< Matendo 14 >

1 Huko Ikonio Paulo na Barnaba waliingia pamoja katika sinagogi la Wayahudi kama ilivyokuwa desturi yao. Huko wakahubiri kwa uwezo mkubwa kiasi kwamba Wayahudi pamoja na watu wa Mataifa wakaamini.
And it came to pass in Iconium, that they went together into the synagogue of the Jews, and so spoke that a great multitude both of Jews and Greeks believed.
2 Lakini wale Wayahudi waliokataa kuamini, wakawachochea watu wa Mataifa, wakatia chuki ndani ya mioyo yao dhidi ya wale walioamini.
But the Jews that disbelieved stirred up and embittered the minds of the gentiles against the brethren.
3 Hivyo Paulo na Barnaba wakakaa huko kwa muda wa kutosha wakihubiri kwa ujasiri juu ya Bwana, ambaye alithibitisha ujumbe wa neema yake kwa kuwawezesha kufanya ishara na miujiza.
They abode therefore a long time there, speaking boldly in reliance on the Lord, who gave testimony to the word of his grace, granting signs and wonders to be wrought by their a hands.
4 Lakini watu wa mji ule waligawanyika, wengine wakakubaliana na Wayahudi na wengine na mitume.
But the multitude of the city was divided; and some held with the Jews, and some with the apostles.
5 Watu wa Mataifa na Wayahudi wakajiunga na baadhi ya viongozi, wakafanya mpango wa kuwatendea mitume mabaya na kuwapiga mawe.
And when a movement was made both of the gentiles, and the Jews with their rulers, to abuse and stone them,
6 Lakini mitume walipopata habari hizi wakakimbilia Listra na Derbe, miji ya Likaonia na sehemu zilizopakana nayo.
they became aware of it, and fled to the cities of Lycaonia, Lystra and Derbe, and the neighboring country;
7 Huko wakaendelea kuhubiri habari njema.
and they were publishing the glad tidings there.
8 Katika mji wa Listra, alikuwako kiwete, ambaye alikuwa amelemaa tangu kuzaliwa na hakuwa ametembea kamwe.
And at Lystra there sat a certain man who had not the use of his feet, a cripple from his birth, who never had walked.
9 Alimsikiliza Paulo alipokuwa akihubiri. Paulo alipomtazama akaona ana imani ya kuponywa.
This man heard Paul speaking; who looking steadily at him, and perceiving that he had faith to be healed,
10 Paulo akapaza sauti, “Simama kwa miguu yako!” Mara yule mtu akasimama upesi akaanza kutembea!
said with a loud voice, Stand upright on thy feet. And he leaped up and walked.
11 Ule umati wa watu ulipoona yaliyokuwa yamefanywa na Paulo, wakapiga kelele kwa lugha yao ya Kilikaonia wakasema, “Miungu imetushukia katika umbo la binadamu!”
And the multitudes, seeing what Paul had done, lifted up their voices, saying, in the language of Lycaonia, The gods have come down to us in the likeness of men.
12 Wakamwita Barnaba Zeu na Paulo wakamwita Herme kwa kuwa ndiye alikuwa msemaji mkuu.
And they called Barnabas, Jupiter; and Paul, Mercury, because he was the chief speaker.
13 Kuhani wa Zeu, ambaye hekalu lake lilikuwa nje kidogo tu ya mji, akaleta mafahali na mashada ya maua penye lango la mji kwa sababu yeye na ule umati wa watu walitaka kuwatolea dhabihu.
Then the priest of Jupiter, that was in front of the city, brought oxen and garlands to the gates, and would have offered sacrifice with the multitudes.
14 Lakini mitume Paulo na Barnaba waliposikia haya, wakararua nguo zao, wakawaendea wale watu kwa haraka, wakawapigia kelele, wakisema,
But the apostles, Barnabas and Paul, when they heard of it, rent their garments, and rushed forth to the multitude, crying out
15 “Enyi watu, kwa nini mnafanya mambo haya? Sisi ni wanadamu tu kama ninyi! Tunawaletea habari njema, tukiwaambia kwamba mgeuke mtoke katika mambo haya yasiyofaa, mmwelekee Mungu aliye hai, aliyeziumba mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo.
and saying, Men, why do ye these things? We also are men of like nature with you, bringing to you glad tidings, that ye may turn from these vanities to the living God, who made heaven and earth and sea, and all things that are therein;
16 Zamani aliwaachia mataifa waishi walivyotaka.
who in the ages past suffered all the nations to walk in their own ways;
17 Lakini hakuacha kuwaonyesha watu uwepo wake: Ameonyesha wema kwa kuwanyeshea mvua toka mbinguni na kuwapa mazao kwa majira yake, naye amewapa chakula tele na kuijaza mioyo yenu na furaha.”
although he left not himself without witness, in that he did good, giving you rain from heaven and fruitful seasons, filling your hearts with food and gladness.
18 Hata kwa maneno haya yote, ilikuwa vigumu kuuzuia ule umati wa watu kuwatolea dhabihu.
And with these words, they hardly restrained the multitudes from sacrificing to them.
19 Ndipo wakaja baadhi ya Wayahudi kutoka Antiokia na Ikonio wakawashawishi wale watu, wakampiga Paulo kwa mawe, wakamburuta hadi nje ya mji, wakidhani amekufa.
But there came thither Jews from Antioch and Iconium; who, having persuaded the multitudes, and stoned Paul, dragged him out of the city, supposing him to be dead.
20 Lakini baada ya wanafunzi kukusanyika akainuka na kurudi mjini. Kesho yake yeye na Barnaba wakaondoka kwenda Derbe.
But the disciples having gathered around him, he rose up, and came into the city. And the next day he departed with Barnabas to Derbe.
21 Wakahubiri habari njema katika mji huo na kupata wanafunzi wengi. Kisha wakarudi Listra, Ikonio na Antiokia,
And when they had published the glad tidings to that city, and had made many disciples, they went back to Lystra, and to Iconium, and to Antioch;
22 wakiwaimarisha wanafunzi na kuwatia moyo waendelee kudumu katika imani. Wakawaonya wakisema, “Imetupasa kuingia katika Ufalme wa Mungu kwa kupitia katika taabu nyingi.”
confirming the souls of the disciples, exhorting them to continue in the faith, and saying that it is through many afflictions that we mast enter into the kingdom of God.
23 Nao baada ya kuwateua wazee katika kila kanisa, kwa kufunga na kuomba wakawakabidhi kwa Bwana waliyemwamini.
And having appointed for them elders in every church, they prayed with fasting, and commended them to the Lord, in whom they believed.
24 Kisha wakapitia Pisidia wakafika Pamfilia.
And having gone through Pisidia, they came to Pamphylia;
25 Baada ya kuhubiri neno la Mungu huko Perga, wakateremkia Atalia.
and when they had spoken the word in Perga, they went down to Attalia,
26 Kutoka Atalia wakasafiri baharini wakarudi Antiokia, ambako walikuwa wamesifiwa kwa ajili ya neema ya Mungu kutokana na ile huduma waliyokuwa wameikamilisha.
and thence set sail for Antioch, whence they had been commended to the grace of God, for the work which they had accomplished.
27 Walipowasili Antiokia wakaliita kanisa pamoja na kutoa taarifa ya yale yote Mungu aliyokuwa ametenda kupitia kwao na jinsi alivyokuwa amefungua mlango wa imani kwa ajili ya watu wa Mataifa.
And when they had arrived and had gathered the church together, they related what great things God had wrought with them, and that he had opened a door of faith to the gentiles.
28 Nao wakakaa huko pamoja na wanafunzi kwa muda mrefu.
And they abode no little time with the disciples.

< Matendo 14 >