< 2 Timotheo 4 >
1 Nakuagiza mbele za Mungu na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu watu walio hai na waliokufa wakati wa kuja kwake na ufalme wake, kwamba:
I charge thee therefore before God, and before the Lord Iesus Christ, which shall iudge the quicke and dead at that his appearing, and in his kingdome,
2 Hubiri Neno; kuwa tayari wakati ufaao na wakati usiofaa; karipia, kemea na utie moyo kwa uvumilivu wote na kwa mafundisho mazuri.
Preach the worde: be instant, in season and out of season: improue, rebuke, exhort with all long suffering and doctrine.
3 Maana wakati utakuja watu watakapokataa kuyakubali mafundisho yenye uzima. Badala yake, ili kutimiza tamaa zao wenyewe, watajikusanyia idadi kubwa ya walimu wapate kuwaambia yale ambayo masikio yao yanayowasha yanatamani kuyasikia.
For the time will come, when they will not suffer wholesome doctrine: but hauing their eares itching, shall after their owne lustes get them an heape of teachers,
4 Watakataa kusikiliza kweli na kuzigeukia hadithi za uongo.
And shall turne their eares from the trueth, and shalbe giuen vnto fables.
5 Kwa habari yako wewe, vumilia mateso, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiza wajibu wote wa huduma yako.
But watch thou in all thinges: suffer aduersitie: doe the worke of an Euangelist: cause thy ministerie to be throughly liked of.
6 Kwa maana mimi sasa ni tayari kumiminwa kama sadaka ya kinywaji, nayo saa yangu ya kuondoka imetimia.
For I am nowe readie to be offered, and the time of my departing is at hand.
7 Nimevipiga vita vizuri, mashindano nimeyamaliza, imani nimeilinda.
I haue fought a good fight, and haue finished my course: I haue kept the faith.
8 Sasa nimewekewa taji ya haki ambayo Bwana, mwamuzi wa haki, atanitunukia siku ile: wala si mimi tu, bali pia wote ambao wamengoja kwa shauku kudhihirishwa kwake.
For hence foorth is laide vp for me the crowne of righteousnesse, which the Lord the righteous iudge shall giue me at that day: and not to me onely, but vnto all them also that loue that his appearing.
9 Jitahidi kuja kwangu upesi
Make speede to come vnto me at once:
10 kwa sababu Dema, kwa kuupenda ulimwengu, ameniacha na amekwenda Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia na Tito amekwenda Dalmatia. (aiōn )
For Demas hath forsaken me, and hath embraced this present world, and is departed vnto Thessalonica. Crescens is gone to Galatia, Titus vnto Dalmatia. (aiōn )
11 Ni Luka peke yake aliye hapa pamoja nami. Mtafute Marko uje naye kwa sababu ananifaa sana katika huduma yangu.
Onely Luke is with me. Take Marke and bring him with thee: for he is profitable vnto me to minister.
12 Nimemtuma Tikiko huko Efeso.
And Tychicus haue I sent to Ephesus.
13 Utakapokuja, niletee lile joho nililoliacha kwa Karpo huko Troa na vile vitabu vyangu, hasa vile vya ngozi.
The cloke that I left at Troas with Carpus, when thou commest, bring with thee, and the bookes, but specially the parchments.
14 Aleksanda yule mfua chuma alinitendea ubaya mkubwa. Bwana atamlipa kwa ajili ya yale aliyotenda.
Alexander the coppersmith hath done me much euill: the Lord rewarde him according to his workes.
15 Wewe pia ujihadhari naye kwa sababu aliyapinga sana maneno yetu.
Of whome be thou ware also: for he withstoode our preaching sore.
16 Katika utetezi wangu wa mara ya kwanza, hakuna hata mmoja aliyeniunga mkono, bali kila mmoja aliniacha. Namwomba Mungu wasihesabiwe hatia kwa jambo hilo.
At my first answering no man assisted me, but all forsooke me: I pray God, that it may not be laide to their charge.
17 Lakini Bwana alisimama upande wangu akanitia nguvu, ili kupitia kwangu lile Neno lihubiriwe kwa ukamilifu, watu wote Mataifa wapate kulisikia. Mimi niliokolewa kutoka kinywa cha simba.
Notwithstanding the Lord assisted me, and strengthened me, that by me the preaching might be fully beleeued, and that al the Gentiles should heare: and I was deliuered out of the mouth of the lion.
18 Bwana ataniokoa katika kila shambulio baya na kunileta salama katika Ufalme wake wa mbinguni. Atukuzwe yeye milele na milele. Amen. (aiōn )
And the Lord will deliuer me from euery euil worke, and will preserue me vnto his heauenly kingdome: to whome be praise for euer and euer, Amen. (aiōn )
19 Wasalimu Prisila na Akila, na wote wa nyumbani kwa Onesiforo.
Salute Prisca and Aquila, and the householde of Onesiphorus.
20 Erasto alibaki Korintho. Nami nikamwacha Trofimo huko Mileto akiwa mgonjwa.
Erastus abode at Corinthus: Trophimus I left at Miletum sicke.
21 Jitahidi ufike huku kabla ya majira ya baridi. Eubulo anakusalimu, vivyo hivyo Pude, Lino, Klaudia na ndugu wote.
Make speede to come before winter. Eubulus greeteth thee, and Pudens, and Linus, and Claudia, and all the brethren.
22 Bwana awe pamoja na roho yako. Neema iwe pamoja nanyi. Amen.
The Lord Iesus Christ be with thy spirit. Grace be with you, Amen. ‘The second Epistle written from Rome vnto Timotheus, the first Bishop elected of the Church of Ephesus, when Paul was presented the second time before the Emperour Nero.’