< Matendo 14 >

1 Huko Ikonio Paulo na Barnaba waliingia pamoja katika sinagogi la Wayahudi kama ilivyokuwa desturi yao. Huko wakahubiri kwa uwezo mkubwa kiasi kwamba Wayahudi pamoja na watu wa Mataifa wakaamini.
二人在以哥念同进犹太人的会堂,在那里讲的,叫犹太人和希腊人信的很多。
2 Lakini wale Wayahudi waliokataa kuamini, wakawachochea watu wa Mataifa, wakatia chuki ndani ya mioyo yao dhidi ya wale walioamini.
但那不顺从的犹太人耸动外邦人,叫他们心里恼恨弟兄。
3 Hivyo Paulo na Barnaba wakakaa huko kwa muda wa kutosha wakihubiri kwa ujasiri juu ya Bwana, ambaye alithibitisha ujumbe wa neema yake kwa kuwawezesha kufanya ishara na miujiza.
二人在那里住了多日,倚靠主放胆讲道,主借他们的手施行神迹奇事,证明他的恩道。
4 Lakini watu wa mji ule waligawanyika, wengine wakakubaliana na Wayahudi na wengine na mitume.
城里的众人就分了党,有附从犹太人的,有附从使徒的。
5 Watu wa Mataifa na Wayahudi wakajiunga na baadhi ya viongozi, wakafanya mpango wa kuwatendea mitume mabaya na kuwapiga mawe.
那时,外邦人和犹太人,并他们的官长,一齐拥上来,要凌辱使徒,用石头打他们。
6 Lakini mitume walipopata habari hizi wakakimbilia Listra na Derbe, miji ya Likaonia na sehemu zilizopakana nayo.
使徒知道了,就逃往吕高尼的路司得、特庇两个城和周围地方去,
7 Huko wakaendelea kuhubiri habari njema.
在那里传福音。
8 Katika mji wa Listra, alikuwako kiwete, ambaye alikuwa amelemaa tangu kuzaliwa na hakuwa ametembea kamwe.
路司得城里坐着一个两脚无力的人,生来是瘸腿的,从来没有走过。
9 Alimsikiliza Paulo alipokuwa akihubiri. Paulo alipomtazama akaona ana imani ya kuponywa.
他听保罗讲道,保罗定睛看他,见他有信心,可得痊愈,
10 Paulo akapaza sauti, “Simama kwa miguu yako!” Mara yule mtu akasimama upesi akaanza kutembea!
就大声说:“你起来,两脚站直!”那人就跳起来,而且行走。
11 Ule umati wa watu ulipoona yaliyokuwa yamefanywa na Paulo, wakapiga kelele kwa lugha yao ya Kilikaonia wakasema, “Miungu imetushukia katika umbo la binadamu!”
众人看见保罗所做的事,就用吕高尼的话大声说:“有神借着人形降临在我们中间了。”
12 Wakamwita Barnaba Zeu na Paulo wakamwita Herme kwa kuwa ndiye alikuwa msemaji mkuu.
于是称巴拿巴为宙斯,称保罗为希耳米,因为他说话领首。
13 Kuhani wa Zeu, ambaye hekalu lake lilikuwa nje kidogo tu ya mji, akaleta mafahali na mashada ya maua penye lango la mji kwa sababu yeye na ule umati wa watu walitaka kuwatolea dhabihu.
有城外宙斯庙的祭司牵着牛,拿着花圈,来到门前,要同众人向使徒献祭。
14 Lakini mitume Paulo na Barnaba waliposikia haya, wakararua nguo zao, wakawaendea wale watu kwa haraka, wakawapigia kelele, wakisema,
巴拿巴、保罗二使徒听见,就撕开衣裳,跳进众人中间,喊着说:
15 “Enyi watu, kwa nini mnafanya mambo haya? Sisi ni wanadamu tu kama ninyi! Tunawaletea habari njema, tukiwaambia kwamba mgeuke mtoke katika mambo haya yasiyofaa, mmwelekee Mungu aliye hai, aliyeziumba mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo.
“诸君,为什么做这事呢?我们也是人,性情和你们一样。我们传福音给你们,是叫你们离弃这些虚妄,归向那创造天、地、海,和其中万物的永生 神。
16 Zamani aliwaachia mataifa waishi walivyotaka.
他在从前的世代,任凭万国各行其道;
17 Lakini hakuacha kuwaonyesha watu uwepo wake: Ameonyesha wema kwa kuwanyeshea mvua toka mbinguni na kuwapa mazao kwa majira yake, naye amewapa chakula tele na kuijaza mioyo yenu na furaha.”
然而为自己未尝不显出证据来,就如常施恩惠,从天降雨,赏赐丰年,叫你们饮食饱足,满心喜乐。”
18 Hata kwa maneno haya yote, ilikuwa vigumu kuuzuia ule umati wa watu kuwatolea dhabihu.
二人说了这些话,仅仅地拦住众人不献祭与他们。
19 Ndipo wakaja baadhi ya Wayahudi kutoka Antiokia na Ikonio wakawashawishi wale watu, wakampiga Paulo kwa mawe, wakamburuta hadi nje ya mji, wakidhani amekufa.
但有些犹太人从安提阿和以哥念来,挑唆众人,就用石头打保罗,以为他是死了,便拖到城外。
20 Lakini baada ya wanafunzi kukusanyika akainuka na kurudi mjini. Kesho yake yeye na Barnaba wakaondoka kwenda Derbe.
门徒正围着他,他就起来,走进城去。 第二天,同巴拿巴往特庇去,
21 Wakahubiri habari njema katika mji huo na kupata wanafunzi wengi. Kisha wakarudi Listra, Ikonio na Antiokia,
对那城里的人传了福音,使好些人作门徒,就回路司得、以哥念、安提阿去,
22 wakiwaimarisha wanafunzi na kuwatia moyo waendelee kudumu katika imani. Wakawaonya wakisema, “Imetupasa kuingia katika Ufalme wa Mungu kwa kupitia katika taabu nyingi.”
坚固门徒的心,劝他们恒守所信的道;又说:“我们进入 神的国,必须经历许多艰难。”
23 Nao baada ya kuwateua wazee katika kila kanisa, kwa kufunga na kuomba wakawakabidhi kwa Bwana waliyemwamini.
二人在各教会中选立了长老,又禁食祷告,就把他们交托所信的主。
24 Kisha wakapitia Pisidia wakafika Pamfilia.
二人经过彼西底,来到旁非利亚。
25 Baada ya kuhubiri neno la Mungu huko Perga, wakateremkia Atalia.
在别加讲了道,就下亚大利去,
26 Kutoka Atalia wakasafiri baharini wakarudi Antiokia, ambako walikuwa wamesifiwa kwa ajili ya neema ya Mungu kutokana na ile huduma waliyokuwa wameikamilisha.
从那里坐船,往安提阿去。当初,他们被众人所托、蒙 神之恩、要办现在所做之工,就是在这地方。
27 Walipowasili Antiokia wakaliita kanisa pamoja na kutoa taarifa ya yale yote Mungu aliyokuwa ametenda kupitia kwao na jinsi alivyokuwa amefungua mlango wa imani kwa ajili ya watu wa Mataifa.
到了那里,聚集了会众,就述说 神借他们所行的一切事,并 神怎样为外邦人开了信道的门。
28 Nao wakakaa huko pamoja na wanafunzi kwa muda mrefu.
二人就在那里同门徒住了多日。

< Matendo 14 >