< Matendo 10 >

1 Katika mji wa Kaisaria palikuwa na mtu jina lake Kornelio, ambaye alikuwa jemadari wa kile kilichojulikana kama kikosi cha Kiitalia.
Муж же некий бе в Кесарии, именем Корнилий, сотник от спиры нарицающияся Италийския,
2 Yeye alikuwa mcha Mungu pamoja na wote wa nyumbani mwake. Aliwapa watu sadaka nyingi na kumwomba Mungu daima.
благоговеин и бояйся Бога со всем домом своим, творяй милостыни многи людем и моляйся Богу всегда:
3 Siku moja alasiri, yapata saa tisa, aliona maono waziwazi, malaika wa Mungu akimjia na kumwambia, “Kornelio!”
виде в видении яве, яко в час девятый дне, Ангела Божия сшедша к нему и рекша ему: Корнилие.
4 Kornelio akamkazia macho kwa hofu akasema, “Kuna nini, Bwana?” Malaika akamwambia, “Sala zako na sadaka zako kwa maskini zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za Mungu.
Он же воззрев нань и пристрашен быв рече: что есть, Господи? Рече же ему: молитвы твоя и милостыни твоя взыдоша на память пред Бога:
5 Sasa tuma watu waende Yafa wakamwite mtu mmoja jina lake Simoni aitwaye Petro.
и ныне посли во Июппию мужей и призови Симона, нарицаемаго Петра:
6 Yeye anaishi na Simoni mtengenezaji ngozi ambaye nyumba yake iko kando ya bahari.”
сей странствует у некоего Симона усмаря, емуже есть дом при мори: той речет тебе глаголы, в нихже спасешися ты и весь дом твой.
7 Yule malaika aliyekuwa akizungumza naye alipoondoka, Kornelio akawaita watumishi wake wawili pamoja na askari mmoja mcha Mungu aliyekuwa miongoni mwa wale waliomtumikia.
И якоже отиде Ангел глаголяй Корнилию, пригласив два от рабов своих и воина благочестива от служащих ему
8 Akawaambia mambo yote yaliyotukia, kisha akawatuma waende Yafa.
и сказав им вся, посла их во Июппию.
9 Siku ya pili yake, walipokuwa wameukaribia mji, wakati wa adhuhuri, Petro alipanda juu ya nyumba kuomba.
Воутрие же, путьшествующым им и ко граду приближающымся, взыде Петр на горницу помолитися, о часе шестем.
10 Alipokuwa akiomba akahisi njaa, akatamani kupata chakula. Lakini wakati walikuwa wakiandaa chakula, akalala usingizi mzito sana.
Бысть же приалчен и хотяше вкусити: готовящым же онем, нападе нань ужас,
11 Akaona mbingu zimefunguka na kitu kama nguo kubwa kikishushwa duniani kwa ncha zake nne.
и виде небо отверсто и сходящ нань сосуд некий, яко плащаницу велию, по четырем краем привязан и низу спущаемь на землю,
12 Ndani yake walikuwepo aina zote za wanyama wenye miguu minne, nao watambaao nchini, na ndege wa angani.
в немже бяху вся четвероногая земли и зверие и гади и птицы небесныя.
13 Ndipo sauti ikamwambia “Petro, ondoka, uchinje na ule.”
И бысть глас к нему: востав, Петре, заколи и яждь.
14 Petro akajibu, “La hasha Bwana! Sijawahi kamwe kula kitu chochote kilicho najisi.”
Петр же рече: никакоже, Господи, яко николиже ядох всяко скверно или нечисто.
15 Ile sauti ikasema naye mara ya pili, “Usikiite najisi kitu chochote Mungu alichokitakasa.”
И (се) глас паки к нему вторицею: яже Бог очистил есть, ты не скверни.
16 Jambo hili lilitokea mara tatu na ghafula ile nguo ikarudishwa mbinguni.
Сие же бысть трищи: и паки взяся сосуд на небо.
17 Wakati Petro akiwa bado anajiuliza kuhusu maana ya maono haya, wale watu waliokuwa wametumwa na Kornelio wakaipata nyumba ya Simoni mtengenezaji wa ngozi wakawa wamesimama mbele ya lango.
Якоже в себе недоумевашеся Петр, что бы было видение, еже виде, и се, мужие посланнии от Корнилиа, вопрошше и уведевше дом Симонов, сташа пред враты
18 Wakabisha hodi na kuuliza kama Simoni aliyeitwa Petro alikuwa anaishi hapo.
и возглашше вопрошаху, аще Симон, нарицаемый Петр, зде странствует.
19 Wakati Petro akiwa anafikiria juu ya yale maono, Roho Mtakatifu akamwambia, “Simoni, wako watu watatu wanaokutafuta.
Петру же размышляющу о видении, рече ему Дух: се, мужие трие ищут тебе:
20 Inuka na ushuke, usisite kwenda nao kwa kuwa mimi nimewatuma.”
но востав сниди и иди с ними, ничтоже разсуждая: зане Аз послах их.
21 Petro akashuka na kuwaambia wale watu waliokuwa wametumwa kutoka kwa Kornelio, “Mimi ndiye mnayenitafuta. Mmekuja kwa sababu gani?”
Сошед же Петр к мужем посланным к нему от Корнилиа, рече: се, аз есмь, егоже ищете: кая есть вина, еяже ради приидосте?
22 Wale watu wakamjibu, “Tumetumwa na Kornelio yule jemadari. Yeye ni mtu mwema anayemcha Mungu, na anaheshimiwa na Wayahudi wote. Yeye ameagizwa na malaika mtakatifu akukaribishe nyumbani kwake, ili asikilize maneno utakayomwambia.”
Они же рекоша: Корнилий сотник, муж праведен и бояйся Бога, свидетелствован от всего языка Иудейска, увещен есть от Ангела свята призвати тя в дом свой и слышати глаголы от тебе.
23 Basi Petro akawakaribisha wakafuatana naye ndani, akawapa pa kulala. Kesho yake akaondoka pamoja nao, na baadhi ya ndugu kutoka Yafa wakafuatana naye.
Призвав же их учреди: наутрие же Петр востав иде с ними, и нецыи от братий, иже от Июппии, идоша с ним:
24 Siku iliyofuata wakawasili Kaisaria. Kornelio alikuwa akiwangoja pamoja na jamaa yake na marafiki zake wa karibu.
и наутрие внидоша в Кесарию. Корнилий же бе чая их, созвав сродники своя и любезныя други.
25 Petro alipokuwa akiingia ndani, Kornelio alikuja kumlaki, akaanguka miguuni pake kwa heshima.
Якоже бысть внити Петру, срете его Корнилий, и пад на ногу его поклонися.
26 Lakini Petro akamwinua akamwambia, “Simama, mimi ni mwanadamu tu.”
Петр же воздвиже его, глаголя: востани: и аз сам человек есмь.
27 Petro alipokuwa akizungumza naye akaingia ndani na kukuta watu wengi wamekusanyika.
И с ним беседуя, вниде и обрете собравшыяся многи:
28 Akawaambia, “Mnajua kabisa kwamba ni kinyume cha sheria yetu Myahudi kuchangamana na mtu wa Mataifa au kumtembelea. Lakini Mungu amenionyesha kwamba nisimwite mtu yeyote kuwa najisi au asiye safi.
рече же к ним: вы весте, яко не лепо есть мужу Иудеанину прилеплятися или приходити ко иноплеменнику: и мне Бог показа ни единаго скверна или нечиста глаголати человека:
29 Ndiyo sababu ulipotuma niitwe nilikuja bila kupinga lolote. Basi sasa naomba unieleze kwa nini umeniita?”
темже и без сумнения приидох призван: вопрошаю вы убо, коея ради вины посласте по мене?
30 Kornelio akajibu, “Siku nne zilizopita, nilikuwa nyumbani nikisali saa kama hii, saa tisa alasiri. Ghafula mtu aliyevaa nguo zilizongʼaa akasimama mbele yangu,
И Корнилий рече: от четвертаго дне даже до сего часа бех постяся и в девятый час моляся в дому моем: и се, муж ста предо мною во одежди светле
31 akasema, ‘Kornelio, maombi yako yamesikiwa na sadaka zako kwa maskini zimekumbukwa mbele za Mungu.
и рече: Корнилие, услышана бысть молитва твоя, и милостыни твоя помянушася пред Богом:
32 Basi tuma watu waende Yafa wakaulize mtu mmoja Simoni aitwaye Petro, yeye ni mgeni katika nyumba ya Simoni mtengenezaji ngozi, ambaye nyumba yake iko kando ya bahari.’
посли убо во Июппию и призови Симона, иже нарицается Петр: сей странствует в дому Симона усмаря близ моря: иже пришед возглаголет тебе.
33 Nilituma watu kwako mara moja, nawe umefanya vyema kuja. Basi sasa sisi sote tuko hapa mbele za Mungu kuyasikiliza yote ambayo Bwana amekuamuru kutuambia.”
Абие убо послах к тебе, ты же добре сотворил еси пришед: ныне убо вси мы пред Богом предстоим слышати вся повеленная тебе от Бога.
34 Ndipo Petro akafungua kinywa chake akasema, “Mungu hana upendeleo,
Отверз же Петр уста, рече: поистинне разумеваю, яко не на лица зрит Бог,
35 Lakini katika kila taifa, kila mtu amchaye na kutenda yaliyo haki hukubaliwa naye.
но во всяцем языце бояйся Его и делаяй правду приятен Ему есть:
36 Ninyi mnajua ule ujumbe uliotumwa kwa Israeli, ukitangaza habari njema za amani kwa Yesu Kristo. Yeye ni Bwana wa wote.
слово, еже посла сыном Израилевым, благовествуя мир Иисус Христом: Сей есть всем Господь:
37 Mnajua yale yaliyotukia katika Uyahudi wote kuanzia Galilaya baada ya mahubiri ya Yohana Mbatizaji:
вы весте глагол бывший по всей Иудеи, наченшийся от Галилеи, по крещении, еже проповеда Иоанн:
38 Jinsi Mungu alivyomtia Yesu wa Nazareti mafuta katika Roho Mtakatifu na jinsi alivyokwenda huku na huko akitenda mema na kuponya wote waliokuwa wameonewa na nguvu za ibilisi, kwa sababu Mungu alikuwa pamoja naye.
Иисуса, Иже от Назарета, яко помаза Его Бог Духом Святым и силою, Иже пройде благодателствуя и исцеляя вся насилованныя от диавола, яко Бог бяше с Ним:
39 “Sisi ni mashahidi wa mambo yote aliyoyafanya katika Uyahudi na Yerusalemu. Wakamuua kwa kumtundika msalabani.
и мы есмы свидетеле всех, яже сотвори во стране Иудейстей и во Иерусалиме: Егоже и убиша, повешше на древе.
40 Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu siku ya tatu na akamwezesha kuonekana na watu.
Сего Бог воскреси в третий день и даде Ему явлену быти,
41 Hakuonekana kwa watu wote, lakini kwetu sisi tuliochaguliwa na Mungu kuwa mashahidi, ambao tulikula na kunywa naye baada ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu.
не всем людем, но нам свидетелем преднареченным от Бога, иже с Ним ядохом и пихом, по воскресении Его от мертвых:
42 Naye alituamuru kuhubiri kwa watu wote na kushuhudia kwamba ndiye alitiwa mafuta na Mungu kuwa hakimu wa walio hai na wafu.
и повеле нам проповедати людем и засвидетелствовати, яко Той есть нареченный от Бога Судия живым и мертвым:
43 Manabii wote walishuhudia juu yake kwamba kila mtu amwaminiye hupokea msamaha wa dhambi katika Jina lake.”
о Сем вси пророцы свидетелствуют, оставление грехов прияти именем Его всякому верующему в Онь.
44 Wakati Petro alikuwa akisema maneno haya, Roho Mtakatifu aliwashukia wote waliokuwa wakisikiliza ule ujumbe.
Еще же глаголющу Петру глаголы сия, нападе Дух Святый на вся слышащыя слово.
45 Wale wa tohara walioamini waliokuja na Petro walishangaa kwa kuona kuwa kipawa cha Roho Mtakatifu kimemwagwa juu ya watu wa Mataifa.
И ужасошася иже от обрезания вернии, елицы приидоша с Петром, яко и на языки дар Святаго Духа излияся:
46 Kwa kuwa waliwasikia wakinena kwa lugha mpya na kumwadhimisha Mungu. Ndipo Petro akasema,
слышаху бо их глаголющих языки и величающих Бога. Тогда отвеща Петр:
47 “Je, kuna mtu yeyote anayeweza kuzuia watu hawa wasibatizwe kwa maji? Wamempokea Roho Mtakatifu kama sisi tulivyompokea.”
еда воду возбранити может кто, еже не креститися сим, иже Дух Святый прияша, якоже и мы?
48 Kwa hiyo akaamuru wabatizwe kwa jina la Yesu Kristo. Wakamsihi Petro akae nao kwa siku chache.
Повеле же им креститися во имя Иисус Христово. Тогда молиша его пребыти у них дни некия.

< Matendo 10 >