< Matendo 11 >
1 Mitume na ndugu walioamini waliokuwa huko Uyahudi wakasikia kuwa watu wa Mataifa nao wamepokea neno la Mungu.
Now the apostles and brethren that were in Judea heard that the Gentiles also had received the word of God.
2 Hivyo Petro alipopanda Yerusalemu, wale wa tohara waliokuwa wameamini wakamshutumu,
And when Peter was come up to Jerusalem, those that were of the circumcision contended with him, saying,
3 wakisema, “Ulikwenda kwa watu wasiotahiriwa na kula pamoja nao.”
Thou wentest in to men uncircumcised and didst eat with them.
4 Ndipo Petro akaanza kuwaeleza kuhusu mambo yote yalivyotokea hatua kwa hatua akisema,
But Peter began and laid the matter in order before them,
5 “Nilikuwa katika mji wa Yafa nikiomba, nami nikapitiwa na usingizi wa ghafula, nikaona maono. Kulikuwa na kitu kama nguo kubwa ikishuka kutoka mbinguni, ikishushwa kwa ncha zake nne, nayo ikanikaribia.
saying, I was praying in the city of Joppa; and in a trance I saw a vision, some thing like a large sheet descending from heaven, let down by the four corners; and it came close to me.
6 Nilipoangalia ndani yake kwa karibu niliona wanyama wenye miguu minne wa nchini, wanyama wa mwitu, watambaao na ndege wa angani.
And looking stedfastly upon it, I observed four-footed creatures and wild beasts, and reptiles, and fowls of the air.
7 Ndipo nikasikia sauti ikiniambia, ‘Petro, ondoka uchinje na ule.’
And I heard a voice saying to me, Rise, Peter, kill and eat.
8 “Nikajibu, ‘La hasha Bwana! Kitu chochote kilicho najisi hakijaingia kinywani mwangu.’
But I said, By no means, Lord: for nothing polluted or unclean hath ever entered into my mouth.
9 “Sauti ikasema kutoka mbinguni mara ya pili, ‘Usikiite najisi kitu chochote Mungu alichokitakasa.’
And the voice answered me a second time from heaven, What God hath cleansed do not thou call polluted.
10 Jambo hili lilitokea mara tatu, ndipo kile kitu kikavutwa tena mbinguni.
And this was done thrice: and then they were all drawn up again to heaven.
11 “Wakati ule ule watu watatu, waliokuwa wametumwa kutoka Kaisaria waliwasili katika nyumba niliyokuwa nikikaa.
And behold at that very time there came three men to the house where I was, sent from Cesarea to me.
12 Roho Mtakatifu akaniambia niende nao bila kuwa na ubaguzi kati yao na sisi. Hawa ndugu sita pia walifuatana nami, nasi tukaingia nyumbani mwa huyo Kornelio.
And the Spirit ordered me to go with them, doubting nothing. And these six brethren also came with me, and we entred into the man's house;
13 Akatuambia jinsi alivyoona malaika aliyekuwa amesimama katika nyumba yake na kusema, ‘Tuma watu waende Yafa wakamlete Simoni aitwaye Petro.
and he told us how he had seen an angel in his house, standing and saying to him, Send men to Joppa, and fetch hither Simon,
14 Yeye atakupa ujumbe ambao kwa huo wewe na wa nyumbani mwako wote mtaokoka.’
whose sirname is Peter, who will tell thee things, by which thou shalt be saved and all thy family.
15 “Nami nilipoanza kusema, Roho Mtakatifu akashuka juu yao kama vile alivyotushukia sisi hapo mwanzo.
And when I began to speak, the holy Spirit fell on them, even as it did upon us at the beginning.
16 Nami nikakumbuka neno la Bwana alivyosema, ‘Yohana alibatiza kwa maji, lakini ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu.’
Then I remembered the word of the Lord, how He said, John indeed baptized with water; but ye shall be baptized with the holy Spirit.
17 Basi ikiwa Mungu aliwapa hawa watu kipawa kile kile alichotupa sisi tuliomwamini Bwana Yesu Kristo, mimi ni nani hata nifikirie kuwa ningeweza kumpinga Mungu?”
As therefore God gave to them the like gift that He did to us, upon our believing on the Lord Jesus Christ, who was I, that I should be able to withstand God?
18 Waliposikia haya hawakuwa na la kupinga zaidi. Nao wakamwadhimisha Mungu wakisema, “Basi, Mungu amewapa hata watu wa Mataifa toba iletayo uzima wa milele.”
And when they heard these things they acquiesced, and glorified God, saying, Then hath God given to the Gentiles also repentance unto life.
19 Basi wale waliotawanyika kwa ajili ya mateso yaliyotokana na kifo cha Stefano, wakasafiri hadi Foinike na Kipro na Antiokia. Nao hawakuhubiri lile Neno kwa mtu yeyote isipokuwa Wayahudi.
Now they that were dispersed by the trouble, which arose about Stephen, travelled as far as Phenicia, and Cyprus, and Antioch, preaching the word to none but the Jews only.
20 Lakini baadhi yao walikuwepo watu wa Kipro na Kirene, ambao walipokuja Antiokia walinena na Wayunani pia wakiwahubiria habari njema za Bwana Yesu.
But some of them were Cyprians, and Cyrenians, who when they came to Antioch, discoursed with the Grecians also, preaching the Lord Jesus.
21 Mkono wa Bwana ulikuwa pamoja nao, nayo idadi kubwa ya watu wakaamini na kumgeukia Bwana.
And the hand of the Lord was with them, and a great number believed, and turned unto the Lord.
22 Habari hizi zilipofika masikioni mwa kanisa huko Yerusalemu, wakamtuma Barnaba aende Antiokia.
And the report of these things came to the ears of the church in Jerusalem; and they sent Barnabas to Antioch.
23 Alipofika na kuona madhihirisho ya neema ya Mungu, akafurahi na kuwatia moyo waendelee kuwa waaminifu kwa Bwana kwa mioyo yao yote.
Who, when he was come, and saw the grace of God, rejoiced, and exhorted them all with steadiness of heart to adhere to the Lord.
24 Barnaba alikuwa mtu mwema, aliyejaa Roho Mtakatifu, mwenye imani, nayo idadi kubwa ya watu wakaongezeka kwa Bwana.
For he was a good man, and full of the holy Spirit, and of faith: and many were added unto the Lord.
25 Kisha Barnaba akaenda Tarso kumtafuta Sauli,
Then Barnabas departed to Tarsus, to seek Saul: and when he found him, he brought him to Antioch.
26 naye alipompata akamleta Antiokia. Hivyo kwa mwaka mzima Barnaba na Sauli wakakutana na kanisa na kufundisha idadi kubwa ya watu. Ilikuwa ni katika kanisa la Antiokia kwa mara ya kwanza wanafunzi waliitwa Wakristo.
And they assembled in the church a whole year, and taught much people: and the disciples were first called Christians at Antioch.
27 Wakati huo manabii walishuka toka Yerusalemu hadi Antiokia.
And in these days came down prophets from Jerusalem to Antioch.
28 Mmoja wao, jina lake Agabo, akasimama akatabiri kwa uweza wa Roho Mtakatifu kwamba njaa kubwa itaenea ulimwengu mzima. Njaa hiyo ilitokea wakati wa utawala wa Klaudio.
And one of them, named Agabus, stood up and signified by the Spirit, that there would be a great famine over all the earth: which accordingly came to pass in the reign of Claudius Cesar.
29 Mitume wakaamua kwamba kila mtu, kulingana na uwezo alio nao, atoe msaada kwa ajili ya ndugu wanaoishi Uyahudi.
And each of the disciples, according to his ability, determined to send relief to the brethren who dwelt in Judea.
30 Wakafanya hivyo, misaada yao ikapelekwa kwa wazee kwa mikono ya Barnaba na Sauli.
Which they also did, sending it to the elders by the hand of Barnabas and Saul.