< 3 Yohana 1 >

1 Mzee: Kwa Gayo rafiki yangu, nimpendaye katika kweli.
The ancient to the dearly beloved Gaius, whom I love in truth.
2 Mpendwa, naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya njema kama vile roho yako ifanikiwavyo.
Dearly beloved, concerning all things I make it my prayer that thou mayest proceed prosperously, and fare well as thy soul doth prosperously.
3 Ilinifurahisha sana baadhi ya ndugu walipokuja na kutueleza juu ya uaminifu wako katika kweli na jinsi unavyoendelea kuenenda katika hiyo kweli.
I was exceedingly glad when the brethren came and gave testimony to the truth in thee, even as thou walkest in the truth.
4 Sina furaha kubwa kuliko hii, kusikia kwamba watoto wangu wanaenenda katika kweli.
I have no greater grace than this, to hear that my children walk in truth.
5 Rafiki mpendwa, wewe ni mwaminifu kwa yale unayowatendea ndugu, ingawa wao ni wageni kwako.
Dearly beloved, thou dost faithfully whatever thou dost for the brethren, and that for strangers,
6 Wameshuhudia kuhusu upendo wako mbele ya kanisa. Utafanya vyema ukiwasafirisha kama inavyostahili kwa Mungu.
Who have given testimony to thy charity in the sight of the church: whom thou shalt do well to bring forward on their way in a manner worthy of God.
7 Ilikuwa ni kwa ajili ya hilo Jina waliondoka, bila kukubali kupokea msaada wowote kutoka kwa watu wasioamini.
Because, for his name they went out, taking nothing of the Gentiles.
8 Kwa hiyo imetupasa sisi kuonyesha ukarimu kwa watu kama hao ili tuweze kutenda kazi pamoja kwa ajili ya kweli.
We therefore ought to receive such, that we may be fellow helpers of the truth.
9 Nililiandikia kanisa, lakini Deotrefe, yeye apendaye kujifanya wa kwanza, hakubali mamlaka yetu.
I had written perhaps to the church: but Diotrephes, who loveth to have the pre-eminence among them, doth not receive us.
10 Hivyo kama nikija, nitakumbuka matendo yake atendayo, akitusingizia kwa maneno ya hila. Wala hatosheki na hayo anayotusingizia, bali pia hukataa kuwakaribisha ndugu, na hata huwazuia wale walio tayari kufanya hivyo na kuwafukuza watoke kanisani.
For this cause, if I come, I will advertise his works which he doth, with malicious words prating against us. And as if these things were not enough for him, neither doth he himself receive the brethren, and them that do receive them he forbiddeth, and casteth out of the church.
11 Rafiki mpendwa, usiige lile lililo baya bali lile lililo jema. Yeyote atendaye mema atoka kwa Mungu, bali atendaye mabaya hajamwona Mungu.
Dearly beloved, follow not that which is evil, but that which is good. He that doth good, is of God: he that doth evil, hath not seen God.
12 Kila mtu ameshuhudia mema kuhusu Demetrio, vivyo hivyo hata na hiyo kweli yenyewe. Sisi pia twashuhudia mema juu yake, nanyi mwajua kwamba ushuhuda wetu ni kweli.
To Demetrius testimony is given by all, and by the truth itself, yea and we also give testimony: and thou knowest that our testimony is true.
13 Ninayo mambo mengi ya kukuandikia, lakini sipendi kuandika kwa kalamu na wino.
I had many things to write unto thee: but I would not by ink and pen write to thee.
14 Badala yake, nataraji kukuona upesi, nasi tutaongea pamoja ana kwa ana. Amani iwe kwako. Rafiki zetu walioko hapa wanakusalimu. Wasalimu hao rafiki zetu walioko huko, kila mmoja kwa jina lake.
But I hope speedily to see thee, and we will speak mouth to mouth. Peace be to thee. Our friends salute thee. Salute the friends by name.

< 3 Yohana 1 >