< Matendo 1 >
1 Katika kitabu changu cha kwanza nilikuandikia, mpendwa Theofilo, kuhusu mambo yote Yesu aliyofanya na kufundisha tangu mwanzo,
První zajisté knihu sepsalť jsem, ó Teofile, o všech věcech, kteréž začal Ježíš činiti a učiti,
2 hadi siku ile alipochukuliwa kwenda mbinguni, baada ya kuwapa maagizo kupitia kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua.
Až do toho dne, v kterémžto dav přikázání apoštolům, kteréž byl skrze Ducha svatého vyvolil, vzhůru vzat jest.
3 Baada ya mateso yake, alijionyesha kwao na kuwathibitishia kwa njia nyingi kwamba yeye yu hai. Katika muda wa siku arobaini baada ya kufufuka kwake aliwatokea na kunena kuhusu Ufalme wa Mungu.
Kterýmžto i zjevoval sebe samého živého po svém umučení ve mnohých jistých důvodích, za čtyřidceti dnů ukazuje se jim a mluvě o království Božím.
4 Wakati mmoja alipokuwa pamoja nao, aliwapa amri hii, “Msitoke Yerusalemu, bali ingojeni ahadi ya Baba, ambayo mmenisikia nikisema habari zake.
A shromáždiv se s nimi, přikázal jim, aby z Jeruzaléma neodcházeli, ale aby očekávali zaslíbení Otcova, o kterémž jste prý slyšeli ode mne.
5 Yohana aliwabatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.”
Nebo Jan zajisté křtil vodou, ale vy pokřtěni budete Duchem svatým po nemnohých těchto dnech.
6 Mitume walipokuwa wamekusanyika pamoja, wakamuuliza Yesu, “Bwana, je, huu ndio wakati wa kuwarudishia Israeli ufalme?”
Oni pak sšedše se, otázali se ho, řkouce: Pane, v tomto-li času napravíš království Izraelské?
7 Yesu akawaambia, “Si juu yenu kujua nyakati na majira ambayo Baba ameyaweka katika mamlaka yake mwenyewe.
I řekl jim: Neníť vaše věc znáti časy anebo příhodnosti časů, kteréžto Otec v moci své položil.
8 Lakini mtapokea nguvu akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu, nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, Uyahudi kote na Samaria, hadi miisho ya dunia.”
Ale přijmete moc Ducha svatého, přicházejícího na vás, a budete mi svědkové, i v Jeruzalémě, i ve všem Judstvu, i v Samaří, a až do posledních končin země.
9 Baada ya kusema mambo haya, walipokuwa wanatazama, akachukuliwa juu mbinguni mbele ya macho yao na wingu likampokea wasimwone tena.
A to pověděv, ani na to hledí, vzhůru vyzdvižen jest, a oblak vzal jej od očí jejich.
10 Walipokuwa bado wakikaza macho yao kuelekea juu alipokuwa akienda zake Mbinguni, tazama ghafula, wanaume wawili waliovaa mavazi meupe wakasimama karibu nao,
A když za ním v nebe jdoucím pilně hleděli, aj, dva muži postavili se podle nich v rouše bílém,
11 wakasema, “Enyi watu wa Galilaya, mbona mnasimama mkitazama juu angani? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda Mbinguni, atarudi tena jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake Mbinguni.”
A řekli: Muži Galilejští, co stojíte, hledíce do nebe? Tento Ježíš, kterýž vzhůru vzat jest od vás do nebe, takť přijde, jakž jste spatřili způsob jeho jdoucího do nebe.
12 Ndipo waliporudi Yerusalemu kutoka Mlima wa Mizeituni, uliokuwa karibu na Yerusalemu, umbali wa mwendo wa Sabato kutoka mjini.
Tedy navrátili se do Jeruzaléma od hory, jenž slove Olivetská, kteráž jest blízko Jeruzaléma, vzdálí cesty jednoho dne svátečního.
13 Walipowasili mjini Yerusalemu, walikwenda ghorofani kwenye chumba walichokuwa wakiishi. Wale waliokuwepo walikuwa: Petro, Yohana, Yakobo, Andrea, Filipo, Tomaso, Bartholomayo, Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda mwana wa Yakobo.
A když přišli domů, vstoupili do vrchního příbytku domu, kdež přebývali, i Petr i Jakub, i Jan a Ondřej, Filip a Tomáš, Bartoloměj a Matouš, Jakub Alfeův a Šimon Zelótes a Judas bratr Jakubův.
14 Hawa wote waliungana pamoja katika maombi. Pamoja nao walikuwepo wanawake kadha, na Maria mama yake Yesu, pamoja na ndugu zake Yesu.
Ti všickni byli trvajíce jednomyslně na modlitbě a pokorné prosbě s ženami a s Marijí, matkou Ježíšovou, i s bratřími jeho.
15 Katika siku hizo Petro akasimama katikati ya waumini (jumla yao wote walikuwa watu wapatao 120), akasema,
V těch pak dnech povstav Petr uprostřed učedlníků, řekl (a byl zástup lidí spolu shromážděných okolo sta a dvadcíti):
16 “Ndugu zangu, ilibidi Andiko litimie ambalo Roho Mtakatifu alitabiri kupitia kwa Daudi kumhusu Yuda aliyewaongoza wale waliomkamata Yesu.
Muži bratří, musilo se naplniti Písmo to, kteréž předpověděl Duch svatý skrze ústa Davidova o Jidášovi, kterýž byl vůdce těch, jenž jímali Ježíše.
17 Yuda alikuwa mmoja wetu, kwa maana na yeye alichaguliwa ashiriki katika huduma hii.”
Nebo byl přičten k nám, a byl došel losu přisluhování tohoto.
18 (Basi Yuda alinunua shamba kwa zile fedha za uovu alizopata; akiwa huko shambani akaanguka, akapasuka na matumbo yote yakatoka nje.
Ten zajisté obdržel pole ze mzdy nepravosti, a oběsiv se, rozpukl se na dvé, i vykydla se všecka střeva jeho.
19 Kila mtu Yerusalemu akasikia habari hizi, kwa hiyo wakapaita mahali hapo kwa lugha yao, Akeldama, yaani Shamba la Damu).
A to známé jest učiněno všechněm přebývajícím v Jeruzalémě, takže jest nazváno pole to vlastním jazykem jejich Akeldama, to jest pole krve.
20 “Kama vile ilivyoandikwa katika kitabu cha Zaburi, “‘Mahali pake na pawe ukiwa, wala asiwepo yeyote atakayeishi humo,’ na, “‘Mtu mwingine aichukue nafasi yake ya uongozi.’
Psáno jest zajisté v knihách Žalmů: Budiž příbytek jeho pustý, a nebuď, kdo by přebýval v něm, a opět: Biskupství jeho vezmi jiný.
21 Kwa hiyo inatubidi tumchague mtu mwingine miongoni mwa wale ambao wamekuwa pamoja nasi wakati wote Bwana Yesu alipoingia na kutoka katikati yenu,
Protož musíť to býti, aby jeden z těch mužů, kteříž jsou s námi bývali po všecken čas, v němž přebýval mezi námi Pán Ježíš,
22 kuanzia ubatizo wa Yohana mpaka siku aliyochukuliwa kutoka kwetu kwenda Mbinguni. Kwa kuwa mmoja wao inabidi awe shahidi pamoja nasi wa ufufuo wake.”
Počav od křtu Janova až do dne toho, v kterémžto vzhůru vzat jest od nás, byl svědkem spolu s námi vzkříšení jeho.
23 Wakapendekeza majina ya watu wawili: Yosefu, aitwaye Barsaba (ambaye pia alijulikana kama Yusto) na Mathiya.
Tedy postavili dva, Jozefa, jenž sloul Barsabáš, kterýž měl příjmí Justus, a Matěje.
24 Kisha wakaomba, wakasema, “Bwana, wewe waujua moyo wa kila mtu. Tuonyeshe ni yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua
A modléce se, řekli: Ty, Pane, všech srdcí zpytateli, ukažiž, kterého jsi vyvolil z těchto dvou,
25 ili achukue nafasi ya huduma ya utume ambayo Yuda aliiacha ili aende mahali pake mwenyewe.”
Aby přijal los přisluhování tohoto a apoštolství, z něhož jest vypadl Jidáš, aby odšel na místo své.
26 Kisha wakawapigia kura, nayo kura ikamwangukia Mathiya, naye akaongezwa kwenye wale mitume kumi na mmoja.
I dali jim losy. Spadl pak los na Matěje, i připojen jest z společného snešení k jedenácti apoštolům.