< Matendo 10 >
1 Katika mji wa Kaisaria palikuwa na mtu jina lake Kornelio, ambaye alikuwa jemadari wa kile kilichojulikana kama kikosi cha Kiitalia.
And there was a certain man in Caesarea, by name Cornelius, a centurion from a cohort that is called Italian,
2 Yeye alikuwa mcha Mungu pamoja na wote wa nyumbani mwake. Aliwapa watu sadaka nyingi na kumwomba Mungu daima.
pious, and fearing God with all his house, also doing many kind acts to the people, and always imploring God;
3 Siku moja alasiri, yapata saa tisa, aliona maono waziwazi, malaika wa Mungu akimjia na kumwambia, “Kornelio!”
he saw in a vision openly, as it were the ninth hour of the day, a messenger of God coming in to him, and saying to him, “Cornelius”;
4 Kornelio akamkazia macho kwa hofu akasema, “Kuna nini, Bwana?” Malaika akamwambia, “Sala zako na sadaka zako kwa maskini zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za Mungu.
and he having looked earnestly on him, and becoming afraid, said, “What is it, Lord?” And he said to him, “Your prayers and your kind acts came up for a memorial before God,
5 Sasa tuma watu waende Yafa wakamwite mtu mmoja jina lake Simoni aitwaye Petro.
and now send men to Joppa, and send for a certain one Simon, who is surnamed Peter;
6 Yeye anaishi na Simoni mtengenezaji ngozi ambaye nyumba yake iko kando ya bahari.”
this one lodges with a certain Simon a tanner, whose house is by the sea; this one will speak to you what you must do.”
7 Yule malaika aliyekuwa akizungumza naye alipoondoka, Kornelio akawaita watumishi wake wawili pamoja na askari mmoja mcha Mungu aliyekuwa miongoni mwa wale waliomtumikia.
And when the messenger who is speaking to Cornelius went away, having called two of his servants, and a pious soldier of those waiting on him continually,
8 Akawaambia mambo yote yaliyotukia, kisha akawatuma waende Yafa.
and having expounded all things to them, he sent them to Joppa.
9 Siku ya pili yake, walipokuwa wameukaribia mji, wakati wa adhuhuri, Petro alipanda juu ya nyumba kuomba.
And on the next day, as these are proceeding on the way, and are drawing near to the city, Peter went up on the housetop to pray, about the sixth hour,
10 Alipokuwa akiomba akahisi njaa, akatamani kupata chakula. Lakini wakati walikuwa wakiandaa chakula, akalala usingizi mzito sana.
and he became very hungry, and wished to eat; and they making ready, there fell on him a trance,
11 Akaona mbingu zimefunguka na kitu kama nguo kubwa kikishushwa duniani kwa ncha zake nne.
and he beholds Heaven opened, and a certain vessel descending to him, as a great sheet, bound at the four corners, and let down on the earth,
12 Ndani yake walikuwepo aina zote za wanyama wenye miguu minne, nao watambaao nchini, na ndege wa angani.
in which were all the four-footed beasts of the earth, and the wild beasts, and the creeping things, and the birds of the sky,
13 Ndipo sauti ikamwambia “Petro, ondoka, uchinje na ule.”
and there came a voice to him: “Having risen, Peter, slay and eat.”
14 Petro akajibu, “La hasha Bwana! Sijawahi kamwe kula kitu chochote kilicho najisi.”
And Peter said, “Not so, Lord; because at no time did I eat anything common or unclean”;
15 Ile sauti ikasema naye mara ya pili, “Usikiite najisi kitu chochote Mungu alichokitakasa.”
and [there is] a voice again a second time to him: “What God cleansed, you do not declare common”;
16 Jambo hili lilitokea mara tatu na ghafula ile nguo ikarudishwa mbinguni.
and this was done three times, and again was the vessel received up to Heaven.
17 Wakati Petro akiwa bado anajiuliza kuhusu maana ya maono haya, wale watu waliokuwa wametumwa na Kornelio wakaipata nyumba ya Simoni mtengenezaji wa ngozi wakawa wamesimama mbele ya lango.
And as Peter was perplexed in himself what the vision that he saw might be, then, behold, the men who have been sent from Cornelius, having made inquiry for the house of Simon, stood at the gate,
18 Wakabisha hodi na kuuliza kama Simoni aliyeitwa Petro alikuwa anaishi hapo.
and having called, they were asking if Simon, who is surnamed Peter, lodges here.
19 Wakati Petro akiwa anafikiria juu ya yale maono, Roho Mtakatifu akamwambia, “Simoni, wako watu watatu wanaokutafuta.
And Peter thinking about the vision, the Spirit said to him, “Behold, three men seek you;
20 Inuka na ushuke, usisite kwenda nao kwa kuwa mimi nimewatuma.”
but having risen, go down and go on with them, doubting nothing, because I have sent them”;
21 Petro akashuka na kuwaambia wale watu waliokuwa wametumwa kutoka kwa Kornelio, “Mimi ndiye mnayenitafuta. Mmekuja kwa sababu gani?”
and Peter having come down to the men who have been sent from Cornelius to him, said, “Behold, I am he whom you seek, what [is] the cause for which you are present?”
22 Wale watu wakamjibu, “Tumetumwa na Kornelio yule jemadari. Yeye ni mtu mwema anayemcha Mungu, na anaheshimiwa na Wayahudi wote. Yeye ameagizwa na malaika mtakatifu akukaribishe nyumbani kwake, ili asikilize maneno utakayomwambia.”
And they said, “Cornelius, a centurion, a man righteous and fearing God, well testified to, also, by all the nation of the Jews, was divinely warned by a holy messenger to send for you, to his house, and to hear sayings from you.”
23 Basi Petro akawakaribisha wakafuatana naye ndani, akawapa pa kulala. Kesho yake akaondoka pamoja nao, na baadhi ya ndugu kutoka Yafa wakafuatana naye.
Having called them in, therefore, he lodged them, and on the next day Peter went forth with them, and certain of the brothers from Joppa went with him,
24 Siku iliyofuata wakawasili Kaisaria. Kornelio alikuwa akiwangoja pamoja na jamaa yake na marafiki zake wa karibu.
and on the next day they entered into Caesarea; and Cornelius was waiting for them, having called together his relatives and near friends,
25 Petro alipokuwa akiingia ndani, Kornelio alikuja kumlaki, akaanguka miguuni pake kwa heshima.
and as it came that Peter entered in, Cornelius having met him, having fallen at [his] feet, worshiped [him];
26 Lakini Petro akamwinua akamwambia, “Simama, mimi ni mwanadamu tu.”
and Peter raised him, saying, “Stand up; I am also a man myself”;
27 Petro alipokuwa akizungumza naye akaingia ndani na kukuta watu wengi wamekusanyika.
and talking with him he went in, and finds many having come together.
28 Akawaambia, “Mnajua kabisa kwamba ni kinyume cha sheria yetu Myahudi kuchangamana na mtu wa Mataifa au kumtembelea. Lakini Mungu amenionyesha kwamba nisimwite mtu yeyote kuwa najisi au asiye safi.
And he said to them, “You know how it is unlawful for a man, a Jew, to keep company with, or to come to, one of another race, but God showed to me to call no man common or unclean;
29 Ndiyo sababu ulipotuma niitwe nilikuja bila kupinga lolote. Basi sasa naomba unieleze kwa nini umeniita?”
therefore also without contradicting I came, having been sent for; I ask, therefore, for what matter you sent for me?”
30 Kornelio akajibu, “Siku nne zilizopita, nilikuwa nyumbani nikisali saa kama hii, saa tisa alasiri. Ghafula mtu aliyevaa nguo zilizongʼaa akasimama mbele yangu,
And Cornelius said, “Four days ago until this hour, I was fasting, and [at] the ninth hour praying in my house, and behold, a man stood before me in radiant clothing,
31 akasema, ‘Kornelio, maombi yako yamesikiwa na sadaka zako kwa maskini zimekumbukwa mbele za Mungu.
and he said, Cornelius, your prayer was heard, and your kind acts were remembered before God;
32 Basi tuma watu waende Yafa wakaulize mtu mmoja Simoni aitwaye Petro, yeye ni mgeni katika nyumba ya Simoni mtengenezaji ngozi, ambaye nyumba yake iko kando ya bahari.’
send, therefore, to Joppa, and call for Simon, who is surnamed Peter; this one lodges in the house of Simon a tanner, by the sea, who having come, will speak to you;
33 Nilituma watu kwako mara moja, nawe umefanya vyema kuja. Basi sasa sisi sote tuko hapa mbele za Mungu kuyasikiliza yote ambayo Bwana amekuamuru kutuambia.”
at once, therefore, I sent to you; you also did well, having come; now, therefore, we are all present before God to hear all things that have been commanded you by God.”
34 Ndipo Petro akafungua kinywa chake akasema, “Mungu hana upendeleo,
And Peter having opened his mouth, said, “Of a truth, I perceive that God is not favoring by appearance,
35 Lakini katika kila taifa, kila mtu amchaye na kutenda yaliyo haki hukubaliwa naye.
but in every nation he who is fearing Him, and is working righteousness, is acceptable to Him;
36 Ninyi mnajua ule ujumbe uliotumwa kwa Israeli, ukitangaza habari njema za amani kwa Yesu Kristo. Yeye ni Bwana wa wote.
the word that He sent to the sons of Israel, proclaiming good news—peace through Jesus Christ (this One is Lord of all),
37 Mnajua yale yaliyotukia katika Uyahudi wote kuanzia Galilaya baada ya mahubiri ya Yohana Mbatizaji:
you have known the word that came throughout all Judea, having begun from Galilee, after the immersion that John preached;
38 Jinsi Mungu alivyomtia Yesu wa Nazareti mafuta katika Roho Mtakatifu na jinsi alivyokwenda huku na huko akitenda mema na kuponya wote waliokuwa wameonewa na nguvu za ibilisi, kwa sababu Mungu alikuwa pamoja naye.
Jesus who [is] from Nazareth—how God anointed Him with the Holy Spirit and power; who went through, doing good, and healing all those oppressed by the Devil, because God was with Him;
39 “Sisi ni mashahidi wa mambo yote aliyoyafanya katika Uyahudi na Yerusalemu. Wakamuua kwa kumtundika msalabani.
and we are witnesses of all things that He did, both in the country of the Jews, and in Jerusalem—whom they slew, having hanged [Him] on a tree.
40 Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu siku ya tatu na akamwezesha kuonekana na watu.
This One God raised up [on] the third day, and gave Him to become visible,
41 Hakuonekana kwa watu wote, lakini kwetu sisi tuliochaguliwa na Mungu kuwa mashahidi, ambao tulikula na kunywa naye baada ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu.
not to all the people, but to witnesses, to those having been chosen before by God—to us who ate with [Him], and drank with Him, after His rising out of the dead;
42 Naye alituamuru kuhubiri kwa watu wote na kushuhudia kwamba ndiye alitiwa mafuta na Mungu kuwa hakimu wa walio hai na wafu.
and He commanded us to preach to the people, and to fully testify that it is He who has been ordained judge of living and dead by God—
43 Manabii wote walishuhudia juu yake kwamba kila mtu amwaminiye hupokea msamaha wa dhambi katika Jina lake.”
to this One do all the Prophets testify, that through His Name everyone that is believing in Him receives forgiveness of sins.”
44 Wakati Petro alikuwa akisema maneno haya, Roho Mtakatifu aliwashukia wote waliokuwa wakisikiliza ule ujumbe.
While Peter is yet speaking these sayings, the Holy Spirit fell on all those hearing the word,
45 Wale wa tohara walioamini waliokuja na Petro walishangaa kwa kuona kuwa kipawa cha Roho Mtakatifu kimemwagwa juu ya watu wa Mataifa.
and those of circumcision [who were] believing were astonished—as many as came with Peter—because the gift of the Holy Spirit has also been poured out on the nations,
46 Kwa kuwa waliwasikia wakinena kwa lugha mpya na kumwadhimisha Mungu. Ndipo Petro akasema,
for they were hearing them speaking with tongues and magnifying God.
47 “Je, kuna mtu yeyote anayeweza kuzuia watu hawa wasibatizwe kwa maji? Wamempokea Roho Mtakatifu kama sisi tulivyompokea.”
Then Peter answered, “Is anyone able to forbid the water, that these may not be immersed, who received the Holy Spirit—even as us also?”
48 Kwa hiyo akaamuru wabatizwe kwa jina la Yesu Kristo. Wakamsihi Petro akae nao kwa siku chache.
He commanded them to also be immersed in the Name of the LORD; then they implored him to remain certain days.