< Matendo 14 >
1 Huko Ikonio Paulo na Barnaba waliingia pamoja katika sinagogi la Wayahudi kama ilivyokuwa desturi yao. Huko wakahubiri kwa uwezo mkubwa kiasi kwamba Wayahudi pamoja na watu wa Mataifa wakaamini.
to be then in/on/among Iconium according to the/this/who it/s/he to enter it/s/he toward the/this/who synagogue the/this/who Jew and to speak thus(-ly) so to trust (in) Jew and/both and Greek, Gentile much multitude
2 Lakini wale Wayahudi waliokataa kuamini, wakawachochea watu wa Mataifa, wakatia chuki ndani ya mioyo yao dhidi ya wale walioamini.
the/this/who then (to disobey *N(k)O*) Jew to awaken/rouse and to harm the/this/who soul the/this/who Gentiles according to the/this/who brother
3 Hivyo Paulo na Barnaba wakakaa huko kwa muda wa kutosha wakihubiri kwa ujasiri juu ya Bwana, ambaye alithibitisha ujumbe wa neema yake kwa kuwawezesha kufanya ishara na miujiza.
sufficient on the other hand therefore/then time to remain to preach boldly upon/to/against the/this/who lord: God the/this/who to testify (upon/to/against *n*) the/this/who word the/this/who grace it/s/he (and *k*) to give sign and wonders to be through/because of the/this/who hand it/s/he
4 Lakini watu wa mji ule waligawanyika, wengine wakakubaliana na Wayahudi na wengine na mitume.
to split then the/this/who multitude the/this/who city and the/this/who on the other hand to be with the/this/who Jew the/this/who then with the/this/who apostle
5 Watu wa Mataifa na Wayahudi wakajiunga na baadhi ya viongozi, wakafanya mpango wa kuwatendea mitume mabaya na kuwapiga mawe.
as/when then to be impulse the/this/who Gentiles and/both and Jew with the/this/who ruler it/s/he to mistreat and to stone it/s/he
6 Lakini mitume walipopata habari hizi wakakimbilia Listra na Derbe, miji ya Likaonia na sehemu zilizopakana nayo.
be aware to flee toward the/this/who city the/this/who Lycaonia Lystra and Derbe and the/this/who region
7 Huko wakaendelea kuhubiri habari njema.
and there to speak good news to be
8 Katika mji wa Listra, alikuwako kiwete, ambaye alikuwa amelemaa tangu kuzaliwa na hakuwa ametembea kamwe.
and one man unable in/on/among Lystra the/this/who foot to sit lame out from belly/womb/stomach mother it/s/he (be already *k*) which never (to walk *N(k)O*)
9 Alimsikiliza Paulo alipokuwa akihubiri. Paulo alipomtazama akaona ana imani ya kuponywa.
this/he/she/it (to hear *N(k)O*) the/this/who Paul to speak which to gaze it/s/he and to perceive: see that/since: that to have/be faith the/this/who to save
10 Paulo akapaza sauti, “Simama kwa miguu yako!” Mara yule mtu akasimama upesi akaanza kutembea!
to say great (the/this/who *ko*) voice/sound: voice to arise upon/to/against the/this/who foot you (upright *NK(o)*) and (to spring *N(k)O*) and to walk
11 Ule umati wa watu ulipoona yaliyokuwa yamefanywa na Paulo, wakapiga kelele kwa lugha yao ya Kilikaonia wakasema, “Miungu imetushukia katika umbo la binadamu!”
the/this/who (and/both *N(k)O*) crowd to perceive: see which to do/make: do (the/this/who *k*) Paul to lift up the/this/who voice/sound: voice it/s/he Lycaonian to say the/this/who God to liken a human to come/go down to/with me
12 Wakamwita Barnaba Zeu na Paulo wakamwita Herme kwa kuwa ndiye alikuwa msemaji mkuu.
to call: call and/both the/this/who (on the other hand *k*) Barnabas Zeus the/this/who then Paul Hermes since it/s/he to be the/this/who to govern the/this/who word
13 Kuhani wa Zeu, ambaye hekalu lake lilikuwa nje kidogo tu ya mji, akaleta mafahali na mashada ya maua penye lango la mji kwa sababu yeye na ule umati wa watu walitaka kuwatolea dhabihu.
the/this/who (and/both *N(k)O*) priest the/this/who Zeus the/this/who to be before the/this/who city (it/s/he *k*) bull and wreath upon/to/against the/this/who gate to bear/lead with the/this/who crowd to will/desire to sacrifice
14 Lakini mitume Paulo na Barnaba waliposikia haya, wakararua nguo zao, wakawaendea wale watu kwa haraka, wakawapigia kelele, wakisema,
to hear then the/this/who apostle Barnabas and Paul to tear the/this/who clothing (it/s/he *NK(o)*) (to rush out *N(k)O*) toward the/this/who crowd to cry
15 “Enyi watu, kwa nini mnafanya mambo haya? Sisi ni wanadamu tu kama ninyi! Tunawaletea habari njema, tukiwaambia kwamba mgeuke mtoke katika mambo haya yasiyofaa, mmwelekee Mungu aliye hai, aliyeziumba mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo.
and to say man which? this/he/she/it to do/make: do and me like to be you a human to speak good news you away from this/he/she/it the/this/who futile to turn upon/to/against (the/this/who *k*) God (the/this/who *k*) to live which to do/make: do the/this/who heaven and the/this/who earth: planet and the/this/who sea and all the/this/who in/on/among it/s/he
16 Zamani aliwaachia mataifa waishi walivyotaka.
which in/on/among the/this/who to pass by generation to allow all the/this/who Gentiles to travel the/this/who road it/s/he
17 Lakini hakuacha kuwaonyesha watu uwepo wake: Ameonyesha wema kwa kuwanyeshea mvua toka mbinguni na kuwapa mazao kwa majira yake, naye amewapa chakula tele na kuijaza mioyo yenu na furaha.”
(and certainly *N(k)O*) no without witness (it/s/he *N(k)O*) to release: leave (to do good *N(k)O*) from heaven (you *N(K)O*) rain to give and time/right time fruitbearing to fill up food and joy the/this/who heart (you *N(K)O*)
18 Hata kwa maneno haya yote, ilikuwa vigumu kuuzuia ule umati wa watu kuwatolea dhabihu.
and this/he/she/it to say hardly to keep from the/this/who crowd the/this/who not to sacrifice it/s/he
19 Ndipo wakaja baadhi ya Wayahudi kutoka Antiokia na Ikonio wakawashawishi wale watu, wakampiga Paulo kwa mawe, wakamburuta hadi nje ya mji, wakidhani amekufa.
to arrive/invade then away from Antioch and Iconium Jew and to persuade the/this/who crowd and to stone the/this/who Paul to drag out/outside(r) the/this/who city (to think *N(k)O*) it/s/he (to die/be dead *N(k)O*)
20 Lakini baada ya wanafunzi kukusanyika akainuka na kurudi mjini. Kesho yake yeye na Barnaba wakaondoka kwenda Derbe.
to surround then the/this/who disciple it/s/he to arise to enter toward the/this/who city and the/this/who the next day to go out with the/this/who Barnabas toward Derbe
21 Wakahubiri habari njema katika mji huo na kupata wanafunzi wengi. Kisha wakarudi Listra, Ikonio na Antiokia,
to speak good news and/both the/this/who city that and to disciple sufficient to return toward the/this/who Lystra and (toward *no*) Iconium and (toward *no*) Antioch
22 wakiwaimarisha wanafunzi na kuwatia moyo waendelee kudumu katika imani. Wakawaonya wakisema, “Imetupasa kuingia katika Ufalme wa Mungu kwa kupitia katika taabu nyingi.”
to strengthen the/this/who soul the/this/who disciple to plead/comfort to abide in/by the/this/who faith and that/since: that through/because of much pressure be necessary me to enter toward the/this/who kingdom the/this/who God
23 Nao baada ya kuwateua wazee katika kila kanisa, kwa kufunga na kuomba wakawakabidhi kwa Bwana waliyemwamini.
to appoint then it/s/he according to assembly elder: Elder to pray with/after fasting to set before it/s/he the/this/who lord: God toward which to trust (in)
24 Kisha wakapitia Pisidia wakafika Pamfilia.
and to pass through the/this/who Pisidia to come/go toward (the/this/who *no*) Pamphylia
25 Baada ya kuhubiri neno la Mungu huko Perga, wakateremkia Atalia.
and to speak in/on/among Perga the/this/who word to come/go down toward Attalia
26 Kutoka Atalia wakasafiri baharini wakarudi Antiokia, ambako walikuwa wamesifiwa kwa ajili ya neema ya Mungu kutokana na ile huduma waliyokuwa wameikamilisha.
and from there to set sail toward Antioch whence to be to deliver the/this/who grace the/this/who God toward the/this/who work which to fulfill
27 Walipowasili Antiokia wakaliita kanisa pamoja na kutoa taarifa ya yale yote Mungu aliyokuwa ametenda kupitia kwao na jinsi alivyokuwa amefungua mlango wa imani kwa ajili ya watu wa Mataifa.
to come then and to assemble the/this/who assembly (to report *N(k)O*) just as/how much to do/make: do the/this/who God with/after it/s/he and that/since: that to open the/this/who Gentiles door faith
28 Nao wakakaa huko pamoja na wanafunzi kwa muda mrefu.
to remain then (there *k*) time no little/few with the/this/who disciple