< Matendo 11 >

1 Mitume na ndugu walioamini waliokuwa huko Uyahudi wakasikia kuwa watu wa Mataifa nao wamepokea neno la Mungu.
And the apostles and brethren that were in Judea, heard that the Gentiles also had received the word of God.
2 Hivyo Petro alipopanda Yerusalemu, wale wa tohara waliokuwa wameamini wakamshutumu,
And when Peter went up to Jerusalem, those who were of the circumcision contended with him,
3 wakisema, “Ulikwenda kwa watu wasiotahiriwa na kula pamoja nao.”
saying: You went in to uncircumcised men, and ate with them.
4 Ndipo Petro akaanza kuwaeleza kuhusu mambo yote yalivyotokea hatua kwa hatua akisema,
And Peter began, and laid the matter before them in order, saying:
5 “Nilikuwa katika mji wa Yafa nikiomba, nami nikapitiwa na usingizi wa ghafula, nikaona maono. Kulikuwa na kitu kama nguo kubwa ikishuka kutoka mbinguni, ikishushwa kwa ncha zake nne, nayo ikanikaribia.
I was in the city of Joppa, praying; and, while in a trance, I saw a vision, some vessel like a great sheet, descending, let down from heaven by the four corners; and it came even to me.
6 Nilipoangalia ndani yake kwa karibu niliona wanyama wenye miguu minne wa nchini, wanyama wa mwitu, watambaao na ndege wa angani.
When I had looked attentively into it, I observed and saw four-footed beasts of the earth, and wild beasts and creeping things and birds of the air.
7 Ndipo nikasikia sauti ikiniambia, ‘Petro, ondoka uchinje na ule.’
And I heard a voice saying to me, Rise, Peter, kill and eat.
8 “Nikajibu, ‘La hasha Bwana! Kitu chochote kilicho najisi hakijaingia kinywani mwangu.’
But I said, By no means, Lord; for nothing common or unclean has ever entered my mouth.
9 “Sauti ikasema kutoka mbinguni mara ya pili, ‘Usikiite najisi kitu chochote Mungu alichokitakasa.’
But the voice answered me a second time from heaven, What God has cleansed, you must not call common.
10 Jambo hili lilitokea mara tatu, ndipo kile kitu kikavutwa tena mbinguni.
This was done the third time, and all was drawn up again into heaven.
11 “Wakati ule ule watu watatu, waliokuwa wametumwa kutoka Kaisaria waliwasili katika nyumba niliyokuwa nikikaa.
And behold, three men who had been sent to me from Cæsarea, immediately came to the house where I was.
12 Roho Mtakatifu akaniambia niende nao bila kuwa na ubaguzi kati yao na sisi. Hawa ndugu sita pia walifuatana nami, nasi tukaingia nyumbani mwa huyo Kornelio.
And the Spirit commanded me to go with them without hesitation. And these six brethren accompanied me. And we entered the man’s house:
13 Akatuambia jinsi alivyoona malaika aliyekuwa amesimama katika nyumba yake na kusema, ‘Tuma watu waende Yafa wakamlete Simoni aitwaye Petro.
and he told us how he had seen an angel in his house, standing and saying to him, Send to Joppa and call for Simon, who is surnamed Peter;
14 Yeye atakupa ujumbe ambao kwa huo wewe na wa nyumbani mwako wote mtaokoka.’
he will tell you words by which you and all your house shall be saved.
15 “Nami nilipoanza kusema, Roho Mtakatifu akashuka juu yao kama vile alivyotushukia sisi hapo mwanzo.
And as I began to speak, the Holy Spirit fell on them, as on us at the beginning.
16 Nami nikakumbuka neno la Bwana alivyosema, ‘Yohana alibatiza kwa maji, lakini ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu.’
Then I remembered the word of the Lord, as he said, John immersed in water, but you shall be immersed in the Holy Spirit.
17 Basi ikiwa Mungu aliwapa hawa watu kipawa kile kile alichotupa sisi tuliomwamini Bwana Yesu Kristo, mimi ni nani hata nifikirie kuwa ningeweza kumpinga Mungu?”
If, then, God gave them the like gift that he gave to us who believed on the Lord Jesus Christ, what was I, that I could withstand God?
18 Waliposikia haya hawakuwa na la kupinga zaidi. Nao wakamwadhimisha Mungu wakisema, “Basi, Mungu amewapa hata watu wa Mataifa toba iletayo uzima wa milele.”
And when they heard these things, they ceased to contend; and they glorified God, saying: Then, indeed, has God given to the Gentiles also repentance in order to life.
19 Basi wale waliotawanyika kwa ajili ya mateso yaliyotokana na kifo cha Stefano, wakasafiri hadi Foinike na Kipro na Antiokia. Nao hawakuhubiri lile Neno kwa mtu yeyote isipokuwa Wayahudi.
Now those who had been dispersed by the persecution that arose after the death of Stephen, traveled as far as Phenicia and Cyprus and Antioch, speaking the word to none but Jews.
20 Lakini baadhi yao walikuwepo watu wa Kipro na Kirene, ambao walipokuja Antiokia walinena na Wayunani pia wakiwahubiria habari njema za Bwana Yesu.
But some of them were men of Cyprus and Cyrene, who, when they had come to Antioch, spoke to the Grecians, preaching the Lord Jesus.
21 Mkono wa Bwana ulikuwa pamoja nao, nayo idadi kubwa ya watu wakaamini na kumgeukia Bwana.
And the hand of the Lord was with them, and a great number believed, and turned to the Lord.
22 Habari hizi zilipofika masikioni mwa kanisa huko Yerusalemu, wakamtuma Barnaba aende Antiokia.
And the report concerning them came to the ears of the church that was in Jerusalem; and they sent out Barnabas to go as far as Antioch.
23 Alipofika na kuona madhihirisho ya neema ya Mungu, akafurahi na kuwatia moyo waendelee kuwa waaminifu kwa Bwana kwa mioyo yao yote.
When he had come, and had seen the grace of God, he rejoiced; and he exhorted them all to remain, with purpose of heart, faithful to the Lord.
24 Barnaba alikuwa mtu mwema, aliyejaa Roho Mtakatifu, mwenye imani, nayo idadi kubwa ya watu wakaongezeka kwa Bwana.
For he was a good man, and full of the Holy Spirit and of faith. And a great multitude was added to the Lord.
25 Kisha Barnaba akaenda Tarso kumtafuta Sauli,
And Barnabas went to Tarsus, to seek for Saul;
26 naye alipompata akamleta Antiokia. Hivyo kwa mwaka mzima Barnaba na Sauli wakakutana na kanisa na kufundisha idadi kubwa ya watu. Ilikuwa ni katika kanisa la Antiokia kwa mara ya kwanza wanafunzi waliitwa Wakristo.
and when he had found him, he brought him to Antioch. And it came to pass, that they met together in the church for a whole year, and taught a great multitude; and the disciples were called Christians first at Antioch.
27 Wakati huo manabii walishuka toka Yerusalemu hadi Antiokia.
In those days prophets came from Jerusalem to Antioch.
28 Mmoja wao, jina lake Agabo, akasimama akatabiri kwa uweza wa Roho Mtakatifu kwamba njaa kubwa itaenea ulimwengu mzima. Njaa hiyo ilitokea wakati wa utawala wa Klaudio.
And one of them, named Agabus, rose and made known, by the Spirit, that a great famine was about to come on the whole habitable land; which took place in the days of Claudius.
29 Mitume wakaamua kwamba kila mtu, kulingana na uwezo alio nao, atoe msaada kwa ajili ya ndugu wanaoishi Uyahudi.
And every one of the disciples determined, as he had the means, to send relief to the brethren that dwelt in Judea;
30 Wakafanya hivyo, misaada yao ikapelekwa kwa wazee kwa mikono ya Barnaba na Sauli.
which also they did; and they sent it to the elders by the hands of Barnabas and Saul.

< Matendo 11 >