< Matendo 14 >
1 Huko Ikonio Paulo na Barnaba waliingia pamoja katika sinagogi la Wayahudi kama ilivyokuwa desturi yao. Huko wakahubiri kwa uwezo mkubwa kiasi kwamba Wayahudi pamoja na watu wa Mataifa wakaamini.
Ikoonionis läksid Paulus ja Barnabas nagu tavaliselt juudi sünagoogi. Nad kõnelesid seal nõnda, et suur hulk juute ja kreeklasi sai usklikuks.
2 Lakini wale Wayahudi waliokataa kuamini, wakawachochea watu wa Mataifa, wakatia chuki ndani ya mioyo yao dhidi ya wale walioamini.
Aga uskmatud juudid õhutasid üles ja ärritasid teiste rahvaste meeled vihale vendade vastu.
3 Hivyo Paulo na Barnaba wakakaa huko kwa muda wa kutosha wakihubiri kwa ujasiri juu ya Bwana, ambaye alithibitisha ujumbe wa neema yake kwa kuwawezesha kufanya ishara na miujiza.
Nõnda jäid Paulus ja Barnabas sinna kauemaks, kuulutades julgesti Issandat, kes andis tunnistust oma armusõnale ja laskis sündida nende käte läbi tunnustähti ja imetegusid.
4 Lakini watu wa mji ule waligawanyika, wengine wakakubaliana na Wayahudi na wengine na mitume.
Aga linna elanikud jagunesid kaheks: mõned olid juutide, teised apostlite poolt.
5 Watu wa Mataifa na Wayahudi wakajiunga na baadhi ya viongozi, wakafanya mpango wa kuwatendea mitume mabaya na kuwapiga mawe.
Teised rahvad ja juudid tahtsid koos oma ülematega apostleid teotada ja nad kividega surnuks visata.
6 Lakini mitume walipopata habari hizi wakakimbilia Listra na Derbe, miji ya Likaonia na sehemu zilizopakana nayo.
Aga nad said sellest teada ja põgenesid Lükaoonia linnadesse Lüstrasse ja Derbesse ja nende ümbruskonda,
7 Huko wakaendelea kuhubiri habari njema.
kus nad jätkasid evangeeliumi kuulutamist.
8 Katika mji wa Listra, alikuwako kiwete, ambaye alikuwa amelemaa tangu kuzaliwa na hakuwa ametembea kamwe.
Ja Lüstras istus maas üks mees, kes oli sünnist saati jalust halvatud ja polnud kunagi kõndinud.
9 Alimsikiliza Paulo alipokuwa akihubiri. Paulo alipomtazama akaona ana imani ya kuponywa.
Ta kuulis Paulust kõnelemas. Kui Paulus talle otsa vaadates nägi, et tal oli usku terveks saada,
10 Paulo akapaza sauti, “Simama kwa miguu yako!” Mara yule mtu akasimama upesi akaanza kutembea!
hüüdis ta: „Tõuse püsti oma jalgadele!“Ja mees hüppas kohe püsti ja kõndis.
11 Ule umati wa watu ulipoona yaliyokuwa yamefanywa na Paulo, wakapiga kelele kwa lugha yao ya Kilikaonia wakasema, “Miungu imetushukia katika umbo la binadamu!”
Kui rahvahulgad nägid, mis Paulus oli teinud, tõstsid nad häält Lükaoonia keeles: „Jumalad on inimeste kujul alla tulnud meie juurde!“
12 Wakamwita Barnaba Zeu na Paulo wakamwita Herme kwa kuwa ndiye alikuwa msemaji mkuu.
Barnabast nad kutsusid Zeusiks ja Paulust Hermeseks, sest tema pidas kõnet.
13 Kuhani wa Zeu, ambaye hekalu lake lilikuwa nje kidogo tu ya mji, akaleta mafahali na mashada ya maua penye lango la mji kwa sababu yeye na ule umati wa watu walitaka kuwatolea dhabihu.
Ja linna ääres asuva Zeusi templi preester tõi pullid ja lillevanikud linnaväravate juurde, sest ta tahtis koos rahvaga neile ohvrit tuua.
14 Lakini mitume Paulo na Barnaba waliposikia haya, wakararua nguo zao, wakawaendea wale watu kwa haraka, wakawapigia kelele, wakisema,
Aga kui apostlid Barnabas ja Paulus seda kuulsid, käristasid nad oma rõivad katki ja tormasid rahva hulka, hüüdes:
15 “Enyi watu, kwa nini mnafanya mambo haya? Sisi ni wanadamu tu kama ninyi! Tunawaletea habari njema, tukiwaambia kwamba mgeuke mtoke katika mambo haya yasiyofaa, mmwelekee Mungu aliye hai, aliyeziumba mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo.
„Mehed, miks te seda teete? Meiegi oleme teiesugused inimesed. Me kuulutame teile evangeeliumi, et te neist kasututest asjadest pöörduksite elava Jumala poole, kes on teinud taeva ja maa ja mere ja kõik, mis on nende sees.
16 Zamani aliwaachia mataifa waishi walivyotaka.
Varasematel aegadel on ta lasknud rahvastel oma teed minna.
17 Lakini hakuacha kuwaonyesha watu uwepo wake: Ameonyesha wema kwa kuwanyeshea mvua toka mbinguni na kuwapa mazao kwa majira yake, naye amewapa chakula tele na kuijaza mioyo yenu na furaha.”
Ja ometi ei ole jätnud andmata tunnistust iseendast, näidates oma headust: ta on andnud teile vihma taevast ja saaki nende aastaaegadel, andnud teile külluslikult toitu ja täitnud teie südant rõõmuga.“
18 Hata kwa maneno haya yote, ilikuwa vigumu kuuzuia ule umati wa watu kuwatolea dhabihu.
Isegi nende sõnadega oli neil raske hoida tagasi rahvahulka, et see neile ei ohverdaks.
19 Ndipo wakaja baadhi ya Wayahudi kutoka Antiokia na Ikonio wakawashawishi wale watu, wakampiga Paulo kwa mawe, wakamburuta hadi nje ya mji, wakidhani amekufa.
Siis Antiookiast ja Ikoonionist tulid mõned juudid ja võitsid rahvahulga enda poole. Nad loopisid Paulust kividega ning lohistasid ta linnast välja, pidades teda surnuks.
20 Lakini baada ya wanafunzi kukusanyika akainuka na kurudi mjini. Kesho yake yeye na Barnaba wakaondoka kwenda Derbe.
Aga kui jüngrid olid kogunenud tema ümber, tõusis Paulus üles ja läks tagasi linna. Järgmisel päeval lahkusid tema ja Barnabas Derbesse.
21 Wakahubiri habari njema katika mji huo na kupata wanafunzi wengi. Kisha wakarudi Listra, Ikonio na Antiokia,
Ja kui nad selles linnas olid evangeeliumi kuulutanud ja suur hulk oli jüngriteks saanud, pöördusid nad tagasi Lüstrasse, Ikoonioni ja Antiookiasse,
22 wakiwaimarisha wanafunzi na kuwatia moyo waendelee kudumu katika imani. Wakawaonya wakisema, “Imetupasa kuingia katika Ufalme wa Mungu kwa kupitia katika taabu nyingi.”
kinnitades jüngrite hingi, julgustades neid jääma ususse. „Me peame sisenema Jumala Kuningriiki läbi paljude katsumuste, “ütlesid nad.
23 Nao baada ya kuwateua wazee katika kila kanisa, kwa kufunga na kuomba wakawakabidhi kwa Bwana waliyemwamini.
Ja kui Paulus ja Barnabas neile igas koguduses olid määranud vanemad, jätsid nad palvetades ja paastudes nemad Issanda hooleks, kellesse nad nüüd uskusid.
24 Kisha wakapitia Pisidia wakafika Pamfilia.
Pärast Pisiidia läbimist jõudsid nad Pamfüüliasse,
25 Baada ya kuhubiri neno la Mungu huko Perga, wakateremkia Atalia.
ja kui nad Perges olid sõna kuulutanud, läksid nad Ataaliasse.
26 Kutoka Atalia wakasafiri baharini wakarudi Antiokia, ambako walikuwa wamesifiwa kwa ajili ya neema ya Mungu kutokana na ile huduma waliyokuwa wameikamilisha.
Ataaliast nad purjetasid Antiookiasse, kus nad olid usaldatud Jumala armu alla töö jaoks, mille nad nüüd olid lõpetanud.
27 Walipowasili Antiokia wakaliita kanisa pamoja na kutoa taarifa ya yale yote Mungu aliyokuwa ametenda kupitia kwao na jinsi alivyokuwa amefungua mlango wa imani kwa ajili ya watu wa Mataifa.
Sinna jõudes kogusid nad koguduse kokku ja andsid aru kõigest, mis Jumal oli nende läbi teinud, ja et ta rahvastele oli avanud usu ukse.
28 Nao wakakaa huko pamoja na wanafunzi kwa muda mrefu.
Ja nad jäid sinna jüngritega kauemaks ajaks.