< 3 Yohana 1 >
1 Mzee: Kwa Gayo rafiki yangu, nimpendaye katika kweli.
Den Ældste til Kajus, den elskede, hvem jeg elsker i Sandhed.
2 Mpendwa, naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya njema kama vile roho yako ifanikiwavyo.
Du elskede! jeg ønsker, at det i alle Ting maa gaa dig vel, og du maa være karsk, ligesom det gaar din Sjæl vel.
3 Ilinifurahisha sana baadhi ya ndugu walipokuja na kutueleza juu ya uaminifu wako katika kweli na jinsi unavyoendelea kuenenda katika hiyo kweli.
Thi jeg blev meget glad, da der kom Brødre og vidnede om Sandheden i dig, hvorledes du vandrer i Sandheden.
4 Sina furaha kubwa kuliko hii, kusikia kwamba watoto wangu wanaenenda katika kweli.
Jeg har ingen større Glæde end denne, at jeg hører, at mine Børn vandre i Sandheden.
5 Rafiki mpendwa, wewe ni mwaminifu kwa yale unayowatendea ndugu, ingawa wao ni wageni kwako.
Du elskede! en trofast Gerning gør du i alt, hvad du virker for Brødrene, og det for fremmede,
6 Wameshuhudia kuhusu upendo wako mbele ya kanisa. Utafanya vyema ukiwasafirisha kama inavyostahili kwa Mungu.
hvilke have vidnet for Menigheden om din Kærlighed; og du vil gøre vel i at fremme deres Rejse saaledes, som det er Gud værdigt.
7 Ilikuwa ni kwa ajili ya hilo Jina waliondoka, bila kukubali kupokea msaada wowote kutoka kwa watu wasioamini.
Thi for Navnets Skyld ere de dragne ud, uden at tage noget af Hedningerne.
8 Kwa hiyo imetupasa sisi kuonyesha ukarimu kwa watu kama hao ili tuweze kutenda kazi pamoja kwa ajili ya kweli.
Derfor ere vi skyldige at tage os af saadanne, for at vi kunne blive Medarbejdere for Sandheden.
9 Nililiandikia kanisa, lakini Deotrefe, yeye apendaye kujifanya wa kwanza, hakubali mamlaka yetu.
Jeg har skrevet noget til Menigheden; men Diotrefes, som gerne vil være den ypperste iblandt dem, anerkender os ikke.
10 Hivyo kama nikija, nitakumbuka matendo yake atendayo, akitusingizia kwa maneno ya hila. Wala hatosheki na hayo anayotusingizia, bali pia hukataa kuwakaribisha ndugu, na hata huwazuia wale walio tayari kufanya hivyo na kuwafukuza watoke kanisani.
Derfor vil jeg, naar jeg kommer, erindre om de Gerninger, han gør, idet han bagvadsker os med onde Ord; og ikke tilfreds dermed, tager han baade selv ikke Brødrene for gode, og dem, som ville det, forhindrer han deri og udstøder dem af Menigheden.
11 Rafiki mpendwa, usiige lile lililo baya bali lile lililo jema. Yeyote atendaye mema atoka kwa Mungu, bali atendaye mabaya hajamwona Mungu.
Du elskede! efterfølg ikke det onde, men det gode. Den, som gør godt, er af Gud; den, som gør ondt, har ikke set Gud.
12 Kila mtu ameshuhudia mema kuhusu Demetrio, vivyo hivyo hata na hiyo kweli yenyewe. Sisi pia twashuhudia mema juu yake, nanyi mwajua kwamba ushuhuda wetu ni kweli.
Demetrius har et godt Vidnesbyrd af alle og af Sandheden selv; ogsaa vi vidne, og du ved, at vort Vidnesbyrd er sandt.
13 Ninayo mambo mengi ya kukuandikia, lakini sipendi kuandika kwa kalamu na wino.
Jeg havde meget at skrive til dig, men jeg vil ikke skrive til dig med Blæk og Pen.
14 Badala yake, nataraji kukuona upesi, nasi tutaongea pamoja ana kwa ana. Amani iwe kwako. Rafiki zetu walioko hapa wanakusalimu. Wasalimu hao rafiki zetu walioko huko, kila mmoja kwa jina lake.
Men jeg haaber snart at se dig, og da skulle vi mundtligt tale sammen. Fred være med dig! Vennerne hilse dig. Hils Vennerne, hver især!