< Matendo 11 >

1 Mitume na ndugu walioamini waliokuwa huko Uyahudi wakasikia kuwa watu wa Mataifa nao wamepokea neno la Mungu.
Now the Apostles and the brethren who were throughout Judaea heard that, the nations also, had welcomed the word of God.
2 Hivyo Petro alipopanda Yerusalemu, wale wa tohara waliokuwa wameamini wakamshutumu,
And, when Peter came up unto Jerusalem, they of the circumcision began to find fault with him,
3 wakisema, “Ulikwenda kwa watu wasiotahiriwa na kula pamoja nao.”
Saying—he went in unto men uncircumcised, and did eat with them.
4 Ndipo Petro akaanza kuwaeleza kuhusu mambo yote yalivyotokea hatua kwa hatua akisema,
But Peter, making a beginning, went on to set forth the matter unto them in order, saying—
5 “Nilikuwa katika mji wa Yafa nikiomba, nami nikapitiwa na usingizi wa ghafula, nikaona maono. Kulikuwa na kitu kama nguo kubwa ikishuka kutoka mbinguni, ikishushwa kwa ncha zake nne, nayo ikanikaribia.
I was in the city of Joppa praying, and saw in a trance, a vision: —coming down a sort of vessel, like a large sheet, by four corners, being let down out of heaven, and it came even unto me:
6 Nilipoangalia ndani yake kwa karibu niliona wanyama wenye miguu minne wa nchini, wanyama wa mwitu, watambaao na ndege wa angani.
Into which steadfastly looking, began to observe, and saw the quadrupeds of the earth, and the wild beasts, and the creeping things, and the birds of heaven.
7 Ndipo nikasikia sauti ikiniambia, ‘Petro, ondoka uchinje na ule.’
Moreover heard a voice also, saying unto me—Rise, Peter! slay and eat.
8 “Nikajibu, ‘La hasha Bwana! Kitu chochote kilicho najisi hakijaingia kinywani mwangu.’
But I said—By no means, Lord, because, a common or unclean thing, hath at no time entered into my mouth.
9 “Sauti ikasema kutoka mbinguni mara ya pili, ‘Usikiite najisi kitu chochote Mungu alichokitakasa.’
And a voice answered, a second time, out of heaven—What things, God, hath cleansed, be not, thou, making common.
10 Jambo hili lilitokea mara tatu, ndipo kile kitu kikavutwa tena mbinguni.
And, this, took place thrice, —and the whole was drawn up again into heaven;
11 “Wakati ule ule watu watatu, waliokuwa wametumwa kutoka Kaisaria waliwasili katika nyumba niliyokuwa nikikaa.
And lo! immediately, three men halted at the house wherein we were, sent from Caesarea unto me.
12 Roho Mtakatifu akaniambia niende nao bila kuwa na ubaguzi kati yao na sisi. Hawa ndugu sita pia walifuatana nami, nasi tukaingia nyumbani mwa huyo Kornelio.
And the Spirit bade me go with them, nothing doubting. And there went with me these six brethren also; and we entered into the house of the man,
13 Akatuambia jinsi alivyoona malaika aliyekuwa amesimama katika nyumba yake na kusema, ‘Tuma watu waende Yafa wakamlete Simoni aitwaye Petro.
And he related to us how he had seen the messenger in his house, standing, and saying—Send away unto Joppa, and fetch Simon, who is surnamed Peter;
14 Yeye atakupa ujumbe ambao kwa huo wewe na wa nyumbani mwako wote mtaokoka.’
Who shall speak words unto thee, whereby thou shall be saved, thou, and all thy house.
15 “Nami nilipoanza kusema, Roho Mtakatifu akashuka juu yao kama vile alivyotushukia sisi hapo mwanzo.
And, as I began to be speaking, the Holy Spirit fell upon them, just as upon us also at the beginning.
16 Nami nikakumbuka neno la Bwana alivyosema, ‘Yohana alibatiza kwa maji, lakini ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu.’
And I was put in mind of the word of the Lord, how he used to say—John, indeed, immersed with water; but, ye, shall be immersed in Holy Spirit.
17 Basi ikiwa Mungu aliwapa hawa watu kipawa kile kile alichotupa sisi tuliomwamini Bwana Yesu Kristo, mimi ni nani hata nifikirie kuwa ningeweza kumpinga Mungu?”
If therefore the like free-gift God gave unto them, as even unto us, when we had believed upon the Lord Jesus Christ, who was, I, that could withstand God?
18 Waliposikia haya hawakuwa na la kupinga zaidi. Nao wakamwadhimisha Mungu wakisema, “Basi, Mungu amewapa hata watu wa Mataifa toba iletayo uzima wa milele.”
And, having heard these things, they held their peace, and glorified God, saying—Hence, even unto the nations, God hath granted repentance unto life.
19 Basi wale waliotawanyika kwa ajili ya mateso yaliyotokana na kifo cha Stefano, wakasafiri hadi Foinike na Kipro na Antiokia. Nao hawakuhubiri lile Neno kwa mtu yeyote isipokuwa Wayahudi.
They, therefore, who had been scattered abroad by reason of the tribulation that took place on account of Stephen, passed through as far as Phoenice and Cyprus and Antioch, unto no one speaking the word, save alone unto Jews.
20 Lakini baadhi yao walikuwepo watu wa Kipro na Kirene, ambao walipokuja Antiokia walinena na Wayunani pia wakiwahubiria habari njema za Bwana Yesu.
And there were some from among them, Cyprians and Cyrenians, who, indeed, coming unto Antioch, began speaking, even unto the Grecian Jews, announcing the glad tidings as to the Lord Jesus;
21 Mkono wa Bwana ulikuwa pamoja nao, nayo idadi kubwa ya watu wakaamini na kumgeukia Bwana.
And the hand of the Lord was with them, and a great number—they who believed—turned unto the Lord.
22 Habari hizi zilipofika masikioni mwa kanisa huko Yerusalemu, wakamtuma Barnaba aende Antiokia.
And the matter was reported in the hearing of the assembly that was in Jerusalem, concerning them; and they sent forth Barnabas, as far as Antioch;
23 Alipofika na kuona madhihirisho ya neema ya Mungu, akafurahi na kuwatia moyo waendelee kuwa waaminifu kwa Bwana kwa mioyo yao yote.
Who, arriving, and seeing the favour which was of God, rejoiced, and went on to beseech all, with the purpose of their heart, to abide [in] the Lord;
24 Barnaba alikuwa mtu mwema, aliyejaa Roho Mtakatifu, mwenye imani, nayo idadi kubwa ya watu wakaongezeka kwa Bwana.
Because he was a good man, and full of Holy Spirit and faith; and a considerable multitude were added unto the Lord.
25 Kisha Barnaba akaenda Tarso kumtafuta Sauli,
He went away, however, unto Tarsus, to seek up Saul;
26 naye alipompata akamleta Antiokia. Hivyo kwa mwaka mzima Barnaba na Sauli wakakutana na kanisa na kufundisha idadi kubwa ya watu. Ilikuwa ni katika kanisa la Antiokia kwa mara ya kwanza wanafunzi waliitwa Wakristo.
And, finding him, he brought him unto Antioch. And so it was with them, that, for a whole year, they were brought together in the assembly, and taught a considerable multitude; also that the disciples, first in Antioch, were called, Christians.
27 Wakati huo manabii walishuka toka Yerusalemu hadi Antiokia.
Now, in these days, there came down from Jerusalem, prophets, unto Antioch.
28 Mmoja wao, jina lake Agabo, akasimama akatabiri kwa uweza wa Roho Mtakatifu kwamba njaa kubwa itaenea ulimwengu mzima. Njaa hiyo ilitokea wakati wa utawala wa Klaudio.
And one from among them, by name Agabus, rising up, gave a sign, through means of the Spirit, that, a great famine, was coming over all the inhabited earth; which, indeed, came to pass under Claudius.
29 Mitume wakaamua kwamba kila mtu, kulingana na uwezo alio nao, atoe msaada kwa ajili ya ndugu wanaoishi Uyahudi.
And, according as any one of the disciples was being prospered, they each one of them set apart [something] for ministering, to send unto the brethren, who dwelt in Jerusalem; —
30 Wakafanya hivyo, misaada yao ikapelekwa kwa wazee kwa mikono ya Barnaba na Sauli.
Which thing they also did, sending it unto the Elders, through the hand of Barnabas and Saul.

< Matendo 11 >