< Matendo 14 >

1 Huko Ikonio Paulo na Barnaba waliingia pamoja katika sinagogi la Wayahudi kama ilivyokuwa desturi yao. Huko wakahubiri kwa uwezo mkubwa kiasi kwamba Wayahudi pamoja na watu wa Mataifa wakaamini.
And it fortuned in Iconium that they went both to gether into the synagoge of ye Iewes and so spake that a gret multitude both of ye Iewes and also of the Grekes beleved.
2 Lakini wale Wayahudi waliokataa kuamini, wakawachochea watu wa Mataifa, wakatia chuki ndani ya mioyo yao dhidi ya wale walioamini.
But the unbelevinge Iewes steryd vp and vnquyeted the myndes of the Gentyls agaynste the brethre.
3 Hivyo Paulo na Barnaba wakakaa huko kwa muda wa kutosha wakihubiri kwa ujasiri juu ya Bwana, ambaye alithibitisha ujumbe wa neema yake kwa kuwawezesha kufanya ishara na miujiza.
Longe tyme a bode they there and quyt them selves boldly with the helpe of the Lorde the which gave testimony vnto ye worde of his grace and caused signes and wondres to be done by their hondes.
4 Lakini watu wa mji ule waligawanyika, wengine wakakubaliana na Wayahudi na wengine na mitume.
The people of the cyte were devided: and parte helde with the Iewes and parte with the Apostles.
5 Watu wa Mataifa na Wayahudi wakajiunga na baadhi ya viongozi, wakafanya mpango wa kuwatendea mitume mabaya na kuwapiga mawe.
When ther was a saute made both of the gentyls and also of the Iewes with their rulers to put them to shame and to stone
6 Lakini mitume walipopata habari hizi wakakimbilia Listra na Derbe, miji ya Likaonia na sehemu zilizopakana nayo.
the they were ware of it and fled vnto Listra and Derba cities of Licaonia and vnto the region that lyeth round aboute
7 Huko wakaendelea kuhubiri habari njema.
and there preached the gospell.
8 Katika mji wa Listra, alikuwako kiwete, ambaye alikuwa amelemaa tangu kuzaliwa na hakuwa ametembea kamwe.
And ther sate a certayne man at Listra weake in his fete beinge creple from his mothers wombe and never walkyd.
9 Alimsikiliza Paulo alipokuwa akihubiri. Paulo alipomtazama akaona ana imani ya kuponywa.
The same hearde Paul preache. Which behelde him and perceaved that he had fayth to be whole
10 Paulo akapaza sauti, “Simama kwa miguu yako!” Mara yule mtu akasimama upesi akaanza kutembea!
and sayd with a loude voyce: stond vp right on thy fete. And he stert vp and walked.
11 Ule umati wa watu ulipoona yaliyokuwa yamefanywa na Paulo, wakapiga kelele kwa lugha yao ya Kilikaonia wakasema, “Miungu imetushukia katika umbo la binadamu!”
And when the people sawe what Paul had done they lifte vp their voyces sayinge in the speache of Lycaonia: Goddes are come doune to vs in the lyknes of men.
12 Wakamwita Barnaba Zeu na Paulo wakamwita Herme kwa kuwa ndiye alikuwa msemaji mkuu.
And they called Barnabas Iupiter and Paul Mercurius because he was the preacher.
13 Kuhani wa Zeu, ambaye hekalu lake lilikuwa nje kidogo tu ya mji, akaleta mafahali na mashada ya maua penye lango la mji kwa sababu yeye na ule umati wa watu walitaka kuwatolea dhabihu.
Then Iupiters Preste which dwelt before their cite brought oxe and garlondes vnto the churche porche and wolde have done sacrifise with the people.
14 Lakini mitume Paulo na Barnaba waliposikia haya, wakararua nguo zao, wakawaendea wale watu kwa haraka, wakawapigia kelele, wakisema,
But when the Apostles Barnabas and Paul herde that they rent their clothes and ran in amonge the people cryinge
15 “Enyi watu, kwa nini mnafanya mambo haya? Sisi ni wanadamu tu kama ninyi! Tunawaletea habari njema, tukiwaambia kwamba mgeuke mtoke katika mambo haya yasiyofaa, mmwelekee Mungu aliye hai, aliyeziumba mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo.
and sayinge: syrs why do ye this? We are mortall men lyke vnto you and preache vnto you that ye shuld turne from these vanyties vnto ye lyvinge God which made heaven and erth and the see and all that in them is:
16 Zamani aliwaachia mataifa waishi walivyotaka.
the which in tymes past suffred all nacions to walke in their awne wayes.
17 Lakini hakuacha kuwaonyesha watu uwepo wake: Ameonyesha wema kwa kuwanyeshea mvua toka mbinguni na kuwapa mazao kwa majira yake, naye amewapa chakula tele na kuijaza mioyo yenu na furaha.”
Neverthelesse he lefte not him selfe with outen witnes in that he shewed his benefites in gevinge vs rayne from heaven and frutefull ceasons fyllinge oure hertes with fode and gladnes.
18 Hata kwa maneno haya yote, ilikuwa vigumu kuuzuia ule umati wa watu kuwatolea dhabihu.
And with these sayinges scase refrayned they the people that they had not done sacrifice vnto them.
19 Ndipo wakaja baadhi ya Wayahudi kutoka Antiokia na Ikonio wakawashawishi wale watu, wakampiga Paulo kwa mawe, wakamburuta hadi nje ya mji, wakidhani amekufa.
Thither came certayne Iewes fro Antioche and Iconium and optayned the peoples consent and stoned Paul and drewe him oute of the cyte supposynge he had bene deed.
20 Lakini baada ya wanafunzi kukusanyika akainuka na kurudi mjini. Kesho yake yeye na Barnaba wakaondoka kwenda Derbe.
How be it as the disciples stode rounde about him he arose vp and cam into the cyte. And the nexte daye he departed with Barnabas to Derba.
21 Wakahubiri habari njema katika mji huo na kupata wanafunzi wengi. Kisha wakarudi Listra, Ikonio na Antiokia,
After they had preached to that cite and had taught many they returned agayne to Lisira and to Iconium and Antioche
22 wakiwaimarisha wanafunzi na kuwatia moyo waendelee kudumu katika imani. Wakawaonya wakisema, “Imetupasa kuingia katika Ufalme wa Mungu kwa kupitia katika taabu nyingi.”
and strengthed the disciples soules exhortinge them to continue in the faith affyrminge yt we must thorowe moche tribulacion entre into the kyngdome of God.
23 Nao baada ya kuwateua wazee katika kila kanisa, kwa kufunga na kuomba wakawakabidhi kwa Bwana waliyemwamini.
And when they had ordened them elders by eleccion in every congregacio after they had yrayde and fasted they comended them to God on whom they beleved.
24 Kisha wakapitia Pisidia wakafika Pamfilia.
And they went thorow out Pisidia and came into Paphilia
25 Baada ya kuhubiri neno la Mungu huko Perga, wakateremkia Atalia.
and when they had preached the worde of God in Perga they descended in to Attalia
26 Kutoka Atalia wakasafiri baharini wakarudi Antiokia, ambako walikuwa wamesifiwa kwa ajili ya neema ya Mungu kutokana na ile huduma waliyokuwa wameikamilisha.
and thence departed by shippe to Antioche fro whence they were delivered vnto the grace of God to the worke which they had fulfilled.
27 Walipowasili Antiokia wakaliita kanisa pamoja na kutoa taarifa ya yale yote Mungu aliyokuwa ametenda kupitia kwao na jinsi alivyokuwa amefungua mlango wa imani kwa ajili ya watu wa Mataifa.
When they were come and had gaddered the congregacion to gedder they rehersed all that God had done by them and how he had opened the dore of faith vnto the getyls.
28 Nao wakakaa huko pamoja na wanafunzi kwa muda mrefu.
And ther they abode longe tyme with the disciples.

< Matendo 14 >