< Matendo 13 >
1 Katika kanisa huko Antiokia ya Shamu walikuwako manabii na walimu, yaani: Barnaba, Simeoni aitwaye Nigeri, Lukio Mkirene, Manaeni aliyekuwa amelelewa pamoja na Mfalme Herode Agripa, na Sauli.
Now there were in the church at Antioch, several prophets and teachers; Barnabas, and Simon called Niger, and Lucius who was from the city Cyrene, and Menaen, a son of the guardians of Herod the Tetrarch, and Saul.
2 Walipokuwa wakimwabudu Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, “Nitengeeni Sauli na Barnaba kwa kazi ile maalum niliyowaitia.”
And while they were fasting and making supplication to God, the Holy Spirit said to them: Separate to me Saul and Barnabas, for the work to which I have called them.
3 Ndipo baada ya kufunga na kuomba, wakawawekea mikono yao na wakawatuma waende zao.
And after they had fasted and prayed, they laid the hand on them, and sent them away.
4 Hivyo, wakiwa wametumwa na Roho Mtakatifu, wakashuka kwenda Seleukia na kutoka huko wakasafiri baharini mpaka kisiwa cha Kipro.
And they, being sent forth by the Holy Spirit, went down to Seleucia, and from there they went by sea as far as Cyprus.
5 Walipowasili katika mji wa Salami, wakahubiri neno la Mungu katika sinagogi la Wayahudi. Pia walikuwa na Yohana Marko kuwa msaidizi wao.
And when they entered the city of Salamis, they announced the word of our Lord in the synagogues of the Jews. And John ministered to them.
6 Walipokwisha kupita katika nchi zote hizo wakafika Pafo, ambapo walikutana na Myahudi mmoja mchawi aliyekuwa nabii wa uongo, jina lake Bar-Yesu.
And when they had travelled over the whole island as far as the city Paphos, they found a certain man, a sorcerer, a Jew, who was a false prophet, and whose name was Bar-Suma.
7 Mtu huyu alikuwa pamoja na Sergio Paulo, mtu mwenye hekima aliyekuwa msaidizi wa mwakilishi wa mtawala wa kile kisiwa. Sergio Paulo akawaita Sauli na Barnaba akitaka kusikia neno la Mungu.
He adhered to a wise man, who was the proconsul, and was called Sergius Paulus. And the proconsul sent for Saul and Barnabas, and requested to hear from them the word of God.
8 Lakini Elima yule mchawi (hii ndiyo maana ya jina lake), aliwapinga Barnaba na Sauli na kujaribu kumpotosha yule mkuu wa kile kisiwa aiache imani.
And this sorcerer, Bar-Suma, (whose name is interpreted, Elymas, ) withstood them; because he wished to divert the proconsul from the faith.
9 Ndipo Sauli, ambaye pia aliitwa Paulo, akiwa amejawa na Roho Mtakatifu, akamkazia macho Elima huyo mchawi,
And Saul who is called Paul, was filled with the Holy Spirit; and he looked upon him,
10 akamwambia, “Ewe mwana wa ibilisi, wewe ni adui wa kila kilicho haki! Umejaa kila aina ya udanganyifu na ulaghai. Je, hutaacha kuzipotosha njia za Bwana zilizonyooka?
and said: O thou full of all subtilties, and all mischiefs, thou child of the calumniator, and enemy of all righteousness; wilt thou not cease to pervert the right ways of the Lord?
11 Nawe sasa sikiliza, mkono wa Bwana u dhidi yako. Utakuwa kipofu, wala hutaona jua kwa muda.” Mara ukungu na giza vikamfunika, naye akaenda huku na huko akitafuta mtu wa kumshika mkono ili amwonyeshe njia.
And now, the hand of the Lord is upon thee, and thou shalt be blind, and shalt not see the sun for a time. And immediately there fell upon him a mist and darkness; and he went about, inquiring who would take him by the hand.
12 Yule mkuu wa kile kisiwa alipoona yaliyotukia, akaamini kwa sababu alistaajabishwa na mafundisho kuhusu Bwana.
And when the proconsul saw what occurred, he was astonished; and he believed the doctrine of the Lord.
13 Kisha Paulo na wenzake wakasafiri toka Pafo wakafika Perga huko Pamfilia. Lakini, Yohana Marko akawaacha huko, akarejea Yerusalemu.
And Paul and Barnabas went by sea, from the city of Paphos, and came to Perga, a city of Pamphylia. And John separated from them, and went away to Jerusalem.
14 Kutoka Perga wakaendelea hadi Antiokia ya Pisidia. Siku ya Sabato wakaingia ndani ya sinagogi, wakaketi.
And they departed from Perga, and came to Antioch, a city of Pisidia: and they entered the synagogue, on the sabbath day, and sat down.
15 Baada ya Sheria ya Mose na Kitabu cha Manabii kusomwa, viongozi wa sinagogi wakawatumia ujumbe wakisema, “Ndugu, kama mna neno la kuwafariji watu hawa, tafadhali lisemeni.”
And after the law had been read, and the prophets, the Elders of the synagogue sent to them, and said: Men, brethren, if ye have a word of exhortation, address the people.
16 Paulo akasimama, akawapungia mkono na kusema: “Enyi wanaume wa Israeli na ninyi nyote mnaomcha Mungu.
And Paul arose, and waved his hand, and said: Men, sons of Israel, and ye that fear God, hear ye.
17 Mungu wa watu hawa wa Israeli aliwachagua baba zetu, akawafanya kustawi walipokuwa huko Misri, kwa uwezo mwingi akawaongoza na kuwatoa katika nchi ile.
The God of this people chose our fathers, and raised them up, and multiplied them, when they resided in the land of Egypt; and, with a high arm, he brought them out of it.
18 Kwa muda wa miaka arobaini alivumilia matendo yao walipokuwa jangwani.
And he fed them in the wilderness forty years.
19 Naye baada ya kuyaangamiza mataifa saba waliokuwa wakiishi katika nchi ya Kanaani, akawapa Waisraeli nchi yao iwe urithi wao.
And he extirpated seven nations in the land of Canaan, and gave them their land for an inheritance.
20 Haya yote yalichukua kama muda wa miaka 450. “Baada ya haya, Mungu akawapa waamuzi mpaka wakati wa nabii Samweli.
And for four hundred and fifty years he gave them judges, until Samuel the prophet.
21 Ndipo watu wakaomba wapewe mfalme, naye Mungu akawapa Sauli mwana wa Kishi wa kabila la Benyamini, aliyetawala kwa miaka arobaini.
And then they asked for themselves a king: and God gave them Saul the son of Kish, a man of the tribe of Benjamin, during forty years.
22 Baada ya kumwondoa Sauli katika ufalme, akawainulia Daudi kuwa mfalme wao. Mungu pia alimshuhudia, akisema, ‘Nimemwona Daudi mwana wa Yese, mtu anayeupendeza moyo wangu, atakayetimiza mapenzi yangu yote.’
And he removed him, and raised up to them David as king: and he testified of him, and said: I have found David the son of Jesse, a man after my heart: he will do all my pleasure.
23 “Kutoka uzao wa mtu huyu, Mungu amewaletea Israeli Mwokozi Yesu, kama alivyoahidi.
From the seed of this man, hath God raised up to Israel, as he promised, Jesus a deliverer.
24 Kabla ya kuja kwa Yesu, Yohana alihubiri toba na ubatizo kwa watu wote wa Israeli.
And, before his advent, he sent John to proclaim the baptism of repentance to all the people of Israel.
25 Yohana alipokuwa anakamilisha kazi yake, alisema: ‘Ninyi mnadhani mimi ni nani? Mimi si yeye. La hasha, lakini yeye yuaja baada yangu, ambaye mimi sistahili kufungua kamba za viatu vya miguu yake.’
And while John was fulfilling his ministry, he said: Who, suppose ye, that I am? I am not he. But lo, he cometh after me; of whom I am not worthy to untie his shoe-strings.
26 “Ndugu zangu, wana wa Abrahamu, nanyi watu wa Mataifa mnaomcha Mungu, ujumbe huu wa wokovu umeletwa kwetu.
Men, brethren, children of the stock of Abraham, and all who, with you, fear God, to you is this word of life sent.
27 Kwa sababu wakaao Yerusalemu na viongozi wao hawakumtambua wala kuelewa maneno ya manabii yasomwayo kila Sabato, bali waliyatimiza maneno hayo kwa kumhukumu yeye.
For, those inhabitants of Jerusalem and their chiefs, did not apprehend it; neither did they apprehend also the writings of the prophets, which are read every sabbath; but they condemned him, and fulfilled all the things written.
28 Ijapokuwa hawakupata sababu yoyote ya kumhukumu kifo, walimwomba Pilato aamuru auawe.
And while they found no ground for his death, they desired of Pilate that they might kill him.
29 Walipokwisha kufanya yale yote yaliyoandikwa kumhusu, walimshusha kutoka msalabani na kumzika kaburini.
And when they had fulfilled all that was written concerning him, they took him down from the cross, and laid him in a sepulchre.
30 Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu.
But God raised him from the dead.
31 Naye kwa siku nyingi akawatokea wale waliokuwa pamoja naye kuanzia Galilaya hadi Yerusalemu. Nao sasa wamekuwa mashahidi wake kwa watu wetu.
And he was seen many days, by them who came up with him from Galilee to Jerusalem; and they are now his witnesses to the people.
32 “Nasi tunawaletea habari njema, kwamba yale Mungu aliyowaahidi baba zetu
And lo, we also announce to you, that the promise, which was made to our fathers,
33 sasa ameyatimiza kwetu sisi watoto wao, kwa kumfufua Yesu, kama ilivyoandikwa katika Zaburi ya pili: “‘Wewe ni Mwanangu; leo mimi nimekuzaa.’
lo, God hath fulfilled it to us their children, in that he raised up Jesus; as it is written in the second psalm: Thou art my Son; this day have I begotten thee.
34 Kwa kuwa Mungu alimfufua kutoka kwa wafu asioze kamwe, alitamka maneno haya: “‘Nitakupa wewe baraka takatifu zilizo za hakika nilizomwahidi Daudi.’
And God hath so raised him from the dead, that he will not return again and see corruption; as he said: I will give to you the sure grace of David.
35 Kama ilivyosemwa mahali pengine katika Zaburi, “‘Hutamwacha Aliye Mtakatifu wako kuona uharibifu.’
And again he said, in another place: Thou hast not given thy devout one to see corruption.
36 “Kwa maana Daudi akiisha kulitumikia kusudi la Mungu katika kizazi chake, alilala; akazikwa pamoja na baba zake na mwili wake ukaoza.
For David, in his generation, served the pleasure of God, and went to rest, and was added to his fathers, and saw corruption.
37 Lakini yule ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu hakuona uharibifu.
But this person, whom God raised up, did not see corruption.
38 “Kwa hiyo ndugu zangu, nataka ninyi mjue kwamba kwa kupitia huyu Yesu msamaha wa dhambi unatangazwa kwenu.
Know therefore, brethren, that through this man remission of sins is proclaimed to you.
39 Kwa kupitia yeye, kila mtu amwaminiye anahesabiwa haki kwa kila kitu ambacho asingeweza kuhesabiwa haki kwa sheria ya Mose.
And every one that believeth in this man, is made just from all things, from which ye could not be made just by the law of Moses.
40 Kwa hiyo jihadharini ili yale waliyosema manabii yasiwapate:
Beware, therefore, lest that come upon you, which is written in the prophets:
41 “‘Angalieni, enyi wenye dhihaka, mkastaajabu, mkaangamie, kwa maana nitatenda jambo wakati wenu ambalo hamtasadiki, hata kama mtu akiwaambia.’”
Behold, ye despisers, and wonder, and perish; for I work a work in your days, which ye will not believe, though a man relate it to you.
42 Paulo na Barnaba walipokuwa wakitoka nje ya sinagogi, watu wakawaomba wazungumze tena mambo hayo Sabato iliyofuata.
And when they had gone from them, they besought them to speak the same things to them the next sabbath day.
43 Baada ya kusanyiko la Sinagogi kutawanyika, wengi wa Wayahudi na waongofu wa dini ya Kiyahudi wakawafuata Paulo na Barnaba, wakazungumza nao na kuwahimiza wadumu katika neema ya Mungu.
And when the synagogue was dismissed, many Jews went after them, and likewise proselytes who feared God. And they conversed with them, and persuaded them to adhere to the grace of God.
44 Sabato iliyofuata, karibu watu wote wa mji walikuja kusikiliza neno la Bwana.
And the next sabbath, the whole city assembled to hear the word of God.
45 Lakini Wayahudi walipoona ule umati mkubwa wa watu walijawa na wivu, wakayakanusha maneno Paulo aliyokuwa akisema.
And when the Jews saw the great assembly, they were filled with envy, and set them selves against the words which Paul spoke, and blasphemed.
46 Ndipo Paulo na Barnaba wakawajibu kwa ujasiri, wakisema, “Ilitupasa kunena nanyi neno la Mungu kwanza. Lakini kwa kuwa mmelikataa, mkajihukumu wenyewe kuwa hamstahili uzima wa milele, sasa tunawageukia watu wa Mataifa. (aiōnios )
And Paul and Barnabas said openly: To you first, ought the word of God to be spoken; but because ye repel it from you, and decide, against yourselves, that ye are not worthy of life eternal, lo, we turn ourselves to the Gentiles. (aiōnios )
47 Kwa maana hili ndilo Bwana alilotuamuru: “‘Nimewafanya ninyi kuwa nuru kwa watu wa Mataifa, ili mpate kuuleta wokovu hadi miisho ya dunia.’”
For so hath our Lord commanded us; as it is written: I have set thee a light to the Gentiles; that thou shouldst be for life unto the ends of the earth.
48 Watu wa Mataifa waliposikia haya wakafurahi na kulitukuza neno la Bwana; nao wote waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini. (aiōnios )
And when the Gentiles heard this, they rejoiced and glorified God. And those believed, who were appointed to life eternal. (aiōnios )
49 Neno la Bwana likaenea katika eneo lile lote.
And the word of the Lord was talked of in all that region.
50 Lakini Wayahudi wakawachochea wanawake wenye kumcha Mungu, wenye vyeo pamoja na watu maarufu katika mji, wakachochea mateso dhidi ya Paulo na Barnaba na kuwafukuza kutoka eneo hilo.
But the Jews stirred up the chiefs of the city, and the opulent women who with them feared God, and set up a persecution against Paul and against Barnabas, and expelled them from their borders.
51 Hivyo Paulo na Barnaba wakakungʼuta mavumbi ya miguu yao ili kuwapinga, nao wakaenda Ikonio.
And when they went out, they shook off the dust of their feet against them, and went to the city of Iconium.
52 Wanafunzi wakajawa na furaha na Roho Mtakatifu.
And the disciples were filled with joy, and with the Holy Spirit.