< Matendo 14 >

1 Huko Ikonio Paulo na Barnaba waliingia pamoja katika sinagogi la Wayahudi kama ilivyokuwa desturi yao. Huko wakahubiri kwa uwezo mkubwa kiasi kwamba Wayahudi pamoja na watu wa Mataifa wakaamini.
And they came and entered into the synagogue of the Jihudoyee, and so spake with them as that many believed of Jihudoyee and of Javanoyee.
2 Lakini wale Wayahudi waliokataa kuamini, wakawachochea watu wa Mataifa, wakatia chuki ndani ya mioyo yao dhidi ya wale walioamini.
But Jihudoyee, of those who were not persuaded, excited the Gentiles to ill-treat the brethren.
3 Hivyo Paulo na Barnaba wakakaa huko kwa muda wa kutosha wakihubiri kwa ujasiri juu ya Bwana, ambaye alithibitisha ujumbe wa neema yake kwa kuwawezesha kufanya ishara na miujiza.
But they much time were there, and openly discoursed concerning the Lord; and He testified of the word of his grace by the signs and the wonders which he wrought by their hands.
4 Lakini watu wa mji ule waligawanyika, wengine wakakubaliana na Wayahudi na wengine na mitume.
And all the society of the city was divided: of them some were with the Jihudoyee, and of them (some) adhered to the apostles.
5 Watu wa Mataifa na Wayahudi wakajiunga na baadhi ya viongozi, wakafanya mpango wa kuwatendea mitume mabaya na kuwapiga mawe.
But there was made a movement by the Gentiles and by the Jihudoyee and their chiefs to maltreat them, and to crush them with stones.
6 Lakini mitume walipopata habari hizi wakakimbilia Listra na Derbe, miji ya Likaonia na sehemu zilizopakana nayo.
And when they knew, they passed away, and escaped to the cities of Lykania, Lystra, and Derbe, and the villages which surround them,
7 Huko wakaendelea kuhubiri habari njema.
and there evangelized.
8 Katika mji wa Listra, alikuwako kiwete, ambaye alikuwa amelemaa tangu kuzaliwa na hakuwa ametembea kamwe.
AND a certain man dwelt in the city of Lystra who was afflicted in his feet, lame from the womb of his mother, (and) who had never walked.
9 Alimsikiliza Paulo alipokuwa akihubiri. Paulo alipomtazama akaona ana imani ya kuponywa.
This heard Paulos discourse. And when Paulos saw him, and knew that there was faith in him to be saved,
10 Paulo akapaza sauti, “Simama kwa miguu yako!” Mara yule mtu akasimama upesi akaanza kutembea!
he said to him with a high voice, To thee I say, in the name of our Lord Jeshu Meshiha, Stand upon thy feet.
11 Ule umati wa watu ulipoona yaliyokuwa yamefanywa na Paulo, wakapiga kelele kwa lugha yao ya Kilikaonia wakasema, “Miungu imetushukia katika umbo la binadamu!”
And leaping, he stood and walked. And the assembly of the people, when they saw what Paulos had done, lifted up their voice in the language of the country, and said, Gods in the likeness of men have come down unto us.
12 Wakamwita Barnaba Zeu na Paulo wakamwita Herme kwa kuwa ndiye alikuwa msemaji mkuu.
And they named Bar Naba, lord of the gods; and Paulos, Hermis, because he was foremost in discourse.
13 Kuhani wa Zeu, ambaye hekalu lake lilikuwa nje kidogo tu ya mji, akaleta mafahali na mashada ya maua penye lango la mji kwa sababu yeye na ule umati wa watu walitaka kuwatolea dhabihu.
And the priest of the lord of the gods, who was without the city, brought oxen and garlands to the gates of the court of the place where they dwelt, and willed to sacrifice to them.
14 Lakini mitume Paulo na Barnaba waliposikia haya, wakararua nguo zao, wakawaendea wale watu kwa haraka, wakawapigia kelele, wakisema,
But Bar Naba and Paulos, when they heard, rent their garments, and sprang up, and came out to the crowd. And they cried,
15 “Enyi watu, kwa nini mnafanya mambo haya? Sisi ni wanadamu tu kama ninyi! Tunawaletea habari njema, tukiwaambia kwamba mgeuke mtoke katika mambo haya yasiyofaa, mmwelekee Mungu aliye hai, aliyeziumba mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo.
and said, Men, what do you? We also are children of men liable to sufferings like you, (and) who preach to you that from these vanities you should turn unto Aloha the living, who made heaven and earth, and the seas, and all that is in them:
16 Zamani aliwaachia mataifa waishi walivyotaka.
who in former generations left all nations to walk in ways of their own;
17 Lakini hakuacha kuwaonyesha watu uwepo wake: Ameonyesha wema kwa kuwanyeshea mvua toka mbinguni na kuwapa mazao kwa majira yake, naye amewapa chakula tele na kuijaza mioyo yenu na furaha.”
yet leaving not himself without witness, while he did them good from heaven, and sent down rain, and multiplied the fruits in their times, and filled with food and gladness their hearts.
18 Hata kwa maneno haya yote, ilikuwa vigumu kuuzuia ule umati wa watu kuwatolea dhabihu.
And when these they had said, they scarcely restrained the people that some one should not sacrifice to them.
19 Ndipo wakaja baadhi ya Wayahudi kutoka Antiokia na Ikonio wakawashawishi wale watu, wakampiga Paulo kwa mawe, wakamburuta hadi nje ya mji, wakidhani amekufa.
But there came thither Jihudoyee from Ikanon and from Antiokia, and stirred up against them the people; and they stoned Paulos, and dragged him out of the city, because they thought that he was dead.
20 Lakini baada ya wanafunzi kukusanyika akainuka na kurudi mjini. Kesho yake yeye na Barnaba wakaondoka kwenda Derbe.
And the disciples gathered to him, and, arising, he entered the city. AND the day after he went forth from thence with Bar Naba, and came to Derbe the city.
21 Wakahubiri habari njema katika mji huo na kupata wanafunzi wengi. Kisha wakarudi Listra, Ikonio na Antiokia,
And when they had preached to the sons of the city, they discipled many. And they returned and came to Lystra the city, and to Ikanon, and to Antiokia,
22 wakiwaimarisha wanafunzi na kuwatia moyo waendelee kudumu katika imani. Wakawaonya wakisema, “Imetupasa kuingia katika Ufalme wa Mungu kwa kupitia katika taabu nyingi.”
confirming the souls of the disciples, and exhorting them to persevere in the faith. And they said to them, that through much tribulation it behoveth to enter the kingdom of Aloha.
23 Nao baada ya kuwateua wazee katika kila kanisa, kwa kufunga na kuomba wakawakabidhi kwa Bwana waliyemwamini.
And they constituted for them in all the churches presbyters, having fasted with them and prayed, and commended them to our Lord in whom they had believed.
24 Kisha wakapitia Pisidia wakafika Pamfilia.
And when they had gone through the country of Pisidia, they came to Pamphylia,
25 Baada ya kuhubiri neno la Mungu huko Perga, wakateremkia Atalia.
and when they had preached in the city Perga the word of the Lord, they went down to Atalia,
26 Kutoka Atalia wakasafiri baharini wakarudi Antiokia, ambako walikuwa wamesifiwa kwa ajili ya neema ya Mungu kutokana na ile huduma waliyokuwa wameikamilisha.
and from thence voyaged by sea and came to Antiokia, because from thence they had been commended to the grace of the Lord for the work which they had accomplished.
27 Walipowasili Antiokia wakaliita kanisa pamoja na kutoa taarifa ya yale yote Mungu aliyokuwa ametenda kupitia kwao na jinsi alivyokuwa amefungua mlango wa imani kwa ajili ya watu wa Mataifa.
And when all the church had convened, they recounted every thing which Aloha had done with them, and that he had opened the door of the faith unto the Gentiles.
28 Nao wakakaa huko pamoja na wanafunzi kwa muda mrefu.
And much time were they there with the disciples.

< Matendo 14 >