< 3 Yohana 1 >

1 Mzee: Kwa Gayo rafiki yangu, nimpendaye katika kweli.
Starješina ljubljenom Gaju koga ljubim u Istini.
2 Mpendwa, naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya njema kama vile roho yako ifanikiwavyo.
Ljubljeni! Želim ti u svemu dobro i da budeš zdrav, kao što je dobro tvojoj duši.
3 Ilinifurahisha sana baadhi ya ndugu walipokuja na kutueleza juu ya uaminifu wako katika kweli na jinsi unavyoendelea kuenenda katika hiyo kweli.
Veoma se obradovah kada dođoše braća i posvjedočiše za tvoju istinu: kako ti živiš po Istini.
4 Sina furaha kubwa kuliko hii, kusikia kwamba watoto wangu wanaenenda katika kweli.
Čuti da moja djeca po Istini žive! - nema mi veće radosti od toga.
5 Rafiki mpendwa, wewe ni mwaminifu kwa yale unayowatendea ndugu, ingawa wao ni wageni kwako.
Ljubljeni, pravi si vjernik u svemu što činiš za braću, i to za došljake.
6 Wameshuhudia kuhusu upendo wako mbele ya kanisa. Utafanya vyema ukiwasafirisha kama inavyostahili kwa Mungu.
Oni posvjedočiše tvoju ljubav pred Crkvom i dobro ćeš učiniti ako ih ispratiš Boga dostojno.
7 Ilikuwa ni kwa ajili ya hilo Jina waliondoka, bila kukubali kupokea msaada wowote kutoka kwa watu wasioamini.
Jer poradi Imena iziđoše i ne primaju ništa od pogana.
8 Kwa hiyo imetupasa sisi kuonyesha ukarimu kwa watu kama hao ili tuweze kutenda kazi pamoja kwa ajili ya kweli.
Mi smo dakle dužni takve primati da budemo suradnici Istine.
9 Nililiandikia kanisa, lakini Deotrefe, yeye apendaye kujifanya wa kwanza, hakubali mamlaka yetu.
Pisao sam nešto Crkvi: ali Diotref, koji hoće da bude prvi među njima, ne prima nas.
10 Hivyo kama nikija, nitakumbuka matendo yake atendayo, akitusingizia kwa maneno ya hila. Wala hatosheki na hayo anayotusingizia, bali pia hukataa kuwakaribisha ndugu, na hata huwazuia wale walio tayari kufanya hivyo na kuwafukuza watoke kanisani.
Zato ako dođem, spočitnut ću mu djela koja čini naklapajući zlobne riječi o nama. Ni to mu nije dosta, nego ne prima braće, a onima koji bi to htjeli, brani i izgoni ih iz Crkve.
11 Rafiki mpendwa, usiige lile lililo baya bali lile lililo jema. Yeyote atendaye mema atoka kwa Mungu, bali atendaye mabaya hajamwona Mungu.
Ljubljeni! Ne nasljeduj zlo, nego dobro. Tko dobro čini, od Boga je; tko zlo čini, nije vidio Boga.
12 Kila mtu ameshuhudia mema kuhusu Demetrio, vivyo hivyo hata na hiyo kweli yenyewe. Sisi pia twashuhudia mema juu yake, nanyi mwajua kwamba ushuhuda wetu ni kweli.
Za Demetrija svjedoče svi, i sama Istina, a i mi svjedočimo. A znaš da je naše svjedočanstvo istinito.
13 Ninayo mambo mengi ya kukuandikia, lakini sipendi kuandika kwa kalamu na wino.
Mnogo bih ti imao pisati, ali neću da ti pišem crnilom i perom.
14 Badala yake, nataraji kukuona upesi, nasi tutaongea pamoja ana kwa ana. Amani iwe kwako. Rafiki zetu walioko hapa wanakusalimu. Wasalimu hao rafiki zetu walioko huko, kila mmoja kwa jina lake.
Nadam se da ću te uskoro vidjeti pa ćemo iz usta u usta govoriti. Mir tebi! Pozdravljaju te prijatelji. Pozdravi prijatelje poimence.

< 3 Yohana 1 >