< Matendo 15 >
1 Baadhi ya watu wakashuka Antiokia kutoka Uyahudi, nao wakawa wanawafundisha wandugu: “Msipotahiriwa kufuatana na desturi aliyofundisha Mose, hamwezi kuokoka.”
And certain ones having come down from Judea were teaching the brethren that, Unless you may be circumcised, according to the custom of Moses, you are not able to be saved.
2 Baada ya Paulo na Barnaba kutokubaliana nao kukawa na mabishano makali, Paulo na Barnaba na baadhi ya wengine miongoni mwao wakachaguliwa kwenda Yerusalemu ili kujadiliana jambo hili na mitume na wazee.
And there being no small contention and disputation to Paul and Barnabas against them, they delegated Paul and Barnabas, and certain others of them, to go up to the apostles and elders in Jerusalem concerning this question.
3 Hivyo wakasafirishwa na kanisa, wakiwa njiani wakapitia nchi ya Foinike na Samaria, wakawaeleza jinsi watu wa Mataifa walivyookoka. Habari hizi zikaleta furaha kubwa kwa ndugu wote.
Then indeed they having been sent away by the church, traveled through both Phoenicia and Samaria, relating the conversion of the Gentiles: and they continued to make great joy to all the brethren.
4 Walipofika Yerusalemu, walipokelewa na kanisa na mitume pamoja na wazee, ndipo Paulo na Barnaba wakawaarifu kila kitu Mungu alichokuwa amefanya kupitia kwao.
And arriving into Jerusalem, they were received by the church, and the apostles, and the elders, and they proclaimed so many things as God did with them.
5 Ndipo baadhi ya walioamini wa madhehebu ya Mafarisayo wakasimama na kusema, “Hao watu wa Mataifa lazima watahiriwe na waagizwe kutii sheria ya Mose.”
And certain one of those from the sect of the Pharisees having believed arose up, saying that, It is necessary to circumcise them, and to command them to keep the law of Moses.
6 Mitume na wazee wakakutana pamoja ili kufikiri jambo hili.
And the apostles and elders were convened to see about this problem.
7 Baada ya majadiliano mengi, Petro akasimama na kusema, “Ndugu zangu, mnajua kwamba siku za kwanza Mungu alinichagua ili kwa midomo yangu watu wa Mataifa wapate kusikia ujumbe wa Injili na kuamini.
And there being much disputation, Peter, having arisen, said to them, Men, brethren, you know that from ancient days God chose among you, that the Gentiles should hear the word of the gospel through my mouth, and believe.
8 Mungu, yeye ajuaye mioyo, alionyesha kwamba anawakubali kwa kuwapa Roho Mtakatifu kama vile alivyotupa sisi.
And God, who knows the heart, witnessed to them, giving to them the Holy Ghost, as also to us;
9 Mungu hakutofautisha kati yetu na wao, bali alitakasa mioyo yao kwa imani.
and made no difference between us and them, purifying their hearts by faith.
10 Sasa basi, mbona mnataka kumjaribu Mungu kwa kuweka kongwa shingoni mwa wanafunzi ambalo baba zetu wala sisi hatukuweza kulibeba?
Now therefore why tempt ye God, to put a yoke on the neck of the disciples, which neither our fathers nor we were able to bear?
11 Lakini sisi tunaamini ya kuwa tunaokolewa kwa neema ya Bwana Yesu Kristo, kama wao wanavyookolewa.”
But through the grace of our Lord Jesus, we believe that we are saved, in the same manner in which they are also.
12 Kusanyiko lote likakaa kimya, wakawasikiliza Paulo na Barnaba wakieleza jinsi Mungu alivyowatumia kutenda ishara na maajabu kwa watu wa Mataifa.
And the whole multitude became silent, and continued to hear Barnabas and Paul, relating how many miracles and wonders God wrought among the Gentiles through them.
13 Walipomaliza kunena, Yakobo akasema, “Ndugu zangu, nisikilizeni.
And after they became silent, James responded, saying, Men, brethren, hear me.
14 Simoni amekwisha kutueleza jinsi Mungu, kwa mara ya kwanza alivyoonyesha kuhusika kwa kujichagulia watu kutoka watu wa Mataifa kwa ajili ya Jina lake.
Symeon hath related how God in the first place interposed to take a people from the Gentiles, in His name.
15 Maneno ya manabii yanakubaliana na jambo hili, kama ilivyoandikwa:
And to this corresponds the words of the prophet; as has been written,
16 “‘Baada ya mambo haya nitarudi, nami nitajenga upya nyumba ya Daudi iliyoanguka. Nitajenga tena magofu yake na kuisimamisha,
After these things I will return, and will build again the throne of David, which has fallen down; and will build again the ruins of the same, and will set it up again:
17 ili wanadamu wengine wote wapate kumtafuta Bwana, hata wale watu wa Mataifa wote ambao wanaitwa kwa Jina langu, asema Bwana, afanyaye mambo haya’
in order that the residue of men may seek out the Lord, even all the Gentiles, on whom my name has been called upon them, says the Lord, who doeth these things
18 ambayo yamejulikana tangu zamani. (aiōn )
known from the beginning. (aiōn )
19 “Kwa hivyo uamuzi wangu ni kwamba, tusiwataabishe watu wa Mataifa wanaomgeukia Mungu.
Therefore I judge, that we should not burden those from the Gentiles turning to God:
20 Badala yake, tuwaandikie kwamba wajiepushe na vyakula vilivyonajisiwa kwa kutolewa sanamu, wajiepushe na uasherati, au kula mnyama aliyenyongwa, na damu.
but to command them to abstain from things offered to idols, and from fornication, and from strangulation, and from blood.
21 Kwa maana katika kila mji kwa vizazi vilivyopita, Mose amekuwa na wale wanaotangaza sheria yake kwa kuwa imekuwa ikisomwa kwa sauti kubwa katika masinagogi kila Sabato.”
For Moses from ancient generations, has those preaching him in every city, being read in the synagogues on every Sabbath.
22 Mitume na wazee pamoja na kanisa lote, wakaamua kuwachagua baadhi ya watu wao na kuwatuma Antiokia pamoja na Paulo na Barnaba. Wakamchagua Yuda aitwaye Barsaba pamoja na Sila, watu wawili waliokuwa viongozi miongoni mwa ndugu.
Then it seemed good to the apostles and the elders, along with the whole church, to send men chosen from them into Antioch along with Paul and Barnabas; Judas called Barsabbas, and Silas, leaders among the brethren:
23 Wakatumwa na barua ifuatayo: Sisi mitume na wazee, ndugu zenu, Kwa ndugu Mataifa mlioamini mlioko Antiokia, Shamu na Kilikia: Salamu.
having written through their hand; The apostles and elders, brethren to the brethren who are from the Gentiles throughout Antioch and Syria and Cilicia greeting.
24 Tumesikia kwamba kuna baadhi ya watu waliokuja huko kutoka kwetu bila ruhusa yetu na kuwasumbua, wakiyataabisha mawazo yenu.
Since we heard that certain ones having come out from us troubled you, disturbing your souls with words which we did not command:
25 Hivyo tumekubaliana wote kuwachagua baadhi ya watu na kuwatuma kwenu pamoja na wapendwa wetu Barnaba na Paulo,
it seemed good to us, being of one accord, having chosen men to send them to you along with our beloved Barnabas and Paul,
26 watu ambao wamehatarisha maisha yao kwa ajili ya jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
men who have imperiled their lives for the name of our Lord Jesus Christ.
27 Kwa hiyo tunawatuma Yuda na Sila, kuthibitisha kwa maneno ya mdomo mambo haya tunayowaandikia.
Therefore we have sent Judas and Silas, themselves also proclaiming the same things by speech.
28 Kwa maana imempendeza Roho Mtakatifu na sisi tusiwatwike mzigo wowote mkubwa zaidi ya mambo haya yafuatayo ambayo ni ya lazima:
For it seemed good to the Holy Ghost, and to us, to lay upon you no more burden than these necessary things,
29 Kwamba mjiepushe na vyakula vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, au kula nyama ya mnyama aliyenyongwa, na mjiepushe na uasherati. Mkiyaepuka mambo haya, mtakuwa mmefanya vyema. Kwaherini.
to abstain from things offered to idols, and from blood, and from things strangled, and from fornication: from which keeping yourselves, you will do well. Fare ye well.
30 Hivyo wakaagwa, wakashuka kwenda Antiokia. Baada ya kulikusanya kanisa pamoja, wakawapa ile barua.
Then indeed they, having been sent away, came down into Antioch, and convening the multitude, they delivered the letter.
31 Nao hao watu wakiisha kuisoma, wakafurahishwa sana kwa ujumbe wake wa kutia moyo.
And having read it, they rejoiced over the consolation.
32 Yuda na Sila, ambao wenyewe walikuwa manabii, wakanena maneno mengi ya kuwatia moyo na kuwajenga katika imani wale ndugu walioamini.
Both Judas and Silas, themselves also being prophets, exhorted the brethren with elaborate speech, and strengthened them;
33 Baada ya kukaa huko Antiokia kwa muda, wakaagwa kwa amani na wale ndugu ili waende kwa wale waliowatuma. [
and having spent the time, they were discharged by the brethren with peace back to the apostles who sent them.
34 Lakini Sila bado akaendelea kukaa huko.]
35 Lakini Paulo na Barnaba walibaki Antiokia ambako wao pamoja na wengine wengi walifundisha na kuhubiri neno la Bwana.
And Paul and Barnabas tarried in Antioch, teaching and preaching the word of the Lord, also along with many others.
36 Baada ya muda, Paulo akamwambia Barnaba, “Turudi tukawatembelee ndugu katika miji yote tuliyohubiri neno la Bwana tuone jinsi wanavyoendelea.”
And after many days Paul said to Barnabas, Having returned let us now visit the brethren in every city in which we preached the word of the Lord, how they are doing.
37 Barnaba alitaka wamchukue Yohana aitwaye Marko waende naye.
But Barnabas advised to take with them John, also called Mark.
38 Lakini Paulo aliona si vyema kwa sababu aliwahi kuwaacha walipokuwa huko Pamfilia, hakutaka kuendelea kufanya kazi naye.
But Paul thought that he would not take with them, him who having departed from them from Pamphylia, and not having gone along with them into the work.
39 Pakatokea ubishi mkali kati ya Paulo na Barnaba kuhusu jambo hili, hivyo wakagawanyika. Barnaba akamchukua Yohana Marko wakasafiri baharini kwenda Kipro.
But there was a paroxysm, so that they parted from one another, and Barnabas, taking Mark, sailed away into Cyprus.
40 Lakini Paulo akamchagua Sila na akaondoka baada ya ndugu kuwatakia neema ya Bwana.
And Paul, having chosen Silas, went out, committed to the grace of the Lord by the brethren;
41 Akapitia Shamu na Kilikia, akiimarisha makanisa ya huko.
and he traveled through Syria and Cilicia, confirming the churches.