< Matendo 12 >
1 Wakati huo huo Mfalme Herode Agripa aliwakamata baadhi ya watu wa kanisa.
Now, about that time, Herod, the king, laid hands on some of the congregation, to afflict them.
2 Akaamuru Yakobo, ndugu yake Yohana, auawe kwa upanga.
And he slew James, the brother of John, with the sword.
3 Alipoona jambo hilo limewapendeza Wayahudi, akaendelea, akamkamata pia Petro. Hii ilitokea wakati wa Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu.
And as he saw that this was acceptable to the Jews, he went on to seize Peter also: and it was in the days of unleavened bread;
4 Baada ya kumkamata alimtia gerezani, chini ya ulinzi wa vikundi vinne vya askari, vyenye askari wanne kila kimoja. Herode alikuwa amekusudia kumtoa na kumfanyia mashtaka mbele ya watu baada ya Pasaka.
and having seized him, he put him in prison, delivering him to the custody of four quaternions of soldiers, intending, after the passover, to bring him out to the people.
5 Kwa hiyo Petro akawekwa gerezani, lakini kanisa lilikuwa likimwombea kwa Mungu kwa bidii.
In the meantime, therefore, Peter was kept in the prison; but earnest and continued prayer was made to God on his account, by the congregation.
6 Usiku ule kabla ya siku ambayo Herode Agripa alikuwa amekusudia kumtoa na kumfanyia mashtaka, Petro alikuwa amelala kati ya askari wawili, akiwa amefungwa kwa minyororo miwili. Nao walinzi wa zamu walikuwa wakilinda penye lango la gereza.
And when Herod was ready to have brought him out, even that very night, Peter was sleeping between two soldiers, bound with two chains; and the guards before the door were keeping the prison.
7 Ghafula malaika wa Bwana akatokea na nuru ikamulika mle ndani ya gereza. Yule malaika akampiga Petro ubavuni na kumwamsha, akisema, “Ondoka upesi!” Mara ile minyororo ikaanguka kutoka mikononi mwa Petro.
And, behold, a messenger of the Lord presented himself, and a light shone in the house; giving Peter a blow on the side, he awoke him, saying, Arise quickly: and his chains fell off from his hands.
8 Yule malaika akamwambia, “Vaa nguo zako na viatu vyako.” Petro akafanya hivyo. Kisha akamwambia, “Jifunge vazi lako na unifuate.”
And the messenger said to him, Gird yourself, and bind on your sandals; and he did so. And he said to him, Throw your mantle round you, and follow me.
9 Petro akatoka mle gerezani akiwa amefuatana na yule malaika. Hakujua wakati huo kuwa yaliyokuwa yakitukia yalikuwa kweli. Alidhani kuwa anaona maono.
And going out he followed him; and he did not know that what was done by the messenger was real; but supposed that he had seen a vision.
10 Wakapita lindo la kwanza na la pili, ndipo wakafika kwenye lango la chuma linaloelekea mjini. Lango likawafungukia lenyewe, nao wakapita hapo wakatoka nje. Baada ya kutembea umbali wa mtaa mmoja, ghafula yule malaika akamwacha Petro.
And passing through the first and second watch, they came to the iron gate that leads into the city; which opened to them of its own accord. And going out, they went through one street, and immediately the messenger departed from him.
11 Ndipo Petro akarudiwa na fahamu, akasema, “Sasa ninajua bila shaka yoyote kuwa Bwana amemtuma malaika wake na kuniokoa kutoka makucha ya Herode Agripa na kutoka matazamio yote ya Wayahudi.”
And Peter, being come to himself, said, Now I know truly, that the Lord has sent his messenger, and has delivered me from the hand of Herod, and from all the expectations of the Jewish people.
12 Mara Petro alipotambua hili alikwenda nyumbani kwa Maria, mama yake Yohana aliyeitwa pia Marko, ambako watu wengi walikuwa wamekutana kwa maombi.
And recollecting, he came to the house of Mary, the mother of John, who was surnamed Mark; where many were gathered together, praying.
13 Petro alipobisha hodi kwenye lango la nje, mtumishi wa kike jina lake Roda, akaja kumfungulia.
And as Peter knocked at the door of the outer gate, a maiden, whose name was Rose, went to inquire who was there.
14 Alipoitambua sauti ya Petro, alifurahi mno akarudi bila kufungua na kuwaeleza kwamba, “Petro yuko langoni!”
And knowing Peter's voice, transported with joy, she did not open the gate: but running in, told them that Peter was standing at the gate.
15 Wakamwambia yule mtumishi wa kike, “Umerukwa na akili.” Alipozidi kusisitiza kuwa ni kweli, wakasema, “Lazima awe ni malaika wake.”
And they said to her, You are distracted: but she confidently affirmed that it was so.
16 Lakini Petro aliendelea kugonga langoni, nao walipofungua lango na kumwona Petro, walistaajabu sana.
But Peter continued knocking; and when she opened the door, they saw him, and were astonished.
17 Yeye akawaashiria kwa mkono wake wanyamaze kimya, akawaeleza jinsi Bwana alivyomtoa gerezani. Naye akaongeza kusema, “Waelezeni Yakobo na ndugu wengine habari hizi.” Kisha akaondoka akaenda sehemu nyingine.
And he made a sign to them with his hand to be silent; and related to them how the Lord had conducted him out of prison. And he aid, Inform James and the brethren of these things: and departing, he went to another place.
18 Kulipokucha kukawa na fadhaa kubwa miongoni mwa wale askari kuhusu yaliyomtukia Petro.
And as soon as it was day, there was no small tumult among the soldiers, what was become of Peter.
19 Baada ya Herode kuamuru atafutwe kila mahali na bila kumpata, aliwahoji wale askari walinzi kisha akatoa amri wauawe. Basi Herode Agripa akatoka Uyahudi akaenda Kaisaria, akakaa huko kwa muda.
And Herod searching for him, and not finding him, examined the keeper, and ordered them to be led away to execution. and passing from Judea to Cesarea, he abode there.
20 Basi Herode Agripa alikuwa amekasirishwa sana na watu wa Tiro na Sidoni. Hivyo watu wa miji hiyo miwili wakaungana pamoja wakatafuta kukutana naye. Wakiisha kuungwa mkono na Blasto, mtumishi maalum wa Mfalme Herode Agripa aliyeaminika, wakaomba mapatano ya amani maana nchi zao zilitegemea nchi ya huyo mfalme kwa mahitaji yao ya chakula.
And he was highly incensed against the Tyrians and Sidonians; but they unanimously came before him; and gaining Blastus, the king's chamberlain, to their interest, they begged for peace; because their country was nourished by that of the king.
21 Katika siku iliyochaguliwa Herode Agripa akavaa mavazi yake ya kifalme, akaketi kwenye kiti chake cha enzi na kuwahutubia watu.
And upon a set day, Herod, being arrayed in a royal habit, and seated upon the throne, made an oration to them.
22 Watu waliokuwa wamekusanyika wakapiga kelele, wakisema, “Hii si sauti ya mwanadamu, bali ni ya Mungu.”
And the people cried out, It is the voice of a God, and not of a man!
23 Ghafula, kwa kuwa Herode hakumpa Mungu utukufu, malaika wa Bwana akampiga, naye akaliwa na chango, akafa.
But immediately a messenger of the Lord smote him, because he did not give glory to God: and being eaten with worms, he expired.
24 Lakini neno la Mungu likaendelea mbele na kuenea, nao wengi wakaambatana nalo.
And the word of God grew and was multiplied.
25 Barnaba na Sauli walipomaliza ile huduma yao iliyowapeleka, wakarudi Yerusalemu wakiwa pamoja na Yohana aitwaye Marko.
And Barnabas and Saul, having fulfilled their ministry, returned from Jerusalem; bringing along with them John, whose surname was Mark.