watu wakiisha kuisoma, wakafurahishwa sana kwa ujumbe wake wa kutia moyo.
And when they had read it, they rejoiced for the consolation it brought.
32 Yuda na Sila, ambao wenyewe walikuwa manabii, wakanena maneno mengi ya kuwatia moyo na kuwajenga katika imani wale ndugu walioamini.
And Judas and Silas, being also prophets themselves; in a copious discourse, exhorted and strengthened the brethren.
33 Baada ya kukaa huko Antiokia kwa muda, wakaagwa kwa amani na wale ndugu ili waende kwa wale waliowatuma. [
And, having made some stay, they were dismissed with peace from the brethren to the Apostles.
34 Lakini Sila bado akaendelea kukaa huko.]
But Silas thought proper to continue there.
35 Lakini Paulo na Barnaba walibaki Antiokia ambako wao pamoja na wengine wengi walifundisha na kuhubiri neno la Bwana.
Paul also, and Barnabas, with many others, continued at Antioch; teaching and declaring the good word of the Lord.
36 Baada ya muda, Paulo akamwambia Barnaba, “Turudi tukawatembelee ndugu katika miji yote tuliyohubiri neno la Bwana tuone jinsi wanavyoendelea.”
And, after some days, Paul said to Barnabas, Let us return and visit the brethren in all the cities in which we have published the word of the Lord; and see how they do.
37 Barnaba alitaka wamchukue Yohana aitwaye Marko waende naye.
And Barnabas determined to take along with them John, surnamed Mark.
38 Lakini Paulo aliona si vyema kwa sababu aliwahi kuwaacha walipokuwa huko Pamfilia, hakutaka kuendelea kufanya kazi naye.
But Peter did not think proper to take with them that person who had withdrawn himself from them from Pamphylia; and went not with them to the work.
39 Pakatokea ubishi mkali kati ya Paulo na Barnaba kuhusu jambo hili, hivyo wakagawanyika. Barnaba akamchukua Yohana Marko wakasafiri baharini kwenda Kipro.
There was, therefore, a sharp fit of anger, so that they separated from each other; and Barnabas, taking Mark along with him, sailed to Cyprus.
40 Lakini Paulo akamchagua Sila na akaondoka baada ya ndugu kuwatakia neema ya Bwana.
But Paul made choice of Silas, and departed; being commended to the grace of God, by the brethren.
41 Akapitia Shamu na Kilikia, akiimarisha makanisa ya huko.
And he went through Syria and Cilicia confirming the congregations;