< Matendo 14 >

1 Huko Ikonio Paulo na Barnaba waliingia pamoja katika sinagogi la Wayahudi kama ilivyokuwa desturi yao. Huko wakahubiri kwa uwezo mkubwa kiasi kwamba Wayahudi pamoja na watu wa Mataifa wakaamini.
在以哥念发生了相同的事情。保罗和巴拿巴来到犹太人的会堂讲道。他们的言语如此令人信服,很多犹太人和说希腊语的朝拜者都相信了耶稣。
2 Lakini wale Wayahudi waliokataa kuamini, wakawachochea watu wa Mataifa, wakatia chuki ndani ya mioyo yao dhidi ya wale walioamini.
但那些拒绝相信耶稣的犹太人,却去煽动异教徒的情绪,毒害他们的心,让他们反对信徒。
3 Hivyo Paulo na Barnaba wakakaa huko kwa muda wa kutosha wakihubiri kwa ujasiri juu ya Bwana, ambaye alithibitisha ujumbe wa neema yake kwa kuwawezesha kufanya ishara na miujiza.
但保罗和巴拿巴在那里停留了很久,以主为名勇敢传道,主也通过他们实现了神迹奇事,以此证实他的恩典之道。
4 Lakini watu wa mji ule waligawanyika, wengine wakakubaliana na Wayahudi na wengine na mitume.
于是城里民众分成了两派,一派服从犹太人,一派支持使徒。
5 Watu wa Mataifa na Wayahudi wakajiunga na baadhi ya viongozi, wakafanya mpango wa kuwatendea mitume mabaya na kuwapiga mawe.
但随后异教徒、犹太人以及他们的首领,决定攻击保罗和巴拿巴,用石头打他们。
6 Lakini mitume walipopata habari hizi wakakimbilia Listra na Derbe, miji ya Likaonia na sehemu zilizopakana nayo.
但两人发现了这个阴谋,于是逃到吕高尼地区,来到路司得和特庇这两座城,
7 Huko wakaendelea kuhubiri habari njema.
在那里传递福音。
8 Katika mji wa Listra, alikuwako kiwete, ambaye alikuwa amelemaa tangu kuzaliwa na hakuwa ametembea kamwe.
路司得城有一个残疾人,双脚都动不了。他生下来就瘸腿,从未走过路。
9 Alimsikiliza Paulo alipokuwa akihubiri. Paulo alipomtazama akaona ana imani ya kuponywa.
他坐在那里听保罗讲道。当保罗看向他,发现相信上帝可以将他治愈,
10 Paulo akapaza sauti, “Simama kwa miguu yako!” Mara yule mtu akasimama upesi akaanza kutembea!
于是保罗大声说:“用你的双脚站起来吧!”那人就跳起来,开始行走。
11 Ule umati wa watu ulipoona yaliyokuwa yamefanywa na Paulo, wakapiga kelele kwa lugha yao ya Kilikaonia wakasema, “Miungu imetushukia katika umbo la binadamu!”
目睹保罗所为,众人用吕高尼语大声说:“上帝以人的样子降临到我们中间!”
12 Wakamwita Barnaba Zeu na Paulo wakamwita Herme kwa kuwa ndiye alikuwa msemaji mkuu.
于是他们称巴拿巴为希腊神宙斯,称保罗为赫米,因为大部分时候都是保罗在讲话。
13 Kuhani wa Zeu, ambaye hekalu lake lilikuwa nje kidogo tu ya mji, akaleta mafahali na mashada ya maua penye lango la mji kwa sababu yeye na ule umati wa watu walitaka kuwatolea dhabihu.
城门外一座宙斯庙的祭司,牵来几头公牛、手拿花环来到城门处,打算在众人面前进行献祭。
14 Lakini mitume Paulo na Barnaba waliposikia haya, wakararua nguo zao, wakawaendea wale watu kwa haraka, wakawapigia kelele, wakisema,
但巴拿巴和保罗两个使徒听说这个消息,便撕开衣服,跳进民众中大喊:
15 “Enyi watu, kwa nini mnafanya mambo haya? Sisi ni wanadamu tu kama ninyi! Tunawaletea habari njema, tukiwaambia kwamba mgeuke mtoke katika mambo haya yasiyofaa, mmwelekee Mungu aliye hai, aliyeziumba mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo.
“各位,怎么能这么做呢?我们也是人,天性与你们一样,我们来此向你们传递福音,就是为了让你们远离这些毫无意义的事,归从永生的上帝,就是那位创造天地大海和世间万物的上帝。
16 Zamani aliwaachia mataifa waishi walivyotaka.
在过往的世界里,他允许各国各行其道,
17 Lakini hakuacha kuwaonyesha watu uwepo wake: Ameonyesha wema kwa kuwanyeshea mvua toka mbinguni na kuwapa mazao kwa majira yake, naye amewapa chakula tele na kuijaza mioyo yenu na furaha.”
尽管如此,他仍然通过行善事留下证明,向你们送来天堂之雨和四季的作物,为你们提供所需的食物,为你们心中带来快乐。”
18 Hata kwa maneno haya yote, ilikuwa vigumu kuuzuia ule umati wa watu kuwatolea dhabihu.
这番话勉强说服了众人,不再向他们献祭。
19 Ndipo wakaja baadhi ya Wayahudi kutoka Antiokia na Ikonio wakawashawishi wale watu, wakampiga Paulo kwa mawe, wakamburuta hadi nje ya mji, wakidhani amekufa.
但有些来自安提阿和以哥念的犹太人,成功挑唆民众用石头打保罗,然后以为他死了,就把他拖到城外。
20 Lakini baada ya wanafunzi kukusanyika akainuka na kurudi mjini. Kesho yake yeye na Barnaba wakaondoka kwenda Derbe.
但就在信徒们围着他时,他竟然站起来,走回了城里。第二天,他跟巴拿巴一同到特庇去。
21 Wakahubiri habari njema katika mji huo na kupata wanafunzi wengi. Kisha wakarudi Listra, Ikonio na Antiokia,
他们在那里向众人传递福音,让许多人都成为信徒,然后他们又回到路司得、以哥念和安提阿。
22 wakiwaimarisha wanafunzi na kuwatia moyo waendelee kudumu katika imani. Wakawaonya wakisema, “Imetupasa kuingia katika Ufalme wa Mungu kwa kupitia katika taabu nyingi.”
他们鼓励信徒坚定信念,守住心中对耶稣的信,他们说:“只有经历诸多苦难,我们才能进入上帝之国。”
23 Nao baada ya kuwateua wazee katika kila kanisa, kwa kufunga na kuomba wakawakabidhi kwa Bwana waliyemwamini.
两人为每个教会指派了长老,然后与众人一起祈祷和禁食,之后就将他们交给所信的主,受到主的关怀,
24 Kisha wakapitia Pisidia wakafika Pamfilia.
然后经过彼西底来到旁非利亚。
25 Baada ya kuhubiri neno la Mungu huko Perga, wakateremkia Atalia.
在别加讲道以后,他们又继续去往亚大利,
26 Kutoka Atalia wakasafiri baharini wakarudi Antiokia, ambako walikuwa wamesifiwa kwa ajili ya neema ya Mungu kutokana na ile huduma waliyokuwa wameikamilisha.
从那里坐船返回安提阿,那里是他们旅程的起点,也是在那里受到上帝的恩典,致力于完成自己的使命,如今使命已经达成。
27 Walipowasili Antiokia wakaliita kanisa pamoja na kutoa taarifa ya yale yote Mungu aliyokuwa ametenda kupitia kwao na jinsi alivyokuwa amefungua mlango wa imani kwa ajili ya watu wa Mataifa.
他们抵达目的地后就召集教会的众人,讲述了上帝通过他们所做的一切,以及他如何向信他的异教徒敞开大门。
28 Nao wakakaa huko pamoja na wanafunzi kwa muda mrefu.
随后两人与信徒们一起生活了很久。

< Matendo 14 >