< 2 Timotheo 4 >

1 Nakuagiza mbele za Mungu na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu watu walio hai na waliokufa wakati wa kuja kwake na ufalme wake, kwamba:
I attest thee before Aloha, and our Lord Jeshu Meshiha, who is to judge the living and the dead at the revelation of his kingdom:
2 Hubiri Neno; kuwa tayari wakati ufaao na wakati usiofaa; karipia, kemea na utie moyo kwa uvumilivu wote na kwa mafundisho mazuri.
preach the word, and stand with diligence in season, and (that) which is not season; confute, and rebuke with all prolongedness of mind and doctrine.
3 Maana wakati utakuja watu watakapokataa kuyakubali mafundisho yenye uzima. Badala yake, ili kutimiza tamaa zao wenyewe, watajikusanyia idadi kubwa ya walimu wapate kuwaambia yale ambayo masikio yao yanayowasha yanatamani kuyasikia.
For the time will come, when sound doctrine they will not hear; but according to their desires will multiply to themselves teachers, in the itching of their hearing.
4 Watakataa kusikiliza kweli na kuzigeukia hadithi za uongo.
And from the truth they will turn away their ear, but to fables will decline.
5 Kwa habari yako wewe, vumilia mateso, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiza wajibu wote wa huduma yako.
But watch thou in every thing, and endure evils, and work the work of an evangelist, and thy ministry fulfil.
6 Kwa maana mimi sasa ni tayari kumiminwa kama sadaka ya kinywaji, nayo saa yangu ya kuondoka imetimia.
But I am sacrificed, and the time when I shall be dissolved cometh.
7 Nimevipiga vita vizuri, mashindano nimeyamaliza, imani nimeilinda.
The good agony I have fought, and my running I have completed, and my faith I have kept.
8 Sasa nimewekewa taji ya haki ambayo Bwana, mwamuzi wa haki, atanitunukia siku ile: wala si mimi tu, bali pia wote ambao wamengoja kwa shauku kudhihirishwa kwake.
And from now there is kept for me the crown of righteousness, which my Lord will give me in that day, because he is a righteous judge: yet, not only to me, but to all them who love his manifestation.
9 Jitahidi kuja kwangu upesi
BE careful to come to me speedily;
10 kwa sababu Dema, kwa kuupenda ulimwengu, ameniacha na amekwenda Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia na Tito amekwenda Dalmatia. (aiōn g165)
for Dema hath left me, and hath loved this world, and is gone to Thessalonika; Krispos to Galatia, Titos to Dalmatia; (aiōn g165)
11 Ni Luka peke yake aliye hapa pamoja nami. Mtafute Marko uje naye kwa sababu ananifaa sana katika huduma yangu.
Luka only is with me. Take Markos and bring him with thee; for helpful to me is he in the ministry.
12 Nimemtuma Tikiko huko Efeso.
But Tykikos have I sent to Ephesos.
13 Utakapokuja, niletee lile joho nililoliacha kwa Karpo huko Troa na vile vitabu vyangu, hasa vile vya ngozi.
The case (for) books which I left at Troas with Karpos, when thou comest bring, and the books, and especially the roll of parchments.
14 Aleksanda yule mfua chuma alinitendea ubaya mkubwa. Bwana atamlipa kwa ajili ya yale aliyotenda.
Alexander the brass-worker many evils hath showed me: our Lord awardeth to him according to his deeds.
15 Wewe pia ujihadhari naye kwa sababu aliyapinga sana maneno yetu.
But be thou also aware of him, for he is much uplifted against our words.
16 Katika utetezi wangu wa mara ya kwanza, hakuna hata mmoja aliyeniunga mkono, bali kila mmoja aliniacha. Namwomba Mungu wasihesabiwe hatia kwa jambo hilo.
In the first defence no man was with me, but all of them left me. May this not be reckoned to them!
17 Lakini Bwana alisimama upande wangu akanitia nguvu, ili kupitia kwangu lile Neno lihubiriwe kwa ukamilifu, watu wote Mataifa wapate kulisikia. Mimi niliokolewa kutoka kinywa cha simba.
But my Lord stood with me, that by me the preaching might be fulfilled, and (that) all the Gentiles might hear: and I was delivered from the mouth of the lion.
18 Bwana ataniokoa katika kila shambulio baya na kunileta salama katika Ufalme wake wa mbinguni. Atukuzwe yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
And my Lord will deliver me from every evil work, and will save me into his kingdom, which is in heaven. To Him be glory for ever and ever. Amen. (aiōn g165)
19 Wasalimu Prisila na Akila, na wote wa nyumbani kwa Onesiforo.
Give salutation to Priskela, and to Akilos, and to the house of Onesiphoros.
20 Erasto alibaki Korintho. Nami nikamwacha Trofimo huko Mileto akiwa mgonjwa.
Erastos remains at Kurinthos; but Trophimos I left ill in Miletos the city.
21 Jitahidi ufike huku kabla ya majira ya baridi. Eubulo anakusalimu, vivyo hivyo Pude, Lino, Klaudia na ndugu wote.
Be careful to come before winter. Ebulos and Pudis, and Linos, and Klaudia, and all the brethren, ask for your peace.
22 Bwana awe pamoja na roho yako. Neema iwe pamoja nanyi. Amen.
Our Lord Jeshu Meshiha be with thy spirit. Grace be with thee. Amen.

< 2 Timotheo 4 >